RUSTEM PASHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2016
- 4,707
- 11,365
Hasa kwa vijana wanaokaa DSM ambapo biashara ya nyama(bucha) haifungamani na utumbo.
Kwa wale wenye mitaji midogo pungufu ya laki 6 ningeomba kidogo wajaribu kufanya uchunguzi wa biashara ya utumbo.
Ukiwa na shillingi laki 6, nenda katengeneze kabati lakio laki 2, Muzani laki moja na nusu, eneo lakuuzia elfu 10 kwa mwezi, nenda kanunue utumbo. Bei ya utumbo kwa kg 1 wanauza elfu moja miatano machinjioni, wewe ukishauchukua uza elfu tatu kwa kg 1 ingawa sehemu zingine wanauza elfu 4 kwa kg 1, mwanzoni patakuwa na changamoto lakini wakishazoea utapiga pesa kiasi.
Ukiuza kwa siku kg 20 utakuwa na faida ya elfu 30 au elfu 25 kwahiyo hapo utakuwa umejiongezea kipato kwa kiasi Fulani.Kuhusu pakuuweka ukibaki ongea na mwenye bucha atakuhifadhia kama ukibaki.
Mimi binafsi nilimpa kazi hii kijana na kwa wiki ananipa elfu 50 ,kwa mwezi laki 2.Hiki kibiashara kufikia sasa kinanilipia kodi ya chumba,umeme,maji kwa mwezi halafu mie nahangaika na mambo mengine.
Leo nimefungua banda la 2 la utumbo nimemuweka pia kijana mwingine, nimeona changamoto nindogo sana kulingana na biashara nyingine ndogondogo zakuwapa vijana wasimamie.
Changamoto hapa nikuamka mapema saa kumi na kuufata machinjioni, ingawa ukimpa kijana ataufata yeye mwenyewe.
Pia ukiweza uza na supu ya utumbo(hii mada ya siku nyingine).
Asenteni.
Kwa wale wenye mitaji midogo pungufu ya laki 6 ningeomba kidogo wajaribu kufanya uchunguzi wa biashara ya utumbo.
Ukiwa na shillingi laki 6, nenda katengeneze kabati lakio laki 2, Muzani laki moja na nusu, eneo lakuuzia elfu 10 kwa mwezi, nenda kanunue utumbo. Bei ya utumbo kwa kg 1 wanauza elfu moja miatano machinjioni, wewe ukishauchukua uza elfu tatu kwa kg 1 ingawa sehemu zingine wanauza elfu 4 kwa kg 1, mwanzoni patakuwa na changamoto lakini wakishazoea utapiga pesa kiasi.
Ukiuza kwa siku kg 20 utakuwa na faida ya elfu 30 au elfu 25 kwahiyo hapo utakuwa umejiongezea kipato kwa kiasi Fulani.Kuhusu pakuuweka ukibaki ongea na mwenye bucha atakuhifadhia kama ukibaki.
Mimi binafsi nilimpa kazi hii kijana na kwa wiki ananipa elfu 50 ,kwa mwezi laki 2.Hiki kibiashara kufikia sasa kinanilipia kodi ya chumba,umeme,maji kwa mwezi halafu mie nahangaika na mambo mengine.
Leo nimefungua banda la 2 la utumbo nimemuweka pia kijana mwingine, nimeona changamoto nindogo sana kulingana na biashara nyingine ndogondogo zakuwapa vijana wasimamie.
Changamoto hapa nikuamka mapema saa kumi na kuufata machinjioni, ingawa ukimpa kijana ataufata yeye mwenyewe.
Pia ukiweza uza na supu ya utumbo(hii mada ya siku nyingine).
Asenteni.