Jiji la Dar es Salaam lilianza kama Kijiji kidogo cha wavuvi kilichojulikana kama
Mzizima. Kijiji hiki kilianzishwa na Wabalawa ambao walichanganyika na Wazaramo kuelekea kwenye maeneo ya Bara la Afrika Mashariki na ambazo zilijulikana kama ‘Caravan Routes’. Ujenzi wa Makao ya Sultani pamoja na bandari ulianza rasmi mwaka 1865 katika eneo la kijiji cha Mzizima. Ujenzi huo ulikamilika mwaka 1866 na Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mwaka huo.
Mara baada ya Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mji ulianza kupanuka na
uchumi wake kukua kwa kasi kubwa japo kwa kipindi kifupi ambapo Sultani Majid
bin Said alifariki mwaka 1870. Kifo cha Sultani huyo kilisababisha kudidimia kwa
maendeleo ya mji wa Dar es Salaam.
Hali hiyo ilianza tena kubadilika mwaka 1884 kufuatia kuanzishwa kwa koloni la Wajerumani la Afrika Mashariki. Mwaka 1891 Serikali ya kikoloni ya Kijerumani iliamua kuhamisha makao makuu ya utawala wake katika Afrika Mashariki kutoka Bagamoyo na kuyaweka Dar es Salaam. Hata hivyo, baada ya Wajerumani kushindwa na Waingereza katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1916, Mji wa Dar es Salaam uliendelea kuwa makao makuu ya utawala wa koloni la Waingereza nchini Tanganyika hadi ilipojipatia uhuru wake mwaka 1961.
Dar es Salaam iliendelea kuwa makao makuu ya Tanganyika huru na hatimaye kuwa
makao makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi mwaka 1972
wakati Serikali ilipoamua kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma. Jiji la Dar es
Salaam liliendelea kubaki kuwa maarufu kwa kuwa Jiji kuu na kitovu cha biashara
nchini Tanzania.
Hadhi ya Mji, Manispaa na Jiji
Mji wa Dar es Salaam ulitangazwa kuwa Mji wenye Serikali yake ya Mitaa mwaka
1920. Hadhi ya Mji wa Dar es Salaam ilipandishwa kuwa ya Manispaa mwaka 1949 na
baadaye kutunukiwa hadhi ya Jiji na Malkia wa Himaya ya Uingereza tarehe 10
Desemba 1961 mara baada ya Tanganyika kupata uhuru wake. Kuanzia kipindi hicho,
Jiji la Dar es Salaam lilikuwa likiongozwa na Halmashauri ya Jiji hadi mwaka 1972
wakati ambapo Serikali ilivunja Serikali zote za Mitaa nchini ili kutekeleza mfumo wa
madaraka Mikoni. Mamlaka za Miji zilirejeshewa madaraka mwaka 1978 ambapo
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lilianza kufanya kazi tena.
Serikali za Mitaa
Kabla ya Ukoloni walitawala Machifu na Wazee wa mila. Wakati wa Utawala wa
Wajerumani (1884-1917) utawala wa kikoloni ulikuwa wa moja kwa moja zaidi maeneo
ya mijini “Direct rule”. Katika kipindi cha utawala wa Waingereza (1917-1961) katika
mwaka 1926 kulikuwa na utawala wa kikabila. Sheria ya Serikali za Mitaa zilianza
mwaka 1953 na Sheria ya Miji mwaka 1946.
Baada ya mwaka 1961 uliondolewa Utawala wa Machifu na kuanza Mfumo wa pamoja
wa Serikali za Mitaa. Mwaka 1972 Serikali za Mitaa ziliondolewa na kuanza Utawala
Mijini na mwaka 1982 Sheria ya Serikali za Mitaa zilirejeshwa tena. Mwaka 1984
ulirejeshwa mfumo wa Serikali za Mitaa na kudumu hadi mwaka 1995. Mpango wa
uboreshaji wa Serikali za Mitaa kuzifanya ziwe na uwezo wa utendaji, uwazi na
uwajibikaji ulianzishwa mwaka 1996 uliojulikana kama “Local Government Reform
Programme”.
Mkoa wa Dar es Salaam wenye eneo na km za mraba 1,800 ulianzishwa kutoka Mkoa
wa Pwani mwaka 1973 ukiwa na Wilaya 3 za Ilala, Kinondoni na Temeke. Mamlaka za
Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dar es Salaam zilizopo sasa zilianzishwa mwaka 2000
baada ya kuvunjwa kwa Tume ya Jiji iliyokuwepo kufuatia kuvunjwa kwa Serikali za
Mitaa mwaka 1996 kulikoendelea hadi mwishoni mwa mwaka 1999.
Huu uzi nitakuwa nawaletea updates za watu wa Dar es salaam. waliopita na waliopo na maeneo mbali mbali na pia nitakuwa nawapatia updates ya kinachoendelea socially, economically na politically.
Nitaambatanisha picha mbali mbali
Library ni kubwa mno kwa kweli...
maulid ya vijana wa sikukuu kkoo. Wa kwanza kushoto ni mbunge wetu wa ilala Mh. Zungu. Katibu wa Saigon Boi Juma Risasi na Mweka hazina wa Saigon Alhaj Mussa Shagow
Hawa ni wadau wa soka wa mkoa wa Dar es Salaam enzi hizo . Mwaka 1986 walichangia kuweka madarakani IDFA. Kutoka kushoto ni Margaret Bwana. Luke luhui. Afisa utamaduni wilaya ilala. Marehem Malik Chanzi. Amin Bakhressa. Chando. Hamisi Kissiwa. Abdallah Kisungura.Mstari wa pili viongozi walikuwa Saidi Kizega. Mussa Shagow. Abdallah Katungunya. Wadau wengine. Gerald Sewe Jaluo. (R.ip) Shabani Kinana(r.i.p)Shaaban Zembwela(r.i.p) Muharami Mkamba na wengineo
Mzizima. Kijiji hiki kilianzishwa na Wabalawa ambao walichanganyika na Wazaramo kuelekea kwenye maeneo ya Bara la Afrika Mashariki na ambazo zilijulikana kama ‘Caravan Routes’. Ujenzi wa Makao ya Sultani pamoja na bandari ulianza rasmi mwaka 1865 katika eneo la kijiji cha Mzizima. Ujenzi huo ulikamilika mwaka 1866 na Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mwaka huo.
Mara baada ya Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mji ulianza kupanuka na
uchumi wake kukua kwa kasi kubwa japo kwa kipindi kifupi ambapo Sultani Majid
bin Said alifariki mwaka 1870. Kifo cha Sultani huyo kilisababisha kudidimia kwa
maendeleo ya mji wa Dar es Salaam.
Hali hiyo ilianza tena kubadilika mwaka 1884 kufuatia kuanzishwa kwa koloni la Wajerumani la Afrika Mashariki. Mwaka 1891 Serikali ya kikoloni ya Kijerumani iliamua kuhamisha makao makuu ya utawala wake katika Afrika Mashariki kutoka Bagamoyo na kuyaweka Dar es Salaam. Hata hivyo, baada ya Wajerumani kushindwa na Waingereza katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1916, Mji wa Dar es Salaam uliendelea kuwa makao makuu ya utawala wa koloni la Waingereza nchini Tanganyika hadi ilipojipatia uhuru wake mwaka 1961.
Dar es Salaam iliendelea kuwa makao makuu ya Tanganyika huru na hatimaye kuwa
makao makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi mwaka 1972
wakati Serikali ilipoamua kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma. Jiji la Dar es
Salaam liliendelea kubaki kuwa maarufu kwa kuwa Jiji kuu na kitovu cha biashara
nchini Tanzania.
Hadhi ya Mji, Manispaa na Jiji
Mji wa Dar es Salaam ulitangazwa kuwa Mji wenye Serikali yake ya Mitaa mwaka
1920. Hadhi ya Mji wa Dar es Salaam ilipandishwa kuwa ya Manispaa mwaka 1949 na
baadaye kutunukiwa hadhi ya Jiji na Malkia wa Himaya ya Uingereza tarehe 10
Desemba 1961 mara baada ya Tanganyika kupata uhuru wake. Kuanzia kipindi hicho,
Jiji la Dar es Salaam lilikuwa likiongozwa na Halmashauri ya Jiji hadi mwaka 1972
wakati ambapo Serikali ilivunja Serikali zote za Mitaa nchini ili kutekeleza mfumo wa
madaraka Mikoni. Mamlaka za Miji zilirejeshewa madaraka mwaka 1978 ambapo
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lilianza kufanya kazi tena.
Serikali za Mitaa
Kabla ya Ukoloni walitawala Machifu na Wazee wa mila. Wakati wa Utawala wa
Wajerumani (1884-1917) utawala wa kikoloni ulikuwa wa moja kwa moja zaidi maeneo
ya mijini “Direct rule”. Katika kipindi cha utawala wa Waingereza (1917-1961) katika
mwaka 1926 kulikuwa na utawala wa kikabila. Sheria ya Serikali za Mitaa zilianza
mwaka 1953 na Sheria ya Miji mwaka 1946.
Baada ya mwaka 1961 uliondolewa Utawala wa Machifu na kuanza Mfumo wa pamoja
wa Serikali za Mitaa. Mwaka 1972 Serikali za Mitaa ziliondolewa na kuanza Utawala
Mijini na mwaka 1982 Sheria ya Serikali za Mitaa zilirejeshwa tena. Mwaka 1984
ulirejeshwa mfumo wa Serikali za Mitaa na kudumu hadi mwaka 1995. Mpango wa
uboreshaji wa Serikali za Mitaa kuzifanya ziwe na uwezo wa utendaji, uwazi na
uwajibikaji ulianzishwa mwaka 1996 uliojulikana kama “Local Government Reform
Programme”.
Mkoa wa Dar es Salaam wenye eneo na km za mraba 1,800 ulianzishwa kutoka Mkoa
wa Pwani mwaka 1973 ukiwa na Wilaya 3 za Ilala, Kinondoni na Temeke. Mamlaka za
Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dar es Salaam zilizopo sasa zilianzishwa mwaka 2000
baada ya kuvunjwa kwa Tume ya Jiji iliyokuwepo kufuatia kuvunjwa kwa Serikali za
Mitaa mwaka 1996 kulikoendelea hadi mwishoni mwa mwaka 1999.
Huu uzi nitakuwa nawaletea updates za watu wa Dar es salaam. waliopita na waliopo na maeneo mbali mbali na pia nitakuwa nawapatia updates ya kinachoendelea socially, economically na politically.
Nitaambatanisha picha mbali mbali
Library ni kubwa mno kwa kweli...
maulid ya vijana wa sikukuu kkoo. Wa kwanza kushoto ni mbunge wetu wa ilala Mh. Zungu. Katibu wa Saigon Boi Juma Risasi na Mweka hazina wa Saigon Alhaj Mussa Shagow
Hawa ni wadau wa soka wa mkoa wa Dar es Salaam enzi hizo . Mwaka 1986 walichangia kuweka madarakani IDFA. Kutoka kushoto ni Margaret Bwana. Luke luhui. Afisa utamaduni wilaya ilala. Marehem Malik Chanzi. Amin Bakhressa. Chando. Hamisi Kissiwa. Abdallah Kisungura.Mstari wa pili viongozi walikuwa Saidi Kizega. Mussa Shagow. Abdallah Katungunya. Wadau wengine. Gerald Sewe Jaluo. (R.ip) Shabani Kinana(r.i.p)Shaaban Zembwela(r.i.p) Muharami Mkamba na wengineo