Uwekezaji: Sio Kila Uwekezaji na Kujenga Nchi, Mwingine ni Kuvuna tu, Uwekezaji wa Total Energies kujenga Nchi!

Uwekezaji: Sio Kila Uwekezaji na Kujenga Nchi, Mwingine ni Kuvuna tu, Uwekezaji wa Total Energies kujenga Nchi!

Angalizo zuri sana umelitoa ndg. Paskali kwa Serikali kwa kuzingatia Masilahi ya Tanzania na watanzania.

Ni kweli Serikali ya awamu hii ya 6 imeifungua Tanzania yaani kwa sasa Tanzania imefunguka kabisaaa.

milango na madirisha yote yamefunguka........ .hili ni jambo jema lkn tuchukue tahadhari maana wapo watakao jipenyeza kwa gia ya uwekezaji kumbe ni wanyonyaji.

Uwekezaji unao lengwa na kukusudiwa na Serikali ya Rais Samia ni ule ambao utawainua watanzania kiuchumi na sio kunyonya uchuminwa watanzania.

kwa sasa sioni tatizo kwenye uwekezaji wa uchimbaji wa madini kwasababu Hayati JPM alisha ziba myanya kwa kufanya marekebisho ya Sheria za madini hivyo kama nchi tunanufaika vilivyo.

ila bado ni muhimu sana tukaweka chujio madhubuti na imara ili kuweza kuchuja wawekezaji na wanyonyaji.
Tatizo kila muwekezaji anatafuta faida kubwa ikibidi hata kwa kufanya udanganyifu, hata hiyo kampuni ya Total sio ya kuiamini kwa 100% lazima kuwe na macho makali.
 
Katika uwekezaji cha kuangaliwa kwanza ni ajira. Maendeleo yanakuja pale mwekezaji anapolipa kodi na wafanyakazi wake wanapolipwa mishahara mizuri. Kwa mfano Toyota ikiamua kujenga kiwanda cha magari Marekani, kitu cha kwanza kinachotajwa ni ajira ngapi zitapatikana kwa Wamarekani. Swali la pili ni kodi kiasi gani watalipa. Hawaulizi Toyota itajenga shule ngapi au hospitali ngapi. Hawaulizi Toyota wataleta maendeleo gani maana wanajua watalipa kodi na kodi zitatumika kuleta kujenga shule, hospitali, barabara na maendeleo mengine. Wafanyakazi watalipwa vizuri watatumia mishahara yao kununua nyumba, gari, na vitu vingi kwa hiyo hela itazunguka kwenye uchumi.

Mwekezaji hana wajibu wa kuwaletea maendeleo. Yeye wajibu wake kutafuta faida kubwa (maximize profits) na kama ni kampuni inayouza hisa ni kuwapa faida shareholders wake na kulipa kodi za nchi zao. Vile vile kuwapa ajira watu wa nchi zao. Msitegemee wawekezaji watawajengea nchi, mtasubiri muda mrefu. Nchi mtajenga wenyewe mkitumia mbinu na maarifa na kuacha ufisadi, tamaa, na ubinafsi.
 
Wanabodi,
Jukwaa la Siasa:
Hapa Jukwaa la Siasa JF, mada nyingi ni mada za politiking, yaani kupiga siasa, lakini sii wengi wanajua kuwa hata mambo ya uchumi mkubwa ni siasa!, hapa tunazungumzia political economy, Siasa Uchumi.

Kila nipatapo fursa, huwaletea zile mada zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Leo nazungumzia mada ya uwekezaji, Tanzania tumefungua milango yetu na kuiacha wazi ikiwemo kuweka vivutio mbalimbali vya uwekezaji ili kuvutia uwekezaji katika sekta mbalimbali. Katika uwekezaji huo, kuna uwekezaji na uwekezaji, sio kila uwekezaji ni uwekezaji wa kujenga nchini, kuna uwekezaji mwingine sio uwekezaji wa kujenga nchi ni uwekezaji wa kuvuna nchi, mfano uwekezaji kwenye sekta ya uchimbaji wa madini, gesi, mafuta, au extractive industry, japo huu ni uwekezaji mkubwa, lakini madini yote duniani yanaitwa diminishing resources, ynafika mahali yanakwisha!. Uwekezaji kwenye sekta ya madini, japo ni uwekezaji mkubwa, lakini sio uwekezaji wa kujenga nchi, ni uwekezaji wa kuvuna nchi, mwekezaji anaingiza mtaji ili kupata mavuno, madini yakiisha, gtunaachiwa mashimo and that is it.

Kuhusu hawa TotalEnergies, naomba kuanza kuanza kwa kuweka hizi facts mezani
  1. Japo Tanzania, tangu tupate uhuru, tuna miradi mingi mikubwa ya uwezekazi iliyoanzishwa, na kuna makampuni mengi yamewekeza Tanzania, hakuna uwekezaji wowote mkubwa, zaidi ya uwekezaji wa kampuni ya mafuta ya TotalEnergies, kupitia mradi wake wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani, Tanga nchini Tanzania, huu ndio mradi wenye thamani kubwa kuliko mradi mwingine wowote nchini Tanzania kwa sasa.
  2. Japo kuna makampuni mengi yanayotoa huduma za mafuta, na vituo vingi vya mafuta, kampuni ya mafuta ya TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, ndio kampuni inayoongoza kwa kuwa na vituo vingi vya mafuta, ambapo mpaka sasa, ina vituo zaidi ya 100 vilivyotapakaa nchi nzima, tena vituo vya TotalEnergies, sio viko maeneo ya mijini tuu, viko hadi vijijini, siku moja nilikuwa maeneo ya vijijini huko Marangu, Moshi, nikashangaa kukutana na kituo cha kisasa cha TotalEnergies, pale kijijini Somanga!.
  3. Japo kuna aina mbalimbambali za mafuta ya petroli na dizeli, kuna Super, Regular, Unleaded, etc, mafuta yanayouzwa kwenye vituo vya TotalEnergies, ndio mafuta yanayoongoza kwa ubora, kutokana ma mafuta ya Total, kuongezwa kiambata cha TotalEnergies Excellium ambacho kinafanya mambo makubwa kwenye
Uwekezaji unaofanywa na kampuni ya TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, huu ndio mfano wa uwekezaji mkubwa wa ukweli wenye lengo la kuisaidia nchi, kujenga nchi na sio kuvuna nchi.
Andamana nami katika makala hii.
View attachment 2033252
Sasa kwa vile kuna wawekezaji wa aina mbili, wawekezaji wachumaji na wavunaji wa rasilimali zetu, na wawekezaji wajenga nchi.
Mnaonaje tukiishauri serikali yetu, wawekezaji wajenga nchi kama TotalEnergies, waongezewe some investment incentives, ili Tanzania tuvutie zaidi wawekezaji wajenga nchi na sio wachuma nchi?.
Paskali.
January hajakupigia simu?,basi atakua hajausoma,
Tumalize kimoja kwanza, JNHP au hapo total energy hatuweki hata senti moja ya serikali?
 
Nina mashaka na makala yako....
Siku zote umekua uki ipigia chapuo hii kampuni...

Naona hii mada sio kwa maslai ya taifa, bali maslai ya Pascal....
Anaweza kuwa underground Market Manager wa hii kampuni
 
Kaka Pascal Mayalla uwekezaji ni kitu muhimu sana hasa kama tunataka kupige hatua za haraka, kinachohitajika ni uwazi zaidi kwa serikali na wawekezaji. Lakini mbali na kuwajengea ujuzi watanzania tunahijati kutengeneza mazingira ambayo yatawalazimu hawa wawekezaji kuingia katika ushirikiano (Partnership/Joint Venture) na wazawa.

Mimi kabisa leo kwamba wadau kama vyuo vikuu wanaweza wakatengeneza mashirika yao ambayo yangeweza kufanya mkono kwa mkono na wawekezaji, mbali na kuwapa tu ajira. Kwamba mwekezaji awe anamiliki asilimia 70% huku mashirikia ya vyuo vikuu yawe yanamiliki asilimia 30%. Tutaanza kidogo kidogo, lakini haya mashirika yetu yatakuja kujaa wataalamu na kumiliki mali nyingi sana tu huko mbeleni.

Changamoto kubwa ambayo tunayo Tanzania, ni wale wazee wajamaa wa kipindi cha Nyerere ambao binafsi huwa siwaelewi kwanini wanachukia sana wawekezaji na ukiwaambia tufanye njia gani, wao huishia kusema TUJITEGEMEE lakini hawatupi njia sahihi ya Tanzania kufanya hivyo. Kiufupi wao ndiyo waliifikisha nchi hapa na siasa zao mbovu, na bado wao wanadhani kwamba walihujumiwa na mabeberu, nothing is ever their fault....
 
Total kawasome vizuri hawa jamaa huko west africa na miradi yao kule Chad na Congo brazzavile... Total from france, kaisome kitu inaitwa french Africa na makampuni kama total influence yake....Moja ya project ya french Africa ni Gabon na Burkin faso..

Total amemnunua Anadarko pale Msumbiji, yuko na project kuubwa sana ya LNG....tayari RPF vijana wa PK wako pale...

Mengine magumu bwana Pasco nenda kayachimbe...
Sasa bwana Samurai unashauri sisi tuwakatae hawa wawekezaji kwasababu ya Chad na Congo ???
 
Kaka Pascal Mayalla uwekezaji ni kitu muhimu sana hasa kama tunataka kupige hatua za haraka, kinachohitajika ni uwazi zaidi kwa serikali na wawekezaji. Lakini mbali na kuwajengea ujuzi watanzania tunahijati kutengeneza mazingira ambayo yatawalazimu hawa wawekezaji kuingia katika ushirikiano (Partnership/Joint Venture) na wazawa.

Mimi kabisa leo kwamba wadau kama vyuo vikuu wanaweza wakatengeneza mashirika yao ambayo yangeweza kufanya mkono kwa mkono na wawekezaji, mbali na kuwapa tu ajira. Kwamba mwekezaji awe anamiliki asilimia 70% huku mashirikia ya vyuo vikuu yawe yanamiliki asilimia 30%. Tutaanza kidogo kidogo, lakini haya mashirika yetu yatakuja kujaa wataalamu na kumiliki mali nyingi sana tu huko mbeleni.

Changamoto kubwa ambayo tunayo Tanzania, ni wale wazee wajamaa wa kipindi cha Nyerere ambao binafsi huwa siwaelewi kwanini wanachukia sana wawekezaji na ukiwaambia tufanye njia gani, wao huishia kusema TUJITEGEMEE lakini hawatupi njia sahihi ya Tanzania kufanya hivyo. Kiufupi wao ndiyo waliifikisha nchi hapa na siasa zao mbovu, na bado wao wanadhani kwamba walihujumiwa na mabeberu, nothing is ever their fault....

paragraph ya mwisho: hawa wazee baada ya kuanguka kwa ujamaa walibaki hawana plan B pamoja na mzee mwenzao JKN....wakabaki na siasa zilezile bila kujifunza na kuelewa uelekeo mpya wa dunia, matokeo yake wamebaki na ideology ileile ya kizamani kichwani kama mji uliotekelezwa na kubakia magofu matupu...

Wazee hawa wangenifunza uelekeo mpya wa dunia na kuwekeza kwa kuwapa maarifa vijana na kuandaa succession plan kwa kizazi kipya bila shaka tusingefika huku...lack of plan and jelous wanaona wao ndio pekee wenye akili yakuliokoa hili Taifa ilihali wao ndio waliolizamisha...kifupi wanataka tutumie akili ile ile iliyofeli tujinasue kwenye tope which is very impossible..

Vijana wa sasa wanahitaji kasi ya maendeleo na sio waoga kurisk na kwenda mbele, Vijana hawa wengi huumia sana nchi yao inapoitwa masikini ilihali sio masikini na inaweza kutoka hapa..Mifumo na hawa wazee wasipokuwa makini watalipa deni kubwa ambalo madhara yake ni damu za watu...

Hatujachelewa, zianzishwe forum kila mahala kuanzia vyuoni, mitaani, mitandaoni, hawa wazee na watu wa system watoke huko walikojifungia wakae na hiki kizazi kuona namna bora ya kufanya reform kwenye mifumo na damu mpya yenye kasi, akili na mawazo mapya iweze kuingia kilingeni na kusongesha Taifa mbele, tuachane sasa na hii mifumo ya watoto wastaafu, michepuko, kamlete, UVCCM, watoto wa vigogo, turudishe Taifa kwa watanzania wote ili kila mwenye akili na uwezo atumikie Taifa hili...
 
Hebu nieleweshe sisi hatuna gesi ya kusindikwa kwenye mitungi na kuuzwa badala yake ile gesi yetu ya ntwara ni ya kutoa umeme tu?
Ni kweli kuwa Taifa ges sio ya serikali bali ni Manji na ges ile inatoka nje ya nchi?
Ni kweli kuwa vinatoka halafu ndio hurudi kama ilivyokuwa milingoti ya umeme ya tanesco?
Ni kweli viongozi waliofanya madudu wao na familia zao hawajisikiki vibaya kwa vile hawaandikwi na kusimangwa mabarabarani na magetini na serikali haina mpango wa kuwafirisi walioingia cha kike kwenye mikataba mikubwa kiasi cha Tanzania kupoteza kuwanda cha karatasi Mufindi.
Kufa kwa shirika la bima ambalo magari yoote nchini walikuwa wanatuhudumia.
Kuuwa reli na shirika lake.
Je nnyie wa media mkizileta fulani ni tajiri wa mpaka kufa lakini alifisadi mradi fulani .watu tuwazoomee na kuwananga.
Nafikiri ni njia ya wananchi kupambana na ufisadi.
 
Kama sio umeshakunywa John Walker muda huu ulipoandika hii mada, basi ni dhahiri umeshapoteza uwezo wako wa uandishi. Nimeangalia hiyo mada yako na kujaribu kuona mahusiano ya huo uwekezaji wa bomba la mafuta la Uganda, na ulichoongelea kuhusu uwekezaji wa Total hapa Tanzania kwenye vituo vya mafuta nimekosa uhusiano. Kama ndio umefikia huku kwenye uandishi, nakushauri jikite kwenye siasa za CCM moja kwa moja, maana ujinga wa hivi ndio huwabeba kwa watu wasio na uelewa wowote.
nabodi,
Jukwaa la Siasa:
Hapa Jukwaa la Siasa JF, mada nyingi ni mada za politiking, yaani kupiga siasa, lakini sii wengi wanajua kuwa hata mambo ya uchumi mkubwa ni siasa!, hapa tunazungumzia political economy, Siasa Uchumi.

Kila nipatapo fursa, huwaletea zile mada zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Leo nazungumzia mada ya uwekezaji, Tanzania tumefungua milango yetu na kuiacha wazi ikiwemo kuweka vivutio mbalimbali vya uwekezaji ili kuvutia uwekezaji katika sekta mbalimbali.

Katika uwekezaji huo, kuna uwekezaji na uwekezaji, sio kila uwekezaji ni uwekezaji wa kujenga nchini, kuna uwekezaji mwingine sio uwekezaji wa kujenga nchi ni uwekezaji wa kuvuna nchi, mfano uwekezaji kwenye sekta ya uchimbaji wa madini, gesi, mafuta, au extractive industry, japo huu ni uwekezaji mkubwa, lakini madini yote duniani yanaitwa diminishing resources, ynafika mahali yanakwisha!. Uwekezaji kwenye sekta ya madini, japo ni uwekezaji mkubwa, lakini sio uwekezaji wa kujenga nchi, ni uwekezaji wa kuvuna nchi, mwekezaji anaingiza mtaji ili kupata mavuno, madini yakiisha, gtunaachiwa mashimo and that is it.

Kuhusu hawa TotalEnergies, naomba kuanza kuanza kwa kuweka hizi facts mezani
  1. Japo Tanzania, tangu tupate uhuru, tuna miradi mingi mikubwa ya uwezekazi iliyoanzishwa, na kuna makampuni mengi yamewekeza Tanzania, hakuna uwekezaji wowote mkubwa, zaidi ya uwekezaji wa kampuni ya mafuta ya TotalEnergies, kupitia mradi wake wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani, Tanga nchini Tanzania, huu ndio mradi wenye thamani kubwa kuliko mradi mwingine wowote nchini Tanzania kwa sasa.
  2. Japo kuna makampuni mengi yanayotoa huduma za mafuta, na vituo vingi vya mafuta, kampuni ya mafuta ya TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, ndio kampuni inayoongoza kwa kuwa na vituo vingi vya mafuta, ambapo mpaka sasa, ina vituo zaidi ya 100 vilivyotapakaa nchi nzima, tena vituo vya TotalEnergies, sio viko maeneo ya mijini tuu, viko hadi vijijini, siku moja nilikuwa maeneo ya vijijini huko Marangu, Moshi, nikashangaa kukutana na kituo cha kisasa cha TotalEnergies, pale kijijini Somanga!.
  3. Japo kuna aina mbalimbambali za mafuta ya petroli na dizeli, kuna Super, Regular, Unleaded, etc, mafuta yanayouzwa kwenye vituo vya TotalEnergies, ndio mafuta yanayoongoza kwa ubora, kutokana ma mafuta ya Total, kuongezwa kiambata cha TotalEnergies Excellium ambacho kinafanya mambo makubwa kwenye
Uwekezaji unaofanywa na kampuni ya TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, huu ndio mfano wa uwekezaji mkubwa wa ukweli wenye lengo la kuisaidia nchi, kujenga nchi na sio kuvuna nchi.
Andamana nami katika makala hii.
View attachment 2033252
Sasa kwa vile kuna wawekezaji wa aina mbili, wawekezaji wachumaji na wavunaji wa rasilimali zetu, na wawekezaji wajenga nchi.
Mnaonaje tukiishauri serikali yetu, wawekezaji wajenga nchi kama TotalEnergies, waongezewe some investment incentives, ili Tanzania tuvutie zaidi wawekezaji wajenga nchi na sio wachuma nchi?.
Paskali.
 
Nina mashaka na makala yako.

Siku zote umekua uki ipigia chapuo hii kampuni.

Naona hii mada sio kwa maslai ya taifa, bali maslai ya Pascal.
Kuwa na mashaka si lazima kuambatane na UHALISIA....

Kwanini tuwe na "negativity" katika mada tajwa?!!

Kwanini tutangulize "ARGUMENTUM AD HOMINEM" katika udadavuaji ?!!!
 
Acha ulevi wa kijinga Pasco, kama una matatizo ya kifamilia tafuta namna nzuri ya kuyamaliza. Mada yako umeweka vitu viwili tofauti na kufanya ni kitu kimoja! Kwanza sio kweli kama huo uwekezaji wa Total Tanzania ndio mkubwa kabisa, isitoshe mradi wa Bomba la Mafuta la Uganda sio mradi wa joint venture baina ya Tanzania na Uganda, bali Tanzania tumetoa njia ya kijiografia kupitisha hilo bomba, tukitarajia kupata kodi kwenye mauzo ya hayo mafuta. Na hili litawezekana kama iwapo huo mradi wa Bomba la mafuta utakamilika Kweli, kwani kuna utapeli mwingi kwenye hilo jambo. Inshort kama unaongelea uwekezaji wa Total Tanzania, tenganisha na huo wa bomba la mafuta la Uganda.
u General Mangi , tujifunze kusoma mada kwa kuangalia contents na sio mtoa mada.

Understanding ya Watanzania wengi kwenye mambo ya serious investments ni mdogo sana, hivyo sishangai mtu badala ya kujadili mada iliyopo mezani, wewe unamjadili mtoa mada. Tujadili mada iliyopo mezani.
P
 
Naona unamuomba nyoka miguu, yeye mwenyewe kapoteza.
Paskali tusaidie ajira wadogo zako. Wewe upo kwenye channel ya hela saizi maana unawajua wakuu huko, siunajua safari hii kama hakuna wa kukushika mkono hutoboi.
Mambo yamerudi kwenye mstari mwendazake alikua anawabania.
Nina kikampuni changu cha marketing hizi propaganda za kuwapgia debe mabeberu sitashindwa niamini mkuu wangu
 
Total kawasome vizuri hawa jamaa huko west africa na miradi yao kule Chad na Congo brazzavile... Total from france, kaisome kitu inaitwa french Africa na makampuni kama total influence yake....Moja ya project ya french Africa ni Gabon na Burkin faso..

Total amemnunua Anadarko pale Msumbiji, yuko na project kuubwa sana ya LNG....tayari RPF vijana wa PK wako pale...

Mengine magumu bwana Pasco nenda kayachimbe...
Umetoa mifano mingi ya kupanua bongo zetu....

Ila ni makampuni gani nguli na ya kibepari duniani yasiyo na KASHFA tofauti?!!!

Afrika tungekuwa na uwezo wa vitendea kazi na miundombinu ikiambatana na UWIANO SAWA WA KIBIASHARA tungeyachimba wenyewe madini na mafuta yetu......


Kuutafuta huo usawa 💯 p ndiko kuliko wagharimu WATAWALA WENGI WA KWANZA barani humu....

Hoja yangu si kushajiisha KUPIGA MAGOTI kwao bali tulipo ni kuhakikisha angalau TUNAFAIDIKA kwa raslimali zetu zilizopo kwa mintaarafu ya "WIN-WIN SITUATION"!!!

#SIEMPRE JMT
#NCHI KWANZA KABLA YA NAFSI ZETU🙏
 
Uwekezaji ni jambo jema lakini tuwe makini na aina ya wawekezaji na terms zao....vyombo vyetu viwe makini 24/7 kuwajua hawa watu na matokeo yawe positive kwa watanzania...

Ni wakati wa kuwekeza kwenye rasilimari watu ili hawa wawekezaji wakija tayari wakutane na trained workforce iliyotayari kwa kazi...Vyombo vyetu visimamie maslahi ya watu wetu 24/7 kuhakikisha watu wetu wanalipwa vizuri, wanapata international training and exposure, healty and safety zinazingatiwa, standard za kazi zinazingatiwa..

Hawa wawekezaji walazimishwe kutoa scholarships kwa watu wetu kusoma vyuo mbalimbali duniani, Majasusi wapandikizwe kulearn new technologies na kuandika reports zitakazokaa huko dip state na tiss..

Supplies na watoa huduma mbalimbali wawe wazawa kwa 90% na Serikali iwezeshe wawekezaji wa ndani kupata mikopo nafuu kutoka kwenye mabank ili wawe na uwezo wa kuwekeza ( hapa sizungumzii watanzania wahindi na waarabu).. Serikali kupitia vitengo vyake ifanye controlling kwa makampuni ya wazawa kuzingatia standards..
 
Back
Top Bottom