Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,171
- 34,394
ha ha ha ha ha hahahhahaha hahahahahhaa Mungu wangu ilikuwajeNilisimamia ubatizo wa fisi nikidhani mtoto,sitamsahau yule mama wa mtoto
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ha ha ha ha ha hahahhahaha hahahahahhaa Mungu wangu ilikuwajeNilisimamia ubatizo wa fisi nikidhani mtoto,sitamsahau yule mama wa mtoto
umehamia msikiti gani Siku hiZi maana hata mi sikuoni kabisa mda was swala kumbe umehamaNilipokimbizwa na paka msikitini mwezi wa ramadhani mwaka jana had leo ule msikiti nimeuhama mimi
Hahaha hapakwetu iko misikiti kamamitatu miwili nimwendokidogo huo nilokimbizwa napaka ndio uko karibu sana na nyumbani,skurud hapo tena naswalia mwengineumehamia msikiti gani Siku hiZi maana hata mi sikuoni kabisa mda was swala kumbe umehama
Sent using Jamii Forums mobile app
PoleNakumbuka nilikuwa darasa la tano mkoani mwanza wilaya ya misungwi shule maalufu sana pale wilayani, nikiwa na rafiki angu kipenzi yeye alikuwa mdogo kwangu.
Jioni kanipitia nyumbani twende tukaluke sarakasi nikamfundishe wakati huo ukijua kuluka salakasi ya nyuma wewe mjanja sana, basi bwana tukafika sehemu kuna tank kama tatu za maji nikamwambia tupite pale kwenye tank tukachukue asali, yani lile tank lina ngazi na bomba moja limeshuka mpaka chini sasa juu lilipo pita bomba kuelekea ndani ya tank kuna uwazi hivi hapo kuna bonge ya mzinga wa nyuki ukitikisa bomba inagusa ule mziga kwahiyo,
Nikamwambia best tutikise kwa nguvu ili nyuki wasambae tupande tuchukue asali, tulifanya lile zoezi kwa muda kama dakika tano nyuki walizagaa kwenye aga sehemu tulipo na ile milio yao iliongezeka kwa kasi ya ajabu mwenzangu akaanza kuogopa na kudai tuondoke huku nyuki wametanda anga zima nilimzuia asiondoke hakunisikia gafla akatoka mbio kuelekea maeneo ya nyumbani kwetu haikuwa mbali na maeneo yalipo matank ya maji.
Alikuwa akilia akitaja jina la mama angu, mama Fulani nakufa nisaidie mama alikuwa anafua uani akamsaidia kumvua tshit nyuki zikamuuma na mama ikabidi wakimbilie nyumba jiran ya mwalimu kuomba msaada kufika wakaingia ndani nyuki wakajaa tena ndani ikabidi wakimbilie nyumban kwa mwalimu mwingine yule rafiki angu kuona vile ikabidi akimbie mpka kwao huku nyuki wakimuuma.
Tuludi kwangu sasa baada ya kusikia kelele za rafiki angu na nyuki walishaanza kuniuma nilikuwa pale kwenye tank nimeganda nimejilinganisha kwenye ukuta nikaingiwa na huruma nikamuokoe jamaa ile natoka naanza kukimbia uelekeo aliokuwepo kundi la nyuki likanifuata niliumwa na nyuki kila sehemu ya mwili sipigi kelele nisije gundulika nilikuwa nimevaa kaoshi wasukuma wataelewa hapa yaani kama singland
Inavitundu vidogovidogo kama neti nyuki walikwama kwenye nguo wakawa wananiuma wameng'ang'ania kwenye nguo, nikageuza kuelekea uwanja wa mpira nilipita katkati ya shule yani parade nyuki walinizidi kwa maumivu nikaanguka macho yamevimba yote sioni vizuri mbele nikavua ile singland kuzuia nyuki kuendelea kuniuma nikaiacha hapo hapo parade
Kisha nikaendelea kutafuta msaada huku nakimbia ovyo, Sikuona mtu hata mmja mtaa mzima wamejifungia ndani nikaenda kwa rafiki angu mwingine nyumbani kwao ili anisaidie nilikuwa nishachoka kukimbia na nyuki bado wananiuma mwili mzima nanukia harufu ya nyuki kama ulishawahi kuua nyuki huwa anaharufu Fulani hiv, nilipofika kwa rafiki baba ake alikuwa ni mwl asieona akamwambia mwanae sitaki nimuone huyo kwangu mwambie aondoke, nikaondoka nikaenda kaa kwenye Shamba la shule nisubili usiku uingie niludi nyumbani cha ajabu nyuki wananifuata tu ikabidi niende kwao na jamaa angu tuliofanya tukio wote nikamkuta amelala kapewa Huduma na mama ake kampaka mafuta ya taa kisha akaenda kwenye kikao cha kujadili waponda nyuki ambao ni sisi, nashukuru rafiki angu akanihudia vzuri lkn kichwa kinaunguruma kama mashine kinauma balaa, masikio yanapiga kelele ziiii, akanipaka mafuta ya taa tukapumnzika wakt huo sina Niko kifua wazi nyuki wameniuma mpka wamejisifu
Mara mama wa rafiki angu kaludi kutoka kwenye kikao kaja chumbani katukuta tumelala mama anafuka huyo anamtukana mwanae,nikaamka kumsalimia mama alipigwa butwaa kama dkk nzima akaongea kilugha yy ni mjita alinihurumia nilivyovimba macho hayaonekani masikio yamekuwa makubwa kiufupi sura haieleweki tumboni Nina nundu na mgongoni, mama wa watu akaogopa nitamletea shida na kwa jinsi nilivyokuwa pia akasema kesho wamesema muende shule wote ili tukachapwe, nikaomdoka kwenda nyumbani, mama alikuwa mkali kuliko maelezo nilijua Leo sijui ila kwakuwa nilikuwa najisikia kuumwa sina namna mama kuniona akaanza kufoka kashika fimbo nilipomsogelea kalibu mama alishindwa kuongea ukali ukamuisha nilisikia sauti ya mama kama anataka kulia hivi nikaingia ndani akaja akanipa panadol nakumbuka nikapanda kulala, akaanza kusema wamesema wazazi tulipe fidia kwani nyuki wameua bata wawili na mwanafunzi mmja wa kike asiyeona kalazwa niliumia sana sikuwa na jinsi, niishie hapo story ni ndefu kuanzia siku hiyo namuogopa nyuki kama nini nikisikia tu mlio wa nyuki huwa nakumbuka kisa kile
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]dah wachawi bnh , ila hata mimi ninapoishi kuna vitu vya ajabu sana mfano usiku nasikia sauti za mtu kutembea, mara taa zitazimika, pia nasikia milango inajifunga ilhali hakuna nafasi ya upepo kuingia kwani madirisha yamefungwa, ila tukaambiwa ni mzimu wa fundi fulani aliyekufa wakati nyumba inajengwa ila siamini hizo story ,pia kuna muda utaweka kitu sehemu flani badae unakuta kimekua placed sehemu tofauti ilhali upo mwrnyewe ndani...
Hakuna mtu aliyepitia mikasa ya wachawi katka umri mdogo kama mimi..
Nishawahi bebwa na wachawi mama akanikuta chini ya mtungi asubuhi..
Mm ningekuwa nishahama zaman sana
Aisee kwa maelezo haya nimekujua vizuri...... KAMA NI IKE AJALI BASI NIMEKUJUA.Wale vijana walipo rudi kwakuwa walikuwa kwenye hali ya uchovu mwenyeji wetu aliwatafutia maziwa na dawa ambazo alienda kuchumba kule mtoni wakapata nguvu kesho yake jioni tukaendelea na safari.
Baada ya miaka kadhaa yule mkubwa tulikuja kukatana chuo ilibidi tutafute siku tukakumbushia story kuanzia hapo tukawa marafiki sana kila wikiend tunakutana tukafanya mambo pamoja tulinunua shamba huko Bagamoyo tukawakwenye mpango wa kulima nanasi lakini nasikitika hatukuweza kutimiza ndoto kwani jamaa alikufa kifo cha ghafla sana.
Tulikuwa mahali siku hiyo maeeneo ya Bagamoyo tunapata moja baridi moja moto baadaye aliamua kuondoka ila akikuwa anawahi pale Kibo complex kuna jamaa alikuwa anamsubiri so aliondoka na mshikaji wetu mwingine ile kufika pale Makutano ya kibo kukunja aligongana na cruser cha ajabu aweza kutoka kwenye gari lakini alipo simama alianguka chini na kufa hapo hapo kufika hospital Rabinsia kumbe damu ilivia kwenye ubongo.
Basi ikiwa mwisho wa naisha yake.
Siku nyingine nitahadithia madhala yalionopata baada ya kifo chake ndugu walivyonisumbua.
Tufamie tu mkuu ila usiwe tu asiejulikanaAisee kwa maelezo haya nimekujua vizuri...... KAMA NI IKE AJALI BASI NIMEKUJUA.
Eeeh mtu mrefu....mim navojijua ningezima kwanzaWenyewe habarini za mchana ,this thread pls tuelezee matukio ya kutisha ambayo wewe binafsi umeshawahi kukutana nayo dunia hii kwenye kuishi kwako, mimi binafsi sitosahau siku moja nilikua kijijini kwetu then ilikua usiku wa saa mbili ninakwenda dukani nikakutana na mtu mrefu kweli amevaa nguo nyeupe ila sura sikuweza kuona, ile nimefika mbele na kugeuka sikumwona tena, hizo mbio zilizofata ni noma nilivyofika dukani nikaomba escort ya kurudi hom
.
.
.
Nawakaribisha tuje kushare experience zetu , pls kama hujawahi kumbwa usicomment mambo yasiyo na busara pia MSILETE SIASA ,maana najua baadhi wataanza sema ,Lissu kupigwa risasi, sijui makinikia mara bombadia..etc so tuchill kwa hayo kwani jukwaa la siasa lipo .
Nawakilisha
Nmecheka sana....pole lknMe nakumbuka nikiwa moja Kati ya mbuga za wanyama kaskazini asubui ya saa10 tukiwa patrol (ndo tunarudi) Kumbe tunapita njia ya viboko (hippopotamus) kulikuwa na Giza kumbuka kwaiyo hatukuwaona mapema Wewe kuja kustukuka hao hapo!! Tulikuwa group na mm ndo nlikuwa mdogo na jinsia tofauti nikamshika mmoja wetu shati asee nilisukumwa nikadondoka chini nikakanyagwa kama ardhi Yaani nilihisi ndo siku yangu mwisho nikabaki Pekee Yang nimeumia natetemeka siwezi hata kunyanyua mguu nikicheki viboko (group) wenyewe wako jirani kabisa wanakuja taratibu ,,Yaani nilibiringita mpaka pembeni na Huku nasali sala zote hata maumivu sikusikia tena [emoji23][emoji23] wakapita bila hata kunigusa ni mungu tuu,,baadae etii ndo wanakuja kunitafuta baada ya kujua sionekani
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Ilikuwa usiku, sikumbuki ilikuwa saa ngapi. Tulikuwa watatu kitandani. Mimi, Dada yangu na binti wa jirani alikuja kutupa kampani ya kulala sababu tulikuwa wadogo na ni wageni katika eneo moja daslam, baadae nilikuja kufahamu kuwa kunaitwa makuburi.
Tulikuwa tumelala mzungu wa nne, Dada na mwenzie wamelala upande wa miguuni huku wanapiga stori, mimi nililala upande wa kichwani nilikuwa kimya. Na ndio niko hivyo hadi sasa.
Pamoja na usiku kuwa mkubwa siku hiyo tulichelewa kupata usingizi. Kwahiyo wakati wenzangu wanapiga stori, mi nilikuwa zangu nimetulia kimya!
Lakini ghafla kilitokea kitu ambacho kilinishtua! Niliona mtu mweupe amesimama pembeni ya kitanda upande wa ukutani! Kilichonishangaza, kitanda kimegusa hadi ukutani, yule mtu amewezaje kusimama?!
Lakini cha ajabu sikuogopa kabisa! Nikabaki kimya namuangalia, huku wenzangu wanaendelea na stori.
Mara akaanza kukizunguka kitanda, nilikuwa namcheki tu ila nilikuwa makini kumfuatilia! Alizunguuka kama mara tatu kisha akasimama na kuanza kuninyooshea mkono. Nikashtuka! Basi ikawa kama mchezo, kadri anavyosogeza mkono na mimi nasogea. Nilisogea hadi kitanda nikakimaliza. Kilichobaki ni kuporomoka tu! Nikaona hapa ni kuwaeleza wenzangu tu! Wanawake bwana! Nilivyowaeleza tu "jamani mtu huyo ukutani!" Ikawa hekaheka humo chumbani, wote wakakurupuka kitandani huku wakipiga kelele! "Mamaaa mtuuuuu!!" Dingi na maza walikurupuka chumbani kwao panga mkononi!! Yule mtu katoweka! Tangu siku hiyo tukawa tunalala na wazee chumbani kwao, na yule binti karudi kwao. Ila baada ya wiki tukaswagwa kwa bibi. Ila baadae wazee walihama kabisà.
Hii ishu ilinitokea mwaka 1984 au 85 juu ya godoro la Sufi. Sitaweza kuisahau huu mkasa!
Ulikosea kumshika mtu shati mfe woote,weee ungetimua kuvyakoMe nakumbuka nikiwa moja Kati ya mbuga za wanyama kaskazini asubui ya saa10 tukiwa patrol (ndo tunarudi) Kumbe tunapita njia ya viboko (hippopotamus) kulikuwa na Giza kumbuka kwaiyo hatukuwaona mapema Wewe kuja kustukuka hao hapo!! Tulikuwa group na mm ndo nlikuwa mdogo na jinsia tofauti nikamshika mmoja wetu shati asee nilisukumwa nikadondoka chini nikakanyagwa kama ardhi Yaani nilihisi ndo siku yangu mwisho nikabaki Pekee Yang nimeumia natetemeka siwezi hata kunyanyua mguu nikicheki viboko (group) wenyewe wako jirani kabisa wanakuja taratibu ,,Yaani nilibiringita mpaka pembeni na Huku nasali sala zote hata maumivu sikusikia tena [emoji23][emoji23] wakapita bila hata kunigusa ni mungu tuu,,baadae etii ndo wanakuja kunitafuta baada ya kujua sionekani
Pole aisehNakumbuka nikiwa na miaka kama 9 hivi, nilikuwa na wenzangu 4 tulitoroka shule ile saa nne asubuhi (muda wa chai) tukaenda kuwinda ndege na kuchimba sungura huko Tabora (Kijiji cha Kigwa). Tuliingia porini tena pori zito kabisa lililoshona mpaka tukapotea bila kujuwa tuliingilia wapi, hivyo tukawa tunatembea tu na kutungua ndege huku tukitafuta sehemu nzuri ya kutokea lile eneo maana tulikuwa katikati ya pori na tulikuwa hatujuwi wapi tulipo kwa hiyo tukawa tunafuata mwanga wa jua tu. Kidogo mbele yetu tukaona kitu kama tawi hivi linataka kuanguka mbele yetu, mwenzetu mmoja akawa jasiri kwenda kulikata ili tuchimbe sungura vizuri kumbe alikuwa nyoka anashuka kuja kutukimbiza. Mwenzetu alipofika tu akagongwa mkononi na usoni then yule nyoka alishuka na kuanza kujipanga kutufuata sie...nasi kuona vile kila mmoja wetu akakimbia kivyake maana tulikuwa hatujuwi wapi tulipo. Mbeleni huko kukawa na uwazi fulani hivi, tukasimama na kujikuta tuko wawili tu wenzetu wengine hatukujuwa walikimbilia wapi. Tukawa tunawaita bila kujibiwa, kurudi kijijini tukawatafuta hatukuwaona. Usiku ule wazazi wao na polisi wakawa wanawatafuta na wakaja mpaka pale kwenye ofisi ya CCM kuulizia watoto wengine kama waliwaona wenzetu hao. Usiku wa manane wakaja mapolisi na wazazi wa wale wenzetu na kuhamsha wazazi wangu wakitaka kuongea nami kwani kuna mtu aliwaambia mara ya mwisho wale wenzetu walikuwa na mimi. Nikawaambia ukweli kuwa tulitoroka shule na kwenda kuwinda maporini ndipo tukakimbizwa na nyoka. Kwa kuwa ilikuwa usiku, wakaniacha nilale na asubuhi wakaja kutaka niwapeleke eneo la tukio. Kufika kule tukakuta mwenzetu aliyegongwa na nyoka kafa pale pale. Mbele kidogo tukalikuta chatu limeshiba karibu na pango fulani hivi na shati la shule likiwa ndani ya lile pango just next na huyo chatu. Yule chatu akauliwa na kuchunwa ndipo akakutwa mwenzetu mwingine. Hili tukio lilitokea mwaka 1979, na sitolisahau maishani mwangu kamwe. Nilipigwa sana na Mama yangu ile siku na mama alikuwa ananipiga huku akilia kwa hasira mpaka akashikwa na watu asiniue. Utoto ni janga baya sana kwani watoto wanadanganyana mno.