Uteuzi wa Job Masima kuwa Balozi Israel ni ishara ya Rais Magufuli kuinoa na kuiimarisha TISS

Uteuzi wa Job Masima kuwa Balozi Israel ni ishara ya Rais Magufuli kuinoa na kuiimarisha TISS

Umeandika kishabiki sana kimsingi vyoote ulivyowasifia hata mataifa mengine wanafanya[emoji1][emoji23][emoji23] na wamekuwa wanafanya kabla ya hao israel na vingine umeongezea chumvi kidogo hasa swala la nyoka
Ungetutajia mkuu kuepusha ubish.
Nyoga kamsome Israel snake robot
 
JK was from Army iliwakumbuka sana wenzie huyu anasemekana nae ni from wale jamaa wa K'Nyama naona awamu hii nae hawatupi wenzie akiiingia mlima tumbaku mwenzangu na mm ntaula
 
Anhaa, mimi ninahitaji akili za ziada? Okay.


Hakuna teuzi za JPM ambazo ni thought through and strategic. Balozi wa Israel kachaguliwa kwa mtindo wa random draws.


Aisee!! inawezekana ni kweli unahitaji akili za ziada!
usiongee uciyoyajua kwenye jumuiya....unaufunua upumbavu wako bure!
 
Nakuelewa, ila kwa sasa ubalozi umekwishafunguliwa na tuna balozi wetu mjini Tel Aviv.

Sikuongelea kwa undani kuhusu mgogoro wa mfereji wa Suez kati ya Israel na mataifa ya kiarabu wakiongozwa na Misri chini ya marehemu Anwar Sadat.

Ila unafamu kwamba nyuma ya mgogoro wa mfereji wa Suez kulikuwa na Marekani na ilokuwa USSR?

Kwa wakti ule Tanzania ilikuwa inafuata siasa za kikomunisti na ilikuwa inawafuata USSR yaani "soviet sphere of influence".

Hiyo ni historia na kuna topic kabisa kuhusu mfereji wa Suez ambayo inajitosheleza.

Bila kwenda ndani sana kwenye suala la mafunzo ni kwamba kwa sasa teknolojia na nyenzo za kisasa zipo na zinatengezwa na Israel na nchi nyingi tu sasa hivi zinaiangalia Israel.

Katika ulimwengu wa leo wa tishio la ugaidi na kila aina ya uhalifu wa kiteknolojia na uhalifu ulosukwa yaani "organised crime" basi unahitaji msaada wa wale wajuzi ambao wapo "available" na Israel wanajaza namba.

Ukizungumza utekaji ndege, utekaji meli na shughuli zozote ambazo zinaleta madhara kiuchumi kwa nchi fulani basi kuna njia za kuweza kujifunza namna ya angalau kuzuia mambo hayo yasitokee hivyo Israel wapo karibu kabisa na eneo la tukio kusaidia.

Ukiingia katika tovuti ya Bloomberg kwenye "innovation index" utapata Data kwamba Israel ni nchi ya tano duniani kwa ubunifu yaani "innovation".

Israel ina wanasayansi na wahandisi 140 katika idadi ya waajiriwa 10,000 ikiwa ni sawa na asilimia 85 kwa idadi hiyohiyo nchini Japan na asilimia 83 nchini Marekani.

Hawa wanasayansi na wahandisi pia wameshiriki kuendeleza mambo mengi katika sayansi ya asili, sayansi ya kilimo kwenye umwagiliaji (drip irrigation), vifaa vya umeme, sayansi ya kompyuta, na hata kumuunda robot.

Kwa mfano leo hii nchii Israel wanakunywa maji ambayo awali yalikuwa ni maji ya bahari baada ya kufanya kitu kinatwa "water conversing" ambapo maji ya bahari yanavunwa na kuchujwa.

Ninaweza kujaza hii sehemu lakini hayo ni machache tu mkuu, jifunze zaidi kuhusu hawa jamaa.

Pia unapojadili hii mada, jaribu sana kuepusha suala la dini maana siko huko.
Mkuu,

Inawezekana kabisa ni kweli hao jamaa wana sifa ulizoorodhesha hapo juu na pengine kuzidi hizo,lakini,hivi tunawseza kunufaika nazo kweli kama ambavyo tumekuwa tukifikiria hapa na kwingineko?

Mleta uzi anaelezea jambo kama ulilolisema wewe,tatizo ambalo ninaliona hapa siyo hawa jamaa au sisi kuwa na ubal;ozi kokote maana tushakuwa na mabalozi kwenye nchi nyingi sana zenye maendeleo kwenye sekta mbali mbali lakini hapa ndipo tulipo....

Tatizo langu siyo wenzetu bali ni sisi,hapa tulipo na namna tunavyofikiria tunaweza kweli kunufaika na kwa sisi kuwa na mahusiano mazuri ya kibalozi na Israel au nchi nyingine yoyote yenye maendeleo yoyote?

Jibu la swali hili ni gumu kidogo kwasababu kama ingekuwa ni rahisi basi leo tungekuwa mbali sana....

Kuna mambo kadhaa ya kujiuliza,hivi ni kweli hawa jamaa wapo tayari kutukwamua hapa tulipo?

Ni kweli tupo kwenye mazingira rafiki ya kunufaika na hawa jamaa?

Ni kweli tumeshindwa kunufaika na maendeleo ya Japan,Marekani,China na nchi nyingine hadi iwe ni jambo la ajabu sana sisi kuwa na mahusiano ya kibalozi na nchi hii?

Ni kweli changamoto zetu zitaondolewa na watu wengine na siyo sisi wenyewe?

Hivi wakati wa changamoto hizi huko kwao walisaidiwa?

Mkuu hapa sijagusia suala la ugaidi ambalo umelitaja ambalo kwa maoni yangu sidhani hata kuna umuhimu wa sisi kulifikiria kwa sasa maana mazingira yetu ni tofauti kabisa na wao....
 
ni muda sasa umepita tokea tupate uhuru, nchi za wenzetu ikiwemo china waliwatumia wanausalama wao kujiimarisha kiuchumi lakini kama hawa Tiss hawapo chini ya chama kilichopo madarakani ni lipi walilolifanya kutuimarisha kiuchumi?

Economic espionage ni nzuri sana katika maendeleo ya nchi na inatumiwa sana na mataifa mengi ili kuinua uchumi sasa sijui nyumbani...
 
hiyo sytle ya maofisa usalama na security guards ipo hivyo karibia viwanja vyote.....labda tuambiane namna yao ya ulinzi iliyo tofauti na nchi nyingine...

Ni kweli mkuu, lakini hakuna mtekaji yoyote wa ndege awe wa kipalestina au kiarabu ambae amefanikiwa kuiteka ndege kutokea uwanja wa ndege wa Ben-Gurion.

Pili, hakuna aina yoyote ya uzembe katika kulinda kiwanja hiki cha ndege kiasi cha kupitisha aina yoyote ya magendo na mizigo ilopigwa marufuku.

Hivyo upo sawa kwamba hata Tanzania tunao hao maofisa usalama na security guards lakini madini na madawa ya kulevya vimekuwa vikipitishwa kwenye viwanja vyetu JNIA na KIA miaka nenda rudi.

Hivyo ni uamuzi wa busara kama Tanzania itashirikiana na Israel katika suala la ulinzi khasa huu wa viwanja vya ndege.

Hivi unafahamu kwamba katika Israel na nchi zingine za Ulaya na Marekani kabla ya kuwa afisa usalama wa uwanja wa ndege au security guard ni lazima upite stage tatu?

Mtandaoni kufanya mtihani, pili katika mazungumzo kwenye simu na mwisho usaili wa ana kwa ana ili kukufahamu , ukifika kwenye usaili wa ana kwa ana basi fahamu wewe umepita.

Mtihani wa mtandanoni ndiyo muhimu zaidi kuliko hatua hizo mbili za mwisho.

Upo hapo mkulu?
 
Wewe unaota. Mambo kama haya yanataka close relationship.
Sasa rais wetu anaogopa kusafiri...kwenye mikutano anatuma watu wa chini yake kuna nchi itatuchukulia serious ?
Tutasikia tu hayo mambo ya misaada
 
TISS ni idara nyeti kama tinavyoaminishwa na mara nyingi tuliaminishwa kuwa ni smartest...

But kinadhalia na kivitendo hakuna jipya ambalo lishawahi kufanywa na idara ya kijajusi ya kibongo, zaid kusifika kwenye mbinu chafu za kuingiza ccm madarakani

Wakitaka hii idara ieshimeke na kutoa matunda chanya, basi iwe idara ya kujitegemea na sio kufungamana na chama dola, na kushirikisha ku recruit vijana ambao ni genuine. .
 
Miaka ya nyuma kidogo ilikua ni ngumu mkumjua afisa usalama wa Taifa nakumbuka niliwahi kujitia chizi mkoa fulani nikaibuka ofisi zao ili kuulizia nafasi za mafunzo nilienda asubuhi ila nilitoka jioni sanaaaa nikiwa nimeweka uchi ID yangu wale jamaa walinikomalia nimeambiwa na nani kua kuna nafasi siwezi sahau,siku hizi nikiwa bar mwehu anaanzisha ugomvi na anakimbilia kutoa kitambulisho kua yeye ni kitengo kuna mmoja alinikera sana alitoa kitambulisho na akasema hadi mshahara wao duh nimeshangaa juzi yule kilazà mwingine anatoa silaha kibwege vile alafu anamlenga mtu mchana kweupe tena mtua ambae hana silaha mbaya zaidi anakuja kudhibitiwa na Kitenge inaonyesha tumeoza kama Masima anapelekwa kwa nia ya kuimarisha kitengo naona ni vyema ila kama kumuimarisha mtu binafsi ni tatizo.
Baadae walikupa kazi?
 
vizur lakini vigezo vya hilo swali la mwisho vizingatiwe, hupaswi kumteua mtu mwenye PHD ya CIVIL ENGINEERING akafanye kazi ya UUGUZI kisa tyuu eti msomi, ni lazima aendane na professional yake aliyonayo!!!
 
Back
Top Bottom