Uteuzi wa Paul Makonda kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa ni moto!

Uteuzi wa Paul Makonda kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa ni moto!

Huyo alikuwa anafata amri za boss wake hajajifanyia hata kimoja kwa mawazo yake.

CCM wanalifahamu hilo ndiyo maana hawakumuadhibu muda wote.
hivi sasa tutajua kama alikua ni yeye mwenyewa ama ni maelekezo kutoka juu
 
Huyo alikuwa anafata amri za boss wake hajajifanyia hata kimoja kwa mawazo yake.

CCM wanalifahamu hilo ndiyo maana hawakumuadhibu muda wote.
umeongea kinyonge sana bibi. inaonyesha hujafurahishwa na uamuzi wa ikulu kumrudisha makonda kwenye mfumo.

umepigwa na kitu kizito.pole sana bibi.
 
makonda na mama wanajuana mda mrefu, nadhani lilikuwa ni swala la when and which position tu, ila ilikuwa wazi kuwa makonda angerudi kwenye uongozi, ukizingatia pamoja na kuwanna kashfa nyingi kama sabaya ila hajaguswa kabisa.
 
Ni moto, si, tu kwa Upinzani bali pia kwa waliolala na kujibweteka kwa kufanya kazi kwa mazoea ndani ya chama na ndani ya serikali iliyopo mamlakani.

Huyu kijana si tu mwanasiasa bali pia mwanaharakati mahiri nchini. Ana hulka za jino kwa jino, sina hakika kama kabadilika.

kwa maoni yangu uteuzi wake unalenga kujibu mapigo ya upinzani dhidi ya chama na serikali iliyopo Madarakani kwa hoja na vihoja.

Uteuzi huu pia unalenga kuudhibiti upinzani na kile kinachodaiwa ni upotoshaji dhidi ya mipango na hatua mbalimbali zinazo chukuliwa na serikali kuwaletea wananchi maendeleo.

Uteuzi huu ni amsha amsha dhidi ya walio lala na kujisahau ndani ya chama Tawala na ndani ya serikali sikivu, hii ni pamoja na mawaziri, wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi na wateule mbalimbali wa Rais.

Kwa kijana huyu ubunifu na uwajibikaji wenye matokeo yanayo jidhihirisha na kuonekana kwa umma ndio itakua pona ya wateule wengi.

Uteuzi wa Paul Christian Makonda kuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa ni moto chini nchini.

swali linabaki ni je, uteuzi huu utaimarisha au utadhoofisha upinzani katika siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu 2025?

Timu Za Wasaka Urais kama Yule Mvaa bendera , na lile kundi la Februari uteuzi huuu ni pigo kubwa sana ..

Kuna kundi jipya linaibuka la kumsaidia mama na 2025 watoe PM na Makamu Halafu Makonda naye atapata jimbo moja pale Mwanza…na uwaziri
 
makonda na mama wanajuana mda mrefu, nadhani lilikuwa ni swala la when and which position tu, ila ilikuwa wazi kuwa makonda angerudi kwenye uongozi, ukizingatia pamoja na kuwanna kashfa nyingi kama sabaya ila hajaguswa kabisa.

Bila mama Makonda angekua segereea Au angekua katunguliwa na maadui zake…..,

Amemsaidia kupata moja ya nyumba za TBA pale Oysterbay na akaaigiza auziwe.

Ameingizwa kwenye payroll na Pamoja na kuwa nje amekua anapokea mshahara

Biashara zake hazijabuguziwa….Maduka manne ya madawa miji ya DAR, MWANZA na Arusha .

Ana uangalizi au ulinzi wa aina fulani hata kama sio moja kwa moja kumekua na watu wa kumtizama asidhurike..

KESI zake zote zimekwamia kwa DPP kwenda mahakamani.

ILIKUA arudi toka mwaka Jana wakawa wanasubiri baadhi ya kesi alizofunguliwa ziishe … [ kina Kubenea wa kesi binafsi nao wamevuta ]


Tatizo pekee linaloenda kutokea ni mgawanyiko ndani ya ccm hasa kwa wafuaasi wa Mwenyekiti ambao hawaataki kabisa kumuona Makonda ……hivyo anaenda kukabiliwa na upinzani mkali ndani .

HUENDA Makonda akadumu Muda mfupi sana kwenye cheo hasa itategemea na siku zake 100 za mwanzo na maoni ya wanachama …na pengine uwezekano ni kurudishwa kuwa Mkuu wa Mkoa au kuingia kama msaidizi wa Rais hasa kuelekea uchaguzi Mkuu.
 
Ni moto, si, tu kwa Upinzani bali pia kwa waliolala na kujibweteka kwa kufanya kazi kwa mazoea ndani ya chama na ndani ya serikali iliyopo mamlakani.

Huyu kijana si tu mwanasiasa bali pia mwanaharakati mahiri nchini. Ana hulka za jino kwa jino, sina hakika kama kabadilika.

kwa maoni yangu uteuzi wake unalenga kujibu mapigo ya upinzani dhidi ya chama na serikali iliyopo Madarakani kwa hoja na vihoja.

Uteuzi huu pia unalenga kuudhibiti upinzani na kile kinachodaiwa ni upotoshaji dhidi ya mipango na hatua mbalimbali zinazo chukuliwa na serikali kuwaletea wananchi maendeleo.

Uteuzi huu ni amsha amsha dhidi ya walio lala na kujisahau ndani ya chama Tawala na ndani ya serikali sikivu, hii ni pamoja na mawaziri, wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi na wateule mbalimbali wa Rais.

Kwa kijana huyu ubunifu na uwajibikaji wenye matokeo yanayo jidhihirisha na kuonekana kwa umma ndio itakua pona ya wateule wengi.

Uteuzi wa Paul Christian Makonda kuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa ni moto chini nchini.

swali linabaki ni je, uteuzi huu utaimarisha au utadhoofisha upinzani katika siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu 2025?
Tulizen mshono , makondonda kwenye siasa bado sana japo anabebwa tu
 
Back
Top Bottom