UVCCM Mwanza" watapeli" mamilioni ya pesa, viongozi wagawana

UVCCM Mwanza" watapeli" mamilioni ya pesa, viongozi wagawana

Nyanswe Nsame

Senior Member
Joined
Jul 9, 2019
Posts
165
Reaction score
181
UVCCM Mwanza" watapeli" mamilioni ya pesa, viongozi wagawana

Katika hali ya kusikitisha Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, wanadaiwa kutapeli zaidi ya milioni 80.

Tuhuma za UVCCM wilaya ya Nyamagana zinawakabili watu wawili ambao ni viongozi, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya, Bonipace Zephania na aliyekuwa Katibu wa UVCCM Nyamagana Maranyingi Matukuta ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM mkoani Dodoma.

Inaelezwa kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na genge lingine la watu zaidi ya watano walitengeneza kikundi hewa na kisha kukiwasilisha halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuchota fedha hizo.

Kwa mjibu wa chanzo cha habari hizi, inaelezwa kuwa, kikundi kilichoundwa cha vijana awali kilikuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wao Kisali Simba lakini baada ya mchakato kukamilika, Mwenyekiti na Katibu walipeleka akaunti ya uvccm Nyamagana na kuwekewa fedha.

Kikundi hicho kilitengenezwa ili kuiaminisha Serikali (Jiji) na namna nzuri fedha hizo zitakavyotumika na kuweka mfumo mzuri wa kukopesheka kutokana na Umoja wa UVCCM kutokuwa na sifa za kupewa mkopo.

Hata hivyo, kikundi hicho kilikidhi vigezo cha kusikitisha hakikupewa fedha licha ya kunaonekana Jiji ndicho kimekopeshwa mamilioni hayo.

Hatua za kukamilika kwa mchakato na mawazo ya namna ya kutengenezwa kikundi hicho, yalifanyika ofisi za kata ya mirongo, chini ya ushauri wa Mtendaji wa kata hiyo.

Fedha zilizochotwa au kuombwa Jiji la Mwanza, lengo lilikuwa ni kwa ajili ya mradi wa kununua bajaji moja kila kata za Jiji la Mwanza.

Hata hivyo, baada ya fedha kupatikana wazo la kununua bajaji kila kata lilikufa na viongozi hao kuanza mchakato upya na kupanga mradi mwingine.

Fedha hizo baada ya kuwekwa katika akaunti ya uvccm wilaya, wapigaji hao wawili walienda kuzitoa katika benki ya NMB tawi la Mwaroni Kirumba.

Baada ya kutolewa kwa fedha hizo, Mwenyekiti na Katibu wake walienda kununua 'hiace used mbili.

Chanzo hiki, kinadai kuwa, hiace mbili zilizonunuliwa, kila moja ilinununuliwa kwa gharama ya shilingi Milioni 35.

Chanzo kinaeleza kuwa milioni 10 iliyobaki waliigawana watu wawili, mgao ambao ulifanyika eneo la mgahawa wa Malikusema mlango mmoja.

Chanzo kingine ambacho kiliomba kutotajwa jina lake kutoka ofisi ya chama cha mapinduzi, kinaeleza hiace hizo ambazo kwa sasa zinafanya kazi ya kubeba wanafunzi shule ya Nyanza English Medium, Hiace moja ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi Milioni 16.

"Brother (kaka) sitaki kuficha kitu na ninachokueleza hapa no ukweli mtu, kama unavyofahamu hivi karibu ulisikia mkuu wa mkoa wa Mwanza anaongelea suala la upigaji wa fedha za makundi maalumu.

"Mkuu alichokuwa anakifanya ni kufunika tu upigaji wa hao vijana wa CCM ambao wao ndio walengwa wakubwa kwa sababu wamekuwa walitengeneza vikundi hewa na kuchota mamilioni ya pesa.

"Tunashangaa mkuu wa mkoa anashindwa kunyooka na kuwataja wakati tayari (Takukuru) Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa, wanaendelea kuwahoji, yeye anashindwa nini kuwa wazi," kilisema chanzo hicho.

Upigaji wa fedha hizo, umewaibua wajumbe na wanachama wa Umoja wa vijana ambao wanalalamikia Umoja wao kutuhumiwa kuchota fedha hizo kitendo ambacho sio cha kweli.

Kwa mjibu wa kikao cha dharura cha uvccm wilaya ya Nyamagana kilichoketi Desemba 24 mwaka 2021 kiliwahoji viongozi hao kuhusu tuhuma hizo.

Baada ya wajumbe hao kuhoji, inadaiwa viongozi hao walidai kuja na majibu sahihi katika vikao vingine vitakavyofatia kwa kuwa hawakuwa na majibu ya maswali waliyotwangwa.

Hata hivyo, mpaka sasa viongozi hao hawajawahi kufanya kikao chochote ili kuwaelezea kuhusu tuhuma hizo na inadaiwa Mwenyekiti amekimbia ofisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti huyo wa UVCCM, Boniphace Zephaniah, alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, alikiri fedha hizo kutolewa na Jiji la Mwanza.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa, fedha hizo ziliingia katika akaunti ya kikundi ambacho hakukitaja jina na kwamba hazikuingia kwenye akaunti ya vijana.

Zephania anadai kuwa, tuhuma hizo zimejaa chuki za kisiasa zaidi wanaodai kupiga fedha hizo ni wale washindani wake aliowashinda kwenye uchaguzi.

"Mtu anayeeneza hizo taarifa anaenda Takukuru na ofisi za Serikali ni mtu mmoja anaitwa Kisali soud Simba ambaye alikuwa mwenyekiti wao zamani na sasae alishaondolewa.

"Taarifa wanazotoa hazina ukweli na ambao wanaongea hivyo vitu hawavijui na hawana uhakika, ila ni kweli hizo hiace zilinunuliwa kila moja shilingi milioni 35 na hizo gari tuliziagiza nje," alisema Zephania.

"Hizo gari zipo pale shule ya msingi nyanza, ni gari mpya na hazina shida yoyote ile na kama zingekuwa na shida Serikali ingekuwa wamezikataa... Mpaka viongozi wa CCM walishaenda wakazikaguwa zipo vizuri," alisema Zephania.

Zephania anakiri kuwa fedha zilizoombwa Jiji zilikuwa ni kwa ajili ya kununua bajaji 10, lakini uongozi wa kikundi hicho ulibadilisha mradi na kununua gari hizo baada ya kuona mradi wa awali haulipi.

IMG-20220426-WA0236.jpg


IMG-20220426-WA0237.jpg


IMG-20220426-WA0234.jpg
 
UVCCM Mwanza" watapeli" mamilioni ya pesa, viongozi wagawana

Katika hali ya kusikitisha Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, wanadaiwa kutapeli zaidi ya milioni 80.

Tuhuma za UVCCM wilaya ya Nyamagana zinawakanili watu wao ambao ni viongozi, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya, Bonipace Zephania na aliyekuwa Katibu wa UVCCM Nyamagana Maranyingi Matukuta ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM mkoani Mbeya.

Inaelezwa kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na genge lingine la watu zaidi ya watano walitengeneza kikundi hewa na kisha kukiwasilisha halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuchota fedha hizo.

Kwa mjibu wa chanzo cha habari hizi, inaelezwa kuwa, kikundi kilichoundwa cha vijana awali kilikuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wao Kisali Simba lakini baada ya mchakato kukamilika, Mwenyekiti na Katibu walipeleka akaunti ya uvccm Nyamagana na kuwekewa fedha.

Kikundi hicho kilitengenezwa ili kuiaminisha Serikali (Jiji) na namna nzuri fedha hizo zitakavyotumika na kuweka mfumo mzuri wa kukopesheka kutokana na Umoja wa UVCCM kutokuwa na sifa za kupewa mkopo.

Hata hivyo, kikundi hicho kilikidhi vigezo cha kusikitisha hakikupewa fedha licha ya kunaonekana Jiji ndicho kimekopeshwa mamilioni hayo.

Hatua za kukamilika kwa mchakato na mawazo ya namna ya kutengenezwa kikundi hicho, yalifanyika ofisi za kata ya mirongo, chini ya ushauri wa Mtendaji wa kata hiyo.

Fedha zilizochotwa au kuombwa Jiji la Mwanza, lengo lilikuwa ni kwa ajili ya mradi wa kununua bajaji moja kila kata za Jiji la Mwanza.

Hata hivyo, baada ya fedha kupatikana wazo la kununua bajaji kila kata lilikufa na viongozi hao kuanza mchakato upya na kupanga mradi mwingine.

Fedha hizo baada ya kuwekwa katika akaunti ya uvccm wilaya, wapigaji hao wawili walienda kuzitoa katika benki ya NMB tawi la Mwaroni Kirumba.

Baada ya kutolewa kwa fedha hizo, Mwenyekiti na Katibu wake walienda kununua 'hiace used mbili.

Chanzo hiki, kinadai kuwa, hiace mbili zilizonunuliwa, kila moja ilinununuliwa kwa gharama ya shilingi Milioni 35.

Chanzo kinaeleza kuwa milioni 10 iliyobaki waliigawana watu wawili, mgao ambao ulifanyika eneo la mgahawa wa Malikusema mlango mmoja.

Chanzo kingine ambacho kiliomba kutotajwa jina lake kutoka ofisi ya chama cha mapinduzi, kinaeleza hiace hizo ambazo kwa sasa zinafanya kazi ya kubeba wanafunzi shule ya Nyanza English Medium, Hiace moja ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi Milioni 16.

"Brother (kaka) sitaki kuficha kitu na ninachokueleza hapa no ukweli mtu, kama unavyofahamu hivi karibu ulisikia mkuu wa mkoa wa Mwanza anaongelea suala la upigaji wa fedha za makundi maalumu.

"Mkuu alichokuwa anakifanya ni kufunika tu upigaji wa hao vijana wa CCM ambao wao ndio walengwa wakubwa kwa sababu wamekuwa walitengeneza vikundi hewa na kuchota mamilioni ya pesa.

"Tunashangaa mkuu wa mkoa anashindwa kunyooka na kuwataja wakati tayari (Takukuru) Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa, wanaendelea kuwahoji, yeye anashindwa nini kuwa wazi," kilisema chanzo hicho.

Upigaji wa fedha hizo, umewaibua wajumbe na wanachama wa Umoja wa vijana ambao wanalalamikia Umoja wao kutuhumiwa kuchota fedha hizo kitendo ambacho sio cha kweli.

Kwa mjibu wa kikao cha dharura cha uvccm wilaya ya Nyamagana kilichoketi Desemba 24 mwaka 2020 kiliwahoji viongozi hao kuhusu tuhuma hizo.

Baada ya wajumbe hao kuhoji, inadaiwa viongozi hao walidai kuja na majibu sahihi katika vikao vingine vitakavyofatia kwa kuwa hawakuwa na majibu ya maswali waliyotwangwa.

Hata hivyo, mpaka sasa viongozi hao hawajawahi kufanya kikao chochote ili kuwaelezea kuhusu tuhuma hizo na inadaiwa Mwenyekiti amekimbia ofisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti huyo wa UVCCM, Boniphace Zephaniah, alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, alikiri fedha hizo kutolewa na Jiji la Mwanza.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa, fedha hizo ziliingia katika akaunti ya kikundi ambacho hakukitaja jina na kwamba hazikuingia kwenye akaunti ya vijana.

Zephania anadai kuwa, tuhuma hizo zimejaa chuki za kisiasa zaidi wanaodai kupiga fedha hizo ni wale washindani wake aliowashinda kwenye uchaguzi.

"Mtu anayeeneza hizo taarifa anaenda Takukuru na ofisi za Serikali ni mtu mmoja anaitwa Kisali soud Simba ambaye alikuwa mwenyekiti wao zamani na sasae alishaondolewa.

"Taarifa wanazotoa hazina ukweli na ambao wanaongea hivyo vitu hawavijui na hawana uhakika, ila ni kweli hizo hiace zilinunuliwa kila moja shilingi milioni 35 na hizo gari tuliziagiza nje," alisema Zephania.

"Hizo gari zipo pale shule ya msingi nyanza, ni gari mpya na hazina shida yoyote ile na kama zingekuwa na shida Serikali ingekuwa wamezikataa... Mpaka viongozi wa CCM walishaenda wakazikaguwa zipo vizuri," alisema Zephania.

Zephania anakiri kuwa fedha zilizoombwa Jiji zilikuwa ni kwa ajili ya kununua bajaji 10, lakini uongozi wa kikundi hicho ulibadilisha mradi na kununua gari hizo baada ya kuona mradi wa awali haulipi.

View attachment 2207021

View attachment 2207023

View attachment 2207024
Duh
 
"Tunashangaa mkuu wa mkoa anashindwa kunyooka na kuwataja wakati tayari (Takukuru) Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa, wanaendelea kuwahoji, yeye anashindwa nini kuwa wazi," kilisema chanzo hicho.
Mkuu Nyanswe Nsame , kwanza asante sana kwa taarifa hii. Pili jambo likiisha kabidhiwa kwa Takukuru, halizungumzwi zungumzwi hadi uchunguzi ukamilike, kama kuna uhalifu then kesi itapelekwa mahakamani.

Ila Duh...!. CCM kwa fitna na majungu, usipime!. Kwa mujibu wa maelezo hayo hiyo milioni 80, kwanza haitoshi kununua Bajaji 10!. Kila bajaj ingeingiza TZS 5,000 Kwa siku. Hivyo Bajaji 10, zingeingiza 50,000 kwa siku, hivyo kuulipa mkopo wa milioni 80, ingechukua miaka 4!. Life span ya bajaj ni just 2 years, hivyo Bajaji zingekufa kabla ya kulipa mkopo. Hivyo ulikuwa ni aumuzi sahihi kuachana na biashara kichaa ya bajaj.

Hiace moja ni 50,000 Kwa siku, hivyo hiace 2 ni TZS. 100,000
Life span ya haice ni miaka 5, deni linalipika ndani ya miaka 2, hivyo miaka 3 ni kizalisha faida.

Tupunguzeni fitna na majungu!
P
 
Unashangaa ili kwenye kundi lako, vijana kuleni hela ili mpate mataji wa kupata madaraka.

Fedha Za ESCROW kundi la wajanja lilidai sio za Umma ili hali fedha hizo zilikua zinahifadhiwa BOT.

Mjadala kama huo umeanza kujitokeza tena kwenye ROYAL TOUR wapo wanaodai ni za umma huku wahusika wakidai sio za umma bali michango binafsi.
 
walivo shiba utazani viboko vya msumbiji. watakula wapi wakati wakubwa wao ni wezi wa kiwango cha kunya tembo
Ndio maana kutwa uvccm wanatukana wapinzani mitandaoni...kazi kubwa wanayoweza ni uchawa ili waendelee kula vya uvunguni.
 
Vikundi vya halali hawapewi hata ukimbie uchi ...hupewi urasimu mwingi sanaaaa
 
Hivi wewe Paskali Mayalla watu wanavyokushangaaga mara unataka ubunge,mara unavizia uteuzi naona wanakupenda sana ndio maana wanakutaka ukae pembeni na kadhia za majizi haya ndani ya chama chenu,hebu fikiria huyo katibu uvccm mpaka leo yupo ndani ya ccm na anapeta tu Sasa kapelekwa mbeya ,hao ndio yule katibu wenu taifa uvccm Kihongosi ameona mbeya watalindwa na spika,Paskali Mayalla usijichafue kulipenda lichama la MAJANGILI jina lako na ukoo wako ni wasafi nadhani baba yako alikuwa afisa usalama taifa enzii za kina Mzena, sio enzi hizi Lumumba buku saba unaingia idarani,haujafika kiwango Cha kuweka njaa yako kwenye mfuko wa rambo,hiyo kazi ungewaachia wahenga kama kina Wilbroad Slaa,huyu wilbroad Slaa ni mhenga ambaye hata wajukuu ,mabinti zake wakisikia MSIMU huu wa siku kuu amepotea Wala hawahangaiki kumtafuta,maana wanajua atakuwa ametekwa na mashangingi mabobezi kama kina Mshumbusi,maana mhenga huyu baada ya kuwa balizi mstaafu wa lumumba,shangingi wabobezi wa kula za wahenga wanamvia apate upenyo hapo lumumba ubalizini( Lumumba ubalizini =korido za Lumumba)
 
Kaka Pascal Mayalla acha kushangaa, hao vijana wa CCM wana maarifa (Rutoism) wanaangalia namna ya kujikwamua kiuchumi na si kama vijana wa vyama vingine ambao wamewekeza kwenye kulalamika tuuuu!

Naona umeona majibu ya Mwenyekiti wa Umoja wa vijana hao Boniphace Zephania ametulia na hakurupuki!

Na ukitaka kujua haraka kama unajua mambo ya fedha kuwa mleta mada hii ni mamluki au ana vinasaba vya vijana wa upinzani ni kwamba iweje fedha ziombwe na kikundi halafu fedha ziwekwe kwenye akaunti ya Umoja wa Vijana wa CCM ?
Kuna maelezo yanapungua hapo!

Maisha lazima yaendelee!
 
UVCCM Mwanza" watapeli" mamilioni ya pesa, viongozi wagawana

Katika hali ya kusikitisha Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, wanadaiwa kutapeli zaidi ya milioni 80.

Tuhuma za UVCCM wilaya ya Nyamagana zinawakanili watu wao ambao ni viongozi, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya, Bonipace Zephania na aliyekuwa Katibu wa UVCCM Nyamagana Maranyingi Matukuta ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM mkoani Mbeya.

Inaelezwa kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na genge lingine la watu zaidi ya watano walitengeneza kikundi hewa na kisha kukiwasilisha halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuchota fedha hizo.

Kwa mjibu wa chanzo cha habari hizi, inaelezwa kuwa, kikundi kilichoundwa cha vijana awali kilikuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wao Kisali Simba lakini baada ya mchakato kukamilika, Mwenyekiti na Katibu walipeleka akaunti ya uvccm Nyamagana na kuwekewa fedha.

Kikundi hicho kilitengenezwa ili kuiaminisha Serikali (Jiji) na namna nzuri fedha hizo zitakavyotumika na kuweka mfumo mzuri wa kukopesheka kutokana na Umoja wa UVCCM kutokuwa na sifa za kupewa mkopo.

Hata hivyo, kikundi hicho kilikidhi vigezo cha kusikitisha hakikupewa fedha licha ya kunaonekana Jiji ndicho kimekopeshwa mamilioni hayo.

Hatua za kukamilika kwa mchakato na mawazo ya namna ya kutengenezwa kikundi hicho, yalifanyika ofisi za kata ya mirongo, chini ya ushauri wa Mtendaji wa kata hiyo.

Fedha zilizochotwa au kuombwa Jiji la Mwanza, lengo lilikuwa ni kwa ajili ya mradi wa kununua bajaji moja kila kata za Jiji la Mwanza.

Hata hivyo, baada ya fedha kupatikana wazo la kununua bajaji kila kata lilikufa na viongozi hao kuanza mchakato upya na kupanga mradi mwingine.

Fedha hizo baada ya kuwekwa katika akaunti ya uvccm wilaya, wapigaji hao wawili walienda kuzitoa katika benki ya NMB tawi la Mwaroni Kirumba.

Baada ya kutolewa kwa fedha hizo, Mwenyekiti na Katibu wake walienda kununua 'hiace used mbili.

Chanzo hiki, kinadai kuwa, hiace mbili zilizonunuliwa, kila moja ilinununuliwa kwa gharama ya shilingi Milioni 35.

Chanzo kinaeleza kuwa milioni 10 iliyobaki waliigawana watu wawili, mgao ambao ulifanyika eneo la mgahawa wa Malikusema mlango mmoja.

Chanzo kingine ambacho kiliomba kutotajwa jina lake kutoka ofisi ya chama cha mapinduzi, kinaeleza hiace hizo ambazo kwa sasa zinafanya kazi ya kubeba wanafunzi shule ya Nyanza English Medium, Hiace moja ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi Milioni 16.

"Brother (kaka) sitaki kuficha kitu na ninachokueleza hapa no ukweli mtu, kama unavyofahamu hivi karibu ulisikia mkuu wa mkoa wa Mwanza anaongelea suala la upigaji wa fedha za makundi maalumu.

"Mkuu alichokuwa anakifanya ni kufunika tu upigaji wa hao vijana wa CCM ambao wao ndio walengwa wakubwa kwa sababu wamekuwa walitengeneza vikundi hewa na kuchota mamilioni ya pesa.

"Tunashangaa mkuu wa mkoa anashindwa kunyooka na kuwataja wakati tayari (Takukuru) Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa, wanaendelea kuwahoji, yeye anashindwa nini kuwa wazi," kilisema chanzo hicho.

Upigaji wa fedha hizo, umewaibua wajumbe na wanachama wa Umoja wa vijana ambao wanalalamikia Umoja wao kutuhumiwa kuchota fedha hizo kitendo ambacho sio cha kweli.

Kwa mjibu wa kikao cha dharura cha uvccm wilaya ya Nyamagana kilichoketi Desemba 24 mwaka 2020 kiliwahoji viongozi hao kuhusu tuhuma hizo.

Baada ya wajumbe hao kuhoji, inadaiwa viongozi hao walidai kuja na majibu sahihi katika vikao vingine vitakavyofatia kwa kuwa hawakuwa na majibu ya maswali waliyotwangwa.

Hata hivyo, mpaka sasa viongozi hao hawajawahi kufanya kikao chochote ili kuwaelezea kuhusu tuhuma hizo na inadaiwa Mwenyekiti amekimbia ofisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti huyo wa UVCCM, Boniphace Zephaniah, alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, alikiri fedha hizo kutolewa na Jiji la Mwanza.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa, fedha hizo ziliingia katika akaunti ya kikundi ambacho hakukitaja jina na kwamba hazikuingia kwenye akaunti ya vijana.

Zephania anadai kuwa, tuhuma hizo zimejaa chuki za kisiasa zaidi wanaodai kupiga fedha hizo ni wale washindani wake aliowashinda kwenye uchaguzi.

"Mtu anayeeneza hizo taarifa anaenda Takukuru na ofisi za Serikali ni mtu mmoja anaitwa Kisali soud Simba ambaye alikuwa mwenyekiti wao zamani na sasae alishaondolewa.

"Taarifa wanazotoa hazina ukweli na ambao wanaongea hivyo vitu hawavijui na hawana uhakika, ila ni kweli hizo hiace zilinunuliwa kila moja shilingi milioni 35 na hizo gari tuliziagiza nje," alisema Zephania.

"Hizo gari zipo pale shule ya msingi nyanza, ni gari mpya na hazina shida yoyote ile na kama zingekuwa na shida Serikali ingekuwa wamezikataa... Mpaka viongozi wa CCM walishaenda wakazikaguwa zipo vizuri," alisema Zephania.

Zephania anakiri kuwa fedha zilizoombwa Jiji zilikuwa ni kwa ajili ya kununua bajaji 10, lakini uongozi wa kikundi hicho ulibadilisha mradi na kununua gari hizo baada ya kuona mradi wa awali haulipi.

View attachment 2207021

View attachment 2207023

View attachment 2207024
🤣🤣🤣majizi
 
Back
Top Bottom