Utitiri wa Kadi: Kwanini tusiwe na Kadi Moja ya Huduma za Usafiri inayoweza kutumika kwenye maeneo yote?

Utitiri wa Kadi: Kwanini tusiwe na Kadi Moja ya Huduma za Usafiri inayoweza kutumika kwenye maeneo yote?

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Habari zenu wakuu. Natumaini mko salama humu jukwaani. Bila kupoteza muda, naomba niende moja kwa moja kwenye mada.

Jana nilikutana na mjadala mtandaoni kuhusu uzinduzi wa kadi mpya za mwendokasi, ambapo sasa bila kadi hii huwezi kufanya safari kwenye usafiri wa mwendokasi. Hii imenifikirisha kuhusu utitiri wa kadi mbalimbali tunazotumia kwa huduma tofauti, kama N-Card kwa ununuzi wa tiketi za michezo na kadi mpya za mwendokasi kwa usafiri. Changamoto hii ya kuwa na kadi nyingi inaleta usumbufu na hatari ya kupoteza kadi hizo.

Nadhani ni wakati wa serikali na taasisi husika kuangalia uwezekano wa kuwa na kadi moja inayoweza kutumika kwa huduma zote kwani itapunguza mzigo wa kubeba kadi nyingi na itarahisisha maisha kwa kuongeza usalama na urahisi wa matumizi kwa wananchi.
1725434062791.png

1725434073447.png

1725434081465.png

Nawakaribisha kwa michango yenu kwenye mjadala huu muhimu!

1725429073139.png
Pia soma:
 
Ngoja waje wenyewe , wewe unaumia na utitiri wa kadi ama wapigaji wanaoiibia serikali kwa matiketi feki ya makaratasi yaliyojazwa kwenye mandoo? na zile mia mia zetu na hamsini wanazosema hawana chenji kila siku kipi Bora?
 
Hizi kadi za mwendokasi zilikuwepo wakaziondoa ili waweze kuiba vizuri. Zimerudishwa tu sio jambo jipya.
 
Habari zenu wakuu. Natumaini mko salama humu jukwaani. Bila kupoteza muda, naomba niende moja kwa moja kwenye mada.

Jana nilikutana na mjadala mtandaoni kuhusu uzinduzi wa kadi mpya za mwendokasi, ambapo sasa bila kadi hii huwezi kufanya safari kwenye usafiri wa mwendokasi. Hii imenifikirisha kuhusu utitiri wa kadi mbalimbali tunazotumia kwa huduma tofauti, kama N-Card kwa ununuzi wa tiketi za michezo na kadi mpya za mwendokasi kwa usafiri. Changamoto hii ya kuwa na kadi nyingi inaleta usumbufu na hatari ya kupoteza kadi hizo.

Nadhani ni wakati wa serikali na taasisi husika kuangalia uwezekano wa kuwa na kadi moja inayoweza kutumika kwa huduma zote kwani itapunguza mzigo wa kubeba kadi nyingi na itarahisisha maisha kwa kuongeza usalama na urahisi wa matumizi kwa wananchi.

Nawakaribisha kwa michango yenu kwenye mjadala huu muhimu!
View attachment 3086491
Serikali ilikuwa na mpango mzuri kuwa na card moja ambayo ita facilitate huduma nyingi, sasa sijui ni nini kinatokea na kila mmoja kuja na kadi yake, mfano N card ilianza vzr sn na iliweza ku-facilitate kwenye ferries na kuingia uwanjani, nilidhani kadi hizo zingekuwa accessed pia kwa ajili ya Dart na si Dart kuja na zao kama kuna changamoto wange mitigate na kuzifanya ziwe sawa jambo ambalo lingesaidia kwa huduma nyingine!! Suala hili ni vema lingeratibiwa na taasisi moja!!!
 
Tutumie N-card haina mambo mengi, na tupunguze mrundikano wa kadi kwenye wallet zetu. Fanyeni tutumie N card tumalize biashara.
 
Habari zenu wakuu. Natumaini mko salama humu jukwaani. Bila kupoteza muda, naomba niende moja kwa moja kwenye mada.

Jana nilikutana na mjadala mtandaoni kuhusu uzinduzi wa kadi mpya za mwendokasi, ambapo sasa bila kadi hii huwezi kufanya safari kwenye usafiri wa mwendokasi. Hii imenifikirisha kuhusu utitiri wa kadi mbalimbali tunazotumia kwa huduma tofauti, kama N-Card kwa ununuzi wa tiketi za michezo na kadi mpya za mwendokasi kwa usafiri. Changamoto hii ya kuwa na kadi nyingi inaleta usumbufu na hatari ya kupoteza kadi hizo.

Nadhani ni wakati wa serikali na taasisi husika kuangalia uwezekano wa kuwa na kadi moja inayoweza kutumika kwa huduma zote kwani itapunguza mzigo wa kubeba kadi nyingi na itarahisisha maisha kwa kuongeza usalama na urahisi wa matumizi kwa wananchi.
View attachment 3086567
View attachment 3086568
View attachment 3086569
Nawakaribisha kwa michango yenu kwenye mjadala huu muhimu!

Pia soma:
N-card ni nini wengine hatujui
 
Kuna mwaka nilijichanganya nikatoka nyumbani na card ya mwendokasi nikidhani ni ya NMB, kufika bank nashanga service denied
 
BISMILLAH.
Al-hamdulillah 🙏.
Namshukuru Mwenyezi mungu.
Kwa Kukutana na Mjadara Huu.
Maana ni mda mlefu. Naweza sana.
Juu ya hili swala la kuwa na Card za malipo hasa katika mifumo ya kibiashara hususani Kuuza na kununua.
Malipo mfano ya Vipando,viwanja. Nk.
Maana khofu Ipo pale Mtu Akirundika mizigo mwisho Nimajuto.
Na kwanini Kuyasubiria Maradhi.
Tuchukue Tahadhar Mapema?
Mimi Ninalo Ombi Kwa Serikal Yetu.
Itizamie juu ya Hili Jambo Tuweze Kuwa salama Katika Hifadhi wa Amana zetu.
Inshallah 🙏
 
Hata mabenki ,bima,hifadhi za jamii, n.k.Mimi mpaka nachanganyikiwa.
 
Unadhani watakula wapi sasa kwa urefu wa namba zao?
 
Za pale Ferry zinauzwaje?bei yake?
 
Hii ni hoja ya msingi sana, kadi zimekuwa nyingi sana hadi kero. Inashangaza kuona hili jambo limefumbiwa macho. Hivi ni kwamba hatuna wataalam wa kusaidia kuifanya kadi itumike katika maeneo tofauti au changamoto ni nini? Ukibeba kadi za bank, vitambulisho na kadi za kusafiria unajikuta umebeba mzigo mkubwa. Kuna kila haja ya kushughulikia hili suala.
 
Kuwa na Smart card moja inayosomana na mifumo yote ya serikali inawezekana ila ndio hivyo wazee wa manunuzi dili mixer wazabuni watapatia wapi 10%?

Hii nchi kila mahala upigaji tu
 
Back
Top Bottom