Aandika Mohammed Ghassani
Uzalendo gani!?
Mpendwa muheshimiwa, anapanda jukwaani huku mbweu anatowa, anukia biriani tutakaohutubiwa, hatuna kitu tumboni
Muheshimiwa ajuwa kwamba watu wana njaa lakini kalewa pawa.
Basi anatuhimiza: “uzalendo ndu’ zanguni!” “uzalendo!” “nchi yetu!”, hii misamiati gani mzalendo hapa petu, hugezwa kwa jambo gani. Ni mtu asiye kitu, fukara na masikini?
- ama ni ule mjitu
- ada uliofurutu
Wenye nyumba tatu tatu?
Kama ndiye mzalendo, akina miye tu nani?
Uzalendo kuridhia, bwana analobaini?
Isiwe kuulizia, ‘utavuruga’ amani hata akikuibia, umwambiye: ‘shukurani!’ maishaye yamwendea ya kwako yadidimia bali ‘sijekumbushia! Ndio huu uzalendo, tutakwao tuamini? Geukia kwa mkubwa, uzalendowe ni nini:
Kujenga kasri kubwa, magari kwa dizaini fedha nchini kuiba, kupeleka ugenini kukuza yake nasaba kwetu kuleta misiba na sisi tuko “twayiba” huyu ndiye mzalendo, nchi inotumaini?
Yeye aponda maraha, mimi kijua kichwani wakati mimi nahaha, yeye yuko shereheni kila sikuye furaha, kila ya kwangu huzuni
Wallahi hii karaha ninacheka sina jiha kicheko kisicho siha kama yeye mzalendo, mimi siye nijuweni!
Kutoka diwani ya andamo: msafiri safarini
Uzalendo gani!?
Mpendwa muheshimiwa, anapanda jukwaani huku mbweu anatowa, anukia biriani tutakaohutubiwa, hatuna kitu tumboni
Muheshimiwa ajuwa kwamba watu wana njaa lakini kalewa pawa.
Basi anatuhimiza: “uzalendo ndu’ zanguni!” “uzalendo!” “nchi yetu!”, hii misamiati gani mzalendo hapa petu, hugezwa kwa jambo gani. Ni mtu asiye kitu, fukara na masikini?
- ama ni ule mjitu
- ada uliofurutu
Wenye nyumba tatu tatu?
Kama ndiye mzalendo, akina miye tu nani?
Uzalendo kuridhia, bwana analobaini?
Isiwe kuulizia, ‘utavuruga’ amani hata akikuibia, umwambiye: ‘shukurani!’ maishaye yamwendea ya kwako yadidimia bali ‘sijekumbushia! Ndio huu uzalendo, tutakwao tuamini? Geukia kwa mkubwa, uzalendowe ni nini:
Kujenga kasri kubwa, magari kwa dizaini fedha nchini kuiba, kupeleka ugenini kukuza yake nasaba kwetu kuleta misiba na sisi tuko “twayiba” huyu ndiye mzalendo, nchi inotumaini?
Yeye aponda maraha, mimi kijua kichwani wakati mimi nahaha, yeye yuko shereheni kila sikuye furaha, kila ya kwangu huzuni
Wallahi hii karaha ninacheka sina jiha kicheko kisicho siha kama yeye mzalendo, mimi siye nijuweni!
Kutoka diwani ya andamo: msafiri safarini