Uzi maalum wa viwanja vya kula bata, Night Club party animals

Uzi maalum wa viwanja vya kula bata, Night Club party animals

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Nimeona sio jambo baya Kama tukawa na Uzi maalum kwa ajili ya viwanja vya starehe, Tukutane hapa

  • Kupeana updates za viwanja
  • ubora wa huduma zitolewazo kwenye viwanja
  • viwanja vya kukwepa
  • Tahadhari tuwapo viwanjani
  • Elimu kwa wageni wasichekwe wakitembelea viwanja 🤣

Tusisahau kutupiamo vimbwanga na vituko tulivyoahi kukutana navyo tukiwa viwanjani

1. TABIA AMBAZO HUTAKIWI KUZIONYESHA, UTAONEKANA MSHAMBA, KUKU MWENYE KAMBA MGUUNI

  • Kushangaa shanga watu - unatolea macho mashoga ukiwakazia macho utatongozwa 😂, wakijua unawashangaa wanaweza kukumwagiwa bia
  • Vibe likikolea usianze habari za kuwaambia wenzako kurudi nyumban eti muda umeenda sana, kwani upo boarding ?
  • acha kuuliza time kila muda, kwa wazoefu nyimbo flani ikipigwa wanajua kabsa sa hivi muda flani
  • Bill ya Lak 2 unaanza kulalamika mbona bill ni kubwa ivyo wakati ni kiwanja kikali
  • kubambia anae cheza na mwingne, hii sio bush party

2. UKISIKIA MANENO HAYA JUA WANAKUKWEPA (acha kuomba omba, acha kuleta stori za matatizo, n.k)

  • umetukuta ndio tulikuwa tunaondoka Muhudumu tunaomba Bill"
  • Mbona meza nyingi, sio lazima tukae meza moja
  • Vp huendi nyumbani
  • Tunahama, hapa jau
  • Nyumbani wanajua upo hapa
  • Sisi tunaenda kuna emergency,
  • subiri tutakupitia
  • Leo kila mtu atumie pesa yake
  • hivi job unaingiaga saa ngapi mkuu

3. VIWANJA VINAVYOJAA WAZUNGU, WACHINA, WATALII, n.k.
  • Havoc, slipway, cliff, wavuvi camp - DSM
  • The Hub, Zeze - Arusha
  • Kendwa rocks - Zanzibar
4. TAHADHARI

  • Ukienda chooni ukirudi nunua kinywaji kingine, usinywe ulichokiacha, kuna uhuni unaitwa spiking
  • Vuta chako au cha mtu ambae mpo karibu, usigongee kwa watu usiowajua, wapo wanaomix madawa.
  • NI vema kutuliza ugomvi kuliko kuukuza, hujui unaetaka kupigana nae ni nani, kaja na kina nani, n.k.
  • No mara waaa, beba mpira, likitokea la kutokea tumia mpira, utasifiwa wewe ni rijali ila majuto kivyako.
 
Walevi wanakuja kukupa mwongozo
IMG-20241018-WA0066.jpg
 
fIkiri kwa sekunde. Wazo la bure hili.

Kwanini usianzishe website ionyeshe hizo klabu ukusanye hela badala ya likes?

Unavuta kote kote.

kama naona 👀batu bameisha anza kutafakari hili. Mniletee mrejesho

ukimeki usimshahu Nkaburu 👉💥
 
weekend bado haijapoa ,karibuni samaki samaki
ukitaka u enjoy viwanja hivyo usiwe na pesa ya mawazo maana bills ni kubwa, in addition to that uwe unatema yai kwasababu wageni ni wengi.

Ila viwanja ni circle, kwenda sehemu yai huletemi vizuri alafu una pesa unaweza kuboreka, ndio maana wengi wanaenda viwanja vya wabongo wenzao kitambaa cheupe, elements, n.k.
 
fIkiri kwa sekunde. Wazo la bure hili.

Kwanini usianzishe website ionyeshe hizo klabu ukusanye hela badala ya likes?

Unavuta kote kote.

kama naona 👀batu bameisha anza kutafakari hili. Mniletee mrejesho

ukimeki usimshahu Nkaburu 👉💥
Kuna google maps na magroup kibao ya viwanja.

Pesa ya website sio rahisi kama unavyodhani, wasomaji elfu moja unaambulia shilingi elf 2 hata mkojo wa punda (balimi) hupati ukitoa makato
 
Kuna google maps na magroup kibao ya viwanja.

Pesa ya website sio rahisi kama unavyodhani, wasomaji elfu moja unaambulia shilingi elf 2 hata mkojo wa punda (balimi) hupati ukitoa makato
mkulu acha kujitafutia vijisababu, hizo google maps na magroup kama zingekuwa ndio vianzio vizuri vya kutafuta chechote, kusingekuwa na app ama mfano website kama ya Travel ositi ambayo natumia nikiwa safarini. Napata kila kitu pale. HOTELI, GARI, CLUB,n.k n.k as opposed yangu mimi kuanza kutafuta google, kisha nitafute, club, nitafute usafiri na hoteli wakati nikiingia travel ositi naserereka
any way who does that nowadays? kuingia magrupu na google kutafuta? Nataka app ama website napata kila kitu.

unafikiri wanatengeneza hela kwa trafik peke yake?

najua kuna watu watachangamkia. Kama sio kenya nigeria na south. Changamka. Unayo idea nzuri ikuze. Panua wigo mkulu.

au

ndio unasema uanchangamsha jukwaa tu ama hapa JF ndimo utatengeneza pesa zaidi.
Website kiasi gani?
 
Ujana maji ya moto. Vunja mifupa wakati meno bado yapo.
Kuna umri ukifika hata kutoka nje unaona kero. Tangu niingie ndani jana saa mbili usiku sijatoka hata nje ya geti. Hapa nasubiri Madrid derby nayo ikiisha niangalie Lakers vs Pacers ikiisha hio saa 8 usiku nilale kesho nowahi shamba.
 
Back
Top Bottom