Utumishi mlikuwa na lengo gani kwa watahiniwa?

Utumishi mlikuwa na lengo gani kwa watahiniwa?

TRA sikuhizi basic salary 900k ndo watu wanakimbilia hiyo? TRA ilikuwa zamani before salary review ya Magufuli
 
Mimi ni mhanga,umeongea ya ukweli Kabisa yani..
Ile asubuhi tuu kupata venue nimetumia 20k Kwa ajili ya boda tuu yani.
Dodoma was not ready for us.
Hili nililiona aisee, watu hawajui ramani ya majengo ilivyo. Wakiona majengo mlimani tu wanaenda kuulizia kama ndio hapo.

Madereva boda boda wanaowapeleka hawajui Vitivo (Faculties) zilivyo, wao wanajua majina ya vijiji tu. Na watahiniwa wao kwa wao labda ubahatike kumpata aliesoma hapo Udom ndo atajua hall lilipo.

Kweli niliwaonea huruma sana walivyotaabika. Nkawaza hiyo pepa watapigaje katika mazingira hayo
 
Sekretarieti ina viongozi vilaza sijui kwanini bado wapo kazini....wazo la kuhamia Dodoma lilikuwa la kijuha sana
Labda wamefuata wazo la wakubwa wao (Serikali), lakini haikua lazima kuanzia Dodoma katika hatua hizi za awali. Wangewaita hata kwenye hatua za mbele wakiwa wachache.

Data za waliowaita wanazo, kila mtu kajaza address yake kwenye account yake ya portal. Wamewasababishia watu usumbufu na mateso bila sababu.
 
CCM ndio iliyoharibu akili za Viongozi na wananchi.
Hata leo umfufue Magufuli umwambie aeleze faida 3 au sababu 3 tu za maana za kuhamia Dodoma hawezi kukuelezea.
 
Hmn bas watu hawakutafuta guest Sana mm nililal mitaa ya nyerere square nilikuta vyumba na vinginevyo vilikuwa havina watu. All in all watu walizid Sana kwasababu watu wanatamani Sana kufanya Kaz TrA
Poleni kwa usumbufu jman, Ila kwa mawazo yangu mimi kufanya mtihani dar bora Dodoma kwa sababu Dodoma ni katikati, hata kama unatoka mkoa gani ulazima wa kufika siku hiyo upo hata kwa kuchelewa, tofauti na dar ambapo mikoa mwingine inatumika siku mbili.
Na kuhusu Suala la kutafuta venue, ni koss la msailiwa kwa sababu unapojiandaa kwa interview yoyote inabidi ufahamu sehemu ya kufanyia mtihani kabla ya siku yenyewe.
All in all tunawaombea matokeo mema
 
NMB 2018/2020 walitangaza nafasi za kazi za bank officers several position na walitumia taratibu nzuri tu za kuhakikisha kila candidate ana fanya test online kupitia email address yake ana tumiwa link ya maswali pamoja na muda wa kufanya hayo maswali mf. test maswali 30 muda wa test n 45 minutes nili upenda huo utaratibu japo wenyewe wali zingua maana kila mtu alitumiwa link siku tofaut tofaut na maswali n hayo hayo ambapo ilipelekea watu kuya jua maswali na kuweza kutafuta majibu mapema

SASA
hawa Ajira portal wao kwanini wasiweke taratibu kama hizi kwamba watu wataarifiwe kuhusu tarehe na muda wa kufanya hizi test kupitia acc zao na mtihani ufanyike kwa wote kwa wakat mmoja kisha ule muda wa dirisha la lile jaribio likiisha basi lifungwe ili masahihisho yafanyike kisha wahusika watakao weza kupita hatua ile wachujwe wachache ambao ndio wata enda kuendelea na hatua ya oral uko Dodoma.

mfano
tazama hapa kweny hii attachment
kwann sisi taasisi yetu hii inashindwa kufanya taratibu kama hizi tena ukizingatia mikusanyiko hai takiwi kwa sasa
Screenshot_20210810-111939_Gmail.jpg
 
Hiyo mitihani nani ana muda wa kusahihisha? Ni kutesa tu vijana wa watu.
 
Mwana ulivotiririka utadhan love story hahaha
Love story tena kaka, nilikua nina issues nyingi za kuandika about that event. Sikua msahiliwa lakini that day nilipata muda mrefu Sana wa ku study Yale matukio.

Wapo waliokataliwa kufanya paper kwa sababu mbalimbali Sasa wakawa wanakaa tu nje. Wapo pia labda paper ya asubuhi hawapigi lakini ya mchana wamo so nkawa napiga nao story wore hao. So pengine nami nlionekana tu kama wale.

Cha ajabu kingine katika nliowabeba lift kuna mmoja alisema paper ya asubuhi alikataliwa sababu alikua copy ya birth certificate, lakini paper ya mchana hakuonyesha Kabisa hata hiyo copy na akapita fresh tu. Sababu tu ni wasimamiz tofauti kila mmoja ana utaratibu wake labda.
 
Poleni kwa usumbufu jman, Ila kwa mawazo yangu mimi kufanya mtihani dar bora Dodoma kwa sababu Dodoma ni katikati, hata kama unatoka mkoa gani ulazima wa kufika siku hiyo upo hata kwa kuchelewa, tofauti na dar ambapo mikoa mwingine inatumika siku mbili.
Na kuhusu Suala la kutafuta venue, ni koss la msailiwa kwa sababu unapojiandaa kwa interview yoyote inabidi ufahamu sehemu ya kufanyia mtihani kabla ya siku yenyewe.
All in all tunawaombea matokeo mema

Dar ni mbali kidogo lkn watu wengi wana ndg na jamaa Dar kuliko huko Dom hivyo hata gharama za kulala lodge zinakua hazipo tofauti kabisa na Dom na pia Dar imaweza ku accommodate hao maelfu ya watu at a go.Dodoma ni utopolo.

Unaongea kirahisi tu,mtu ametoka huko mkoani ameingia jioni,atoke hapo lodge akodi boda kutafuta huo ukumbi arudi nayo tena na hio boda mpk lodge hizo gharama unajua ni sh. Ngapi na kesho asubuhi apande tena bodaboda kwenda na kurudi tena?
 
Dar ni mbali kidogo lkn watu wengi wana ndg na jamaa Dar kuliko huko Dom hivyo hata gharama za kulala lodge zinakua hazipo tofauti kabisa na Dom na pia Dar imaweza ku accommodate hao maelfu ya watu at a go.Dodoma ni utopolo.

Unaongea kirahisi tu,mtu ametoka huko mkoani ameingia jioni,atoke hapo lodge akodi boda kutafuta huo ukumbi arudi nayo tena na hio boda mpk lodge hizo gharama unajua ni sh. Ngapi na kesho asubuhi apande tena bodaboda kwenda na kurudi tena?
Brother kwa aliekuwepo pale Mazingira yalikua ni magumu ajabu. Ni kama kupeana adhabu fulan au kukomoana hivi. Mimi nilishiriki lile zoezi ingawa sikua msahiliwa nimeona.

Huyu jamaa haelewi, rahisi Sana kuandika kwenye simu au keyboard. Hivi mtu umeingia usiku hujui hata utalala wapi unaanzaje kwenda Campus kuanza kuzunguka kutafuta kumbi? Sio mechi ya mpira hii useme timu inakagua Uwanja kabla.
 
2016.Nilishasafir kwakuunga unga ivo nikafika dar asubuh kutoka Arusha nafika kimara ikabidi nishike boda Hadi kingamboni interview ilikua pale chuo Cha Mwl Nyerere.napanda Panton nafika nakutana na watu washapiga pepa na stl ndo inaondoka na wasimamizi
 
kwani pepa zinalipiwa?
Bila shaka hujasoma mtiririko wa comments.

Pepa hailipiwi, kutokana na usumbufu ambao watu wanaupata jinsi alivyoelezea mleta mada, tunaona ni bora pepa zifanyike kwenye kanda halafu walipishwe kidogo ili kusaidia maandalizi ya huo mtihani(ukumbi, wasimamizi n.k)

Mfano mtu akiwa Dar akalipia 5,000/= tu akaletewa pepa Dar, ni nafuu kuliko na aende Dodoma ambapo atagharamia usafiri(go and return), malazi, chakula, n.k
 
2016.Nilishasafir kwakuunga unga ivo nikafika dar asubuh kutoka Arusha nafika kimara ikabidi nishike boda Hadi kingamboni interview ilikua pale chuo Cha Mwl Nyerere.napanda Panton nafika nakutana na watu washapiga pepa na stl ndo inaondoka na wasimamizi
Daahh
 
Bila shaka hujasoma mtiririko wa comments.

Pepa hailipiwi, kutokana na usumbufu ambao watu wanaupata jinsi alivyoelezea mleta mada, tunaona ni bora pepa zifanyike kwenye kanda halafu walipishwe kidogo ili kusaidia maandalizi ya huo mtihani(ukumbi, wasimamizi n.k)

Mfano mtu akiwa Dar akalipia 5,000/= tu akaletewa pepa Dar, ni nafuu kuliko na aende Dodoma ambapo atagharamia usafiri(go and return), malazi, chakula, n.k
Sahihi kabisa,

Ufuate pepa ya bure Dodoma lakini ugharamikie Guest House/Lodge siku 2 x 20,000 = 40,000/-.
Nauli Go & Return 22,000 x 2 = 44,000/-,
Kula njiani wakati wa Safari 10,000/-
Bodaboda za kutafuta ukumbi TZS 5,000/-

Au uletewe pepa Mkoa ulipo kwa gharama ya 5,000/- na nauli yako ya kwenda chumba Cha mtihani kipi bora?

Tena hapa Gharama nimeweka zile minimum kabisa
 
Wakuu Kwema?

Mimi kwa Sasa niko Dodoma kikazi, mnamo ijumaa Usiku alinipigia Jamaa yangu mmoja akaniambia mdogo wake kaja Dodoma kufanya Interview lakini kakosa pa kulala, hivyo anaomba nimu accommodate sababu kashatafuta chumba kakosa. Kwakua alienipigia ni Mshikaji wangu sana nkaona isiwe tabu, dogo atapata pa kulala na sehemu za Monde, Nyama Choma, na hata mambo mengine yale akitaka namuonyesha tu.

Dogo akafika saa nane usiku kachoka hoi anadai kadandia lift kaunga gari mbili mpaka pale. Akadai mtiti wa watu aliouacha Mbezi Stand ulikua sio wa kawaida, abiria wanapanda Saratoga wanalipishwa nauli mpaka 35,000/- wakati ki uhalali ni 20,000/- tu. Wengine barabaran wanasubiri Gari za lift.

Dogo akazidi kudai ashazunguka sana vyumba hakuna, eti kuna mpaka wadada waliokua wakilala kwenye vyumba vya wanaume ambao hawakua wao.

Yaan mtu anasikia mdada anaulizia mapokezi kuhusu chumba anatoka anamwambia mdada waunganishe tu nguvu hata wanaweza kupiga discussion usiku. Yaliyoendelea kwenye hizo "discussion" za kustukizana mie sikuwepo.

Asubuhi nkasema nimpeleke dogo huko Udom sababu Usafiri ulikua wa tabu Sana na ilikua Saturday sikua na mishe zingine. Njiani karibu na Njia Panda ya Social foleni ilikua ni kubwa ki Dodoma Dodoma, lakini tulifika. Nilichogundua wageni walikua ni wengi kwa kumbi zilizokua zikifanyia mitihani, wengi wao waliishia kulipia bodaboda mara mbili mbili wakati wanatafuta kumbi husika walizopangiwa. Kumbi zilikua hata 20 na zingine ziko umbali hata wa kutumia Gari au bodaboda.

Pale Udom kwa sasa chuo kimefungwa. Hakuna kantini, hakuna duka wala kiosk. Watu wametoka makwao (guest houses/lodges) toka alfajir hawajala wala kunywa chochote. Hata ukisikia kiu unafanya tu kumeza mate. Angalau kuishi kwangu Dom nafaham vijiji vya jirani na chuo hivyo dogo wake mshikaji nikampelekea wanapaita Nong'ona baada ya pepa ya Kwanza. Wengine niliona wakipiga mihayo tu, kadhaa nkatoka nao wengine wachache nkafanya kuwaambia tu.

Nje ya vyumba vya mitihani tahadhari ya Corona haikuwepo. Distance ya 1meter kati ya mtu na mtu haikuwepo Kabisa. Sio kwenye kusubiri tu, hata mistari ya foleni ya kukaguliwa hakukua na hii tahadhari. Ni kama mkazo uliwekwa kwenye barakoa tu, sio distance maintaining.

Kisha akaingiapepa ya pili, then tukarud town. Usafiri ulikua shida Sana, watu walipanda mpaka Toyo/Guta kurud mjini. Nilichukua kadhaa, wajawazito wawili na mmoja Dogo alisema anamjua wamemaliza nae. Kuhusu ugumu wa mtihani hilo namuachia dogo Mwenyewe ila watu walipata tabu kweli.


Lakina labda tufanye hesabu kidogo, Dogo anasema pepa ya Kwanza aliofanya waliitwa around 9,000 na ya pili hivyo hivyo nazan, tukiweka assumption kwamba wa huku ndio wa kule basi tuseme walikua hao hao 9,000. Na labda 2,000 hawakuja. Kwa ngazi ya Diploma (Wale Assistants) labda nao 3,000 hivi approximately. Hiv kweli Dodoma ina Guest houses za kutosha watu 10,000?? Guest/Lodge moja ikichukua wageni 10 basi zitahitajika guests 1,000 kubeba huu umati, zipo kweli hizi hapa Dodoma?

Dogo alihitajika kurudi jana,gari hakuna zimejaa. Sema kuna mdau mwenzangu hapa Job alikua anaenda Dar na Private nikamuombea lift. Dogo anasema jana njiani alikutana na watu wengi tu wakisimamisha magari kuomba lift. Jamaa aliekua nae alibeba watatu kwa 30,000 each. Mwenzake aliemuona kule Udom ali book na return kumbe.

Naandika huu uzi nikijiuliza swali moja tu, why ilikua lazima kuwajaza watu wote hawa Dodoma? Hakukua na uwezekano wa tume kutumia office zake za zonal? Mbona wakati tume Iko Dar es Salaam wale wa mikoani walishawahi kufanyia mitihani huko waliko? Si ni hata bas mngewaita Dodoma kipindi cha Oral wakiwa wameshachujwa wamebaki wachache? Ni Ubinafsi gani kwa wao kuokoa Gharama huku wakiwatesa watahiniwa kiasi kile?
Sijaelewa kitu apa
 
Back
Top Bottom