Klabu ya
Simba Sports Club leo Jumapili inajitupa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kuanza harakati za kupambana kimataifa kwa kucheza na klabu ya
Gendarmarie Nationale FC, ya nchini Djibout kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Simba SC, Mnyama wanarejea michuano ya kimataifa huku wakiwa na matokeo mazuri kwenye Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
VPL, hali inayoaminiwa na mashabiki na wanachama wao kuwa huenda furaha ikawa chachu ya wachezaji wao kuendeleza furaha.
Utashuhudia pambano hili Live kupitia Azam Sports 2 kuanzia saa 10: jioni. Kaa nasi kukuletea yatakayojiri, usikose ukaambiwa
Vikosi vya timu zote zimetoshana nguvu kwa upande wa Simba SC;
Aishi Manula, Shomari Kapombe, Asante Kwasi, James Kotei, Yusuf Mlipili, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Said Ndemla, John Bocco, Emmanuel Okwi.
Sub; Emmanuel Mseja, Mzamir Yassin, Mwinyi Kazimoto, Moses Kitundu, Paul Bukaba, Ally Shomari, Juuko Murshid.
Coaches; Pierre Lechantre - Head Coach
Masoud Djuma - Assistant Coach Mohamed Aymen - Fitness Coach Muharam Mohamed - Gk Coach
Timu uwanjani tayari kwa mtanange huu. Na Rais Mstaafu Ndugu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni mgeni rasmi kwenye mchezo huu tayari anakagua timu zote mbili.
Wakati wowote mpira utaanza hapa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Naam mpira umekwisha ananza uwanja wa Taifa
00' Simba SC 0-0 Gendarmarie Nationale FC.