Uzi wa vyakula tu

Matumbo?? Hivi ngoja nijifunze kiswahili kwanza.

Kati ya maneno haya mawili ipi ndio jina halisi ya hiyo aina ya nyama?
A)Matumbo
B) Utumbo
Wabongo naskiaga wakisema 'Utumbo' ila mimi jirani na wengi wetu huku tushazoea 'Matumbo' japokuwa nafkiri haliko sanifu. Hebu nipe elimu mkuu!
[emoji3577]
Utumbo ni utumbo hauna wingi bali una aina, mfano utumbo mkubwa, utumbo mdogo, utumbo taulo, utumbo bomba, utumbo kitabu nk
Matumbo ni wingi wa neno tumbo (stomach) kwa mfano
Tumbo lake limejaa gesi, matumbo yao yamejaa gesi
Kuna watu wana matumbo makubwa na kuna watu wana matumbo madogo nknk

Hivyo kuviita vile vya ndani 'matumbo' sio Kiswahili sanifu japo majirani zetu ndio wamezoea [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…