Uzi maalum wa kupata connection za ajira na machimbo mengine

Ni kweli kabisa. Nami nilienda hapo mwezi uliopita, nilikuwa na vigezo karibia vyote isipokuwa urefu tu nd'o uliniangusha.
 
Nimekuja dar kujaribu bahati yangu maana najua ajira ni changamoto. Nimefika dar kwakuwa sina mtaji ikabidi nitegemee nguvu zangu. Nikaanza kutafuta kazi ya kufyatua tofali(za block) kama siku tatu hivi, sijafanikiwa maana kila chimbo nikienda watu wapo wa kutosha. SASA kama kuna mtu yyt yupo na connection ya vibarua, tenda mbalimbali anistue nipo tayari kufanya kazi.
 
Ingependeza kwa yule anayesema anatafuta aeleza na taaluma yake na ngazi ya taaluma hiyo pamoja na uzoefu wako, itasaidia kwa anayetaka kusaidia, kuliko kusema tu "Mi natafuta"
 
Bsc in Agricultural engineering and Mechanization
Nina experience katika
-Computer Aided design
-Machine maintainance
-Irrigation systems design
-Infustrial automation
-Agronomy
-Industrial safety and risks management
--Value chain analysis
 
Natafuta ajira
Nina 1
Diploma mifugo
2.advance BA
3.PGD IBM

Uzoefu mauzo 5yrs
 
Kama kichwa cha habari kinavyo someka
ningependa uzi huu uwe maalum kwa kupeana connection mbalimbali za kazi .

Katika kuzunguka kwangu kote kutafuta kibarua/kazi nimebaini kuwa bila kujuana na mtu ni vigumu kupata kibarua/kazi .

bila connection ni ngumu kupata kazi hivyo basi ni vizuri tupeane connection mbalimbali za kazi

Uzi huu utumike kuwakutanisha watu mbalimbal mwisho wa siku kupeana connection za kazi kutokana na ombi la muhusika.

Tupo watu mbalimbali jamii forum tukitafuta kazi/kibarua lakini kutokana na kutokuwa na connection tunakosa Hivyo basi uzi huu uwe msaada kwetu.

Elezea unahitaji connection ipi katika kazi kisha subiri kupewa connection na wadau mbali mbali katika kai/ajra Na tenda

Lengo ni kusaidiana na si vinginevyo. Tuweke roho mbaya pembeni kisha tuungane pamoja katika gurudumu la maendeleo Kwa taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…