Jamal Malinzi
JF-Expert Member
- Feb 9, 2013
- 710
- 650
asante
kwa majibu
naomba unijibu kuhusu ilipo Moro United
Okay,
Nadhani haya uliyofafanua hapa ya mtaala wa michezo ni kama alivyopata kufafanua Bw. Mweisigwa akihojiwa na TBC kama sikosei mwezi uliopita...
Lakini najiuliza huu ni mpango wenu TFF au kuna msaada toka serikalini?
Kuna wakufunzi wa kutosha au kwa kuanzia kuna shule kadhaa zitahusika? (Nakumbuka ziara uliyoifanya Alliance Academy na ahadi uliyotoa ya kuiingiza shule ile katika mpango kama huu ulioeleza hapa).
Ndigu Malinzi, kwanza nakupongeza kwa kushinda kiti cha Urais wa TFF,
Nina swali langu dogo tu kuhusu wachezaji wa kigeni, je utaratibu tuliotangaziwa kuwa wachezaji hao wataruhusiwa watatu tu kwa klabu, uongozi wako unauafiki?
na nini athari za kuwa na wachezaji wa kigeni kwa wingi?
Ndugu na jamaa yangu Jamal Malinzi, we ni shuhuda wanawake angalau wanatutoa kimasomaso kwenye match za kimataifa, japokuwa hatuna ligi wala timu zenye hadhi. Mpango ukoje kuhakikisha soka la wanawake linakua?
Ndugu yangu Asprin mambo matatu makubwa tunayahangaikia kuhusu women football na ninaamini tutafanikiwa punde:
1.kuanzisha ligi ya vilabu vya wanawake
2.kuanzisha taifa cup ya wanawake
3.kuingiza watoto wa kike kwenye youth programmes nao wafundishwe mpira wakiwa wadogo.
TFF tumeamua pamoja na ufinyu wa bajeti kila mashindano ya kimataifa ya wanawake tutaingiza timu ili tupate uzoefu,leo tumejisajili All africa games Congo brazaville 2015 tunaingiza timu ya wanawake na CAF tumewafahamisha rasmi.
Kwa hili ntawatakieni kila la kheri, kama ambavyo unajua mie na wanawake tuko damdam. Ushauri ningeomba timu za ligi kuu zingekuwa na timu za wanawake, afu ikawepo hata ligi ya mtoano kupunguza gharama. Natamani siku moja nishuhudie warembo wa Simba wakitafuna nyama ya manungayembe ya Yanga. (samahani kama nimekukwaza)
Thanks for your prompt response.Electronic ticketing tumeanza ila kwa kweli kwa yaliyotokea leo mkwakwani Tanga itabidi kesho tuchukue hatua za dharura kulinda usalama wa watazamaji wa mpira.Taarifa nilizoletewa leo kutoka Tanga si nzuri.
Wazo zuri la vilabu vya premier kuwa na timu za wanawake,ngoja tulifanyie kazi.
Ngolombwe this is a two edged sword,upande mmoja unataka wachezaji wa kigeni wawe wachache ili wa kwako wapatw fursa ya kucheza na kukuza kipaji,upande wa pili ligi lazima ichangamke na ivutie public,sponsors na advertisers,wachezaji wa kigeni wanaongeza hii ladha na kupandisha hadhi na ushindani wa vilabu kwenye ligi.Inabidi kupata uwiano (balance).Sasa je hiyo balance ni wachezaji wangapi wa kigeni kwenye ligi?
1.Ni kweli tumewaagiza Dorefa wawambie Mpwapwa stars watches eligible ya mkoa kwa mujibu wa taratibu za Dorefa.Muda wa kutosha ulitolewa Walter vielelezo vya madai Yao mpaya Leo hatujaviona.Mkuu Malinz Nina Maswal Mawl 1. Vip Kuhusu Rufaa Ya Mpwapwa Staz. Kwan Tunaskia Katbu Wa Dorefa Anae Dai Kuwa Ww N Baba Yake Ameifuta Rufaa Na Kaja Tff Kuchukua Barua Ya Kuwataka Mpwapwa Wacheze Ligi. Hii Ipoje 2. Mnampango Gan Na Kuanzisha Mashndan Ya FA??
Nakubaliana na wewe asilimia Mia SHERRIF ARPAIO tuna Kazi kubwa ya kufanya katika kukabiliana na changamoto za uingiaji,ukaaji na usalama wa watazamaji uwanja wa taifa na viwanja vingine.Thanks for your prompt response.
Ila mkuu ujue yaliotokea siku ile ya mechi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast June last year pale Taifa ni aibu tupu, na ni hatari sana kwa walioingia uwanjani na tunaomba isitokee tena. Nimeapa sitohudhuria mechi yoyote tena pale uwanja mpya hadi marekebisho yatakapofanyika, na siku peke yangu tuko wengi sana.
Tickets zikikatwa based on seat numbers, na ikawa enforced itakuwa ni permanent solution ya tatizo hili
Kwanza nikupongeze ndugu Jamal Malinzi kwa kuchaguliwa kuongoza shirikisho la mpira wa miguu Tanzania na nikupongeze pia kujitokeza kujibu maswali hapa JF.
Swali langu linahusu mgawanyo wa mapato yanayotokana na viingilio kwenye mechi mbali mbali. vilabu vya Tanzania ndo vinavyomiliki wachezaji na ndo vinavyohangaika kuhakikisha wachezaji wao wapo katika hali nzuri kimwili pamoja na kiakili, kuyafanya yote hayo vilabu vinaingia gharama kubwa sana ambayo ni pamoja na kuwalipa mishahara, posho, kuwatibu wanapougua au kuumia, kuwasafirisha pamoja na gharama ya kambi.
Mashabiki wanaingia uwanjani kwa ajili ya kwenda kuona soka linalochezwa na hawa wachezaji wanaomilikiwa, kutunzwa na kuhudumiwa na vilabu lakini linapokuja suala la mgawanyo wa mapato vilabu vilivyoshiriki kwenye mechi husika vinapata mgawo ambao ni chini ya asilimia hamsini ya mapato yote kitu ambacho mimi nadhani si haki, je TFF ikiwa chini yako, mna mpango wowote wa kupunguza haya makato ya kinyonyaji?
Nitachukua mechi kati ya Yanga na Ashanti pamoja na ile ya Simba na Rhino zilizochezwa wiki iliyopita kama rejea kwenye swali hili.
Mechi ya Yanga na Ashanti iliingiza ≈TZS86.04M, na kila klabu iliingiza kiasi cha ≈TZS 20.65M, ukichukua timu zote mbili zilipata 48.001% ya mapato yote.
Mechi ya Simba na Rhino iliingiza ≈TZS53.82M, na kila klabu ilipata mgawo wa ≈TZS12.60M, jumla timu zote mbili zilipata 46.823% ya mapato yote.
Kutokana na rejea hapo juu pamoja na maelezo niliyotoa, hivi TFF hamuoni kama vilabu hivi mnaviumiza ukizingatia zenyewe ndo zinaingia gharama kubwa lakini kuna wengine wanapata mgawo bila kutoa jasho lolote? Kwa nini msiweke angalau vilabu husika vipate japo 55%-60% ya mapato yote halafu wale wengine kama malipo ya Uwanja, gharama za mechi, Bodi ya Ligi, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) wakapunguziwa mgawo wao?
Lini mtabadilisha jina la timu ya taifa? Hili jina la Taifa Stars halina mvuto na limepitwa na wakati, na pengine lina nuksi ama gundu na huenda ndio maana timu yetu imekwama toka iliporudi Lagos in 1980.
I think it's time now we switch to something else for instance Kilimanjaro or Serengeti ambayo yataitangaza Tanzania kwenye mambo mengi hasa utalii. Just my thought!
Angalia hata Nigeria na Zambia wameshabadili.