Uvumi unaendelea kuhusu unga kutiwa vitu vya kupunguza nguvu za kiume na kuchochea ushoga

Uvumi unaendelea kuhusu unga kutiwa vitu vya kupunguza nguvu za kiume na kuchochea ushoga

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,311
Reaction score
15,640
Kuna uzushi umeenea sana kwenye magroup ya WhatsApp kuhusu unga wa mahindi kama inavyoonekana kwenye picha.

Mwanzoni nilipuuzia ila kila group naikuta. Kimsingi wabongo elimu ya fortification (uongezaji virutubishi kwenye unga kwa ajili ya kupunguza utapiamlo na udumavu bado hawajaielewa.

Kuna kazi kubwa inahitajika kwenye elimu maana inaonekana hata mamlaka zetu hazitilii maanani.

Kiufupi unga wote wa ngano tunaokula kwenye maandazi, chapati, mikate etc umeongezwa virutubishi kisheria tangu mwaka 2011, ila sababu kwenye unga wa mahindi haikutiliwa mkazo basi sasahivi inaonekana ni kitu kipya.

Na ni virutubishi vilevile kama kwenye unga wa ngano (Iron, Zinc, Folic Acid, Vitamin B12).

Nawasilisha.

IMG-20240402-WA0015.jpg


===

UFAFANUZI WA TBS

IMG_20240407_080529_828.jpg

Hivi karibuni, kumekuwepo na taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayoeleza kuhusu kiwanda cha "Mr and Mrs Jonsson-Johnsson Varmland Hagfors kuzalisha unga wa mahindi (sembe) ujulikanao kwa jina la "Jonsson Lishe- Sembe Mswed" unaosemekana "kuwekwa madawa ya kuua nguvu za kiume na kuongezea hormones za ushoga".

TBS inapenda kuujulisha umma kuwa mzalishaji huyo anamiliki kiwanda cha kuzalisha unga wa mahindi ulioongezewa virutubisho (fortified maize flour) kilichoko mkoa wa Tanga, wilayani Lushoto ambacho mifumo yake ya uzalishaji pamoja na ubora wa bidhaa hiyo vimethibitishwa na TBS na kupewa Leseni ya kutumia alama ya Ubora yenye namba 5657. Hata hivyo, kiwanda hiki kilisimamisha uzalishaji toka mwezi Januari 2024 kutokana na kukosa malighafi.

Aidha, baada ya uchunguzi TBS imebaini kuwa mzalishaji huyo amefungua kiwanda kingine nyumbani kwake katika mkoa wa Pwani wilayani Bagamoyo kinachozalisha unga wa mahindi ulioongezewa virutubisho (fortified maize flour), ambacho kilifanyiwa ukaguzi na kugundulika hakijathibitishwa na TBS. TBS ilichukua sampuli ya unga wa mahindi unaozalishwa na kiwanda cha Bagamoyo na kuifanyia uchunguzi wa kimaabara na kuthibitisha kuwa imeongezewa virutubisho kwa mujibu wa Kiwango cha bidhaa hiyo. Utaratibu wa kuongeza virutubisho vya vitamini na madini kwenye unga wa mahindi unakubalika kwa mujibu wa Kiwango cha Kitaifa na hufanyika kwa lengo la kuboresha hali ya lishe kwa walaji.

Hata hivyo, TBS imechukua hatua za kusimamisha uzalishaji na usambazaji wa bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha Bagamoyo hadi hapo mhusika atakapokamilisha taratibu za kupata leseni ya kutumia. alama ya ubora.

TBS kupitia mifumo yake ya kiudhibiti itaendelea kuhakikisha kuwa bidhaa hiyo pamoja na bidhaa nyingine za chakula zinaendelea kukidhi matakwa ya viwango ili kulinda afya ya watumiaji.
 
Hali ya ujinga nchi hii bado ni 90% WaTz ni watu wa mihemko sana na hawako tayari kujifunza pale wanapoona kitu hawakielewi, binafsi huwa nakaa kwenye page za habari za mitandao ya nje, mfano TSR ambayo ni udaku tu, lakini ikiwekwa mada hapo hiyo argument itakayoibuka hapo, watu wadogo kabisa kiumri wanavyojenga hoja!

Kuhusu huo unga, ni ujinga wa waTz baadhi au lah ni vita ya kibiashara.
 
Hali ya ujinga nchi hii bado ni 90% WaTz ni watu wa mihemko sana na hawako tayari kujifunza pale wanapoona kitu hawakielewi, binafsi huwa nakaa kwenye page za habari za mitandao ya nje, mfano TSR ambayo ni udaku tu, lakini ikiwekwa mada hapo hiyo argument itakayoibuka hapo, watu wadogo kabisa kiumri wanavyojenga hoja!

Kuhusu huo unga, ni ujinga wa waTz baadhi au lah ni vita ya kibiashara.
Nakumbuka hata juisi za Azam kuna mtu alijiskia tu akazusha eti zinaleta kansa
 
Kuna nini nyuma ya hivi virutubishi?

Mbona wazee wetu wame survive miongo Kwa miongo pasipo hayo mavirutubisho?
Acha kupotosha watu wewe kaa kimya kama hujui... Goitre unadhani iliishaje?
images (51).jpeg
 
Matatu yanayoisumbua nchi hii nayo ni
(a) Ujinga
(b)Maradhi na
(c) Umasikini

Na,bila kufutika Hilo nambamoja tusitarajie lolote chanya kutoka jamini mwetu

Mbumbumbu ,wanawezaje kuingilia mambo ya TFDA
 
434576816_1435017733777934_2946312535536047630_n.jpg

Kuna taarifa huyu mzungu anaeitwa Carl eric jonsson ana miliki kiwanda cha kutengeneza unga nchini Tanzania, ameoa mtanzania.
Huo unga inasemekana wanaweka vitu vinavyo ua nguvu za kiume na kuongeza hormon za kike kwa watoto wa kiume. Lengo lao kuu ni kusambaza na kueneza ushoga Tanzania. Tunaomba Serikali mfuatilie hili kusaidia kizazi chetu na tunaiomba serikali ifuatilie kiwanda hiki. Please okoa kizazi
hiki. chanzo.
View: https://www.facebook.com/100018091626510/posts/1435017770444597/?mibextid=oFDknk&rdid=GWiUeD4jNtS5WqXp
 
Back
Top Bottom