Uzamiaji Afrika Kusini: Mikasa katika harakati za kuzamia Afrika Kusini kwa njia za panya

Uzamiaji Afrika Kusini: Mikasa katika harakati za kuzamia Afrika Kusini kwa njia za panya

Stoty ipo powa sana,napia miaka ya nyuma nadhani ulii tupia facebook,hii ni konk zaidi ya KeaganPaul.
 
Punguza ujinga na kejeli kwenye story za watu unaboa, ujuaji mwingi haufai, hatakama za kutunga wengine zinatuburudisha.
Mie nadhani una lako jambo. Unacholalamikia ni nini? Kama stori imeshawekwa yote huna haja ya kusubiria vipande. Kama stori kuwa fake watolee povu hao members wanaosema ni fake. Sasa shida yako ni nini? Au una personal issues against me? Maana sioni sababu ya kuni-attack. Hebu soma comments zote utawapata wanaosema hii stori ni fake licha ya kuwa ni copy and paste na sio mimi.
 
Huyo jamaa ana agenda binafsi na mimi. Kakomaa kuniattack on baseless issues.

Hivi ukiacha ile story yako, kuna nyingine ya SA ambayo imeshafika mwisho?

Na ulijibu maswali mengi wadau waliyouliza.

Insecurities ni tatizo, sasa mtu kawekewa uthibitisho kwamba ni fake, lakini badala amfate huyo anakomaa na wewe.
 
Hivi ukiacha ile story yako, kuna nyingine ya SA ambayo imeshafika mwisho?

Na ulijibu maswali mengi wadau waliyouliza.

Insecurities ni tatizo, sasa mtu kawekewa uthibitisho kwamba ni fake, lakini badala amfate huyo anakomaa na wewe.
Shangaa na wewe. Kuna watu wapumbavu hasa, ukiambiwa wapumbavu inabdi uamini kweli ni wapumbavu. Mtu keshawekewa stori nzima, haitaji tena kusubiria vipande vipande vya mleta uzi lakini bado kakomaa kutukana watu, mbaya zaidi anayemtukana hata hahusiki na anachokilalamikia. Watu kibao wamecoment story ni fake licha ya kuwa copied lakini huyu jamaa kanikomalia utadhani hawaoni hao wanaosema stori ni fake.
 
SEHEM YA 5

Tulibaki pale pale porini kama dakika arobaini nyingine tukiwa hatujui
la kufanya, ghafla nikamuona rafiki yangu Jim ambae nilibaki nae pale
porini anaanza kufurahi kwa kurukaruka nikamuuliza kulikoni mwenzan-
gu akaniambia dogo tumetajirika.
Akaendelea kusema wewe si unatafuta hela sasa zimejileta zenyewe, si-
kumuelewa lakini baadae akaniambia kwamba nafasi kama hiyo alikuwa
anaiombea sana kwa muda mrefu sasa imewadia akaniamuru inuka twende,
basi tukaanza safari ya kuelekea barabarani, nikamshauri kwamba kwa nini
tusirudi Lilogwe tukawakomboe jamaa zetu akasema dogo we achana nao,
bosi wao atakuja kuwatoa.
Baada ya muda mfupi ikapita gari dogo ya abiria coster, tukapanda ilikuwa
inaelekea Boda ya kasumulo upande wa Tanzania Sehemu ambayo tulikuwa
tunaelekea haikuwa mbali sana kutoka pale mwendo wa masaa kama mawili
na nusu hivi, kabla hatujafika boda ya Kasumulo ilikuja gari ya polisi ile ile ya
mwanzo ambayo iliwachukua jamaa zetu ikatupita na kisha ikapaki Mbele ya
gari yetu.
Baada ya hapo wakashuka askari na kuamuru abiria wote tushuke, ikafanyika
searching ya nguvu pale na hatimae mimi na yule jamaa yangu tukabainika
kwamba tumebeba mihadarati kwa hivyo tukakamatwa na kurejeshwa tena
Lilogwe polisi central, tulipofika pale polisi tulikuta wale wenzetu wapo kaunta
bado wanachukuliwa maelezo, walipo tuona wakakubaliana kwamba waseme
hawatujui ili wasiingie kwenye mtego wa madawa lakini pia itakuwa rahisi
kututoa tukiwa wawili kuliko timu nzima ikiwekwa ndani.
Tulichukuliwa maelezo na kisha tukawekwa sero, kesho yake ikawa ni siku ya
kusafirishwa kutoka Malawi mimi kuja Tanzania na Jim kwenda kwao Zam-
bia kwa sheria za kimataifa mhalifu anatakiwa arejeshwe kushitakiwa nchini
kwao. Kwa hivyo, mimi niliungana na watanzania wengine watatu ambao naowalikuwa wanarudishwa kwa makosa mbalimbali.
Polisi ya Malawi walikuwa tayari wameshawasiliana na wenzao wa Tanzania
kwa hivyo tulipofika tu pale boda tulikuta gari jingine la polisi wa Tanzania lik-
iwa na askari wa kikosi cha FFU. Tuliposhushwa tu makabidhiano ya kimaan-
dishi yakafanyika na baada ya muda mfupi safari ya kuelekea Mbeya ikaanza,
sikuwa na hofu sana kutokana na uzoefu wangu kwenye matukio kama hayo.
Tuliondoka Boda pale saa mbili asubuhi, tulipofika Mbeya maeneo ya Uyole
kwenye muda wa saa tano hivi askari mmoja alishauri kwamba kwa kuwa
tumeondoka Boda kasumulo Kyela bila ya kula sisi na wao wenyewe tupit-
ie kwenye mgahawa tule mana tusipokula tukifika centra itatuchukua muda
mrefu sana kutuchukua maelezo. Wazo lake likakubalika na mkuu wao wa
msafara na kisha tukaamuliwa kushuka wote kwenda kula, tulipofika ndani
wakatutoa pingu tukaagiziwa chakula, walikuwa ni askari wastarabu sana.
Tukaanza kula, nikiwa nakula nilichungulia sehemu ya jikoni ya ule mgahawa
nikaona kuna mlango wa kutokea nje, pia ilikuwa ili uende chooni unapita
kwenye korido la kupitia karibu na hapo jikoni, nikawaza kwamba ngoja nijari-
bu bahati yangu ya mwisho ya kujiokoa na jela. Nikaomba kwa afande kuwa
naomba niende chooni akakubali kwa kujiamini kwamba choo kipo mle mle
ndani alikuwa hajauona ule mlango wa jikoni.
Nikaenda uani kweli lakini sikukojoa kwa sababu nilijua zile dakika za kukojoa
ndio za kuzitumia kwenye jaribio langu la kutoroka, kwa sababu nilijua ikipita
muda wataanza kuwa na wasiwasi. Kwa hivyo nikageuka haraka nikainama
nikatokea sehemu ya jikoni nikamkuta dada anapika nikatoa dola kumi pale
kumonesha yule dada akasema hapana baba nenda tu zitakusaidia mbele ya
safari.
Nikatoka pale kwa mbio za wastani nikatembea mita kama 40 hivi, nikakumbu-
ka lile begi lenye mali limebaki kwenye gari ya polisi. Nikaanza kurudi kuelekea
gari ya polisi ilipo huku roho nyingine inaniambia niondoke, nikapiga moyo
konde nikaenda hadi pale kwenye defender la polisi nikachukua kile kibegi na
kutokomea nacho Uyole ya kati. Kilichobaki kikaendelea Mimi sijui ila nina-
chokumbuka ni kwamba mimi nilipona kwenye hiyo issue kimaajabu, nadhani
itakuwa ni Mungu mwenyewe aliamua kuniokoa.
Nilipofika maeneo ya Uyole ya kati nilivuka upande wa pili wa barabara, Mbeya
sikuwa mwenyeji kwa hivyo faida tu niliyo kuwa nayo ni kwamba nilikuwa
naongea lugha ambayo naijua vizuri yaani Kiswahili. Nilitembea hadi eneo
linaloitwa Igawilo karibu na eneo wanaita Road kuna baa moja inaitwa Mbigu-
ni ambayo inaambata na vyumba vya wageni, nikachukua chumba pale kwa
ajili ya kulala nilipo kamilisha taratibu za kukabidhiwa chumba nikatoka nje
kutafuta chakula.
Nikiwa pembeni kidogo ikafika gari ya polisi ikiwa na speed kali na haraka
sana hata kabla haijasimama vizuri askari waliruka na kuizunguka ile bar. Ba-
hati nzuri nilikuwa mbali kidogo kwa hivyo nikajivuta pembeni kidogo nikawa
nachungulia kwa mbali ili nione kitakachotokea na hasa kuhusu begi langu
nililoacha ndani. Baada ya msako wa kama dakika 10 hivi niliwaona wametoka
na lile begi langu lenye mihadarati, kwa kiasi fulani sikusikitika sana kwa saba-
bu niliona wamenitua mzigo ambao sikuwa najua pa kuupeleka.
Nikaondoka pale na usiku huo huo nikafika Mbalizi. Nikaulizia njia ya kwenda
Chunya na kaondoka usiku ule ule na gari aina ya Fuso iliyojaa shehena ya
bidhaa za dukani, nilikwenda nayo hadi sehemu moja hivi inaitwa Mkwajuni
ambapo tulifika saa moja asubuhi. Nilivyolisoma eneo la mjini pale Mkwa-
juni nikaona kuna kituo cha polisi, nikahisi watakuwa wanataarifa zangu kwa
hivyo nikaamua kuondoka na kwenda sehemu moja hivi inaitwa Saza sehemu
ambayo nilijua hawatanishangaa kutokana na ukweli kwamba eneo lile lina
machimbo ya madini ya dhahabu kwa hivyo si rahisi wenyeji kukushitukia ku-
tokana na eneo hilo kutapakaa wageni wengi. Nikaweka kituo kwa siku kadhaa
pale huku nafanya tafakari mwanana kabisa ya safari yangu ya kuzamia Afrika
ya kusini ilivyoshindwa kutimia.
Hivyo ndivyo jaribio langu la kwanza la kwenda kuzamia Johannesburg Af-
rika ya kusini lilishindikana katika utaratibu huo uliojaa maajabu ya kutisha,
nilijikuta nimerejea Tanzania bila gharama zozote za nauli wala chakula, nil-
isafirishwa na kulishwa kwa sehemu kubwa na polisi wenyewe, kilichobaki
kinaendelea kwa yule jamaa yangu mganda Kiteba pale Lusaka sikujua, pale
Malawi kwa wale vijana wa bosi mzungu sikujua na hata kwa bwana Jim am-
bae alisafirishwa kutoka Malawi kurudi kwao Zambia sikujua, nilichojua tu
ni kwamba serikali ya Zambia, Malawi na Tanzania zilikuwa zinanitafuta kwa
matukio yaliyotokea.
Pamoja na hayo, nia na sababu ya kurejea tena safari yangu ya kuzamia Afrika
ya kusini ilikuwa pale pale na ndio kwanza nilianza kujipanga upya mara moja
nikiwa pale pale Saza-Mkwajuni Chunya mahali ambapo siku hizi ni makao
makuu ya wilaya mpya ya Songwe.
 
SEHEM YA 5

Tulibaki pale pale porini kama dakika arobaini nyingine tukiwa hatujui
la kufanya, ghafla nikamuona rafiki yangu Jim ambae nilibaki nae pale
porini anaanza kufurahi kwa kurukaruka nikamuuliza kulikoni mwenzan-
gu akaniambia dogo tumetajirika.
Akaendelea kusema wewe si unatafuta hela sasa zimejileta zenyewe, si-
kumuelewa lakini baadae akaniambia kwamba nafasi kama hiyo alikuwa
anaiombea sana kwa muda mrefu sasa imewadia akaniamuru inuka twende,
basi tukaanza safari ya kuelekea barabarani, nikamshauri kwamba kwa nini
tusirudi Lilogwe tukawakomboe jamaa zetu akasema dogo we achana nao,
bosi wao atakuja kuwatoa.
Baada ya muda mfupi ikapita gari dogo ya abiria coster, tukapanda ilikuwa
inaelekea Boda ya kasumulo upande wa Tanzania Sehemu ambayo tulikuwa
tunaelekea haikuwa mbali sana kutoka pale mwendo wa masaa kama mawili
na nusu hivi, kabla hatujafika boda ya Kasumulo ilikuja gari ya polisi ile ile ya
mwanzo ambayo iliwachukua jamaa zetu ikatupita na kisha ikapaki Mbele ya
gari yetu.
Baada ya hapo wakashuka askari na kuamuru abiria wote tushuke, ikafanyika
searching ya nguvu pale na hatimae mimi na yule jamaa yangu tukabainika
kwamba tumebeba mihadarati kwa hivyo tukakamatwa na kurejeshwa tena
Lilogwe polisi central, tulipofika pale polisi tulikuta wale wenzetu wapo kaunta
bado wanachukuliwa maelezo, walipo tuona wakakubaliana kwamba waseme
hawatujui ili wasiingie kwenye mtego wa madawa lakini pia itakuwa rahisi
kututoa tukiwa wawili kuliko timu nzima ikiwekwa ndani.
Tulichukuliwa maelezo na kisha tukawekwa sero, kesho yake ikawa ni siku ya
kusafirishwa kutoka Malawi mimi kuja Tanzania na Jim kwenda kwao Zam-
bia kwa sheria za kimataifa mhalifu anatakiwa arejeshwe kushitakiwa nchini
kwao. Kwa hivyo, mimi niliungana na watanzania wengine watatu ambao naowalikuwa wanarudishwa kwa makosa mbalimbali.
Polisi ya Malawi walikuwa tayari wameshawasiliana na wenzao wa Tanzania
kwa hivyo tulipofika tu pale boda tulikuta gari jingine la polisi wa Tanzania lik-
iwa na askari wa kikosi cha FFU. Tuliposhushwa tu makabidhiano ya kimaan-
dishi yakafanyika na baada ya muda mfupi safari ya kuelekea Mbeya ikaanza,
sikuwa na hofu sana kutokana na uzoefu wangu kwenye matukio kama hayo.
Tuliondoka Boda pale saa mbili asubuhi, tulipofika Mbeya maeneo ya Uyole
kwenye muda wa saa tano hivi askari mmoja alishauri kwamba kwa kuwa
tumeondoka Boda kasumulo Kyela bila ya kula sisi na wao wenyewe tupit-
ie kwenye mgahawa tule mana tusipokula tukifika centra itatuchukua muda
mrefu sana kutuchukua maelezo. Wazo lake likakubalika na mkuu wao wa
msafara na kisha tukaamuliwa kushuka wote kwenda kula, tulipofika ndani
wakatutoa pingu tukaagiziwa chakula, walikuwa ni askari wastarabu sana.
Tukaanza kula, nikiwa nakula nilichungulia sehemu ya jikoni ya ule mgahawa
nikaona kuna mlango wa kutokea nje, pia ilikuwa ili uende chooni unapita
kwenye korido la kupitia karibu na hapo jikoni, nikawaza kwamba ngoja nijari-
bu bahati yangu ya mwisho ya kujiokoa na jela. Nikaomba kwa afande kuwa
naomba niende chooni akakubali kwa kujiamini kwamba choo kipo mle mle
ndani alikuwa hajauona ule mlango wa jikoni.
Nikaenda uani kweli lakini sikukojoa kwa sababu nilijua zile dakika za kukojoa
ndio za kuzitumia kwenye jaribio langu la kutoroka, kwa sababu nilijua ikipita
muda wataanza kuwa na wasiwasi. Kwa hivyo nikageuka haraka nikainama
nikatokea sehemu ya jikoni nikamkuta dada anapika nikatoa dola kumi pale
kumonesha yule dada akasema hapana baba nenda tu zitakusaidia mbele ya
safari.
Nikatoka pale kwa mbio za wastani nikatembea mita kama 40 hivi, nikakumbu-
ka lile begi lenye mali limebaki kwenye gari ya polisi. Nikaanza kurudi kuelekea
gari ya polisi ilipo huku roho nyingine inaniambia niondoke, nikapiga moyo
konde nikaenda hadi pale kwenye defender la polisi nikachukua kile kibegi na
kutokomea nacho Uyole ya kati. Kilichobaki kikaendelea Mimi sijui ila nina-
chokumbuka ni kwamba mimi nilipona kwenye hiyo issue kimaajabu, nadhani
itakuwa ni Mungu mwenyewe aliamua kuniokoa.
Nilipofika maeneo ya Uyole ya kati nilivuka upande wa pili wa barabara, Mbeya
sikuwa mwenyeji kwa hivyo faida tu niliyo kuwa nayo ni kwamba nilikuwa
naongea lugha ambayo naijua vizuri yaani Kiswahili. Nilitembea hadi eneo
linaloitwa Igawilo karibu na eneo wanaita Road kuna baa moja inaitwa Mbigu-
ni ambayo inaambata na vyumba vya wageni, nikachukua chumba pale kwa
ajili ya kulala nilipo kamilisha taratibu za kukabidhiwa chumba nikatoka nje
kutafuta chakula.
Nikiwa pembeni kidogo ikafika gari ya polisi ikiwa na speed kali na haraka
sana hata kabla haijasimama vizuri askari waliruka na kuizunguka ile bar. Ba-
hati nzuri nilikuwa mbali kidogo kwa hivyo nikajivuta pembeni kidogo nikawa
nachungulia kwa mbali ili nione kitakachotokea na hasa kuhusu begi langu
nililoacha ndani. Baada ya msako wa kama dakika 10 hivi niliwaona wametoka
na lile begi langu lenye mihadarati, kwa kiasi fulani sikusikitika sana kwa saba-
bu niliona wamenitua mzigo ambao sikuwa najua pa kuupeleka.
Nikaondoka pale na usiku huo huo nikafika Mbalizi. Nikaulizia njia ya kwenda
Chunya na kaondoka usiku ule ule na gari aina ya Fuso iliyojaa shehena ya
bidhaa za dukani, nilikwenda nayo hadi sehemu moja hivi inaitwa Mkwajuni
ambapo tulifika saa moja asubuhi. Nilivyolisoma eneo la mjini pale Mkwa-
juni nikaona kuna kituo cha polisi, nikahisi watakuwa wanataarifa zangu kwa
hivyo nikaamua kuondoka na kwenda sehemu moja hivi inaitwa Saza sehemu
ambayo nilijua hawatanishangaa kutokana na ukweli kwamba eneo lile lina
machimbo ya madini ya dhahabu kwa hivyo si rahisi wenyeji kukushitukia ku-
tokana na eneo hilo kutapakaa wageni wengi. Nikaweka kituo kwa siku kadhaa
pale huku nafanya tafakari mwanana kabisa ya safari yangu ya kuzamia Afrika
ya kusini ilivyoshindwa kutimia.
Hivyo ndivyo jaribio langu la kwanza la kwenda kuzamia Johannesburg Af-
rika ya kusini lilishindikana katika utaratibu huo uliojaa maajabu ya kutisha,
nilijikuta nimerejea Tanzania bila gharama zozote za nauli wala chakula, nil-
isafirishwa na kulishwa kwa sehemu kubwa na polisi wenyewe, kilichobaki
kinaendelea kwa yule jamaa yangu mganda Kiteba pale Lusaka sikujua, pale
Malawi kwa wale vijana wa bosi mzungu sikujua na hata kwa bwana Jim am-
bae alisafirishwa kutoka Malawi kurudi kwao Zambia sikujua, nilichojua tu
ni kwamba serikali ya Zambia, Malawi na Tanzania zilikuwa zinanitafuta kwa
matukio yaliyotokea.
Pamoja na hayo, nia na sababu ya kurejea tena safari yangu ya kuzamia Afrika
ya kusini ilikuwa pale pale na ndio kwanza nilianza kujipanga upya mara moja
nikiwa pale pale Saza-Mkwajuni Chunya mahali ambapo siku hizi ni makao
makuu ya wilaya mpya ya Songwe.
oya endelea kushusha vitu....hyo link ya kitabu waliyoituma huku haifunguki

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu naona umeamua Kudandia gari kwa mbele kama Hii stori ulikua nayo kwanini usiitoe siku zote mpaka mimi Nimeaza kuiposti wewe ndo unajifanya Kuingilia......Acha utoto.
Huyu dogo mpuuz Sana kadandia na kaaribu mazima wee ulikuwa unapangiliaa vxr mno
 
Back
Top Bottom