Uwekezaji Simba: Wako wapi wawekezaji wengine wawili waliotajwa kwenye kanuni za Tume ya Ushindani?

Jamaa umeongea kwa uchungu sana ila ndio ukweli huo.giza lipo kubwa tu nikiangalia sioni mstari kutenganisha uwekezaji na udhamini wa Mo maana nanusa mgongano wa kimaslahi na atakayeumia na Simba sio Mo
 
Mtopolo unateseka ukiwa kidimbwi gani wewe?
 
Hiyo sheria imetungwa wakati simba wameanza mchakato wao tayari kihalali....
Hivyo wao haiwahusu.
Jamani muwe mnafuatilia haya mambo kabla ya kuanzisha nyuzi.
Kwani huko Yanga kuna mwenye akili timamu hata mmoja? Yamejaa mapooza tupu
 
Jamaa umeongea kwa uchungu sana ila ndio ukweli huo.giza lipo kubwa tu nikiangalia sioni mstari kutenganisha uwekezaji na udhamini wa Mo maana nanusa mgongano wa kimaslahi na atakayeumia na Simba sio Mo

Hawaoni kwa sababu kasema anawasaidia toka mfukoni. HAWAJIULIZI 20B ZIKIISHA BAADA YA MIAKA MINNE ITABIDI WAENDELEE KUTEGEMEA HISANI YAKE WAKATI WAMESHAUZA NUSU YA TIMU AU WAANZE KUBANA MATUMIZI. MO NAYE ATAANZA KUVUTA 49% YA FAIDA WAKATI ANAZUIA MIKATABA MINGINE NDO KITANUKA. NA ILI KINUKE NI PALE WATANI WAO WATAKAPOTAKEOVER UPANDE WA MATOKEO UWANJANI.
 
Naona kabisa mgogoro badae kati ya familia ya Mo na Simba sports
 
Ha..ha...ha.
Eti B20 zikiisha.
Kwanini usiulize kwanza maana ya Uwekezaji wa Hisa kabla ya kuandika ktk jukwaa?
Ungeuliza ungeambiwa hiyo B20 ni Mtaji na haitumiki kuendeshea ghalama za Timu.
Faida itakayozalishwa na hiyo B20 ndiyo kiasi itaendesha Timu na kiasi itatoa gawio kwa mwenye hisa.
B20 kwa mwaka inaweza kuzalisha hadi B5 ikisimamiwa vizuri kibiashara.

Mfano,
Hiyo B20, inaweza tu kuwekwa ktk Dhamana ya Serikali (Gvt Bond) na ikazalisha pesa nzuri za kuendeshea timu ktk mwaka mwingine.
B20 haiwekwi tu ili ichotwe na kuisha, la isingewekwa, tahmini ya faida ilishafanywa na kujiridhisha kuwa faida itapatikana.
Wataalamu wa mambo ya Bishara na Fedha ndio wataendesha hiyo biashara na huenda sio mwenye hisa.
Hiyo ni biashara kama biashara nyingine.
Mwenye hisa atahakikisha analinda Mtaji wake usitetereke bali uzidi kuimarika kwa kuongezeka.

Maky Yanga, huko YouTube kawabatiza jina lingine baada ya kutoa sare ya moja moja na Big Bullet.
"Utapu tapu"
 
Hata angetaka bure tungempa tu sababu ipo siku timu ikianza kuboronga ataikimbia na hatuwezi kukataa
 
Ungeliuliza kuwa Je, huu mchakato wa uwekezaji ulianzaje? Basi ungepata majibu ya maswali yako.

Hii ni kwasababu asilimia zaidi ya 80+ ya nyinyi Vijana hamujui huu mchakato ulianzaje bali munarukia tu juujuu baada ya kusikia stori za 20B kutoka kwa Utopolo.

Jengine ni kwamba Mzee Said Salim Bakhressa A.K.A BAKHRESSA hajishughulishi na Maswala ya Mpira wala si Mshabiki wa Mpira na wala haimiliki Timu ya AZAM kama Watu wanavyoamini, Anayemiliki Timu ya AZAM ni Mtoto wa BAKHRESSA. Hivyo Sheria za FIFA haziruhusu Mtu mmoja kumiliki Timu 2, hivyo huyu Mtoto wa Bakhressa anayemiliki Azam haruhusiwi kumiliki 49% share za Simba, sasa kutokana na kutokujua sheria hii ya umiliki wa Timu na kutokujua huu Mchakato ulianzaje ndiyo umebeba Mawazo ya Utopolo, Kitenge, Edo na Oscar kusema eti Simba ilimpotezea ama kumkataa Bakhressa! Kwa akili hizi Utakataa na wewe ukiitwa Utopolo?
 
SIFA ZA UTOPOLO:



√ Baada tu ya Mchakato kuanza:

- Walianza kupiga kelele kuwa MO kala hasara kwa kununua 49% kwa 20B kwani hawezi kurudisha hizo hela zake, hivyo hatozitoa hizo 20B kwani Simba haijafikia thamani hiyo.
Hii ni kwasababu Simba ya wakati huo ilikuwa ni ya kawaida sana.



✓ Baada ya MO kuiboresha Simba:
  • Walianza kubadili maneno kwa kusema MO kainunua Simba kwa hela ndogo (20B).
  • MO anaiibia Simba kwa kuingiza Mihela mingi kama faida.
  • MO aweke 20B aache janja janja.



√ Baada ya MO kuweka 20B:
  • MO Kaweka Bango tu hajaweka hela (Wanataka waone mpaka muamala ukifanyika au Wapewe Bank ya Akaunti ya Simba).
  • Sasahivi wanapiga Ramli ya kutokea Mgogoro wa kimaslahi kati ya Simba na MO.



Yaani wana zilezile sifa za Nyani wakiacha Mti mmoja wanarukia Mwengine.
 

Sasa mbona unachanganya Mada, Nani ni Yanga hapa?

Tunajadili hoja ya Hisa unakuja na matokeo ya Malawi. That is failure yetu Watz.

Kama Mo ameteketeza B21 kwa miaka 4. Faida mnaitoa wap?.. usajili mnafanya na pesa gani?.. Pindi matokeo ya Uwanjani yakibadilika Simba kama klabu mnaweza kusaidia timu kupata fedha siku Mudi akigoma kutoa za mfukoni ambazo haziko bound ktk Mkataba?
 

Watu gani wa biashara unaowataja ww?

Sema Kampuni za Mohammed.

Timu imeuzwa mwaka 2021 kwa Valuation ya Mwaka 2016 . Then mnataka tufurahi kabisa yaan
 
Yaani siwez nunua
Hisa kwenye timu mbili za mpira?

Kwani Mbona Mo, Dada yake na Familia Yake ndo kampuni tatu zilizokubalika kununua 49% za Simba lakini HUNDI ni moja ya 20B kutoka kwa mtu mmoja. Imewezekanaje hapo then AZAM washindwe.

Hauoni Mo kawazunguka hapo
 
Ziishe ziende wapi sasa?.. Hivi unajua hata maana ya hisa?.
 
Tume ya Ushindani ilitaka kuwe na wawekezaji watatu kama kanuni zinavyosema. Mbona Mo ametoa 20B yeye mwenyewe kununua hizo 49% zote?
Hili swali ulitakiwa uwaulize Tume ya Ushindani wa Biashara, maana wao ndio wanaoruhusu au kuzuia mchakato kila hatua fulani inapofika. Kwa upande wa Simba, hizo 49% hata zikiwa kutoka kwa wawekezaji kumi au watatu au mmoja, hazitabalisha thamani ya 49%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…