KERO Utupaji wa takataka kwenye makazi ya Watu umekithiri kwa kisingizio cha kuziba makorongo hasa maeneo ya Mivumoni na Marobo (Tegeta) pamoja na Kinzudi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257

Maeneo ya Kinzudi
Your browser is not able to display this video.


Your browser is not able to display this video.

Utupaji wa takataka kwenye makazi ya Watu umekithiri kwa kisingizio cha kuziba makorongo ambacho ni kinyume na uhifadhi wa mazingira.

Walianza kwenye viwanja vilivyo mabondeni, makazi ya watu na sasa wanamwaga kwenye mito iliyochimbika baada ya mvua kukatika.

Adha, hii ilianzia Salasala, Kinzudi na sasa wamehamia Mivumoni na Marobo mitaa ya Tegeta kwenye mabonde na mito midogomidogo.

Matokeo yake ni harufu mbaya sana pamoja na Wadudu na kushamiri kwa vimelea vya magonjwa, madhara yake ni mabaya sana kwa sasa na baadae.

Kwa sasa Mivumoni kwenye korongo la kuelekea Marobo hakufai kwa harufu, wadudu pamoja na uharibifu mkubwa sana wa mazingira yanayozunguka makazi ya watu.

Hawa jamaa hawasikii la kuambiwa ikionekana kushirikiana na serikali za mitaa husika hasa ya Mivumoni.

Your browser is not able to display this video.


Maeneo ya Kinzudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…