Uzi maalumu kwa ajili nyimbo za injili za zamani(Old school Gospel songs) za Tanzania!

Uzi maalumu kwa ajili nyimbo za injili za zamani(Old school Gospel songs) za Tanzania!

Hii mingine miwili

1. Parapanda ya Bwana italia siku ile
Atakaporudi Yesu kuchukua kanisa lake
Tujitayarisheni, siku hiyo ya kutisha
Ole kwa wale wote, wasiomuamini Yesu

Ndipo Bwana atasema ondokeni kwangu,
Ninyi nyote mliolaaniwa na Baba yenu,
Wataomboleza na kusaga meno, watakapotupwa kwenye moto wa milele....

2. Unafikiria nini, ulimwengu ni wa shida
Tena unajidanganya wewe, na mambo ya ulimwengu

Kanisani umeacha ulikuwa unategemewa. ...............
Uko vizuri mpendwa Bwana Yesu asifiwe
 
mwenye nyimbo za kwenye album ya Rafiki pesa anisaidie aise
Huyu jamaa alikuwa anaitwa chande nadhani
Nilikuwa na rafiki yangu
Rafiki pesa tulipendana sana
Maisha yangu yalikuwa mazuri
Nitakacho hunipatia
 
Kuna wimbo unaimbwa
Katika maisha yetu bwana yesu ni jawabu katika shida zetu ndiye yeye bwana wetu tusifadhaike.
shida zetu zoye yesu ata zibariki na kutupa raha nyingi siku zote.

Huu wimbo mwenye nao naomba hautupie na anayejua eameimba kwaya gan anisaidie.
 
Cosmas Chidumule!
Yanini Magonjwa!

Hizi ndizo kweli 'Old is Gold'
Mkuu kuna baadhi wanaomba nyimbo za siku hizi/New or Latest
Ombi Mkuu unaweza tenganisha hili ukawa na ' Nyimbo za Injili - Old is Gold na New or latest Gospel'
Tusichanganye mambo Mkuu tafadhali maana kuna muziki wa Injili wa kutangaza injili na muziki wa Injili biashara. Kuna Mkuu mmoja alisema ' huu ni muziki wa Injili kweli tuepukane na wapaka poda'
 
Hizi ndizo kweli 'Old is Gold'
Mkuu kuna baadhi wanaomba nyimbo za siku hizi/New or Latest
Ombi Mkuu unaweza tenganisha hili ukawa na ' Nyimbo za Injili - Old is Gold na New or latest Gospel'
Tusichanganye mambo Mkuu tafadhali maana kuna muziki wa Injili wa kutangaza injili na muziki wa Injili biashara. Kuna Mkuu mmoja alisema ' huu ni muziki wa Injili kweli tuepukane na wapaka poda'
Unapendekeza New School Tuweke za Kuanzia Miaka Ipi?
 
Back
Top Bottom