Uzi wa kijobless na mbinu za kidigree (utatu wenye utata

Uzi wa kijobless na mbinu za kidigree (utatu wenye utata

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
UZI WA KIJOBLESS NA MBINU ZA KIDIGREE
(Utatu wenye utata
1737457439984.jpg
)

GAP YEAR......!!!

Kati ya mwaka 2017_2018, inaweza kuwa mwanzoni au mwishoni mwa miaka hio kumbukumbu zangu hazijakaa vizuri.

Nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni ya kusambaza vinywaji. Yaani mimi ndio nilikuwa natembea na gari kusambaza vinywaji vijijini.

Ndio Mimi nilipewa eneo la vijijini kuhakikisha vinywaji vinasambaa kila kijiji. Nilikuwa afisa mauzo wa upande wa vijijini.

Ilikuwa ni pombe, nilisambaza ile pombe mpaka vijana wa vijijini wakaacha kulima, wakawa walevi waliokubuhu. Hapo kuna kukubuhu na kupindukia sasa wale vijana walikubuhu.

Ile pombe ilikuwa inatengenezwa mkoa mmoja tu, na huo ambao uliwekwa kuwa wa majaribio kabla haijaanza Tanzania nzima.

Kiufupi ile pombe ilifungiwa, sijui sababu hasa ni nini lakini ikafungiwa kiwanda kikafa. Hapo ndio tunapata hio GAP YEAR.

GAP YEAR ni kipindi ambacho unakaa unakuwa huna kazi ya kufanya, huna shughuli yoyote kiufupi kichwa chako kinakuwa karakana ya shetani.

Baada ya kampuni kufungwa, mimi nilikuwa nimepanga mjini, nyumba kubwa tu. Basi kwenye ile nyumba tulikuwa tunakaa watu wanne. Mimi, Familia mbili na Mdada mmoja alikuwa hajaolewa.

Huyo Mdada tumuite Kamsi. Kipindi nakaa kwenye nyumba hio nilikuwa nakaa na mpenzi wangu yeye tumuite Uche.

Hata hivyo mimi nilikuwa sio mtu wa kushinda nyumbani sana kwa mwezi naweza kushinda mara mbili au moja.

Kipindi kampuni inafungwa Uche alikuwa amepata kazi mkoa mwingine hivyo katika hio GAP YEAR nilibahatika kuweka mazoea na Kamsi.

Kamsi alikuwa mpole, hakuwa kama wadada wa mjini wale wengine. Lakini Kamsi alikuwa analala ndani na analipa kodi anavaa na anakula nyie Dunia inamaajabu.

Tuachane na maajabu ya Kamsi. Basi Kule alikokuwa anafanya kazi Uche ile kampuni ilikuwa inatoa rikizo kwa mwaka mara moja tu.

Hapo ni miezi mitatu toka Uche aondoke. Kama nilivyosema awali kichwa kisichokuwa na kazi ni karakana ya shetani.

Nikawa namtaka Kamsi, lakini nitampataje Kamsi na anamfahamu Uche. Nikaja na mpango mahususi wa kijobless zaidi.

Basi nikaanza kurusha ndoano zangu kwa Kamsi, lakini kila nikirusha zinagoma Kamsi anadai anamjua mtu wangu na hataki kuharibu mahusiano yangu.

Nikaona huu ni mwezi wa tatu na Uche kupata likizo ni mwezi wa 12, I mean nina miezi tisa ya kupiganisha hapa katikati ikabidi nimkane Uche.

Nikamwambia sikia Kamsi Uche ni moja ya wanawake washenzi sana, katoka hapa kaenda huko kupata kazi kaolewa na mfanyakazi mwenzake😭😭😭

Nikaanza kulia, hapa nilikuwa nalia baada ya kukumbuka sina kazi na kodi inakaribia kuisha weeeee weeee wee nililia na mengi.

Kamsi akawa ananibembeleza kwa kunipa pole bhana.

Kuna rafiki yangu wa kike anaitwa Joy. Siku mbili mbele nikampigia Joy nikampa mpango.

Nikamwambia Sikia joy nakupa hii namba ya Mdada anaitwa Kamsi, mpigie mwambie unaitwa Uche. Then mwambie ni kweli umeolewa uko jifanye unajutia kwa ulichonifanyia, then mwambie mimi ni husband material hivyo kama anaweza awe na mimi hakuna shida.

Basi bhana joy ni mwana sana sio kama josh, lakini wait hawa wawili majina yao yanaanza na Jo hawa me siwaaminigi mjue, joy sio josh wa kiume kweli hebu tuone.

Basi kweli siku tatu mbele Kamsi akawa ananambia kuwa kaongea na Uche, kumbe kweli kaolewa hivyo kunibembeleza kwingi like utapata mwingine.

Basi bhana Kamsi akaanza kuwa karibu na mimi. Wiki moja mbele akanambia jumapili nitakuja kukutembelea.

Nikashangaa huyu Kamsi tunakaa nae nyumba moja anasema jumapili atakuja kunitembela, weeeee hapa lazima unyama nipate.

Eeh mnasemaga sijawahi fanikiwa kupata DEMU na hapa nimefanya nini mtoto Kamsi kanasa kwenye mtego mwenyewe makofi kwa joy tafadhali.

Siku masaa yakapita, kweli bhana Jumapili hii hapa ikafika, nikaenda kununua kuku, soda, wine na nikapika pilau.

Toka asubuhi me sikumuona Kamsi bhana, mimi sikujali nikapika niliungua sana siku ile lakini kwa upendo wangu kwa Kamsi sikujali.

Vitu vikaiva bhana vinanukia kwelikweli. Basi saa tisa hivi ugeni mzito ukafika kwangu.

Guess what..... Alikuwa na JOY, KAMSI NA UCHE.

WEEEEEEEEEH WEEEEEEEEEH, wimbo wa KASONGO ulipiga kichwani wote ukaisha ndani ya sekunde, nikabaki nimesimama mlangoni.

Mnakumbuka nilisema ile nyumba kodi ilikuwa inaelekea kuisha🥹🥹

Ninachoweza kuwaambia ile ndio ilikuwa siku ya mwisho mimi kuonekana pale,. nilihama nyumba ile bila kuchukua chochote, Kiufupi SIKU ILE NILIKIMBIA KAMA SWALA 😂😂😂

nikarudi nyumbani mwenda kwao sio mtumwa 😂.

Lakini hawa wakina JO wanashida gani wakuu.

Kilichokuwa kinafanyika kumbe Kamsi na JOY. Ni marafiki, pia Kamsi na Uche ni marafiki na mimi sikuwa najua yote hayo.

Hapo ndio ilikuwa mbwa Kala mbwa.

Siku hiyo hiyo naona wameniunga kwenye group la Whatsapp bhana, wanajiita THREE WIFE ONE HUSBAND.

alafu Joy akaweka status akasema LEO NIMESHIBA KAMA MAMBA😭😭 Umeshiba kwa chakula la nani ubwa wewe.

Kule kwa group walikuwa wanasema hawaondoki mpaka mimi nirudi tuyajenge. Muyajenge na nani kwani mimi Fundi...?

Nimerudi nyumbani, huku nyumbani nikazua msala mwingine. Huu ni mkubwa zaidi ya nilio ukimbia weeeeeeeeeh ikabidi nirudi kwangu. Maana wale majamaa walikuwa serious hadi wakalipia kodi ya miezi sita wakaamia kwangu kabisa.

Narudije kule, mpango sio mpango kama huna mwana kama Nango....!

wait for part two( it's not over until it's over ).

Pichani ni mimi nikiwa kwenye kuandaa DIKO LA KAMSI👇👇👇👇
 
Ipo hivi....

Wakati upo shuleni ulikuwa unaona mtaani fursa nyingi sana.Kipindi unasoma ulikuwa unaona wanaokaa mtaani hawana kazi ni wazembe sana

Sasa siku hizi wewe umemaliza shule upo mtaani hata zile fursa ulizokuwa unaziona pindi unasoma zimekimbia😂😂 hadi unatamani ungekuwa na daftari uziandike ukimaliza shule uanze kuzishughurikia tu😂😂.

Saivi wewe ndo umekuwa unatafuta connection kuliko connection yenyewe

Kitu ambacho ulikuwa hukijui kipindi hicho ni kwamba.....

Maisha ni kama ndoa tu.Walio ndani ya ndoa wanaona mabachera wanafaidi wakati mabachera wanaona walio oa wanafaidi.hapo kila mtu anaona mwenzake anafaidi kama wewe unavyoona wanafunzi wanafaidi saizi😂😂😂

NB;Wale tuliolingana umri punguzeni kufanikiwa wanangu jamii inaniona Mimi Mzembe hukuu

😂😂😂😂😂😂🏃‍♂️
1737457783560.jpg
🏃‍♂️🏃‍♂️
 
UZI WA KIJOBLESS NA MBINU ZA KIDIGREE
(SIX DADAZ)

Nipo kwenye ukurasa wa facebook naperuzi huku nikilike picha za wadada ambao niliwaomba urafiki.

Hii ni baada kukimbia msala wa kina Uche. Hapa nimerudi nyumbani kupumzika si mnakumbuka niliwaambia mwenda kwao si mtoro.

Sawa, mara naona inakuja picha ya wadada sita wakiwa wamevaa sare, shati jeupe n vigauni vifupi vinaishia juu ya mapaja.

Nailike ile picha nakuendelea na kushuka chini, lakini kuna kitu kinanambia acha ufala kaziangalia zile pisi vizuri. Napandisha haraka kwa spidi ya ngiri mkia juu hadi naipata ile picha.

Naingia kwenye page ya Muhusika. Tumuite Linah.

Picha inavutia sana naangalia kwa umakini nagundua katika wale sita kuna wawili nawajua, sina mazoea nao ila nilikuwa nawaona tu.

Maana niliwaacha madarasa kama matatu sekondari, ila mmoja huyu yeye tulimaliza nae japo pia sina mazoea nae.

Wakati wenzangu wanaozoea na wadada shuleni mimi nilikuwa naona wanashobo, kumbe ndio wanatengeneza connection hivyo. ningekuwa na mazoea na huyo Mdada isingekuwa tabu mimi kuwazoea wale six dadaz. Sio kesi tuendelee.....

Nikaona sio kesi acha nicomment.

"Linah mambo" eeh kwani alijibu sasa labda kama nilijijibu mimi.

Nikaona sio mbaya kwakuwa kwenye ile picha aliwatag wenzake nikawatafuta wote inbox.

Mungu ni mwema wawili kati ya sita wakajibu, nikaomba namba ya simu. Mmoja kati ya wawili akanipa ok hatua ya kwanza done. Twende hatua ya pili.

Kwanza mpaka muda huo sielewi ni nini nakitaka kwa hawa six dadaz me nimechukua tu namba ya simu.

Kikawaida nina namba 4 hadi 6. Lakini ninazotumia sana ni mbili. Facebook nina account tatu ila ninayo tumia sana ni moja.

Hata mtu akiniuliza za nini mimi mwenyewe sijui ila tu nilijikuta ninazo.

Basi huyu alienipa namba tumuite ENJO.

ENJO nikamtafuta kwenye namba nyingine tu sio ninayotumia mara nyingi, nikawa nachat nae huko na pia nikawa napost mambo ya picha picha sana.

Basi huyu ENJO akajua mimi ni cameraman, hivyo akaanza kunitafuta sana tukawa tunachat sana, status zake alikuwa anawapost sana wenzake wale dadaz.

Wakati huo mimi sitaki kabisa maswala ya wadada akili yangu bado haijapoa na yale maswala ya kule nilikotoka, pia wakati huo laini zangu zikawa hazipatikani natumia hizi nyingine tu ambazo Uche hana namba zake.

Taratibu taratibu nikaanza kuzoeana na wale member wengine wa six dadaz, sijui ikawaje yani sijui nikajikuta nina namba zao wote.

Tukawa tunachat mambo safi, shavu likaanza kuja kitambi ndio hicho sasa. Ni miezi miwili yanatokea yote haya. Hapo hata wazo la kurudi kule kwangu likawa halipo.

Katika mazoea haya kuna Mdada mmoja ndio alikuwa kama queen wa group huyu tumuite Suzy. Hapo wanabaki wanne hatuwajua si ndio.

Baada ya mazoea nikaona acha nipiganishe kwa Suzy nijipoze hapa kwanza. Nikaanza kurusha ndoano kwa Suzy. Mambo hayakuwa rahisi kama ninavyofikiria aiseeee

Lakini Mungu sio mwanadamu Suzy akakubali, lakini wakati huo huyu Linah kumbe alikuwa ananipenda ila anashindwa kuniambia.

Hivyo alivyokuja akasema ooh sijui sisimizi kameza ndovu nini sijui mara ooh usinichukulie hivyo me nakupenda.

Kwanza wakati nakubaliwa na Suzy aliniambia nisiwaambie wengine, wakati nini namkubali linah nikamwambia asiwaambie wengine

Ok six dadaz wawili done, bado wanne. Lile kundi lilikuwa na wadada wazuri jamani hata kama ungekuwa wewe tu usingevumilia.

Nikaanza kwa mwingine huyu alikuwa anaitwa Paulina. Huyu hakuwa na mambo mengi kama wenzake kwanza alikuwa wakishua kinoma yani nasikia baba ake anamiliki bunduki. Huyu nikaanza nae mazoea kwa kumleta vizawadi zawadi mara suprise kibao mwisho Mdada akafall nae makubaliano ni yale yale USIMWAMBIE MTU.

50/50 sio mimi sio mswati ni Sanga madigree. Wakabaki wawili Jasmine na Irene.

Kumbuka baada ya kuwapata hawa wanne kule kwenye group lao walikuwa wananisifia sana. Hivyo wananisifia lakini kila mtu anasema sitoki nae, zile sifa zinafanya Jasmine aanza kujileta kwangu akizani nina maajabu.

To make story long shot, jasmine na ireni niliwapata pia. Hapo mimi ndio nikawa KING OF SIX DADA'Z.

kilichonisaidia mimi ni ile kauli ya USIMWAMBIE MTU😃😃.

siku zikaenda siku zikarudi, birthday ya Paulina ikafika.

Sasa hapa kila mmoja alikuwa ameachana na mpenzi wake, wanaume sita waliachwa kwa ujinga wangu🥲🥲.

Wote sita wakaniambia siku ya birthday ya Paulina nataka nikutambulishe wakujue.

Kumbuka hapo wameachana na wapenzi wa maisha yao, alafu kule kwenye group walikuwa wanatambishiana kuwa siku ya birthday ya Paulina nawatambulisha shemeji yenu mpya ni suprise.

Suprise yenyewe ndio mimi nilienusulika kutolewa roho na wakina joy na Uche.

Siku ya shughuli ikifika ukumbi ukakodiwa......

Kabla ya siku hii kufika nikurudishe wiki moja kabla, kila Mdada alikuwa anataka nivae nae sare, kwahiyo kuna tulioshona sare, pia wengine tukanunua nguo za dukani sare, walinunua wenyewe me sina hela bhana.

Basi siku husika ikafika nikasema leo nipo ni kuumbuka bhana, kumbe sijui Jasmine aliwashwa na nini akasema kwenye group kuwa tunadate. Yaani majina yanayoanzia na kina J bhana.

Wee si ndio kila mtu akawa anasema anatoka na mimi kwa nini kwenye group pasichangamke.

Kumbe BIRTHDAY girl baada ya kusikia vile pressure ikapanda akazimia, mzee wake akapewa taarifa si niliwaambia anabunduki, huku hawa watano wakakodi vingoma waje wanisute kwa mzee Sanga.

Hali ikawa si hali naenda wapi sasa, wakati huo nikairudisha ile laini hewani ambayo nilikuwa siitumii. Nikakuta sms nyingi za uche akisema nirudi kashanisamehe.

Mimi ni nani niendelee kubaki nyumbani wakati nimesamehewa bhana.

"Nimefutiwa deni, nimefutiwa deni mwenzenu SIDAIWI TENA"haka kawimbo kalikuwa kanapiga kichwani. Nakuwekea kwa comment ukasikilize.

Kumbe mzee Wangu nae kapata taarifa ya kilichotokea mji mzima unajua, hapo nikapanda gari kurudi kwangu.

Kwa kina joy wapo watatu JOY, UCHE NA KAMSI hawa ni nusu Shari huku nyumbani wapi sita si ndio Shari kamili.

Kwakweli nikaona kheri nusu Shari kuliko Shari kamili.😃😃

Safari ikaanza kurudi kwangu bhana, safari ya masaa sita niliona kama dakika mbili weeee tukawa tumefika.

Kwakweli usilolijua ndio usiku wa kiza sio. Kumbe Kamsi anaurafika na Six dadaz. Unakumbuka nilisema anakaa ndani hafanyi kazi ila anaishi kumbe Paulina na Kamsi ni ndugu. Huku yupo kusimamia biashara zakina Kamsi tu, na mchezo mzima amesimuliwa kila kitu anakijua.

Ile mimi nafika tu pale nikaingia ndani nikamkuta Uche peke yake akanikumbatia mara mlango ukafungwa....

Mimi nilijua ananikumbatia kanimiss, kumbe mwenzangu ananishika vizuri nisikimbie.

Kushoto kulia KAMSI NA JOY, SIJAKAA VIZURI SIX DADA'Z WAKAINGIA wakati huo wapo watano.

Kumbe Kamsi aliwaambia naenda kule.

Mara nasikia wanasema mzee wake Paulina yupo njiani anakuja....

HAYA KUMEKUCHA KUMECHANGAMKA WAMENIWEKA MTU KATI AWEEEEEEEEEH......

(labda kama kut
1737457821361.jpg
akuwa na sehemu ya tatu)

Pichani ni mimi nikiwa nimezungukwa na kundi la watu tisa sijui kama kuna kutoka salama
 
Around 2014_2017 nilikuwa nafanya kazi kwenye duka la kuuza nguo huko mbeya.

Sasa mimi kikawaida nilikuwa nafika saa mbili dukani, siku nikiwahi sana nafika saa moja na nusu au nadakika arobaini.

Kikawaida soko lilikuwa linafunguliwa saa 12 asubuhi na kufungwa saa moja usiku. Kuna huyu mdada mmoja tulikuwa tunauza nae kwenye soko moja.

Kila siku nilikuwa nikifika sokoni lazima nimkute amefungua, siku nikikuta hajafungua basi siku hiyo haji kabisa sokoni.

Kuna siku nilikuwa narudi nyumbani jioni ndio nikagundua yule mdada anakaa karibu na ninapokaa mimi, yani kutoka ninapokaa hadi anapokaa yule mdada ni dakika tano tu.

Huyo mdada hatutashinda tukimuita mdada acha tumpe jina tumuite Belema.

Siku moja nilikuwa napita dukani kwake akanambia mbona umechelewa sana, nikamjibu hii ndio mida yangu ya kufika.

Wakati nataka kuondoka nikasema ngoja nijaribu bahati yangu, nikamwambia nipe namba yako uwe unaniamsha asubuhi niwahigi kuamka ili niwe nawahi kama wewe.

Kabla hatujafika mbali kipindi nachukua namba nilikuwa sina hisia nae kabisa nilikuwa namuona kama mshikaji wangu tu.

Akanipa namba, siku inayofuata saa kumi na moja akanipigia simu akasema yeye ndio anajiandaa hivyo na mimi niwe najiandaa anakuja kunipitia twende kazini.

Saa kumi na mbili na dakika kumi hivi akanipigia simu kuwa yupo nje, basi nikamkaribisha ndani akagoma, nilikuwa tayari nimejiandaa hivyo tukaondoka.

Kuanzia siku hiyo ndio ikawa ratiba yetu, asubuhi tunavyoenda kazini na jioni tunvyorudi kazini tulikuwa tupo wote.

Kuna kitu wazungu wanaita kudevelop filling kama sijakosea, huwa inatokea mtu ulikuwa humpendi au unamchukulia rafiki yako lakini ghafla ukaanza kumpenda kimapenzi.

Zile night walk na morning walk zikazalisha hicho kitu, sijui ni kwangu tu au hata kwake. Lakini alikuwa na wivu na mimi, na mimi nilikuwa na wivu na yeye.

Hakuna aliyewahi kumwambia mwenzake anampenda lakini asilimia 99 ya waliokuwa wanatuona pamoja walikuwa wanajua sisi ni wapenzi.

Long story short, Belema alikuja kuolewa na mtu mwingine kabisa, na alinilaumu sana kwamba alionyesha hisia zake kwangu lakini mimi nilishindwa kujiongeza, lakini hata mimi nilimwambia nilionyesha hisia zangu pia lakini yeye alishindwa kujiongeza.

Aliolewa na alihama mkoa, lakini kila mmoja alimpenda mwenzake ila ukimya ndio ulituponza.

Huyo mkaka&mdada unaempenda hebu mwambie huenda nae nakupenda 😁😁.

Akikwambia nilikuwa nakuchukulia kama kaka angu& dada angu mwambie unawajua ndugu
1737457926550.jpg
zako wote😂😂 huna dada kama yeye.
 
UZI WA KIJOBLESS NA MBINU ZA KIDIGREEE

Miaka ya nyuma kidogo, nilikuwa na date na mdada mmoja hivi. Huyu mdada tumuite Adola.
(sio jina lake halisi)

Huyu Adola alikuwa na rafiki yake mmoja mzuri sana, yule rafiki yake alikuwa na sifa za Wife material ninaemtaka. Kiufupi rafiki wa Adola ndio alikuwa mwanamke wa ndoto zangu.

Baada ya kumuona rafiki yake Adola ndio nikakumbuka ule msemo wa kabla hujamtongoza hakikisha unawajua marafiki zake wote 🥲.
Huyu rafiki yake tumuite Purity
(Sio jina lake halisi)

Basi kipindi mimi nadate na Adola alikuwa anapenda sana kumuongelea Purity na mara nyingine kuja nae mpaka nyumbani kabisa
(Ile niliyokuwa nakaa ni nyumba sio geto, maana ilikuwa na sifa za kuitwa nyumba. Ghetto wanakaa wakina Abyas Mzigua Kaisal Ally na Molito Brand na wewe hapo unaesoma nyie ndio mnakaa magetoni)

Siku moja nikachukua namba ya Adola ili nichukue namba ya future wife wangu Purity.

Kwanza Adola hakuwahi kunivutia kivile, basi tu wakati namfuata ni kama kila msichana aliamua kunikataa, nikasema nitadate na chochote ilimradi linapumua. Hicho chochote ndio Adola sasa.

Dakika, masaa, siku hatimaye miezi ikapita, namba ya Purity ninayo sijawahi futa. Kama bahati hivi Adola akawa ameondoka ameenda dar jiji la kitapeli.

Kufika dar akaanza kujikuta matawi sana mimi sio level zake, basi tukawa tumeachana, ikawa ni muda wa kwenda kwa Purity.

Remember Purity anajua kuwa natoka na rafiki yake Adola, maana hata kwenye simu kila mmoja alimsave mwenzake TWINIE. ila matwinie haya bhana.....

Purity namba yake ninayo na sijawahi mtafuta, nitaanzaje kumtafuta na akisema namba nimeipata wapi itakuwaje. Basi hapo nikaja na mpango kabambe ili isiwe ngumu kuingia kwenye maisha ya Purity

Kuna huyo rafiki yangu mmoja, yeye tumuita Josh.

Josh alikuwa ni mwanangu sana hajawahi kunisnich hata mara moja, alikuwa mwana mwana kweli.

Nikamfuata, nikamwambia kila kitu kuhusu huyo Adola na Purity.

Mpango ulikuwa hivi, mimi nitampa namba ya Purity ili achat naye na wakutane kama marafiki wakianza kuzoeana Josh aje anitambulishe mimi kwa Purity ndio nichukue namba. (Sijui kama mnaelewa nyie majamaa mmevurugwa na ada za januari)

Basi kweli mpango ukaenda kama ilivyokuwa bhana wakakutana, wakafahamiana wakawa marafiki, basi siku moja Josh akamleta Purity nyumbani.

Ikawa like

Josh😛urity meet my friend CRARENCY

Purity: wooooa waoooo kumbe ni huyu namjua ni shemeji yangu

Mimi kimoyomoyo (shemeji which, shemeji where who is your shemeji )

Basi siku hiyo ndio nikachukua namba ya Purity. Kwanza tukubaliane hapa mpango wa kuchukua namba ya Purity ulifanikiwa kwa asilimia 100. Chukua mbinu hiyo.

Basi wakati nachat na Purity alikuwa anapenda sana kuniita shem shem jina nilikuwa silipendi hilo, siku moja ikabidi nimwambie ukweli kuwa tulishabwagana na rafiki yake Adola saivi nasearch for new members.

Akanambia hilo mbona nalijua toka muda sana, nikasema ndio uache kuniita shem tupishe maisha mengine yaendelee

Akanambia mimi nakuita shem sio kwa Adola ni kwa rafiki yako Josh. Kwani hakukwambia kuwa tumeanza kudate.

Weeeeeeeeeee, weeeee, weeeee.

Anyway kumuuliza Josh kuhusu ilo akawa anasema lemi teli you samusing (let me tell you something) kale kasauti mnakajua, kama hukajui nakaweka status WhatsApp na facebook ukimaliza kusoma nenda kakaone.

Basi bhana wiki ijayo ni harusi ya Josh na Purity.

Nitamuomba Dj niingie na wimbo wa sio mwana sio mwana huyo sinichi sio mwana,😭😭😭 sijasema nina wivu mimi ila Josh......

Kitu najaribu kukuelekeza hapa ni kwamba wife wako yupo sehemu yoyote huenda huyo shemeji yako ndio wife& husband wako we jaribu bahati yako kama Josh.

🥲🥲🥲 Naandika huku naugulia maumivu ukicheka block inakuhusu.

Pichani ni mimi baada ya kuambi
1737458024885.jpg
wa Josh ndio sababu ya mimi kuitwa shem na sio Adola 😭😭😭
 
UZI WA KIJOBLESS

Usiwai mpeleka mdada kwenye restaurant yenye hujui bei ya chakula inavyokuwa UZI....🧵

Kuna hii siku nimetoka na dem wangu mali safi a girl fine yaani toto si toto kumpeleka out coz ever since we started dating sijai mpeleka hata out. Si me nika figure out nita mpeleka wapi kwanza place ya kukula juu yeye alikuwa used na hizi food za mgahawani so I needed her intestines to feel something different.

That day she wore her best outfits ungedhani tunaenda mahali ingine special sana ama kwa an important occasion,me nilikuwa nimeva tu hizi nguo zangu normal in fact hata nilizichukua kwa Kamba zenye alifua jana my friend. Kwanza nikasema si nimpeleke Uhuru park one day tukiachana akuwe akionyesha boy wake eti... kuna ex wake mwingine alimpelekanga Uhuru park kuona greatness. Mbele nyuma I wanted to spend like 100k kwa huyu dem coz kwa pocket nilikuwa na 250k niki add na fuliza ya 100k hapo inakuja kitu 350k. Si nikasema baas deal done I want to give her the best treatment she will live to remember.

Tulifika Uhuru park tuka zurura hapo ndani kwanza unajua madems huwa wanapenda ice cream sana nika mchukulia ya 3k na me nika take ile ya 1k just to quench our thirst. Nilikuwa naona venye ana enjoy kwanza kuna time nili mweka kwa merry-go-round akadhani amefika heaven na tuko tu hapa uhuru park.

Kidogo hivi naskia gaidi inaanza kunishow eti ako njaa sana so she needed something to eat. Kwa roho nikasema "si ndio amekula tu ice cream ya 3k like 30 mins ago how comes ashaanza kuskia njaa saa hii?" But anyway today was her day nikasema whatever mchumba wants,mchumba gets.

So si tulitoka hapo ndani ndio nisake a very fine hotel at least kwa maisha yake akuwe amekula vitu expensive once in a while before arudi kwa baba huko heaven. Ku check google maps,nikaangalia top rated hotels within good luck nilipata moja hapo baas sisi nayo kwa uber hadi kwa gate..

Hoteli yenyewe iko na parking kubwa jameni na magari za kifahari ndio wame park hapo mimi nime leta msupa wangu humu tu ndani tukiwa kwa uber, but siku tense since mwanaume ni kujiamini ama namna gani? Tuli seat place ingine hapo yenye iko na very fine view..

kienyeji kangu kakaanza kuchukua ma selfie na ku record ma short videos of course for them memories. One of the waitresses aka come na nika mshow "Can we have two bottles of water please?" Hiyo time si haka ka dem kangu kana kagua menu hapa since ye ndio nili mwambia a order anything I'll pay.

Maji ikafika then food ika follow,wueh kumbe dem ali order kuku full, butter nun, vanilla milkshake hadi na chipps. Bado siku tense sana coz nilipiga hesabu nikasema hii food haiezi pita 50k na juu niko na some 250k kwa mfuko, kila kitu iko sawa. Tulikula tuka maliza na bill ika come nashindwa hii ni nini refu hivi na sijafanya shopping..

My fren, total bill ilifika aje 450k? Hata sijashiba vizuri na wanataka nilipe 450k??? Dem naye hata ashtuki kazi ni kusokota meno na toothpick na hajui sina pesa ya kulipa hii food tumekula. Wakaona na delay manager akaitwa eti nimekataa kulipa bill ya food. Akaniita kando since hakuwa anataka kuni embarrass mbele ya watu na plus mbele ya dem wangu.

Aliniambia niwache ID,na simu yangu kwanza nipeleke dem home ndio nikujie hizo vitu zangu,si nikachukua dem vizuri as if nothing is wrong hadi home saa hiyo akili inapiga hesabu mbaya sana. Kuendea ID yangu na Simu niliskia tu "Ita askari na ufunge gate" Niliosha vyombo hapo one full week na ni mchana na usiku hakuna kurudi kwa nyumba ukisikia kulala unaeka mguu kwa maji.

Hapo ndio nilijua zoea maisha yenye unaishi,yaani ishi kwa league yako ningekula kwa mgahawa kama kawa hizi mashida zote hazinge nipata anywhere juu ya kutaka ku treat dem poa. Kama we ni wa mga
1737458221109.jpg
hawa,zoea tu hapo mzee.
 
Wote sita wakaniambia siku ya birthday ya Paulina nataka nikutambulishe wakujue.

Kumbuka hapo wameachana na wapenzi wa maisha yao, alafu kule kwenye group walikuwa wanatambishiana kuwa siku ya birthday ya Paulina nawatambulisha shemeji yenu mpya ni suprise.

Suprise yenyewe ndio mimi nilienusulika kutolewa roho na wakina joy na Uche.
Hahaha,
Dogo una vituko balaa!
Hii siyo chai kweli?!
 
UZI WA KIJOBLESS NA MBINU ZA KIDIGREE
(Utatu wenye utataView attachment 3208738)

GAP YEAR......!!!

Kati ya mwaka 2017_2018, inaweza kuwa mwanzoni au mwishoni mwa miaka hio kumbukumbu zangu hazijakaa vizuri.

Nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni ya kusambaza vinywaji. Yaani mimi ndio nilikuwa natembea na gari kusambaza vinywaji vijijini.

Ndio Mimi nilipewa eneo la vijijini kuhakikisha vinywaji vinasambaa kila kijiji. Nilikuwa afisa mauzo wa upande wa vijijini.

Ilikuwa ni pombe, nilisambaza ile pombe mpaka vijana wa vijijini wakaacha kulima, wakawa walevi waliokubuhu. Hapo kuna kukubuhu na kupindukia sasa wale vijana walikubuhu.

Ile pombe ilikuwa inatengenezwa mkoa mmoja tu, na huo ambao uliwekwa kuwa wa majaribio kabla haijaanza Tanzania nzima.

Kiufupi ile pombe ilifungiwa, sijui sababu hasa ni nini lakini ikafungiwa kiwanda kikafa. Hapo ndio tunapata hio GAP YEAR.

GAP YEAR ni kipindi ambacho unakaa unakuwa huna kazi ya kufanya, huna shughuli yoyote kiufupi kichwa chako kinakuwa karakana ya shetani.

Baada ya kampuni kufungwa, mimi nilikuwa nimepanga mjini, nyumba kubwa tu. Basi kwenye ile nyumba tulikuwa tunakaa watu wanne. Mimi, Familia mbili na Mdada mmoja alikuwa hajaolewa.

Huyo Mdada tumuite Kamsi. Kipindi nakaa kwenye nyumba hio nilikuwa nakaa na mpenzi wangu yeye tumuite Uche.

Hata hivyo mimi nilikuwa sio mtu wa kushinda nyumbani sana kwa mwezi naweza kushinda mara mbili au moja.

Kipindi kampuni inafungwa Uche alikuwa amepata kazi mkoa mwingine hivyo katika hio GAP YEAR nilibahatika kuweka mazoea na Kamsi.

Kamsi alikuwa mpole, hakuwa kama wadada wa mjini wale wengine. Lakini Kamsi alikuwa analala ndani na analipa kodi anavaa na anakula nyie Dunia inamaajabu.

Tuachane na maajabu ya Kamsi. Basi Kule alikokuwa anafanya kazi Uche ile kampuni ilikuwa inatoa rikizo kwa mwaka mara moja tu.

Hapo ni miezi mitatu toka Uche aondoke. Kama nilivyosema awali kichwa kisichokuwa na kazi ni karakana ya shetani.

Nikawa namtaka Kamsi, lakini nitampataje Kamsi na anamfahamu Uche. Nikaja na mpango mahususi wa kijobless zaidi.

Basi nikaanza kurusha ndoano zangu kwa Kamsi, lakini kila nikirusha zinagoma Kamsi anadai anamjua mtu wangu na hataki kuharibu mahusiano yangu.

Nikaona huu ni mwezi wa tatu na Uche kupata likizo ni mwezi wa 12, I mean nina miezi tisa ya kupiganisha hapa katikati ikabidi nimkane Uche.

Nikamwambia sikia Kamsi Uche ni moja ya wanawake washenzi sana, katoka hapa kaenda huko kupata kazi kaolewa na mfanyakazi mwenzake😭😭😭

Nikaanza kulia, hapa nilikuwa nalia baada ya kukumbuka sina kazi na kodi inakaribia kuisha weeeee weeee wee nililia na mengi.

Kamsi akawa ananibembeleza kwa kunipa pole bhana.

Kuna rafiki yangu wa kike anaitwa Joy. Siku mbili mbele nikampigia Joy nikampa mpango.

Nikamwambia Sikia joy nakupa hii namba ya Mdada anaitwa Kamsi, mpigie mwambie unaitwa Uche. Then mwambie ni kweli umeolewa uko jifanye unajutia kwa ulichonifanyia, then mwambie mimi ni husband material hivyo kama anaweza awe na mimi hakuna shida.

Basi bhana joy ni mwana sana sio kama josh, lakini wait hawa wawili majina yao yanaanza na Jo hawa me siwaaminigi mjue, joy sio josh wa kiume kweli hebu tuone.

Basi kweli siku tatu mbele Kamsi akawa ananambia kuwa kaongea na Uche, kumbe kweli kaolewa hivyo kunibembeleza kwingi like utapata mwingine.

Basi bhana Kamsi akaanza kuwa karibu na mimi. Wiki moja mbele akanambia jumapili nitakuja kukutembelea.

Nikashangaa huyu Kamsi tunakaa nae nyumba moja anasema jumapili atakuja kunitembela, weeeee hapa lazima unyama nipate.

Eeh mnasemaga sijawahi fanikiwa kupata DEMU na hapa nimefanya nini mtoto Kamsi kanasa kwenye mtego mwenyewe makofi kwa joy tafadhali.

Siku masaa yakapita, kweli bhana Jumapili hii hapa ikafika, nikaenda kununua kuku, soda, wine na nikapika pilau.

Toka asubuhi me sikumuona Kamsi bhana, mimi sikujali nikapika niliungua sana siku ile lakini kwa upendo wangu kwa Kamsi sikujali.

Vitu vikaiva bhana vinanukia kwelikweli. Basi saa tisa hivi ugeni mzito ukafika kwangu.

Guess what..... Alikuwa na JOY, KAMSI NA UCHE.

WEEEEEEEEEH WEEEEEEEEEH, wimbo wa KASONGO ulipiga kichwani wote ukaisha ndani ya sekunde, nikabaki nimesimama mlangoni.

Mnakumbuka nilisema ile nyumba kodi ilikuwa inaelekea kuisha🥹🥹

Ninachoweza kuwaambia ile ndio ilikuwa siku ya mwisho mimi kuonekana pale,. nilihama nyumba ile bila kuchukua chochote, Kiufupi SIKU ILE NILIKIMBIA KAMA SWALA 😂😂😂

nikarudi nyumbani mwenda kwao sio mtumwa 😂.

Lakini hawa wakina JO wanashida gani wakuu.

Kilichokuwa kinafanyika kumbe Kamsi na JOY. Ni marafiki, pia Kamsi na Uche ni marafiki na mimi sikuwa najua yote hayo.

Hapo ndio ilikuwa mbwa Kala mbwa.

Siku hiyo hiyo naona wameniunga kwenye group la Whatsapp bhana, wanajiita THREE WIFE ONE HUSBAND.

alafu Joy akaweka status akasema LEO NIMESHIBA KAMA MAMBA😭😭 Umeshiba kwa chakula la nani ubwa wewe.

Kule kwa group walikuwa wanasema hawaondoki mpaka mimi nirudi tuyajenge. Muyajenge na nani kwani mimi Fundi...?

Nimerudi nyumbani, huku nyumbani nikazua msala mwingine. Huu ni mkubwa zaidi ya nilio ukimbia weeeeeeeeeh ikabidi nirudi kwangu. Maana wale majamaa walikuwa serious hadi wakalipia kodi ya miezi sita wakaamia kwangu kabisa.

Narudije kule, mpango sio mpango kama huna mwana kama Nango....!

wait for part two( it's not over until it's over ).

Pichani ni mimi nikiwa kwenye kuandaa DIKO LA KAMSI👇👇👇👇
Ogopa Sana kichwa chako kua KARAKANA YA SHETANI
 
Back
Top Bottom