Management wanajifanya hawalioni, kuna uwezekano huyu tunayejibizana naye humu ndiye mnywa supu ila anajishaua tuMpaka malori Yani, unakuta foreman anaenda kunywa chai ,hafu wafanyakazi wamekaa kwenye Lori wanamsubiria . Saa tatu au nne . Tena hili la kunywa supu mda wa kazi ni limeota mizizi Yani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huwa najiuliza hili shirika linashindwa vitu vidogo je huko kwenye mabwawa inakuwaje!!!?Rungu Spray iliwashinda kununua?
Brilliant!!!Yaani whistle blower unataka atoe namba ya simu tena? Hivi wengine akili zenu zinafanyakazi kweli?? Amekueleza eneo cha kwanza kabisa ungecheki na ofisi zenu za huko Kyela ama ofisi ya serikali ya huko.
Jibu ni dhahiri, wazembe, hamjali, hamuwajibiki kwa taarifa mnazopewa na wananchi except viongozi,Umeulizwa kwa nini ni shirika la hovyo? Toa jibu
Mhh usiwahukumu kiasi hicho ,wanafanya kazi njema ,makosa yaweza tokea hata kwako unakofanyia kazi.mhhh watumie namba za simuNi shirika la hovyo kabisa kuwahi kutokea
Halafu kuna kijamaa kijingakijinga kinajiita tanesco humu kinakanusha ati hakuna kitu kama hichoUPDATES:
Baadaya ya kubandikwa kwa bandiko hili. Leo mchana tanesco wamefika enelo la tukio na kuanza kuchimba mashimo ya kusimamisha nguzo 2 zilizo anguka wiki iliyopita.
Siwapi namba yangu watu wazembeMhh usiwahukumu kiasi hicho ,wanafanya kazi njema ,makosa yaweza tokea hata kwako unakofanyia kazi.mhhh watumie namba za simu
Humuamini aliyeleta taarifa kwa kuwa labda hajaweka picha ila unaamini taarifa ya aliyefuatilia japo nae hajaweka picha. Ajabu sana!!Tatizo ni nini hasa?
Huyu bwana amefanya follow-up na kuleta mrejesho kuwa hakuna ajali yoyote iliyotokea zaidi ya nguzo kuinama, na aliyeleta tuhuma athibitishe beyond reasonable doubt. Sasa weye povu linakutoka, why??
Mkuu ukiona Jamiforums hawajauondoa uzi hapa ujue wamefuatilia wamejiridhisha kuwa una ukweli, vinginevyo kama ingekuwa uzushi wangesha block jana ileileHumuamini aliyeleta taarifa kwa kuwa labda hajaweka picha ila unaamini taarifa ya aliyefuatilia japo nae hajaweka picha. Ajabu sana!!
Unamtaka mtoa taarifa athibitishe tuhuma beyond reasonable doubt, jambo ambalo lingeweza kufanywa tu na TANESCO (wakati wa kukanusha taarifa /lalamiko) kwa kupiga picha ya hilo eneo ikionesha nyuki na hizo nguzo zilizolala. Kama ni nguzo zimelala na sio kuanguka kwa nini wao wasipige picha?
Ilo nampa heko hata mimiTANESCO ndilo shirika pekee ambalo linajibu kila shutuma hapa JF.
Pamoja na hoja zenye dharau na kejeli ila mhusika wa TANESCO anazijibu bila kutukana.
Hakika anajua customer service
Sent from my TECNO W2 using JamiiForums mobile app
Tunataka matokeo ya kazi siyo maneno.Wakati mwingine tushukuru hata Shirika kuona umuhimu wa kuwajibu taarifa zenu humu
Ukweli wanakera Sana,umeme ni nishati ya hatari ikiwa haiko kwenye usalama wa mtumiaji,lakini tanesco wamelisahau Hilo,wameuchukulia umeme Kama vile nishati ya kuni au mkaa!!!Fanyeni tracking kwenye hiyo number iliyowasiliana nanyi siku hiyo na kwakuwa si jambo la kificho basi waliohusika na huo uzembe wawajibishwe maramoja kuliokoa shirika na lawama
Ni kweli kuna kifo kimetokea kwa ajili ya hiyo nguzo? Wenyewe wanasema hakuna kifo. Tuamini lipi?Wilayani Kyela, Katika kata ya Serengeti siku ya jumamosi 27-02-2021 ilipata kuanguka nguzo mojawapo ya umeme wa Tanesco Hata kukapelekea kukosekana kwa umeme katika katika kata hiyo. Ikumbukwe leo ni Ijumaa ya tarehe 05-03-2021.
Wana-Serengeti wakafanya jitihada ya kuwasiliana na mamlaka za umeme (Tanesco Kyela - 0787028355) ili waweze kufanya marekebishi ya nguzo hiyo kwa sababu ilikuwa imedondoka katika maeneo ambapo watoto wanapenda kucheza cheza na pia kuweza kurejesha huduma za umeme haraka kwa wakaazi wa eneo hilo.
Cha kushangaza tangu wapewe taarifa ya kudondoka kwa nguzo hiyo wameshindwa kuchukua hatua stahiki na haraka zaidi. Ukijaribu kuwasiliana nao wanatoa majibu ya ajabu ajabu wa wananchi. Tangu jumapili ya wiki iliyopita mpaka leo hii ni siku 6 zimepita hawajafika katika eneo ili kutimiza wajibu wao. Wananchi wamekuwa wakidhani labda idara ya tanesco ya umeme haina pesa ili kuweza kulipa mafundi waje kutimiza wajibu hata wakajaribu kuona uwezekano wa kuchangisha mapema ili zoezi lianze.
Jioni ya leo mmoja wa mwanafunzi wa shule ya msingi ajulikanaye kawa jina la Albert Mwakajila (6) amefariki kutokana na kuchezea nyaya ya umeme ambayo imedondoka na nguzo hiyo.
Wananchi wa kata ya Serengeti wanaomba msaada kutoka ofisi za Tanesco mkoani mbeya ili kufuatilia suala hili mapema iwezekanavyo ili kuondoa hatari ya umeme kwa watoto wa eneo hilo.
Kata ya Serengeti wilayani Kyela imekosa umeme tangu siku ya jumamosi usiku wa tarehe 27-02-2021
Nawasilisha.
UPDATES:
Baadaya ya kubandikwa kwa bandiko hili. Leo mchana tanesco wamefika enelo la tukio na kuanza kuchimba mashimo ya kusimamisha nguzo 2 zilizo anguka wiki iliyopita.