UTI- Naomba msaada kupata ufumbuzi wa hili tatizo

majitatz

Member
Joined
Sep 25, 2017
Posts
6
Reaction score
3
Nina kama mwezi hizi nilikua nasikia muwasho na maumivu nikikojoa, nikaenda hospitali nikapipa nikaambiwa nina UTI nyingi, Nikapewa dawa inaitwa NITROFULANTION nikamaliza dozi ila bado nikaendelea kupata shida, nikaenda kupima tena nikaambiwa bado tatizo lipo nikapewa dawa inaitwa NIRFLOXACILIN nimemaliza dozi jumapili, bado shida ipo na nimeanza kutoka usaa kidogo sasa nimechanganyikiwa naomba ushauri wa dawa sahihi ili tatizo langu liishe. naomba kuwasilisha.
 
una weka kwenye glass ya maji kijoko cha chai 2kwa cku21 . Iwe backing soda sio powder
 
unaitumiaje mkuu
Acha ujinga wewe.... Unaijua baking soda? Unajua imetengenezwa kwa machemical gani? Unajua madhara yake?


Ulienda hospital gani kupima? Nenda hospital kubwa inayoeleweka. Usiende kusema unataka kupima UTI, nenda eleza tatizo hadi lilipofikia ili wakupime kila kitu kuanzia Magonjwa ya zinaa hadi UTI.

Achana na jamii forum
 
mi nikajua ukipima mkojo wanajua moja kwa moja shida iliyo kwenye mkojo
 
Kheri wewe akili unae ita wengine wajinga ila kwa huu huu ujinga wangu nimesaidia watu wakapona bila ttzo lolote
 
Umempa ushauri kupitia Jamiiforums halafu unamwambia aachane na Jamiiforums ?
 
Nitajie chemical composition ya baking soda na ina madhara gani kwa binadam na kwnn ina tumiwa kwenye mapishi kma mlenda na waoka mikate
 
Kidogo cha chai mara 2 kwa siku kwa cku 3 hadi 5 kulingana na ukubwa wa ttzo
unainywa hayo maji yaliyokua mixed na baking soda? baking soda unawek kiasi gani mkuu
 
Mtoa mada ungejitambulisha kwanza wewe ni Me au Ke,hizo dalili unazotoa zinatia shaka

Nenda kapime tena hospital nyingine upate uhakika kama unaumwa UTI na hakikisha unamaliza dozi
 
nunua dawa moja hivi inaitwa Amoxicillin-clavulanic acid iko poa sana kwa hao wadudu na dawa uliopewa sio mbaya ila mara nyingi wanapewa wa mama wajazito.Huenda dawa uliopewa ina effect kidogo na hao wadudu au tayari kuna resistance kwa hizo dawa. ila pia kapime uchek hali ya ugonjwa.
 
hii kitu sio nzuri hata kidogo na haina effect on bacterial labda kwenye v2 vingine sodium bicarbonate Amoxicillin-clavulanic
lazima kutakuwa na utofauti wa utendaji kazi kwenye hizi compounds mbili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…