A
Anonymous
Guest
Kuna changamoto ambayo bila kuifuchua inaweza kuzidi kuwa kubwa na kusababisha ubadhirifu, rushwa na mengine mengi yasiyofaa kwenye jamii yetu.
Uongozi wa Halmashauri ya Arusha DC imekuwa ikifanya michezo michafu kwenye utoaji wa tenda wa kukusanya ushuru wa Halmashauri pamoja na kuchezea mfumo mzima wa ukusanyaji mapato, fedha zinaenda mifukoni mwa watu badala ya kwenda Serikalini
Ipo hivi, Mwaka 2023 kuna mtu alipewa tenda ya kukusanya mapato ya Halmashauri baada ya kushinda Tenda iliyotangazwa, lakini kilichokuja kubainika baadaye ni kuwa hakushinda kihalali.
Kwanza alishinda kwa kuwa Afisa Ugavi wa Halmashauri aliyekuwa akisimamia mchakato na mshindi wa tenda wana ukaribu wa aina fulani.
Hilo tuliliacha likapita, tukasema this time tutajipanga na kufikisha ujumbe kwa usahihi na ikiwezekana kuongeza ushindani katika uombaji wa tenda.
Wakati mchakati ukiendendelea tukagundua kuwa wahusika hasa Afisa Ugavi wa Halmashauri ama na wenzake kadhaa au yeye mwenyewe, wanashiriki kuuchezea Mfumo wa NeST unaotumika kuomba tenda, ambapo wale wanaoomba hasa wa Arusha na wana maslahi hawawezi kuona maombi hayo.
Namaanisha hivi mfano Juma na Bakari wao wamejisajili ndani ya mfumo na wana maslahi na tenda hiyo, hawawezi kuona tenda, kisha wale wengine waliojisajili ambao hawana maslahi wanaweza kuona maombi hayo, ni kama ilivyo kwenye Mfumo wa Status wa WhatsApp, ambapo mtu anaweza kuziba usione alichopost.
Kwa nini wnafanya hivyo, wanafanya hivyo ili watumaji maombi wawe walewale waliolengwa.
Yule aliyeshinda Tenda mwaka jana, safari hii akasajili kampuni sit ana zote zikaomba, hivyo mtu mwingine akiangalia kwenye mfumo anaona maombi yapo na watu wameomba lakini kiuhalisia kuna mambo yanayoendelea na mtu wa karibu na watu hao ndio atajua kinachoendelea, mwingine taona kila kitu kipo sawa.
Mkuu wa Wilaya alijulisha juu ya suala hilo lakini naye kapotezea, aliingilia lakini hakuwa na nia ya kuondoa tatizo sugu linaloendelea.
Kwa ufupi ushindani wa Tenda katika Halmashauri ya Arusha DC haipo fair kwa maana hakuna haki.
Wale wenzetu waliojaribu kufikisha taarifa hii TAKUKURU, ikabainika kuwa pale katika ofisi hiyo Afisa anayesimamia ni mmoja wa watu mbao ana ukaribu na timu ile ya Watu wa Halmashauri.
Hivyo, ukifikisha taarifa TAKUKURU Arusha ili wasaidie Taifa lipate malipo stahiki, taarifa zitawafikia wahusika hata kabla ya Ofisi hiyo kufanya maamuzi.
Uongozi wa Halmashauri ya Arusha DC imekuwa ikifanya michezo michafu kwenye utoaji wa tenda wa kukusanya ushuru wa Halmashauri pamoja na kuchezea mfumo mzima wa ukusanyaji mapato, fedha zinaenda mifukoni mwa watu badala ya kwenda Serikalini
Ipo hivi, Mwaka 2023 kuna mtu alipewa tenda ya kukusanya mapato ya Halmashauri baada ya kushinda Tenda iliyotangazwa, lakini kilichokuja kubainika baadaye ni kuwa hakushinda kihalali.
Kwanza alishinda kwa kuwa Afisa Ugavi wa Halmashauri aliyekuwa akisimamia mchakato na mshindi wa tenda wana ukaribu wa aina fulani.
Hilo tuliliacha likapita, tukasema this time tutajipanga na kufikisha ujumbe kwa usahihi na ikiwezekana kuongeza ushindani katika uombaji wa tenda.
Wakati mchakati ukiendendelea tukagundua kuwa wahusika hasa Afisa Ugavi wa Halmashauri ama na wenzake kadhaa au yeye mwenyewe, wanashiriki kuuchezea Mfumo wa NeST unaotumika kuomba tenda, ambapo wale wanaoomba hasa wa Arusha na wana maslahi hawawezi kuona maombi hayo.
Namaanisha hivi mfano Juma na Bakari wao wamejisajili ndani ya mfumo na wana maslahi na tenda hiyo, hawawezi kuona tenda, kisha wale wengine waliojisajili ambao hawana maslahi wanaweza kuona maombi hayo, ni kama ilivyo kwenye Mfumo wa Status wa WhatsApp, ambapo mtu anaweza kuziba usione alichopost.
Kwa nini wnafanya hivyo, wanafanya hivyo ili watumaji maombi wawe walewale waliolengwa.
Yule aliyeshinda Tenda mwaka jana, safari hii akasajili kampuni sit ana zote zikaomba, hivyo mtu mwingine akiangalia kwenye mfumo anaona maombi yapo na watu wameomba lakini kiuhalisia kuna mambo yanayoendelea na mtu wa karibu na watu hao ndio atajua kinachoendelea, mwingine taona kila kitu kipo sawa.
Mkuu wa Wilaya alijulisha juu ya suala hilo lakini naye kapotezea, aliingilia lakini hakuwa na nia ya kuondoa tatizo sugu linaloendelea.
Kwa ufupi ushindani wa Tenda katika Halmashauri ya Arusha DC haipo fair kwa maana hakuna haki.
Wale wenzetu waliojaribu kufikisha taarifa hii TAKUKURU, ikabainika kuwa pale katika ofisi hiyo Afisa anayesimamia ni mmoja wa watu mbao ana ukaribu na timu ile ya Watu wa Halmashauri.
Hivyo, ukifikisha taarifa TAKUKURU Arusha ili wasaidie Taifa lipate malipo stahiki, taarifa zitawafikia wahusika hata kabla ya Ofisi hiyo kufanya maamuzi.