Anko Sam
JF-Expert Member
- Jun 30, 2010
- 3,254
- 903
[/COLOR said:CLACET] Kabla sijaendelea niseme kwa dhati TRA hawakisii bali naamini
[/COLOR said:ni research ambazo wanafanya na kwa taarifa tu kuna idara ya
research iliyo na wanataaluma wa kufa mtu kazi zao ni nyingi
ikiwepo hii ya kuestablish best estimates za bei
Umetuambia tufananishe a bei ya Toyota RAV4 GX 5D Wagon 2013 - $23,300.
Lakini hujasema hiyo $ 23,300 ni FOB, CIF or retail price ikiwa TZ
Kufananisha lazima tufananishe vitu vilivyo ktk mazingira sawa.
Kwa kuwa site uliyoweka ni ya Toyota, then hiyo bei ni ya gari mpya
ikiwa japan, na haijalipiwa freight, insurance na kodi. Bei za TRA ni Retail Prices
yaani zimejumuisha kodi zote pamoja na faida kuanzia mtengenezaji hadi retail seller.
Pia tambua bei za mitandaoni saa nyingine ni promotion tu kuvutia watu waweze kujua
na mambo mengine, so ukitaka kujua bei halisi ya Toyota model hiyo kwa nn
usiende hapo toyota tz ukapata quatation? very ease way to clear your doubt zote.
Bei kuwa sawa toka 2000 ->2003 ???
Hapa tambua madhumuni ya kodi sio tu kukusanya mapato bali ina malengo
mengine ya kuadjust consuption za watu na for public interest at large.
Pia assumption ni kuwa consumers are rational ktk consumption.
Ukiambiwa utalipa kodi sawa kati ya 2000 model na 2003 model, ww utanunua ipi?
Kati ya model hizo 2 ipi unategemea kukupa more satsfaction.
The idea behind ni ku discourage kununua magari mabove ili kulinda walaji
na mazingira pia
Kuwa na Model Zote
Kwa TRA kuweza kuwa na Model zote ni ideal situation, and won't be possible
or impacticable. Hilizopo ni gari ambazo zinanuliwa kwa sana TZ na in case kuna
ambayo haipo then hiyo ni exception na exception haikosi soln, kama ilivyo kwenye
mahakama wanapotumia maamuzi yakimahakama yaliyofanywa na watoa maamuzi hapo
kabla au yaliyotolewa maamuzi nchi nyingine zenye
mifumo sanwa nasi (precedent) ktk kuamua swala ambalo linakuwa gumu au linakosa kifungu
sahihi kulitolea ufafanuzi.
Cheers,
Twende taratibu mkuu hapo kwenye nyekundu, kwa hiyo TRA wanaestablish bei za magari katika mchakato wa kukokotoa kodi wanatumia retail price, kwa maana bei ya gari pamoja na kodi (KODI IPI) wakati kodi ndiyo wanakokotoa?
Hivi wa TRA wanafananishaje uchumi wa sisi watanzania na wajerumani au nchi zilizoendelea? Kuweka hizi formular ni kama wanatukomoa, yaani used vehicle unailipia usafirisahji, ushuru, kodi na mpaka faida ya middle men hata kama hayupo! Kodi zenyewe eti toka ikiwa mpya, kisha wanazuruzunga kwa tena unailipia kodi ikifika nchini, huku si ni kukomoana!
Hizi bei za kifisadi kwenye chart ya TRA mimi sikubaliani nazo, inakuwaje MSRP (Manufacturer's Suggested Retail Price) inakuwa ndogo mara dufu zaidi ya TRA RSP (Retail Suggested Price)? Mfano:-
- Prius ya 2014 Brand New MSRP ni US$ 24,500-27,000 wao TRA RSP ni US$ 53, 890
- BMW X3 ya 2013 Brand New MSRP ni US$ 48,500 wao TRA RSP ni US$ 116,567
- Corolla ya 2014 Brand New MSRP ni US$ 16,900 wao TRA RSP ni US$ 37,187 - 41,319
- RAV4 EV ya 2014 Brand New MSRP ni US$ 49,800 wao TRA ni US$ 77,945
Kwa mwendo huu wa kulinganishwa na uchumi wa wazungu, NI WIZI MTUPU. Kama ndiyo hivyo tunataka shule na hospitali zitoe huduma sawa na Ujerumani au uingereza.