Uzi maalum wa wana Mzizima aka Dar es Salaam

Uzi maalum wa wana Mzizima aka Dar es Salaam

Una ushahidi gani? Kwanini Watanzania huwa mnaleta habari zisizo jitosheleza? Unknown person can claim something with no evidence!.

Mzizima kuna watu Walimiliki Bustani za Mnazi Mmoja na kuzigawa bure kina Rupia,Karimjee kuna watu kama Agakhan na community yake walitisha,Azizi Ally kiasi Mkuu tupe Hostoria za aina hiyo... Sio Kukaa kijiweni na kunywa Kahawa kama Mzee Mo Saidi hihihihi
Mlaleo,
Sisi watu wa pwani ni kawaida ya kuwa na barza yako ambayo baada
ya kazi huwa unakwenda hapo kwa mazungumzo.

Kunywa kahawa ni moja ya utamaduni wetu mfano wa nyie kwenda
kilabu cha pombe na kunywa ulevi.
 
Hivi wewe mzee huwa unaelewa vichwa vya mada husika au ndio kupost post tu vitu hovyo tu hata sehemu zisizo husika... Thead mtu kaanzisha kuhusu DSM Mzizima and then anapost mambo ya Tanga,Mara shughuri za Ibada wapi na wapi? au na nyie mkiwa mnaswali kuna time mnaacha na mnaanza zungumzia Diamond katoa wimbo gani au leo Njenje au Sikinde wanapiga wapi? lazima ueshimu uhalisia wa jambo lihusulo. kuchanganya changanya mwishowe wasomaji tunashangazwa tunajikuta tupo jukwaa la Dini au la mkoa husika!

Najua povu litakutoka kisa umepost picha za vinanda news isiyo na kichwa wala miguu ndio maana kama facebook vile, nasema kuna vitu vingine tunasoma hadi tunajuta why tumesoma comments.

Unaposema ati nakerwa na Waislam??? are Mental Man? how come unajenga kichwani mwako thought kama hiyo? are you Ok? unahitajika ukapimwe Mkojo Mzee maana kama ushambenga wewe umepitiliza... Sijawahi kerwa zaidi ya kucrash sifa za kijinga tu mtu aletazo.

Nyerere alikuwa na Akili zake na sio hao wazee uwasemao nadhani hujui Siasa ndio maana unatatizwa sana na uwepo wa watazamaji au wasindikizaji katika Siasa ukidhani wao ndio wasababishaji haswa... Siasa ni Kipaji hata kama hukuwa na maneno matamu kama Kawawa ukiwa na Nyota ya uongozi utafanikiwa tu sasa hao wazee walishindwa hadi wakaona wakomae na mwenye akili. siasa zilikuwepo na Waingereza hawakuwa wakoloni bali walitushikia tu Uongozi hadi tutakapokuja weza jiongoza wenyewe. blah blah za Tanu na kadharika ni sehemu ya Matokeo tu.

Mlaleo,
Nimefanya masahihisho para ya kwanza na ya mwisho.
Ungeanza kwanza na kujifunza kuandika ingekuwa bora.

Sikasirishwi na kuitwa mzee maana naona hii lugha yako
ya kifedhuli unadhani nitakereka.

Nilikuwa kijana tena kijana kweli kweli na nilikula maisha:

xS31qIiS0sL4yg_FUI4-ArPHycC3xNg_tNJfaOZdNKIAM6YZ-nLFkvhIQupfLd1x9AcOKu96PWGmmnKLuaZxUjuN9qvQmD0erEFJ_7LD6ISIMBFEdsWrce0LAJc8gfhwATEtu_GdEm8tyTO6gaDZp9cBg8nIImeUJzGqMncWt2gDcsWJ_30YnIl06GjpQU0nWbMzvpX-AFAm58WyZR-7Z9mKKSOCJ5TdZRqvpY1FOmaqjzFO4-cxK2zwB3ezejAntWlQI3dJ3bWSTFx778_0mfKLdeUQS_fjBvjzovEHv1W2b8q_exZ_bG8tsYIrnbE-QqyoIklWIScTc0tZsMHwYi6z-5kiqHuSJXMDXut7g9A2DTa2bm7xK7m-c3BgrO0DghF0Iza_f8bfsjbIQ1UMFGZ7YWxmpGfAHZggWA35g6U_nHgfelKMHGf3gJldrGIUbWjRFrndbtDVJZlwoF4Wu-KoJ_j5ejMo5fpInj3NHdM9vCFi3CF_pcR1PA4S-3uuVPP7vMU8wuKsYjsspjLcTj7SkcziKJZBmaFTxn-X7_RgsadbFg7IgOE3Sgp8i7Q5CyvA3NDwVqeA5XmMR-wWoYas9QbNHXZ0rSGorqKcnKo=w480-h360-no


London 1991.

Ukipenda nitakuwekea za Paris, Alexandira, Addis na kwingi tu.

Mwaka kesho February nikiwa hai nitakuwa na miaka 66.
Alhamdulilah.
 
Mlaleo,
Nimefanya masahihisho para ya kwanza na ya mwisho.
Ungeanza kwanza na kujifunza kuandika ingekuwa bora.

Sikasirishwi na kuitwa mzee maana naona hii lugha yako
ya kifedhuli unadhani nitakereka.

Nilikuwa kijana tena kijana kweli kweli na nilikula maisha:

xS31qIiS0sL4yg_FUI4-ArPHycC3xNg_tNJfaOZdNKIAM6YZ-nLFkvhIQupfLd1x9AcOKu96PWGmmnKLuaZxUjuN9qvQmD0erEFJ_7LD6ISIMBFEdsWrce0LAJc8gfhwATEtu_GdEm8tyTO6gaDZp9cBg8nIImeUJzGqMncWt2gDcsWJ_30YnIl06GjpQU0nWbMzvpX-AFAm58WyZR-7Z9mKKSOCJ5TdZRqvpY1FOmaqjzFO4-cxK2zwB3ezejAntWlQI3dJ3bWSTFx778_0mfKLdeUQS_fjBvjzovEHv1W2b8q_exZ_bG8tsYIrnbE-QqyoIklWIScTc0tZsMHwYi6z-5kiqHuSJXMDXut7g9A2DTa2bm7xK7m-c3BgrO0DghF0Iza_f8bfsjbIQ1UMFGZ7YWxmpGfAHZggWA35g6U_nHgfelKMHGf3gJldrGIUbWjRFrndbtDVJZlwoF4Wu-KoJ_j5ejMo5fpInj3NHdM9vCFi3CF_pcR1PA4S-3uuVPP7vMU8wuKsYjsspjLcTj7SkcziKJZBmaFTxn-X7_RgsadbFg7IgOE3Sgp8i7Q5CyvA3NDwVqeA5XmMR-wWoYas9QbNHXZ0rSGorqKcnKo=w480-h360-no


London 1991.

Ukipenda nitakuwekea za Paris, Alexandira, Addis na kwingi tu.

Mwaka kesho February nikiwa hai nitakuwa na miaka 66.
Alhamdulilah.
 
Hakika mzizima palifana haswa n kumbukumbu hz mpk raha
 
Huyo hapo juu ni Maalim Subeit wa Egyptian Music alikuwa bingwa wa muziki wa Taarab kuanzia miaka ya 1940 na pia alikuwa mwalimu akifundisha Kitchele Government School.
 
UNAFAHAMU NENO KURASINI LILIZALIWAJE?

Kurasini ni miongoni mwa maeneo maarufu ya jiji la Dar es Salaam.

Jiji la Dar es Salaam ni maarufu sana kwa shughuli za kibiashara kwa nchi za Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika.

Eneo la Kurasini lenyewe limekuwa maarufu zaidi kutokana na uwepo wa Bandari na Bandari Kavu ama maeneo ya kuhifadhia makontena.

Lakini licha ya umaarufu huo, ni watu wangapi wanafahamu jina Kurasini lilivyozaliwa?


Kurasini inatokana na neno "Cool Ras Inn."

Cool Ras Inn lilikuwa ni jina la sehemu ya watu kustarehe baada ya harakati za kutwa nzima za kuujenga uchumi na hasa watu weupe.

Eneo hili la starehe liliitwa hivyo kutokana na eneo lenyewe kwa ujumla kuwa na sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (Tazama kipande cha ramani)

Wakazi wengi wa eneo hili walishindwa kutamka "COOL RAS INN" na hivyo wakatamka KURASINI.

Upungufu huo wa utamkaji ulishika hatamu mpaka eneo lote likajulikana kama Kurasini.


 
TOANGOMA, NI TOANGOMA KWELI?

Toangoma ya sasa ni miongoni mwa maeneo maarufu sana ya Dar es Salaam.

Umaarufu huu unatokana na uwepo wa miundombinu bora ya kimakazi na mpangilio wa mitaa yake.

Toangoma ina mtaa maarufu wa Masaki ambao unaelekeza ilipo stendi kuu ya eneo hili la Toangoma, mtaa huu umejengeka vilivyo.

Wengi tunalifahamu jina hili la Toangoma, lakini huenda hatufahamu jina hili limetokeaje.

Jina Toangoma limetokana na wenyeji wa Dar es Salaam (Mzizima) kwa maana ya Wazaramo wa miaka ya kale ambao walikuwa wakitoka maeneo mengine ya uliokuwa Mkoa wa Pwani kama vile Kimbiji, Puna, Mwembe Mgodo, Kijiji cha Ujamaa Gezaulole, Mjimwema, Mwembe Mtengu na mengineyo ambao walikuwa wakikutana eneo hilo huku wakiwa na ngoma zao kwa ajili ya kuja kukutana na wenzao wa Mtoni kwa Aziz Ally, Buguruni na kwingineko.

Walipokuwa wakifika eneo hili la Toangoma walikuwa wakitua ngoma zao na kuweka kambi kwa muda. Walikula na kupumzika hapo kabla ya kuanza safari yao.

Kutokana na mazoea ya kukutana eneo hilo na "kutua" yaani kushusha ngoma zao kwa ajili ya mapumziko eneo hilo likajulikana kwa jina la "TUANGOMA".

Kadiri miaka ilivyosonga na muingiliano wa kijamii utamkaji wa 'Tuangoma' ulibadilika na kuwa 'Toangoma'.

Hivi ndivyo neno Toangoma lilivyotoholewa kutoka Tuangoma na kuwa Toangoma tunayoifahamu leo.

Source: Kona ya Wahenga.


 
KUTOKA MLONGA ANZILA MPAKA MLOGANZILA!

Mloganzila si eneo ama jina geni kwa baadhi ya watu ingawa wengi wetu jina hili ni geni masikioni mwetu.

Mloganzila ni eneo kilipojengwa Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Muhimbili (MUHAS). Eneo hili lipo Kisarawe mkoa wa Pwani.

Picha inayoonekana si ya Ulaya bali ni moja ya majengo ya Chuo hicho kilichojengwa kwa msaada wa Serikali ya Korea Kusini.

Kona ya Wahenga tulipata nafasi ya kwenda kutembelea eneo hili na tulipenda kufahamu asili na maana ya neno Mloganzila. Tulikutana na Mzee mwenyeji wa eneo hili na alitueleza yafuatayo;

"Jina Mloganzila linatokana na uwepo wa Bwana mmoja miaka hiyooo ambaye wengi hatukumjua jina lake halisi mpaka alipofariki."

"Bwana huyu alikuwa pandikizi la mtu lililoshiba hasa, alikuwa na misuli iliyotokeza na mikononi mpaka miguuni. Alikuwa na vigimbi na kifua kipana kama Simba. Licha ya umbo hilo kama mbuyu Bwana huyu alikuwa mkimya na mpole sana, watu wengi tulimuogopa kwa kweli."

"Bwana huyu alikuwa akipenda sana kuimba na kuongea njiani akiwa peke yake huku ameweka shoka, jembe na panga lake begani. Alitembea mithili ya askari wapitao mbele ya Rais kutoa saluti."

"Kutokana na kile kitendo chake cha kuongea njiani ndipo sisi wazaramo kwa lugha yetu tukawa tunamuita " MLONGA ANZILA" tukimaanisha "Msema njiani." Jina hili lilikuwa sana ikafika wakati hata watu wa Kibaha, Kiluvya,Kongowe na Mlandizi walimfahamu. Yaani ilikuwa ukiuliza tu kwa Mlonga Anzila hata mtoto mdogo alikuwa anakupeleka."

"Miaka ilivyosonga na kuingia kwa wazungu kulipelekea kubadilika kwa uhalisia wa jina hili. Wazungu walishindwa kutamka neno Mlonga Anzila na wakatamka Mloganzila. Athari hiyo iliendelea mpaka leo hii."

"Kwa hiyo vijana wangu hiyo ndiyo asili na maana ya neno Mloganzila. Ni matumaini yangu mmeridhika."

Kona ya Wahenga tunasema asante Babu kwa kutupatia asili na maana ya jina ama neno Mloganzila.

Tuendelee kujuzana.


 
UFAHAMU MTAA WA UHURU DAR ES SALAAM.

Mtaa wa Uhuru ni miongoni mwa mitaa maarufu na mikongwe ya jiji la kibiashara la Dar es Salaam.

Ukiwauliza watu wengi toka mikoani wanapofika Dar es Salaam mitaa ya kwanza kuanza kuifahamu watakwambia ni Mtaa wa Uhuru na mwingine Msimbazi.

Lakini je ni wangapi wanafahamu kuwa Mtaa wa Uhuru (Uhuru Street) ulikuwa hauitwi hivyo awali?

Uhuru Street kabla ya kuitwa hivi ulijulikana kama KICHWELE STREET, hili ndilo jina lake la awali.

Wazee wanaeleza kuwa eneo la mtaa wa Kichwele lilitokana na mama mmoja maarufu kwa kuuza ndizi kipindi hicho alipokuwa akiuza ndizi zake mpaka mida ile ya jua kuzama na watu kumuuliza 'mama huendi kwako muda umeshaenda sana' nae alikuwa akiwajibu kwa lugha inayoelezwa kuwa ni kiluguru ama kikutu akisema 'kinichwele hano' yaani jua litanichwea hapa.

Watu wakawa wakihitaji ndizi wanaambiana 'kanunue kwa mama kichwele' na hapo ndipo eneo hilo lilipopata jina.

Mtaa huu ulibadilishwa kutoka Kichwele kwenda Uhuru kutokana na Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kupita Pugu Road (Sasa Nyerere Road), Buguruni, Ilala mpaka kufika Lumumba wakati akitoka Umoja wa Mataifa UN (Kipindi kile unajulikana kama UNO yaani United Nations Organization) kudai Uhuru wa Tanganyika.

Wazee wengi watakumbuka jinsi walivyotembea kwa miguu kutoka Uwanja wa Ndege wa Zamani (Terminal 1) huku wakisindikizwa na nyimbo maarufu ya kabila la Wazaramo iliyojulikana kama BABA KABWELA UNO (Baba karudi kutoka Yuno yaani UN).

Hivyo kubadilishwa kwake kulitokana na kutoa heshima kwa harakati za kudai Uhuru wa Tanganyika na baadae Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Picha inayoonekana ilipigwa mwaka 1910 yaani hapo hata Vita vya Pili vya Dunia [World War II (WWII)].

Karibu tukujuze.

Kona ya Wahenga.

 
UNAJUA "FIRE" PALIKUWA PANAITWAJE?

Vijana wengi wa Dar es Salaam leo hii ukiwauliza "Unapafahamu MWEMBETOGWA?" watabaki wanakuangalia tu kwa mshangao.

Sasa kuanzia leo noamba mfahamu kuwa sehemu ambayo siku hizi inajulikana kama "Fire" au 'Faya' pale ambapo kuna traffic lights zinazoongoza gari za kwenda/kutoka Kariakoo kuelekea Muhimbili na kwenda/kutoka Jangwani/Magomeni kuelekea Posta ile sehemu enzi zetu ilikuwa ikiitwa Mwembe Togwa.

Kwa nini paliitwa MWEMBETOGWA?

Kwa sababu, kwanza palikuwa na mwembe mkubwa pili, pakiuzwa togwa fulani maridadi sana.
Vijana wengi wa Dar es Salaam kipindi kile tulipenda kwenda pale kujiburudisha na kinywaji hicho murua.

Haya sasa nadhani mmefahamu kuwa pale FAYA palikuwa pakiitwa MWEMBETOGWA.
 
Unajua kwamba eneo la MNAZI MMOJA Dar es Salaam miaka ya 1960-1970 lilikuwa maarufu kwa jina la TUA TUGAWE?

Unajua jina hilo lilipatikana vipi?

Jina hilo lilitokana na uwepo wa wababe wa mji enzi hizo katika eneo hilo ambao walikuwa wakiwasubiri kina mama wanaopeleka vyakula kwa mafundi na kuwapora.

Kina mama walipofika maeneo yale na vyakula vyao waliambiwa "Hebu TUA TUGAWE". Jamaa walijipakulia vyakula vyao kisha kuwaachia kina mama vilibyobaki.

 
17021796_447433318981356_6688860930682555036_n.jpg


The Revolutions hao! Unamuona Wazir wa Njenje aliechuchumaa! Dula wa Tatunane(wa pili kulia) Wadau wa zamani malizieni wakiobaki!
Kutoka kushoto:
Steven Mnguto, Mohamed Mrisho (Moddy), Joseph Rebello, Teddy Mbarak, Marehemu Chukky Salim, Abdallah Omari(Dullah), Mabrouk Hamis(Babu Njenje).
Aliechuchumaa: Waziri Ally.
Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri Ally picha hii walipiga maeneo ya ilikuwa Kilimanjaro Hotel mwaka 1982
 
Back
Top Bottom