Nina kama mwezi hizi nilikua nasikia muwasho na maumivu nikikojoa, nikaenda hospitali nikapipa nikaambiwa nina UTI nyingi, Nikapewa dawa inaitwa NITROFULANTION nikamaliza dozi ila bado nikaendelea kupata shida, nikaenda kupima tena nikaambiwa bado tatizo lipo nikapewa dawa inaitwa NIRFLOXACILIN nimemaliza dozi jumapili, bado shida ipo na nimeanza kutoka usaa kidogo sasa nimechanganyikiwa naomba ushauri wa dawa sahihi ili tatizo langu liishe. naomba kuwasilisha.