Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kweli ni mada ngumu sana hii, ila ni very interesting kujifunza. Knowledge is power! Nimekumiss sana my ex-shemeji.
Unajua mkuu,walioanzisha nadharia ya HIV/AIDS wanajua wazi mikanganyiko iliyopo kuhusu dhana hii,ndio maana wanakuna vichwa kutunga nadharia nyingine za uongo ili kurubuni akili za watu na kuwafanya wasiwe na mashaka na suala zima la HIV/AIDS.Mifano;
1.Watu waliopima HIV+ kwa miaka mingi sana lakini hawaugui hata kama hawatumii ARVs huitwa CARRIERS.
2.Wanandoa wanaoishi pamoja muda mrefu lakini mmoja ni HIV+ lakini mwingine ni HIV- huitwa DISCORDANT COUPLES.
3.Baada ya kuona watu wenye huyo HIV wanaugua kwa viwango na kasi tofauti katika maeneo tofauti duniani wakaja na nadharia ya HIV-1 na HIV-2.
SWALI:
Je,mimi niliyejidunga damu ya mtu alipima HIV+ na baada ya muda mrefu nilipima HIV- watatumia nadharia gani kujibu huu mkanganyiko?
I feel my brain is expanding. Nimeamua kufuta series nyingi kwenye pc yangi ili niweke haya mambo ya knowledge..
Kwa kweli mambo mengi ni hoax.. Elimu inahitajika mnoooo. Mbona hatuwasikii wagonjwa wengi wa ukimwi nchi za wenzetuu?
3. Kuna virus wengi sana kutoka kwenye familia kubwa sana, ambao kimsingi wote wanaweza kupimwa kwa kipimo cha viral load. Ila hicho unachokizungumzia hapa ni specific kwa HIV kwa sababu lengo kuu ni kujua wingi wa copy za virusi walio katika mwili wa binadamu..., kuangalia kiwango cha virusi waliopo mwilini kwa maana ya Viral load. Hiyo CD4 test ilikuwa inaangalia masalia ya seli hai za CD4 ambazo ndio kimsingi hushambuliwa zaidi na hao HIV, ...
He he heee,yaani hata hilo neno 'window period' umekaririshwa,hii ndio kasumba chafu nayotaka kuiondoa kutoka kwa walio wengi.Watu wanadhani wanafikiria kwa akili/uwezo wao wenyewe kumbe wanafikiria kwa kutumia akili za kupandikizwa na wengine.
Tujitahidi kujikwamua kutoka kwenye vifungo vya kufikiri ambavyo wamiliki wa viwanda vya madawa wametuweka,watu hawajui kama kuna watu wanaofikiri kwa niaba yao.Hawajui pia kwamba maneno wanayotamka sio ya kwao bali ni ya wengine ambao ndio wameshikilia akilia zao.Hii ndio kazi ya kitengo cha mindcontrol.Mind control ni kitengo kinachofanya kazi kwa utaalam na siri kubwa sana,huwezi kuona kirahisi jinsi kitengo hiki kinavyofanya kazi,sasa hivi athari zake zimeshajitokeza katika sekta nyingi sana ikiwemo hii ya afya.
Nilijidunga mwaka mmoja uliopita,hadi leo ni HIV-.Hiyo window period yenu ni muda gani?
Mgunduzi wa HIV,Robert Gallo naye amekuja na yake;baada ya kuona kwamba watu wenye HIV hawaumwi hata kama hawatumii ARVs kwa muda mrefu,akasema 'eti' HIV anaweza kuchukua miaka hata 10 kuanza kusababisha ugonjwa.He he heee,HIV/AIDS regime ina vituko sana.Yaani hapa maana yake wanasubiri sababu nyingine zisababishe ugonjwa halafu waanze kumsingizia HIV.Miaka 10 ni mingi sana kwa mtu yeyote kukaa bila kuumwa,hivyo mtu akiumwa tu basi wataanza kusingizia HIV.
Ila we jamaa Deception hoja zako zinamashiko usije tufanya watu tukapiga kavukavu
Mkuu multikasuku , shukrani sana kaka kwa mchango wango mzuri. na nimepata hoja zaidi za msingi kama ifuatavyo:
In RED, hapo maelezo yako yanajikanganya, au labda mimi ndo sijaelewa. Unasema kwamba Viral Load ni kuangalia kiwango cha virusi waliomo mwilini. Hapo hapo tena unasema viral load tunayozungumzia hapa ni 'specific' for HIV tu. Now narudia swali langu: Kwa kuzingatia ukweli kwamba mwilini wanaingia virusi wa aina mbali mbali, Je hicho kipimo cha Viral Load, kinapima/kuonesha kiwango cha virusi wote kwa pamoja in general (without isolating/specifying the type)? mfano: virusi 'wote' waliopo mwilini ni kiasi hiki. AMA kinapima na kuonesha kiwango cha virusi mwilini per type (i.e kinapima na kutoa matokeo in isolation per specific virus type)? mfano: virusi wa Hepatitis B mwilini ni kiwango fulani; virusi wa influenza ni kiwango hiki; virusi vya HIV ni kiwango hiki, n.k.
And if kipimo hicho (viral load) ni specific for HIV only, why kisiitwe ''HIV Load'' ili kumantain hiyo sense of 'specification' ??
In BLUE, umeeleza kuhusu CD4, kwamba CD4 ndo kimsingi hushambuliwa zaidi na hao virusi wa HIV...
HOJA: Ndugu Deception katuhabarisha kwamba Kuna watu wana CD4 below 50 na wana afya njema kabisa, na kuna watu wana CD4 nyingi tu na wanaugua mara kwa mara. Je wewe unalisemeaje hili ??
Vile vile, Dr Kary Mullis (mgunduzi wa PCR) yeye mwenyewe anaeleza kwamba CD4 has nothing to do with health of someone, a lot of things can cause CD4 to go down, a lot of things also can cause CD4 to errupt!
Je wewe unalisemeaje hili ?
Kwa nyongeza, kuhusu ANTIBODIES za HIV:
(a) Kuna madai kwamba kuna baadhi ya magonjwa kama MARALIA kali, TB, Kaswende, n.k huweza pia kuusababisha mwili u-produce hizo 'specific antibodies' against HIV. JE HILI UNALISEMEAJE ?
(b) Kuna madai kwamba MIMBA (ujauzito) yaweza pia kuusababisha mwili u-produce hizo 'specific antibodies' against HIV. JE HILI UNALISEMEAJE ?
(c) Kuna wajawazito ambao wanatest HIV+ na hawatumii ARVs (hawatumii zile dawa za kuzuia maambukizi from mother to child) lakini wanazaa watoto ambao hawana maambukizi (HIV-)! JE HILI WEWE UNALISEMEAJE ?
Tupe knowledge zaidi kiongozi.
......Sasa WHY hiki kirusi cha HIV ndo kinabebeshwa mzigo wote wa kuharibu/kushambulia kinga za mwili ilihali kumbe kuna vitu vingine vinavyoweza kusababisha immune kushuka? Hii dhana ya HIV/AIDS ina utata mwingi for real .
In BLUE, umetupia swali kwamba je wewe uliejidunga damu ya mtu alietest HIV+ lakini mpaka leo hii wewe unatest HIV-. Katika hili, wataalamu wa dhana ya HIV/AIDS wanasema kwamba kuna baadhi ya watu (wachache sana) ambao damu zao ni 'naturally' resistant to HIV. Pengine labda na wewe mkuu damu yako ni aina hiyo.
Pia Dr Luc Montaigner (mgunduzi wa HIV) yeye mwenyewe anaeleza kwamba if someone has 'good immunity', the body can get rid of the Virus in few weeks after intection!...
Huu ugonjwa una controversial kubwa sana na hauwezi kuwa solved mpaka pale dunia itakapoweka political power na commercial interest pembeni. Tuache scientists wapiganishe facts za kisayansi.
Nadharia iliyo kwenye main stream imeshafeli huu mwaka wa 31, sasa why dunia inakataa mawazo mbadala? Na hawa denialist scientists sio watu wa kubeza ni watu wenye CV kubwa tu katika ulimwengu wa sayansi, na wengine wana noble prize kwasababu ya inventions ambazo wamezifanya katika ulimwengu wa sayansi. Sasa why hawapewi nafasi kama tuna nia ya dhati ya kutafuta solution?
Mimi binafsi naamini hawa denialists wakipewa nafasi historia mpya inaenda kuandikwa kwenye ulimwengu wa sayansi, na hicho ndicho hawa waanzilishi wa hypothesis ya HIV/AIDS wanakiogopa, ile expertise yao kuja kuonekana useless ikiwa itathibitika kwenye mainstream kuwa HIV is not the cause of AIDS.
Unayo yaongea niliwahi msikia Thabo Mbeki akizungumza
sikuelewa....ina maana wanao lazwa muhimbili hawana UKIMWI?
au UKIMWI ni nini?
Hutaki kujibu hoja zangu za msingi,badala yake una copy na ku paste mzigo wa maandishi ambayo hayako kimpangilio na yana ukakasi kuyasoma.Ni afadhali ungetoa link watu wafuatilie wenyewe.Kwa akili yako unadhani hayo mimi siyajui,mambo hayo nilishayajua muda mrefu sana huko nyuma,wewe unastuka leo hii.
Pia hata huna uelewa wa western medical system ilivyo,ndio maana nilikwambia wewe bado sana.Walioandika hayo mambo ni hao hao wenyewe,wewe hujui hilo,sasa toka lini mtu akaikashifu kazi yake mwenyewe?
Huna hata dira na hujui uzungumze nini,hoja za msingi hutaki kujibu.OK,wewe unawapinga HIV/AIDS denialists,sasa mimi nimekubandikia link mojawapo inayoonesha pro HIV/AIDS,Prof Luc Montagnier akisema mambo ambayo ni tofauti kabisa na ninyi madaktari wengine mnavyosema,nikakuuliza,Je,mgunduzi huyu naye amepotosha?Kama kapotosha tuambie ukweli ni upi?Ninyi wote mnategemea basics za HIV/AIDS kutoka kwa huyu mgunduzi,sasa tuambie kama amepotosha kwenye ile video.
Maswali haya muhimu unayakimbia na badala yake unashusha mzigo wenye ukakasi kuusoma huku ukijiona kama ni mjanja sana kumbe hamna kitu.Lakini sikushangai kwa kuwa hata darasani ndivyo mlivyokuwa,mnapenda sana ku copy kazi za wengine,mitihani pia mlikuwa mnaibia.Ndio maana huna uwezo wa kujadiliana na mimi kwa hoja.
Usikimbie hoja za msingi,jibu hoja kama wewe kweli unajua,usituwekee rundo la maandishi ya ku copy hapa,andika unachokijua kwa kiswahili ili kila mtu akuelewe una hoja gani.
Halafu unaposema mimi sikujidunga hiyo damu,mimi ni muongo,Je,una uhakika kama kweli mimi ni muongo?Ulishawahi kuniona?Nilikupa nafasi tukutane ili uone kwa macho yako mwenyewe nikifanya hivyo,Je,uliitumia hiyo nafasi kuthibitisha kama mimi ni muongo?Vita kati yangu na ninyi mnaonufaika kwa kudhulumu uhai wa wengine wasioelewa haitaisha hadi muda wangu wa kuishi hapa duniani utakapokwisha.Mnanuka dhambi na hamna hata chembe ya huruma,mnawalisha watu ARVs maisha yao yote,mnategemea nini?Mtu akifa mnasema HIV ndio amehusika,hivi hamjiulizi mtu kula dawa zenye sumu kila siku maisha yake yote anapata athari gani?Ubongo wenu una matatizo sana ninyi.
Mkiambiwa ARVs zina madhara makubwa na ndio yanayoua,eti mnasema "si wote wanaopata madhara hayo",hivi unafanya uchunguzi wako wewe?au unakurupuka tu kupinga.Sasa nakupa homework,fanya uchunguzi wako kwenye vituo vya afya kwa wale wote waliolazwa hospitali wanaotumia ARVs utaona wana matatizo yafuatayo;
1.Moyo, 2.Ini, 3.Figo, 4.Cancer yoyote ile, 5.Matatizo ya damu/anaemia, 6.Kisukari. Matatizo mengine madogomadogo ni; Nywele kuwa dhaifu/kunyonyoka,ngozi kufubaa/kuota vipele/vidonda/kuwasha,kuvimba vitezi shingoni nk.
Haya yote ni madhara ya ARVs na ndio yanayowaua,hakuna hata tatizo moja hapo juu linalosababishwa na HIV.
Don't take my words,just do your own research,fanya uchunguzi wako wewe mwenyewe na uje hapa tena kutoa marejesho.
Watu hamna elimu ya kutosha halafu mnakurupuka kupinga tu.
... Antibody test ina zaidi ya 99% specificity .....
Hii ni rare phenomena as far as hiv test is concerned. Ila ili kutoa utata huu, ndio maana ukipima kipimo cha kwanza ukoanekana uko positive, utapima kipimo kingine ambavyo kiko more superior ili ku-confirm majibu. (ref. Determine'''bioline'''unigold'''western blot'''hiv DNA pcr'''electron microscope.)
...kwakuwa hiv primarily hu-infect na kuathiri seli zenye CD4 receptors,.....
Lakini pia jiulize , wangapi wanakutwa na ukimwi na hawatumii dawa ila wanaumwa magonjwa yanayoendana na ukimwi na kufa. ARV zimewauwa hapo?
Mtu na mkewe wanakufa kwa magonjwa yanayoendana, na wote walikutwa na HIV, hushtuki?
Pia, damu ya mama na mtoto wakati yuko tumboni hazichanganyiki, ukielewa hii utaelewa kwanini sio lazima mama azae mtoto positive. Soma zaidi