Uzi maalumu wa kuweka tetesi na Taarifa za usajili Ligi Kuu ya NBC kwa msimu ujao 2022/2023

Mwaka jana alivua bukta akabaki na chupi yeye kama yeye. Safari hii atamvu Manara na yeye mwenyewe afu watatembea uchi na Manara ili kuonesha mapenzi yao kwa timu na Mashabiki kwa ujumla.
 
timu nzima ya Mikia aka Makolo FC ni mbovu na inafaa itimuliwe yote kwa kukubali kupasuliwa na Feisal na kusababisha mashabiki wake kujazana mahospitalini kutibiwa majeraha ya moyo!

pia wawatimue MOooo, Barabara na Matofali
Hhahhaa hapo kwenye Mo wakikusikia mi simooo
 


Vyanzo vinadai kwamba Al Ahly wanataka kumtoa Miquisone kwa mkopo. Simba wameonesha nia ya kutaka kumchukua ingawa inaelezwa pia Kaizer Chiefs wanamtolea macho. Kwa sasa Miquisone ni majeruhi.

Kazi itabaki mikononi mwa viongozi wa Simba.
 
Tukiwa tunaelekea Ukingoni mwa Ligi kuu Tanzania Bara, Dirisha La Usajiri linatagemea Kufungulia Mwezi Juni Kuanzia Tarehe 14. Dirisha la Usajiri litaenda Hadi Msimu wa Ligi kuu Utakapo Tarajia Kuanza.

Club Tayari zimeanza kuachana na Wachezaji pamoja na Makocha Wao…. Hatua Inayo toa Mwanga kwa Wachezaji kuanza kutafuta Timu na Makocha kuanza kutafuta Timu za Kufundisha.

Tayari Simba Imeachana na Pablo Franco Martin kocha wao mkuu na sasa timu ipo chini ya Kocha Msaidizi.

Yanga wamesha Achana na Mchezaji wao Saido Ntibanzokiza na sasa yupo huru.

Tuwe kwenye huu Uzi kwa Tetesi na Taarifa kamili za Usajiri wa Timu za Ligi kuu Tanzania Bara. Kuweza kupeana Taarifa Zilizo na Zisizo Rasmi.

NB: Huu Uzi ni Kwaajiri ya Timu za Tanzania, wachezaji wanaondoka Tanzania Na Kujiunga pia na Timu za Tanzania Zitakazo shiriki Ligi Kuu Msimu Ujao.
 
Hizi taarifa za singida big stars kama ni kweli itapendeza
 
Mayele naye ameanza kutikisa kiberiti Yanga...……………….!
 
Ushauri wa bure wananchinkama mnataka kuingia hatua ya makundi champions leagu tukamnunue yule beki wa wydad....alikochafua sana kwenye final
 
Farid Mussa anahusishwa na kujiunga na Simba Sports Club. Je Wananchi watakubali kumuachia. Simba atawasaidia kama dili likitiki?

 
Farid Mussa anahusishwa na kujiunga na Simba Sports Club. Je Wananchi watakubali kumuachia. Simba atawasaidia kama dili likitiki?

View attachment 2249259
Ahmed Ally kaongea shombo kuwa hawasajili mchezaji ambae hajafika Robo Fainal CAF,watu wakamuuliza wakina Kibu,Gadiel,Mhilu na wengineo walifika Robo final ipi ya CAF,kakimbia akaunti yake.
 
Fiston Kalala Mayele anatakiwa na Ibenge Berkane taarifa zinasema jamaa pale ana mwaka mmoja jmebaki , hivyo lolote linaweza kutokea.

 
Ni mzuri ila injury zinamsumbua sana simba wanahitaji straiker, huyu na Cesor Manzoki ndiyo wapo kwenye makaratasi ya simba hadi mda huu

Anaitwa Samir Nurkovic

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…