V.V.U na Upimaji wake (Coincidences)


kijana hongera upo vizuri sana kwa kujenga hoja zenye logic na kuuliza maswali.pia haupo biase.i like you!
 
Last edited by a moderator:

Tujadili kwa makini sana alichokisema mdau hapo juu kwenye nyekundu,halafu tupime wapi kuna ukweli;

1.kwa bahati nzuri inatokea kwa wagonjwa wachache (hasa pale wanapoanza kutumia dawa...

Suala hili huwa nalisema mara nyingi sana,watu wanaounga mkono HIV/AIDS hypothesis hupenda sana kusema maneno haya,'eti' madhara haya huwatokea watu wachache.Halafu pia mimi sikuzungumzia madhara ya muda mfupi,naomba watu wawe na kumbukumbu kwenye hili jambo,mimi nazungumzia madhara ya muda mrefu(long term side effects),yaani madhara yanayomtokea mtumiaji baada ya kuzitumia ARVs kwa muda mrefu.Madhara yanayoua ni yale yaliyojijenga baada ya matumizi ya muda mrefu ya ARVs,na ndio nguvu yangu ya majadiliano nimeiweka hapa.Sijawahi kuona au kusikia madhara ya muda mfupi ya matumizi ya ARVs kwamba yameua mtu,bali madhara ya muda mrefu ndio huua watumiaji wa ARVs.Hivyo naomba tu focus hoja zetu kwenye mahara ya muda mrefu.

Angalizo:
Madhara haya ya muda mrefu anayapata KILA mtumiaji wa ARVs,si watu WACHACHE,la hasha,bali watumiaji WOTE wa ARVs hupata madhara haya ila muda unatofautiana kutegemea na lifestyle zao.Wengine (kwa mfano) baada ya miaka 2,wengine 3,4....10 nk,kwa vyovyote vile mwisho wa siku lazima apate madhara,ARVs HAZIBAHATISHI katika kusababisha madhara.

2....Hivyo si sahihi na ni UONGO ambao inabidi tuukemee kuwa ARVs ni fatal zinaua kinga na kusababisha UKIMWI....

Sasa naomba mwenye akili na azitumie hapa:

KUMBUKENI HAYA MANENO:
Kinga ya mwili hukinga mwili dhidi ya magonjwa ya kuambukizwa na yasiyoambukizwa.Magonjwa ya kuambukizwa ni kama vile malaria,TB nk,na magonjwa yasiyoambukizwa ni kama vile cancer,vitiligo nk.Kinga ya mwili sio CD4 peke yake,kuna mambo mengi sana.CD4 zinahusishwa zaidi na kukinga pathogens/vijidudu,lakini matatizo mengi yanayowakumba wale wanaotumia ARVs kwa muda mrefu HAYAHUSIANI na vijidudu,kumbukeni na fuatilieni hilo,usiridhike na anachosema mtu mwingine,fuatilieni wenyewe,kila mtu atasema anachoamini,sasa ili kujiridhisha fuatilieni ninyi wenyewe mahospitalini na mitaani.

Sasa twende kwenye mada:
Mimi nasema na nilishasema mara nyingi kwamba ARVs husababisha UKIMWI baada ya kuzitumia kwa muda mrefu.Naomba msome post yangu ya muda mrefu hapo chini kwa umakini mkubwa.


Kinga kupungua si lazima seli za kinga zife,hata uwezo wake wa kufanya kazi ukipungua maana yake kinga imeshuka pia,hii ni kimantiki zaidi ya kidarasani.

Nitatoa mfano mmoja kuhusu cancer:

Kitaalam,kila siku kila mtu mwili wake hupata seli za cancer lakini hatuugui cancer kwa sababu kinga ya mwili huziua seli za cancer.Kuna aina tofauti za kinga za cancer,unaweza kuzigawanya katika makundi mawili ambayo ni First line defense na second line defense,nadhani haya ni maneno rahisi watu kuyaelewa.Sasa twende ndani zaidi....

First line defense inahusisha kimengenyo kiitwacho TRYPSIN kitolewacho na kongosho/pancreas.Trypsin kazi yake ni kumengenya PROTINI,seli za cancer zimezungukwa na ukuta wa protini ambao una charge -ve.Sasa seli nyeupe za za damu nazo zina charge -ve,sasa seli nyeupe haziwezi kuvamia na kuua seli za cancer kwa kuwa(as a matter of principle) charge zinazofanana hukwepana,hii karibu kila mtu analijua.

Sasa basi,kimeng'enyo cha trypsin kazi yake ni kumengenya ukuta wa protini wa seli za cancer na kuziweka uchi zishambuliwe na seli nyeupe za damu.Sasa ili process hii ikamilike lazima seli nyeupe ziwe vital,yaani ziwe na afya na pia kongosho iwe na afya njema.Sasa kama damu ina acid nyingi hili haliwezi kufanikiwa kirahisi,process nzima itashindwa kutokea,na hatimaye mtu hupata cancer,very very simple.Hivyo ukiona mtu kapata cancer ujue moja ya mambo makubwa yaliyomtokea ni hili.

Sasa nimetoa link ya youtube ili watu wajionee side effect za ARVs.Lakini pia nimetoa link nyingine ambayo hutumiwa na serikali ya Marekani('wale wanaomiliki HIV') ili watu wasinishambulie kwa kuniambia kwamba nimetoa ma link ya uongo ya youtube.

Link hiyo ya pili niliyotoa ni ya haohao wanaunga mkono HIV/AIDS,si link ya HIV/AIDS dissidents,nadhani tumeelewana hapo,hata ukilinganisha link niliyotoa na ile aliyotoa mkuyati og utaona zinaendana.Angalia hapa chini;

mkuyti og ametoa link hii:
http://www.niaid.nih.gov/topics/hivaids/understanding/howhivcausesaids/pages/hivcausesaids.aspx

Mimi nimetoa link hii:
https://aidsinfo.nih.gov/drugs/290/tenofovir-disoproxil-fumarate//patient
https://aidsinfo.nih.gov/drugs/290/tenofovir-disoproxil-fumarate/0/patient

NIH(National Institute of Healthy) ni taasisi ya afya ya Marekani inayofanya kazi bega kwa bega na CDC,AMA na WHO.

Ukiangalia kwenye link niliyotoa chini kabisa utaona chapa ya mwewe,hii ni ishara kwamba link hii ni ya wamiliki wa HIV/AIDS hypothesis.Mkuze huyo mwewe na usome kilichoandikwa juu yake.Skulazimika kusema yote haya,lakini nasema hivi ili kuondoa lawama.

Pia TDF ni mfano tu,lakini wewe ingiza jina la dawa YOYOTE ile ya ARVs kwenye link hiyo utaona kwamba SIDE EFFECTS zote ni zilezile,sasa kama una ubongo jiulize kwa nini.

Pia kama mtu haamini hiyo link,basi atafute kikopo chochote cha dawa za ARVs ndani yake kuna karatasi pana sana ukiikunjua imeeleza vilevile kama kwenye link hii.Ila uzuri wa karatasi hizi za kwenye vikopo ni kwamba zimeingia ndani zaidi kiasi kwamba ukizisoma vizuri utaona matatizo yote yanayowatokea wale waliolazwa mahospitalini wanaotumia ARVs yameandikwa kwenye hizo karatasi.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu mimi hata sio much know, nataka tu kujua hilo. Maana this whole things nowadays naona inaleta tu confusion na si kingine. Mfano nimekuuliza swali kama umewahi kumuona huyo mdudu, umekuja na maelezo mengi ambayo yamezidi kuniconfuse.

Swali langu ni je Ulishawahi kumuona yeye mwenyewe kama vile unavyopima Malaria na kumuona yule parasite wa malaria??????
 
jamani nimeweka link inayoprove
hiv husababisha aids na mambo mengine mengi. nasubiri kujua wangapi watasoma na kutoa maoni. ukimya huu unanifanya niamini kwamba sisi ni kizazi kolichozoea kutafuniwa (spoon feeding). nimesema kabisa kwamba hoja zote zilozotolewa humu ziko ndani ya hilo bandiko, kama zilivyo, pamoja na majibu yake kisayansi na ki statistic na epidemiologically. tukubaliane, hapa tunaongea kuhusu scientific proof, na sayansi hujibiwa kwa sayansi na si kwa siasa kama wengi wenu mnavyotaka.

nawawekea tena hii link

PROOF THAT HIV CAUSES AIDS
 

Mie nimesoma na nimekutana na hiki kitu,
"in many developing countries, where diagnostic facilities may be minimal, healthcare workers use a World Health Organization (WHO) AIDS case definiton based on the presence of clinical signs associated with immune deficiency and the exclusion of other known causes of immunosuppression, such as cancer or malnutrition. An expanded WHO AIDS case definition, with a broader spectrum of clinical manifestations of HIV infection, is employed in settings where HIV antibody tests are available."

Hiyo paragraph imeniachia maswali, hivi ni kweli wataalamu wetu wa afya wanajua wanachofanya? au wanafuata muongozo fulani hivi kutoka kwa wenyewe kwenye hili suala la HIV? Si ndio hawahawa walimpasua mtu kichwa aliyekua anatakiwa kupasuliwa mguu?

Kwa upande mwingine, kwa nini hawa wanaopingana na conventional wisdom on hiv-aids, wanabanwa katika kutoa maoni yao? kwa mfano tu, kwa nini kitabu cha "Why we will never win the war on Hiv" cha kina Duesberg kiko banned? Hawa wamiliki wa hiv wanaogopa nini kitawekwa wazi na hicho kitabu? Kama jamaa wanaongea upuuzi why not let the public be the judge of that?
 


Mkuu hao Co-founders wa HIV ambao ni Robert Gallo na Luc Montagnier kuna vitu vikubwa wameshindwa kuvifanya ambavyo mmoja wa Denialist wa kwanza ku question hiyo Hypothesis ameweza kuvifanya katika ulimwengu wa sayansi.

Denialists huyu ni Peter Duesberg, Robert Gallo anamjua Peter Duesberg ni nani katika ulimwengu wa sayansi. Duesberg amedeal na retrovirus kwa miaka zaidi ya 30. Ni mtu wa kwanza ku map genetic structure ya retroviruses, so ni mtu ambaye anafahamu strong and weakness ya retrovirus, pia ni yeye ndiye aliyegundua genes (ONCOGENES) ambazo zinasababisha kansa .

Na ndiyo maana aliposikia Gallo aki claim kwamba virusi aina ya retroviruses kuwa wanasababisha kushuka kwa kinga ya mwili akushangaa sana kwasababu sio mara ya kwanza Gallo kuclaim kitu kama hicho. Aliwahi kuja na kitu kama hicho miaka ya 70. Ali claim kwamba virusi hao hao aina ya retroviruses wanasababisha kansa kwa binadamu lakini baada ya scientist kuja na critics alishindwa kuprove madai yake scientifically. Na ndiyo ikaja kuwa proved kwamba kansa si ugonjwa wa kuambukizwa, na hii case ya UKIMWI inafanana kabisa na hii case ya kansa.

Ni vigumu kuamini kwamba HIV is not the cause of AIDS mpaka uichimbe historia ya UKIMWI duniani na siyo tanzania, ndiyo utaujua ukweli. Since day 1, ukweli kuhusu UKIMWI ndipo ulipopotoshwa.

Kitu ambacho unapaswa kufahamu ni kwamba HIV/AIDS defendants kamwe hawawezi kukubali kuwa HIV is not the cause of AIDS ingawa wanaujua ukweli, na hii si kwa bahati mbaya, wanaogopa kuwa responsible juu mamilioni ya watu waliopoteza maisha kwa wrong treaments inayoambatana na UKIMWI na pia knowledge yao ya sayansi kuonekana uselesss kwenye hii dunia.

Kitu cha pili, kamwe HIV/AIDS defendants hawawezi kushiriki scientifically debate na deanilists, kwasababu wanaujua ukweli uliopo nyuma ya pazia.

Mwisho HIV/AIDS defendants hawajashindwa kupata chanjo au dawa ya UKimwi bali wameshindwa kujua nini chanzo cha ukimwi na hapa ndiyo turning point ya kukosa vaccine au antibiotic ya huu ugonjwa kwa miongo 3 (Miaka 31) sasa. Wameishia kubuy time tu na kutengeneza pesa tu. Wameshindwa kukiri kwamba wameshindwa, wanaona aibu sasa, wanaishia kukipa HIV magical power tu. Mara kinajificha, mara kinapumbaa.

Wewe si medical expert nenda ka trace history of medicine katika ulimwengu wa sayansi kwa magonjwa ambayo yalikuwa yakisababishwa na virus na ambayo yalikuwa yakuambukizwa yamekuwa controlled vipi. Yote yamekuwa controlled na vaccine na antibiotic, hiyo ni success history katika ulimwengu wa medicine. Na ugonjwa wa mwisho ulikuwa ni Polio miaka ya 50 huko.

Magonjwa ambayo yameshindwa kupata chanjo au antibiotic ni magonjwa ambayo si ya kuambukizwa na ambayo hayasababishwi na virusi mfano kansa.

Msikilize Dr. Peter Duesberg anachokizungumza hapa;

https://www.youtube.com/watch?v=JTxvmKHYajQ
 


Umeuliza maswali ya msingi sana Mkuu. Kitu cha kushangaza scientist anakimbia uwanja wake wa science ambapo ndiipo anatakiwa kupiganisha facts, anakimbilia kwenye politica power. Denialists wako banned kwa sababu ya politica power, tangu mtu wa kwanza ku question hii hypothesis, huu ni mwaka wa 28 hakuna permanent solution juu ugonjwa wa UKMWI.

Na wakati walipoanza ku question hii hypothesis walikuwa wananyimwa hata air time kwenye vituo vya TV na Radio kuzungumza. Kadiiri siku zilivyokuwa zikisogea Great Scientist walikuwa waki join kwenye movement baada ya kufanya research zao na kujua kuna tatizo. Majarida ya sayansi yaliogopa hata kuchapisha facts zao. Watu walipewa order kutotoa ushirikiano na Denialists ili tu kulinda maslahi ya watu wachache kwenye huu ulimwengu.

Sasa kama tunataka kutatua tatizo why tunaogopa mawazo mbadala hali ya kuwa hypothesis iliyo kwenye mainstream imeshindwa kutoa solution ya kudumu kwa miaka 31?

Maendeleo ya elimu yaliyotokea yalitokea kwasababu ya nadharia zilizotangulia kupinduliwa na nadharia mpya. Sasa why watu wanaogopa?
 


Wakuu pakamwam , mkuyati og ,

Ahsanteni sana kwa maelezo yenu ya kitaalaamu, hakika sasa naanza kuwaelewa, na nimejifunza kitu.
Hapo juu (kwenye RED), naona kama ni hoja ya maana, baada ya kuitafakari deeply mara mbili mbili. Kweli kabisa kuna kitu cha kuwekana sawa katika hili, yawezekana kumbe tunachanganya hii terminology ''UKIWMI''.

Kwa mimi nilivyowaelewa sasa, kuna AINA mbili za Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI), pia kuna AIDS ambayo ndo magonjwa yenyewe mtu anaanza kuugua. Kwamba:

(a) Kuna UKIMWI unaosababishwa na mwili kukosa vitu/kitu fulani kwenye mfumo mzima wa kinga. Upungufu huu wa Kinga ndo kitaalaamu unaitwa ''Immuno Defficiency''.

(b) Kuna UKIMWI unaosababishwa na Kirusi ambae anaitwa 'HIV'. Upungufu huu wa Kinga naona kitaalaamu hauna jina !

(c) Halafu kuna AIDS, haya ndo yale magonjwa yenyewe sasa mtuu anaanza kuonesha dalili ama kuugua kabsa.

Hivyo basi, UKIMWI na AIDS kumbe ni vitu viwili tofauti:

UKIMWI
kirefu chake ni Upungufu wa Kinga Mwilini, yaani kinga za mwili zimeshuka/zimepungua.
AIDS kirefu chake ni Acquired Immuno Defficiency Syndrome, hii ni magonjwa/ugonjwa spesific mtu anaanza kuugua. WIKIPEDIA: ''A syndrome is a set of medical signs and symptoms that are correlated with each other and, often, with a specific disease.''

So ukiwa na UKIMWI, then ndo AIDS inaibuka. Yaani kwamba Kinga zako zikipungua (UKIMWI), then ndo unaanza kuonesha dalili za kuugua/ugonjwa (AIDS). Therefore kwa tafsiri yangu mimi binafsi, AIDS kwa kiswahili ni 'magonjwa yanayopatikana/yanayoibuka baada ya Upungufu wa Kinga Mwilini'. I sincerely stand to be corrected!


Sasa basi, kwa nia njema kabisa ya kujifunza, naombeni wakuu mnieleweshe zaidi kwenye hoja zifuatazo:

1. Upungufu wa Kinga (ukimwi) unaosababishwa na ukosefu wa kitu fulani kwenye immune system, kitaalaamu unaitwa ''Immuno Defficiency''. JE, upungufu wa kinga (ukimwi) unaosababishwa na kirusi HIV, kitaalaamu unaitwaje??

2. JE, AIDS (ambayo ndo magonjwa yenyewe) yanapatikana/yanaibuka kwenye Ukimwi (a) au Ukimwi (b) ??

3. Pia hebu naombeni sana muichambue hii terminology ya 'AIDS'. Tuangalie the real meaning ya neno 'AIDS', please msibeze hii hoja maana mimi nahisi kabsa ni kama kuna logic fulani ivi ambayo either namiss kuielewa ipasavyo, or inanimisslead. NOTE: ''Immuno Deficiency'' ipo ndani ya neno ''AIDS'', na pia kumbuka kuwa ''Immuno Deficiency'' ndo UKIMWI (a) hapo juu.

AIDS = Acquired Immuno Deficiency Syndrome.

Je, neno ''aqcuired'' linarefer kwenye Immuno Deficiency? ama linarefer kwenye Syndrome? Kwamba, ni Acquired Immuno Deficiency which then causes Syndrome? ama ni Acquired Syndrome caused by Immuno Deficiency?

Je, kwa medical context, neno 'acquired' linamaanisha nini hapo?

Wakuu mnisamehe sana kama naonekana kuwachosha, ila lengo langu ni kujifunza masuala haya kutoka kwenu mliosomea taaluma hii. Tuweke biasness pembeni na tuelimishane hizi issues za HIV/AIDS. Dhumuni kuu ni wasomaji wajifunze kwa manufaa yao wenyewe, coz kumekuwa na controversies ambazo kwakweli ni za wazi wazi kabisa kumfikirisha mtu yeyote mwenye common sense.

CC: multikasuku , Eiyer , Deception , H1N1 , everlenk , mzee wa kigonzile Econometrician
 
Last edited by a moderator:

salaam mkuu,

kwanza naomba niseme kwamba science is an open book, kila mtu ana uhuru wa kutoa hoja zake ila tu ziendane na misingi ya sayansi. pili, hakuna mwenye hati miliki ya matokeo ya kisayansi. wapo watu wamefanya gunduzi nyingi tu, ila walikuja mbele yao wameendeleza gunduzi hizi na kuzi perfect. kwenye science everything is a function of time. kwa maana hyo basi, both R.gallo and L.montagnier did their part katika ugunduzi, na walifika uwezo wao ulipofikia. sio wao tu walioweza kufanya research juu ya hiv, wengine walikuja na kufanya tafiti nzuri kuliko wao.

hapa naona umekazana sana na P. deusberg, tell you what, kufanya research 30 years juu ya retroviruses na pia kugundua oncogenes ni impressive. remember, he is not the only one to work with retroviruses na kugundua vitu. nilisema kwamba medical science is not stagnant however slow it may seem katika ugunduzi wa baadhi ya vitu vipya. unahisi kama asingegundua oncogenes mpaka sasa tungekuwa hatujui oncogenes ni nini hasa? kama you think only his ideas matter, mbona hujiulizi kwanini yeye hakuweza kuelezea nini kinasababisha hiyo "AQUIRED IMMUNODEFICIENCY SYNDROME -AIDS"?

labda tu nikuulize na wewe, do you believe in Kocchs postulates kuhusu origin of disease causing microbes? (zimeelezewa mwanzoni kabisa mwa article ile niliyoweka). tell you what, P. Deusberg does believe in those postulates, na HIV fits perfectly in all of the postulates and criteria.

this is science, so how do you explain the overwhelming evidence kuhusu HIV-AIDS? umezisoma?? please tell me about that.
kama u dont agree with the evidenve, basi kataa pia kwamba mdudu P. Falciparum hasababishi Malaria, maana mdudu huyu anafit ktk kocchs postulates the same way HIV does. again, medicine has principles governed and determined by keen medical research findings. au research ambazo ni credible kwako ni zile za denialists only? kama ni hivyo, basis your judgement is highly biased and polarised.

unasema kwamba kansa ilikuja kugundulika kwamba sio ugonjwa wa kuambukiza wala hausababishwi na virusi. narudia tena, medicine as a science is not stagnant,, do you know kwamba kuna baadhi ya kansa husababishwa na virusi? wajua kwamba HPV husababisha kansa ya shingo ya kizazi? Unajua kwamba EBV husababisha kaposis sarcoma? unakubaliana na findings hizi? na je, unajua kwamba kuna squamous cell carcinoma caused by HIV virus? na unajua kwmba wengi wa virusi niliowataja hapo wanauwezo wa kuwa transmitted kutoka mtu mmoja kwenda mwingine, mfano HPV kwa njia ya kujamiiana?

ugumu hapa ni kwamba tunajadili mambo tofauti. wewe hoja zako zime base sana katika siasa, mimi natoa scientific facts . katika ku-prove hili, naomba nitoe mfano mdogo tu : umedai kwamba kama HIV inasababisha ukimwi, kwanini wanasayansi wameshindwa kupitia kinga ama "antibiotic" kutibu AIDS? labda tu nikuulize, kwanza :naomba nitajie ugonjwa moja tu unaosababishwa na virus wenye TIBA kisayansi(hapa namaanisha maana sahihi ya tiba, kama vile mtu anavyotibiwa malaria) pili: nani kakwambia kwamba "antibiotics" zinatibu virus? Hivi unaelewa hata maana ya antibiotics na nature ya magonjwa ambayo antibiotics hutibu? Mbona unachanganya madesa? .nasema tena, uelewa wetu ni tofauti,, I will always be your doctor, unless uende kusomea taaluma yangu then you will know and understand what I know in detail. ndio maana nikisema hapa kwamba issue ya HIV ni pana kuliko tunavyofikiria hapa, wengine wanakimbilia kutoa majibu mepesi.

ni hayo tu mkuu
 

Naheshimu ulichokiandika...ila sidhani kama huyu Deception yuko kibiashara' ukimsoma between the line utagundua kama huyu jamaa anamuonekano wa kujitolea tu kwa watu wenye matatizo haya ya HIV
 
sijaelewa bado.
Inawezekana labda hili gonjwa ni unfriendly sana ndo maana inaniwia ngumu kuelewa.
 

Samahani Doctor...sisi wengine tuna ndugu zetu ambao wana tatizo hili la HIV na wako kwenye dozi. Je unashauri watumie dawa gani ambazo ni mzuri ili wasipate hayo matatizo ya ini na figo?(kama kweli yapo) Maana ukimsoma Deception anasema hizo ARV ndizo zinazosababisha matatizo ya ini na figo au hata cancer. Sasa je,dawa gani ya ARV ambayo ni mzuri kiasi kwamba mtu akitumia hatapata hayo matatizo?
 

asante kwa swali mkuu.

kama nilivyosema mwanzo, hapa tatizo ni lugha na interpretion.

labda nikupe historia kidogo. miaka ya 70 ambapo HIV ilikuwa haijagundulika bado, term AIDS halikuwepo. ila immunodeficiency syndrome(s) zilikuwepo. term AIDS ilikuja baada ya kuingia na kugundulika kwa kirusi cha HIV. term "aquired" inamaanisha kwamba mtu anapata immunodeficiency kutokana na madhara ya kirusi cha HIV kuingia mwilini,, aquisation of the HIV. term AIDS inamaanisha development of diseases baada ya kushuka kwa kinga ya mwili kunakosababisha na mdudu HIV. term AIDS only applies to diseases that attack the body due to weakened immunity caused by the HIV virus, and not otherwise. hapa ndipo katika article niliyoweka inaonyesha kuwa watu wengi(more than 98%) of all with immunodeficieny have HIV virus. prevalence ya sababu nyingine za immunodeficiency is very very low, less than 1%. pia, moja ya arguments tulizojadili ni kuwa kuna watu wenye upungufu wa kinga ila hawaumwi. hiyo article imesema kwamba, magonjwa nyemelezi yako much much more prevelent in patients wenye kinga ndogo ya mwili na virusi vya ukimwi pamoja, as compared to wale wenye kinga ndogo ya mwili bila virusi vya ukimwi. naamini umeisoma vizuri article.

tukibaki kwenye historia, miaka ya mwanzo mwa 80 wakati HIV- AIDS haijaingia tanzania, neno UKIMWI halikuwepo(i stand to be corrected). UKIMWI ni neno specific kumaanisha magonjwa yanayosababishwa na upungufu wa kinga kutokana na kirusi cha HIV. same applies to AIDS.

mtu unapopata maambukizi mapya tunasema umepata maambukizi ya virusi vinavyosababisha ukimwi. unapoanza kuugua sasa baada ya kinga kushuka, tunasema umepata maradhi ya UKIMWI, kwa maana ya maradhi yatokanayo na kushuka kinga sababu ya HIV.
kuhusu upungufu wa kinga ambao hausababishwi na HIV, neno ukimwi hutumika kimazoea tu, lakini maana halisi halikidhi.

mfano, upungufu wa kinga unaosababishwa na leukemia, huitwa leukemia associated immunodeficiency ,, kiswahili chake sasa sijui. ila nadhani inaweza kuwa translated,, mimi sio mtaalamu sana wa kiswahili sanifu. nadhani unaona ugumu ulipo, ila concept ziko wazi!

mwisho, pia "syndrome" may mean a group of diseasea that progress/run/occur togather.
 
Last edited by a moderator:

Samahani Doctor,nimekuja na swali lingine...inasemekana somtime baadhi ya watumiaji wa ARV (wenye tatizo la HIV) ikatokea ameenda kupima tena anaweza kakutwa kuwa yupo negative. Je hii ni kweli au ni uongo? Kama ni kweli ni kitu gani kinachosababisha huyu mtu aonekane negative wakati alikuwa positive? Msaada tafadhari. Sisi wengine haya majanga yameingia kwenye familia zetu.
 
Facts for HIV;
A very clever virus which has managed to manipulate its existence by binding into the host DNA machinery to the extent that it is difficult to eliminate it/fight it unless you sacrifice your own cells.


Salaam mkuu multikasuku,

Hapo kwenye RED: Mwanzo unasema kwamba it is difficult to eliminate/fight HIV (a very clever virus) unless you sucrifice your own Cells. Ghafla tena unasema kwamba ARVs hazina madhara kabisa kwenye hizo cell. Mara tena unasema kwamba ARVs zina madhara hasi kama dawa zingine. Ama hizo ARVs hazi-fight huyo HIV??

Mkuu, kama wewe mwenyewe hujuwi unachokiongea ama unajikanganya kiasi hicho, mimi nishike kipi hapo??? Simaanishi kukutusi, bali sikuelewi mkuu, na mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kukuelewa hayo maelezo yako!

Hapo kwenye BLUE: Awali ulieleza kwamba ARVs zinazuia Virusi kuzaliana (to stop replication). Sasa hivi tena unasema kwamba kazi ya ARVs ni kupunguza kiwango cha Virusi. Sasa mkuu nishike lipi hapo???

Kwa uelewa wangu:

KUPUNGUZA VIRUSI inamaanisha ni kuangamiza idadi fulani ya virusi na kuviondoa!
KUZUIA KUZALIANA
inamaanisha ni kuzuia kuongezeka kwa Virusi ila idadi iliyopo inaendelea kuwepo kama ilivyo.

Sasa mkuu tuweke sawa, ARVs zinafunction ipi kati ya hizo mbili?

If ARVs zinapunguza kiwango cha Virusi, inamaana kwamba ARVs zina uwezo wa kuua/kuangamiza na kuondoa Virusi mwilini. BUT WHY ziishie kwenye kuwapunguza tu na sio kuwamaliza kabsa?

Please mkuu, tulia usijikanganye tena. Haya ni mambo ya msingi sana watu kuelewa. I sincerely like your passion of sharing this knowledge. Maintain the spirit mkuu!

CC: pakamwam, Eiyer , Deception , H1N1 , everlenk , mzee wa kigonzile
 

Mkuu hujanitag ila naomba nijibu. Principles ya dawa nyingi(sio tu ARV) ni kuzuia wadudu kuzaliana kwa njia tofauti tofauti. Hapa siongelei dawa ambazo huua wadudu moja kwa moja, maana tatizo kubwa la mdudu HIV ni kwamba a functioning and effective HIV virus anakaa ndani ya celli zenye CD4 positive receptor, maana hizo ndio celli zinazopokea mdudu huyu. Hivyo basi, huwezi kuua mdudu ambaye yuko ndani ya celli Bila kuua celli yenyewe. Sijui unapata maana hapo? Lakini pia, kila seli ina uwezo wa kuishi kwa muda fulani tu specific, halafu inakufa. That applies to all cells you know, pamoja na zile zinazojenga mwili wako. Hivyo basi, ARV zinapunguza na uwezo wa kirusi ku-infect new uninfected cells, ama zile infected cells kutoa virusi zaidi wenye uwezo wa ku-infect new uninfected cells. Kumbuka, kila cell ina muda fulani wa kuishi ambapo ukipita muda huo celli hufa. Kwa maana hiyo basi, kama kirusi kitashindwa kuzaliana kwa spidi inayotakiwa ili concentration yake ipande kwenye damu, basi itafika wakati kitakufa (natural death, pamoja na death due to immune mechanism of the body) chukua mfano :mmezaliwa sita (6) ktk familia, wanne mkapata matatizo ya ugumba hivyo mkashindwa kuzaa, wawili tu ndio wakazaa watoto. Mtoto mmoja akawa tasa, mwingine mzima. Itafika wakati mkazeeka na kufa, ama mkafa kwa sababu mbalimbali ikiwepo ugumu wa maisha je, familia yenu itabaki na watu wangapi baada ya miaka say 40 or 50? Concept hii inajaribu kueleza virusi vinapungua vipi mwilini, kama hujaelewa feel free to ask.
Ila fahamu kwamba dawa hizi haziko 100% effective, some viruses will always survive and infect new cells,, ila namba ni ndogo ndogo ndogo saana. That's why watu wanaotumia dawa sahihi vizuri, kuna kipindi ukipima HIV viral load utakuta it's almost undetectable. Hii haimaanishi kwamba virusi hakuna, ila vinakuwa kidogo sana kwenye damu, ila vingi vimebaki kwenye reservoirs (very inactive infected cells, with long half life) kwenye bone marrow na lymph nodes.
scientists wanahangaika kutafuta dawa ambayo itazuia kabisa virusi hivi kuweza ku-infect new cells, ama kuua infected cells kabla hazijatoa new infective HIV viral "cells", Bila kuua seli zingine ambazo hazina virusi (cells of the same type, eg. Cells carrying CD4 Receptor) maana ukiua hizi selli zote, utapata severe immunosuppression ambayo hata ukipata mafua tu yatakuwa so severe in way that yanaweza kukuua.

Kuelewa zaidi kwa lugha rahisi, click link hapo chini

HOW ARVs WORK
 

Doctor mkuyati og nimekuelewa vizuri sana nami ndivyo navyoelewa kwa ufahamu wangu mdogo juu ya utendaji wa ARV kwa mgonjwa ,sasa huwa natatizwa sana juu ya hili, tunajua kwamba Tabia ya mdudu HIV ni kujibadilisha badilisha , umesema huwezi ua mdudu aliyeko kwenye cell bila kuua cell yenyewe,kwahiyo ARV atamuua kwanza cell ili aweze kupambana na mdudu HIV,na mdudu HIV anachofanya huwa anaziteka kwanza cell zile na huishi ndani yake ni kama vile cell yenyewe(nipo tayari kusahihishwa kama siko sawa),sasa kama HIV anabadilika hizi ARV zinaenda kuzuia nini? Na iwapo cell mpya zimezaliwa huoni HIV ataziteka kwa urahisi maana kwanza alijibadilisha ARV akaenda kutibu ambacho sicho ,na tunajua dawa yoyote ni sumu hamuoni kuwa mnazirundika tu hizi dawa mwilini mwa mtu na mwishowe mtu anapata magonjwa mengine ambayo hayakuwepo kutokana na hizo sumu?
 
Last edited by a moderator:

Mkuu, heshima kwako.

Naomba kutofautiana na wewe kwa mara nyingine. Linapokuja swala la taaluma, sanasana taaluma za science kama medicine, kama hujui kitu afadhali ukae kimya.

Kwanza, unadai kwamba tafiti na article ya link niliyoweka imetokana na wamarekani ambao kwa Mtazamo wako, wako biased. Wewe reference yako ni kutoka watu wa wapi ambao hawako biased? Tuwekane sawa hapo kwanza. Ama ulitaka nikuwekee link ya watu wa Urusi? Unahisi ingekuwa tofauti?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…