Uzi wa kuelezea matukio ya kutisha uliyowahi kukumbana nayo maishani, either ya kichawi,anything scary

Uzi wa kuelezea matukio ya kutisha uliyowahi kukumbana nayo maishani, either ya kichawi,anything scary

1) Miaka hiyo ya 1993 nikiwa kijijini Mengwe Rombo Kilimanjaro tulikua tunapenda sana kuwinda ndege kwa manati na kuwatega na mitego...
Mimi ndio nilikua kama kubwa la maadui, tukaenda kuwinda kwenye mapango ilikua mida ya jioni hivi, ila kwa mbali ndani tukaona macho yanawaka kama taa nyekundu hivi, mara mngurumo wa hatari tukausikia hapo, hizo mbio zake sikumbuki nikifika je nyumbani ila kuna mtoto mmoja alithurika ikajulikana walikua fisi, yule mtoto hakukaa sana akafariki...
Kijijini nimepita misuko suko mingi sana ambapo ningeshakufa muda tu
2) Tulikua na kawaida ya kwenda kuiba matunda na mazao kama mahindi kwenye mashamba ya watu kisha tunakutana sehemu tunayachoma tunakula weee, hiyo tabia ikawa inachukiwa sana na wana Kijiji, siku moja mzee mmoja alitufukuza na mishale ikawa inapita tu pyuuuuu kama muvi sie tunakimbia mashambani, ila bahati mbaya mshale mmoja ulimpata mwenzenu mguuni ila hatukukamatwa...
Hadi naletwa Dar mwaka 1995 nilishafanya visa vingi tu, miaka ikaenda nikapewa habari wale watoto tuliokua tunaiba wote mahindi walilogewa mahindi wakavimba matumbo wakafa wote walikua wanne, means namie ningekumbwa huko ningekufa pia
Maisha haya acha tu
 
1) Miaka hiyo ya 1993 nikiwa kijijini Mengwe Rombo Kilimanjaro tulikua tunapenda sana kuwinda ndege kwa manati na kuwatega na mitego...
Mimi ndio nilikua kama kubwa la maadui, tukaenda kuwinda kwenye mapango ilikua mida ya jioni hivi, ila kwa mbali ndani tukaona macho yanawaka kama taa nyekundu hivi, mara mngurumo wa hatari tukausikia hapo, hizo mbio zake sikumbuki nikifika je nyumbani ila kuna mtoto mmoja alithurika ikajulikana walikua fisi, yule mtoto hakukaa sana akafariki...
Kijijini nimepita misuko suko mingi sana ambapo ningeshakufa muda tu
2) Tulikua na kawaida ya kwenda kuiba matunda na mazao kama mahindi kwenye mashamba ya watu kisha tunakutana sehemu tunayachoma tunakula weee, hiyo tabia ikawa inachukiwa sana na wana Kijiji, siku moja mzee mmoja alitufukuza na mishale ikawa inapita tu pyuuuuu kama muvi sie tunakimbia mashambani, ila bahati mbaya mshale mmoja ulimpata mwenzenu mguuni ila hatukukamatwa...
Hadi naletwa Dar mwaka 1995 nilishafanya visa vingi tu, miaka ikaenda nikapewa habari wale watoto tuliokua tunaiba wote mahindi walilogewa mahindi wakavimba matumbo wakafa wote walikua wanne, means namie ningekumbwa huko ningekufa pia
Maisha haya acha tu
Ndo uache wizi wa kiwaki
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]dah wachawi bnh , ila hata mimi ninapoishi kuna vitu vya ajabu sana mfano usiku nasikia sauti za mtu kutembea, mara taa zitazimika, pia nasikia milango inajifunga ilhali hakuna nafasi ya upepo kuingia kwani madirisha yamefungwa, ila tukaambiwa ni mzimu wa fundi fulani aliyekufa wakati nyumba inajengwa ila siamini hizo story ,pia kuna muda utaweka kitu sehemu flani badae unakuta kimekua placed sehemu tofauti ilhali upo mwrnyewe ndani...
Hee mkuu bado unaendelea kuishi nyumba hiyo?
 
Walozi sio watu wazuri kabisa. Kuna mkasa mwingine nilikutana nao miaka hii ya 2000s. Mimi huwa napenda sana kurudi home usiku au hata nikisafiri nifike sehemu usiku ili asubuhi watu washtukie niko mtaani.
Sasa siku moja nimetoka mizunguuko yangu ya kawaida ilikuwa Moro hiyo. Mida ya saa tano usiku narudi home huku nawaza ntawaambia wazee sababu gani ya kuchelewa. Maana walikuwa sheria saa tatu nisiwe nje ya nyumba.
Sasa nikawa nakaribia nyumbani, na kwa macho napaona ila hakuna njia ya mkato ya kupita bali kuna kauchochoro kakuzunguuka ndio utokee njia kubwa ndio uingie ndani.
Nikawa nakiwaza hicho kichochoro maana kina simulizi mbovu kweli, nikapiga Moyo konde ila nikaamua kuongeza spidi ili nivuke ilo eneo haraka.
Basi nikachanganya mwendo balaa huku nywele na mwili wote unanisisimka. Ile nimefika katikati ya kile kichochoro, hamad! Nikakutana na kitu ambacho hadi leo sijakielewa, kwamba kilimaanisha nini? siku itabidi nimuulize Mshana Jr.
Nilikuta bonge la kinu cha kutwangia kimewekwa katikati ya ile njia. Ni Mungu tu alinilinda, maana kwa ile spidi ningekivaa tu!! Niliogopa sana, ila akili ilifanya kazi haraka, nikapita kwa pembeni. Hiyo spidi niliyotoka nayo hapo, hata bombadier isingefua dafu. Sikuwasimulia nyumbani hadi nilipokuwa nimeanza maisha yangu, maana ningekula hamsa vilevile na uhenga wangu.[emoji28]
Hahaha
 
Tulikuja stuka tunachomolewa kwenye foleni na kuamriwa tutoke eneo LA kanisa mara moja,nkimuuliza nini tatizo yule maza hata majibu aliyokuwa ananipa hayaeleweki na mbaya zaidi waliochomolewa walikuwa kibao ila kichwa kiliuma niliposikia padri anaongea kwa upole Yesu alikataa kujaribiwa tuache Tabia za ajabu.me nkaona nisepe na kijiji nkawaachia show yao ila ubatizo uliendelea na watu wala hawakustuka yan kama MTU kaanguka kifafa,na mi nlikuja kujua kesho yake kama nimebeba fisi bila kujua
Daah jamani
 
Your brain has two sides, "left and right" ..
In the left there's nothing right, and in the right there's nothing left... Sort yourself bruhv
Hehehehee nimecheka kama mwehu
 
binafsi nina matukio matatu moja nikilishuhudia mengine ni yakusikia.

miaka ya 95 nikiwa mdogo lakini nikiwa na ufahamu jumamosi fulani saa 12 kasoro asubuhi hali ya hewa ikiwa mawangu nadhani ilikua ni kipindi mvua za masika zikikaribia kuisha, kwa wale wenyeji wa moshi nadhan hali hii munaifahamu. kunakua na mawingu yametanda kiasi cha mtu alie mbele yako mita 5 huwezi kumuona.
siku hio nilikua nikienda jumuia kwa wakaliki haswa wa kule moshi mnajua jumuia livyokua ni muhimu kuhudhuri na mimi nilingwa kwenye msingi huo nikiwa toka mdogo, na tulikua tunasali nyumba kwa nyumba.

sasa nilivyokaribia hio nyumba iliokua na zamu ya kusali na hali mawingu yakiwa yametanda niliona watu kama watoto hivi wakiwa wameungana mwili isipokua kichwa. yaani mwili ni ni mmoja na vichwa viwili.
sasa yale mawingu yalizuia tusionane mmapena hamaki tukakaribiana, waliponiona walismama kidogo kama vile walistuka nikaona wanaywea kushuka chini yaani kama mshumaa unavyoisha, lakini kwa kasi mara wakaisha wakawa kama jiwe na mwishowe sikuona kitu.
sikuogopa sana nilienda kusali zangu lakini liletukio sikulisahau mpaka leo.
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15]
 
Siku moja enzi hizo tuliharibikiwa na gari maeneo fluni panaitwa makuyuni tukiwa tunatoka Dodoma tunaelekea Moshi kwa Bus enzi hizo ni ua kampuni ya Ralway hakuna mabasi mengine nilikuwa nipo darasa la saba

Kipindi hicho barabara ni mbovu sana gari inachukuwa siku mbili kufika moshi.

Ikabidi konda na abiria mmoja wafuate spear Dodoma nayo ilichuwa siku mbili.

Ilibidi tujiongeze tutafute nyumba za jirani ili angalau tupate huduma kama chakula, kuoga na kadhalika wazee na familia zingine walifanya hivyo.

Kutola hapo kwenye bus mpaka kwenye nyumba ni umbali wa kama kilometa tano hivi tukakuta nyumba mbili tu lakini tunashukuru nyumba tuliofika tukawaeleza shida zetu walituelewa ambapo alikuwa anaishi watu wawili tu kijana mmoja na mke wake ambaye alikuwa mrembo kweli wengi tulishangaa kwanini waliamua kuishi porini ili hali kwa muonekano walikuwa ni watu wastaarabu sana.

Basi baada ya wazazi wetu kupokelewa wakaanza mandalizi ya kupika na mambo mengine sisi watoto tulikuwa mimi na mdogo wangu na watoto wawili wa familia moja kama kawa hao tukaenda eneo fulani kama shamba hivi lakini kulikuwa na mteremko unaelekea kwenye mto pembeni ya uo mto kulikuwa na ndizi mbivu basi tukazikimbilia tukazichuma tukaanza kula.

Kwakuwa ule mto haukuwa na maji tukavuka hao upande wapili tunaona matunda ambayo siyakumbuki na mapera basi tuliendelea kuchuma na kula ilikuwa kama saa 12 jioni.

Baadaye tukaona kijumba kidogo tukaenda mpa kwenye hicho kijumba tukamkuya bibi mzee sana anachuma mboga kribu na nyumba yake tukasalimia tukamweleza sikumbuki nini lakini akatuletea mziwa tukanywa.
Mara kukawa na wingu zito sana na radi dakika kumi nyingi mvua ilinyesha tukaanza kukimbia nimemshika mdogo wangu ambaye alikuwa analia sana na mdogo wake na yule mwenzetu naye alikuwa analia basi yule bibi alituzuia eti mvua itakatika na pale mtoni hamuwezi pita tulichanganyikwa lakini mimi nilgoma nikaondoka na mdogo wangu nikawacha wale wenzetu kufika pale kwenye mto mto unapitisha maji ila sio mengi cha ajabu ngambo ya pili tulimuona yule Bibi na fimbo yake amekunja uso daa tulitetemeka sana anatunyooshea ile fimbo turudi.
Nyuma ya yule bibi tukaona kwa mbali mwanga wa tochi na sauti za watu kama wanaongea ndiyo hauweni kumbe mzee na wenzake wanatutafuta.
Yule bibi kuona watu akaja upande wetu huku akivuka mto tukampisha tukanza kumuita mzee huku tunatetemeka dogo analia tumeloa chakari mzee alivyotuona yeye mwenyewe alitetemeka kwa hofu.
Tukawaambia wenzetu wapo kwa bibi mmoja kule juu basi mjomba wao na mwenyeji waliwafuata kwa yule bibi huku mwenyeji akisema huyu bibi ni mchawi sana asije wazuru watoto wakakimbia kufika pale wakawakuta wapo ndani kwa yule bibi wanaota moto lakini wamejikunyata wamelegea sana hawajiwezi huku huyo bibi akiwa amejilaza kwenye kitanda chake anatamka sijui maneno gani.

Yule mwenyeji nasikia akamkoromea akamwambia lolote litakalo walata hawa watoto tunakumaliza ndiyo ikiwa salama yao.
Kufika pale kwa mwenyeji hapo ni usiku sasa kama saa 2:30 kunagiza tunawahadithia kilichotokea mh..wazazi waliogopa sana tukagombezwa sana...

Hayo ndiyo nakumbula lakini ilikuwa siku mbaya sana na sitaisahau maishani.
Duuh pole sana
 
Shukurani kwa mtoa uzi

Siku ambayo sitakuja kuisahau kamwe Maishani mwangu ni kipindi nasoma shule flani kule mkoani ruvuma nikiwa kidato cha sita, nikiwa naishi bweni , ni wiki kadhaa toka nijiapize moyoni mwangu kua ulokole siutaki tena,
Tukiwa tupo bwenini purukushani za viongozi a.k.a vilanja zikiwa zinaendelea za kututaka tuondoke bwenini, nikiwa naharaka ya kubeba material yangu niende darasan Mara niliona Pete( ndio pete unayoijua wewe ya kuvaa kidoleni) iliwa kwenye kitanda flani bila ya kujiuliza na kutafakari niliichua na kuondoka nayo adi darasani, nikiwa naendelea kusoma nikakumbuka juu ya ile Pete akiri yangu ikanituma nivae, nami bila kusita nikaivaa nikaendelea kusoam , Muda wa prepo ulipo isha nilirudi bwenini! Tukiwa tunaendelea na story Mara nikasikia mtu anasema kwa sauti ya chini na akiwa anauliza majirani wake kua kuna mtu amechukua Pete yake! Nilimsikia lakini nilimpuuza na nikapanga nimpe kesho yake, kwa hiyo nililala Nayo! MUNGU wangu nikiwa nimelala sikumbuki ilikua saa ngapi ! ilikuja ndoto ya ghafla nikaona Mtu akiwa amevaa nguo Nyeusi toka juu adi chini na USO wake akiwa ameufunika mkononi akiwa ameshika fimbo flani akaja adi pembeni ya kitanda changu na kuniangalia kwa sekunde kadhaa halafu akaninyooshea fimbo yake kisha akapotea nilistuka na nliogopa sana, nilipo tazama wenzangu nlisikia sauti za kukoroma tu hakna aliejua nini kilinitokea, nililala tena ghafla niliota namuona jirani yangu anapaa juu kitandani kwake akiwa amelala vile vile hiyo ndoto ikakata,------- lakini ghafla tulishitishwa na kelele za juu sanaa kama mtu analia kwa sauti kubwa ,wote tuliamka nakuanza kumuhoji , jamaa akasema nimeona mtu ananipaisha juu ndo nmeanguka! Kumbukumbu zangu zilirejea kwenye ndoto yangu! Lakini sikumwambia mtu yeyote , amini usiamini kesho nilipata msala msala wa ajabu ambao ulisababisha nikafukuzwa shule siku hiyo hiyo, Sitokuja kusahau hii kitu
Pete ya watu urirudisha?
 
Kuna mtu alipata madhara yyte? Na wale vijana wenyeji waliwaambiaje kuhusiana na hilo tukio?
Wale vijana walipo rudi kwakuwa walikuwa kwenye hali ya uchovu mwenyeji wetu aliwatafutia maziwa na dawa ambazo alienda kuchumba kule mtoni wakapata nguvu kesho yake jioni tukaendelea na safari.
Baada ya miaka kadhaa yule mkubwa tulikuja kukatana chuo ilibidi tutafute siku tukakumbushia story kuanzia hapo tukawa marafiki sana kila wikiend tunakutana tukafanya mambo pamoja tulinunua shamba huko Bagamoyo tukawakwenye mpango wa kulima nanasi lakini nasikitika hatukuweza kutimiza ndoto kwani jamaa alikufa kifo cha ghafla sana.

Tulikuwa mahali siku hiyo maeeneo ya Bagamoyo tunapata moja baridi moja moto baadaye aliamua kuondoka ila akikuwa anawahi pale Kibo complex kuna jamaa alikuwa anamsubiri so aliondoka na mshikaji wetu mwingine ile kufika pale Makutano ya kibo kukunja aligongana na cruser cha ajabu aweza kutoka kwenye gari lakini alipo simama alianguka chini na kufa hapo hapo kufika hospital Rabinsia kumbe damu ilivia kwenye ubongo.

Basi ikiwa mwisho wa naisha yake.

Siku nyingine nitahadithia madhala yalionopata baada ya kifo chake ndugu walivyonisumbua.
 
aisee haya mambo kumbe yapo kweli eeh...mimi mwezi ulioisha tu natoka home mida ya saa 5 na robo hivi usiku naenda kwa rafiki nilikua na shida binafsi...na ni nyumba tatu mbele kutoka home...huezi amini njiani NILIKUTANA NA UNGO MPYAA...yan MPYAA kabisa...niliupita nikaenda kwa rafiki ila sikupita tena njia iyo wakati wa kurudi.
Yapo sana mkuu
 
Mimi leo 26 october 2017 naamka asubuhi nakuta anga lote la njano nikahisi leo ndio mwisho wa dunia mara nakuta dogo nae anashangaa hii hali ilidumu kwa dk kadhaa .sijui kama wakazi wengine wa dar wameona hii hali
 
Mimi leo 26 october 2017 naamka asubuhi nakuta anga lote la njano nikahisi leo ndio mwisho wa dunia mara nakuta dogo nae anashangaa hii hali ilidumu kwa dk kadhaa .sijui kama wakazi wengine wa dar wameona hii hali
mida ka ya saa 12 asubuhi...mimi niliifurahia asee
 
Back
Top Bottom