Uzi wa kuwaunganisha wenye ujuzi na wenye mitaji


Tatizo unakaa sana ndani umekua mvivu, huoni watu wanaimport vitu kama bags toka china wanauza insta, mzigo wa 3m mtu anatengeneza hadi 7mil. Ukiona hujafanikiwa usidhani ni kila mtu bora uulize wanafanyeje kuliko kupiga kelele, narudia tena ukiona una business ndogo haiingizi two times the capital achana nayo tafuta nyingine unapoteza muda. Endelea na mawazo yako ya kimaskini
 
Wazo ni zuri,ingekuwa vizuri kama ungeweka breakdown hapa ili huyo atakayetoa mtaji wa 20M awe na uhakika wa fedha zake kabla ya kufika huko pm.
Siwezi nikaweka hapa kila kitu , wale walio na hamu ya kufanya biashara watakuja PM na tutajadili vema,
 
Nimevutiwa na maujuzi yenu Mungu awafungulie njia kwa kweli na Equation X uliefikiri hili pia Mungu akubaliki pia naamini mtafanikiwa tu...
 
Apo ni mashine tuu yenye ubora na yenye uwezo wa kuchakata zaidi ya tani 2 Kwa siku itakuwa vizuri zaidi tutacheki China ya vigezo tunavyotaka na malengo ya kazi maana malighafi ipo na soko lipo

Sent using Jamii Forums mobile app
Brilliant idea ila pesa yake ni kubwa kwangu.... inawezekana kupata fund kwenye mambo haya ya mazingira umewahi kujaribu kushiriki kwenye kupata fund kama Tony Elemelu, Total startup, pia kuna ya DenMark Embassy...? Jaribu kushiriki unaweza kupata fund hata kama ni usd 10k sio mbaya kuanzia
 

It sound very nice. unakaaonao after 4:30 wanaenjoy πŸ˜€πŸ˜€
 
Hio mikoba china inatoka jana inafika leo?vipi kwenye kutafuta wateja anauuza wote kwa wakati mmoja au kwa mtu mmoja ndani ya kipindi cha wiki moja tangu aanze kuutafuta kuhifadhi na kusafirisha???.
Yaani wiki moja bwana mdogo flani hivi anatunza 1mil plus na sii ya urithi unasema hafikirii unataka awe kama wewe?kila mtu anaamini kwenye lile afanyalo kwanza mshahara wa chini serikalini ni bei gani?na wanaolipwa wanaanzia na umri wa miaka mingapi na ukumbuke kutofautisha wiki na mwezi
 
Ujuzi : bachelor of economic
Wazo : Nataka kuanzisha project ya onloan with deposit

Tatizo : start-up capital and operation capital & Notes board advertise biasahara inalipa na inaweza kutengeneza faida ya kama million 200+ kwa mwaka kwa Kuanza na mkoa mmoja wa Dar as salaam ila lengo ni ku operate Tanzania nzima nahitaji mtu au watu wa kushirikiana nao nimeshaandaa kila kitu ni kuregister company na kuanza kazi inaitajika start-up capital ya 10 million na operation 10m total 20 million.

Kwasasa nafanya kazi ili nipate mtaji mkubwa wa kufinance project zangu
 
Wadau mimi ni Instrumentation Engineer.
Nina uzoefu mkubwa wa kufunga plant/ factory, nimefunga plant nying sana Tanzania, mfano machine za juicy, Soda, maji ya kunywa, mafuta ya kujipaka, dawa za meno nk.zote ktk industrial level. Ninaweza kuisimamia project toka ktk level ya michoro mpaka final product inatoka na zaidi naweza kufanya kazi zote kwa mikono yangu sio kwa kidole au mdomo. Kwa sababu za kimaadili sitataja bidhaa wala kampuni niliyokwisha ifanyia kazi. Kwa bahati mbaya biashara hii inazidi kianguka siku hadi siku. Nina baadhi ya wateja wangu tena wakubwa tu nawadai lkn nao hawawezi kunilipa kutokana na kuwa na migogoro na taasisi za serikali. Hivyo najikuta sina mtaji.
Ila huwa sikati tamaa kwa sasa nafanya stadi niwe na kiwanda changu kidogo cha bidhaa ambayo ni kati ya FMCG goods ( Fast Moving consumer Goods) na mungu akiniweka salama na afya mpaka desemba mwakani (2020) nitakuwa katika hatua za uwekezaji wa awali. Japo kwa sasa nipo ktk makaratasi tu.
Km kuna mtu anaweza.kuona kuwa uwezo wangu tu ni mtaji namkaribisha japo sina pesa kwa sasa.
 

Imekaa poa kiongozi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…