Uchaguzi 2020 Uteuzi wa Van Zeland kuwa Mgombea Ubunge Mvomero kwa upande wa CCM, haujatutendea haki wananchi wa Wilaya ya Mvomero

Uchaguzi 2020 Uteuzi wa Van Zeland kuwa Mgombea Ubunge Mvomero kwa upande wa CCM, haujatutendea haki wananchi wa Wilaya ya Mvomero

Mathanzua

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
17,251
Reaction score
22,929
Mvomero sio Wilaya kongwe,na kwa hiyo kimaendeleo iko nyuma sana.Wilaya hii ina matatizo mengi, ya msingi yakiwa upatikanaji wa maji,migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo imedumu kwa miaka mingi sasa.Awamu zote zinaonekana kushindwa kabisa kutatua tatizo hili,sababu kubwa ikiwa viongozi kuwa mgongano wa kimaslahi. Lipo pia tatizo la kilimo,hasa upande wa ugani na umeme.Lipo pia tatizo la miundombinu ya elimu, ambalo limefanya wananchi wengi wa Wilaya hii kukosa elimu na hivyo kuwafanya wawe nyuma sana kimaendeleo.

Lipo tatizo kubwa mama la uongozi katika Wilaya hii.Sina haja ya kusema awamu zilizopita uongozi ulikuwaje,itoshe tu kusema kwamba Wilaya hii tangu kuanzishwa kwake haijawahi kupata viongozi committed kwa maendeleo ya Wilaya hii,tangu ngazi za chini kabisa mpaka juu.Si ajabu kwa hiyo kwamba maendeleo ya Wilaya hii ni duni sana.

Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi,tena uchaguzi wa mhula wa pili awamu ya tano.Tulitegemea basi kwamba Wilaya yetu ingeangaliwa kwa jicho la pekee,ili ipate viongozi makini na wazuri ambao watasukuma mbele maendeleo yetu.Kilichotokea hata hivyo ni tofauti kabisa.Van Zealand ambaye ameteuliwa kugombea kwa tiketi ya CCM hawezi kutusaidia kabisa.

Huyu bwana amekuwa mwenyekiti wa Halmashauri kwa muda mrefu,na katika kipindi chake chote alichokuwepo hali ya Wilaya yetu haijaboreka na matatizo ya wananchi yapo pale pale, au hata kuzidi. Katika hali ya kawaida kabisa, hili lingetosha kumuengua. Na kwa nini ameteuliwa yeye kupeperusha bendera ya CCM wakati aliyepita kwenye kura za maoni ni Makala?

Niseme wazi, kwetu Makala angekuwa bora zaidi kuliko Zeland,ingawa of course naye ana matatizo yake.Van Zeland tunamjua, yuko kimaslahi zaidi na naamini ameingia huko kwa ajili ya maslahi yake binafsi,na wala sio kuwatumikia wananchi.

Ipo minong'ono mingi kuhusu michezo michafu,na inasemekana hata tambo zake mwenyewe zinaashiria hili. Katika hili naiomba TAKUKURU iingilie kati,huenda labda ikatunusuru.

Mwisho,binafsi najiuliza sana,hivi kwa nini CCM ilitangaza hadharani kwamba si lazima anayepita kwenye kura za maoni ateuliwe yeye kupeperusha bendera ya CCM?Hivi chama hakikuona kwamba mwanya huu ungeweza kutumiwa vibaya na watu wasio waaminifu kama ilivyotokea Mvomero, ingawa nia ilikuwa njema?
 
Maendeleo duni ya wilaya ya Mvomero yanachangiwa na uwepo wa idadi ndogo ya watu.. Eneo kubwa la Mvomero ni mapori na wafugaji ambao ndio wengi wamejichimbia ndani ndani.
Mkuu wewe ni mwenyeji wa Wilaya ya Mvomero?Maana kwa comment hii inaelekea huijui.Anyway,concern yangu ipo palepale,kwa hiyo tuna haki ya kupata viongozi wazuri.
 
CCM imekuwepo tangu 1961, unategemea leo ikuletee maendeleo kwa miaka 5?
Kama imewezakana kufanya so much in the past 5 years,tunaamini CCM itafanya vizuri zaidi katika miaka 5 hii ijayo.We are hopeful kwamba CCM tukipata Rais mwingine mzuri kama Magufuli or even a better one,tuta-piga hatua,we are optimistic.
 
Kama imewezakana kufanya so much in the past 5 years,tunaamini CCM itafanya vizuri zaidi katika miaka 5 hii ijayo.We are hopeful kwamba CCM tukipata Rais mwingine mzuri kama Magufuli or even a better one,tuta-piga hatua,we are optimistic.
Ukiulizwa amefanya nini unaweza kutaja hata mambo 5?
 
Mkuu wewe ni mwenyeji wa Wilaya ya Mvomero?Maana kwa comment hii inaelekea huijui.Anyway,concern yangu ipo palepale,kwa hiyo tuna haki ya kupata viongozi wazuri.
Jibu langu la mwanzo liliegemea kwenye makao makuu ya wilaya.. Yani kata ya Mvomero.

Ok.. Tuzungumzie kata chache za Mvomero kama Mzumbe, Mlali, Mvomero, Melela, Doma, Mlali na Mtibwa.. Ulitaka nini kikubwa kifanyike ili kuchochea maendeleo kwenye wilaya yetu inayouzungumka mji wa Morogoro, ili mbunge aanze navyo?
 
Jibu langu la mwanzo liliegemea kwenye makao makuu ya wilaya.. Yani kata ya Mvomero.

Ok.. Tuzungumzie kata chache za Mvomero kama Mzumbe, Mlali, Mvomero, Melela, Doma, Mlali na Mtibwa.. Ulitaka nini kikubwa kifanyike ili kuchochea maendeleo kwenye wilaya yetu inayouzungumka mji wa Morogoro, ili mbunge aanze navyo?

1. Tatizo la wafugaji na wakulima limalizwe once and for all.Hii itawezekana kama viongozi watazuiwa kuwekeza mifugo kwa Wamasai,hii imefanya umalizwaji wa tatizo hili kuwa mgumu kwa sababu ya conflict of interest.Wamasai pia watengewe maeneo yao ya ufugaji,na tunaomba suala la carrying lizingatiwe.

2. Tatizo la maji:Tunataka miradi zaidi ya maji ili kuwasogezea wananchi maji karibu zaidi.Kwa sasa sehemu nyingi maji yako mbali,na wananchi wanapata taabu sana,na wengi wanakunywa maji machafu ya mabwawa ambayo ni hatarishi kwa afya zao.Miradi pia iliyopo kama ya World Bank usimamizi ni mbovu sana,na sehemu zingine ambapo miradi hii ipo, wananchi either hawapati maji kabisa au wanapata kwa masaa machache sana.Hakuna sababu yeyote kimsingi kwa nini vijiji ambavyo miradi hii ipo wananchi wasipate maji masaa ishirini na nne.Mbunge alifuatilie hili kwa ukaribu sana.Na sio gumu,kila miradi uliopo ukipata seed money ya 2,000,000/= inawezekana.

3. Elimu:Madawati,madarasa,na vyoo vya shule nyingi ni hoi sana.Tunataka matatizo haya yashuhulikiwe kwa ajili ya usalama wa watoto wetu.
Swala la nyumba za waalimu pia ni muhimu sana.Tunaomba mbunge alipigie kelele hili,waalimu wengi wanakaa maeneo duni sana,na hii inashusha sana ari yao ya kufundisha.Kwa Wilaya yetu swala hili ni muhimu sana,kwa vile makazi mengi ni duni,kwa hiyo waalimu hawapati nyumba nzuri za kupanga.

4. Huduma za ugani:Wahudumu wa kilimo yaani VEOs, ni wachache sana,na hata waliopo uwezo wao ni mdogo sana.Wananchi wanataka enough and competent VEOs.Kwa sasa wakulima wengi hawana huduma ya ugani,na hata VEOs waliopo input yao ni ndogo sana.Jambo hili ni muhinu kwa kuwa matatizo kwenye kilimo sasa yamekuwa mengi mno.Hili tatizo limekuwa kuwa zaidi in the past 2 years.Literally wakulima had to fend for themselves.

4. Umeme:Vijiji Vingi umeme wa REA bado haujafika.In fact hata sehemu ambapo miundo mbinu ya kuweza kusambaza umeme wa REA kiurahisi ipo, bado umeme haujasambazwa.Mbunge afuatilie swala hili ili wananchi wapate umeme.

5. Usimamizi na ukarabati wa miundombinu:Miundombinu ya barabara inaharibiwa maeneo mengi ya Wilaya.Tunataka viongozi wajikite zaidi kwenye kuhakikisha kwamba miundo mbinu iliyopo haiharibiwi,either na mifugo au kitu kingine chochote kile.Pia Tunataka ukarabati wa barabara zetu ufanyike kwa wakati,tusisubiri mpaka kiongozi mkuu awe anakuja au wakati wa uchaguzi ukiwa unakaribia ndio tuanze kuhangaika.
 
Maendeleo duni ya wilaya ya Mvomero yanachangiwa na uwepo wa idadi ndogo ya watu.. Eneo kubwa la Mvomero ni mapori na wafugaji ambao ndio wengi wamejichimbia ndani ndani.
Warudishwe kijijini ili maendeleo yawepo
 
Makala alishawahi kuwa mbunge wa hilo jimbo miaka ya nyuma,alileta maendeleo gani katika hilo jimbo?
 
Back
Top Bottom