Uzi maalumu wa kumpongeza Rais Samia kwa miaka miwili akiwa madarakani

MHE. MARTHA N. GWAU - MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA MADARAKANI "SINGIDA TUNASIMAMA NA SAMIA"

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Mhe. Martha Nehemia Gwau katika kuadhimisha Miaka Miwili ya Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Madarakani amesema "Singida Tunasimama na Samia"

"Kwa niaba ya Wanawake Mkoa wa Singida, natumia nafasi hii kukupogeza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutimiza Miaka 2 tangu ulipoapishwa kuwa Rais wetu" - Mhe. Martha Gwau(Mb)

#SingidaTunasimamaNaSamia
#SingidaTunakupaHongera
#KazIendelee
 
Mengine sawa kama anajitahidi ila kwenye kilimo hakuna kilichofanyika Bashe anawambia vijana kulima Zabibu wakati sisi tunataka mchele,Mahindi na maharagwe kwenye kilimo Samia na waziri wake wamefeli sana zaidi2 ni mradi tu wa kupiga hela huo.
Diplmacia hakuna kitu kaleta maridhiano,leo hii Chadema wanatangaza kuunga mkono ushoga na rais yupo Kimya tu,diplmacia gani hiyo?.
Yaani tuna rais yeye kageuza nchi shimo la taka tu ilimradi apate tu mikopo na hiyo mikopo inashia tu midomoni kwa watu na kununua MaV8.Mwambien kwamba nchi imekwama ajitafakari haache kucheka na manyani Ata wekwa kwenye historia mbili muhimu
1:kuwa rais wa kwanza Tanzania mwanamke.
2:chama kufia mikononi mwake.
 
Nenda kalime kwenu Burundi
 

"MIAKA MIWILI YA RAIS Dkt. SAMIA MADARAKANI, TUKUTANE ISAKAMALIWA, IGUNGA."

Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa anawakaribisha Wananchi wote kwenye Mkutano wa hadhara utakaofanyika kwenye Viwanja vya Senta ya Kijiji cha Isakamaliwa, Jimbo la Igunga tarehe 25 Machi, 2023 kuanzia Saa Nne Asubuhi.

Mheshimiwa Ngassa (MB) atatumia Mkutano wa hadhara kueleza kwa Wananchi Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na mafanikio ya Miaka Miwili ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha Mheshimiwa Ngassa (MB) atazindua ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isakamaliwa.

"KAZI NA MAENDELEO"

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga
24 Machi, 2023
 

NUKUU ZA MBUNGE WA JIMBO LA IGUNGA NICHOLAUS NGASSA KWENYE MKUTANO WA KUELEZEA WANANCHI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) NA MAFANIKIO YA MIAKA MIWILI YA UONGOZI WA Mhe. Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ULIOFANYIKA KIJIJI CHA ISAKAMALIWA.

"... Ndugu zangu, Miaka Miwili ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Wetu, Jimbo letu la Igunga, Tumepata Fedha za Ujenzi wa Barabara za Mjini, Vijijini na Madaraja, Tumesambaza Maji ya Ziwa Victoria kwenye Vijiji na Vitongoji, Tumesambaza Umeme Mjini na Vijijini na kwasasa Mkandarasi anaendelea kuvifikia Vijiji vichache vilivyobakia, Tumejenga madarasa kwenye shule za Msingi na Shule za Sekondari, Tumejenga Maabara, Vituo vya Afya na Zahanati, Tumejenga Wodi ya Wagonjwa Mahututi (ICU) na Wodi ya kisasa ya Mama na Mtoto kwenye Hospitali yetu ya Wilaya na ivi karibuni Serikali imetuletea Mashine ya Mionzi ya kisasa (Digital X Ray)..."

"... Aidha Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imeendelea na Sera ya Elimu bila Malipo kuanzia Darasa la Kwanza mpaka Kidato cha Sita. Serikali imetupatia ruzuku ya pembejeo za kilimo, mikopo kwa vikundi vya kina Mama, Vijana na Ndugu zetu wenye Ulemavu..."

".... Vijana Wetu wa Igunga waliopata fursa kwenda Vyuo Vikuu wameendelea kupatiwa Mikopo ya Elimu ya Juu, Maafisa Ugani na Watendaji wa Kata wamepatiwa Usafiri (Pikipiki) kwa ajili ya kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kiutendaji na Walimu Wetu wamepatiwa vishikwambi ili kuwasaidia katika majukumu ya Ualimu..."

"... Ndugu zangu ni Mambo mengi tumeyafanya kwenye utekelezaji wa Ilani ya CCM na Miaka Miwili ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Wetu. Tunaomba muendelee kutuunga mkono katika utekelezaji wa Ilani yetu, Tumuombe Rais Wetu na wasaidizi wake Mwenyezi Mungu awajalie afya njema na nguvu katika kuliongoza Taifa letu la Tanzania..."






"KAZI NA MAENDELEO"

Imetolewa na:
Nassor Saleh Amor
Katibu wa Mbunge
26 Machi, 2023
 
Limebaki moja tu. La Igunga kuwa makao makuu ya mkoa wa Igunga...
 
Ujinga mtupu. Katibu wa mbunge unaandika vitu vidogo kama hivi unaita mafanikio? Jinga kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…