Value Retention ya bodi ya mikopo ni msiba kwa watoto wa watanzania maskini

Value Retention ya bodi ya mikopo ni msiba kwa watoto wa watanzania maskini

Kwa hiyo suluhisho ni kutoa ufadhili wa masomo kwa wanachuo wanaopata nafasi vyuo vikuu vya umma pekee na kufutilia mbali hiyo bodi ya mikopo.
Bado sijaona mantiki ya pendekezo lako. Unapofika level ya chuo kikuu hakuna tofauti kati ya anaedahiliwa private na yule wa public ki uchumi. Wote ni watanzania na wengi wanatoka kwenye family zisizomudu gharama kamili ya masomo. Ufaulu wa mtu ni kisababishi kikubwa kinacho pelekea mtu kudahiliwa chuo cha umma au binafsi. Hivyo ukiwafutia mkopo wa vyuo binafsi unawabagua na wengi watashindwa kujigharamia. Kumbuka wazazi wa wote hulipa kodi. Dawa hapa ni kuongeza kiwango cha hela inayotengwa kwa mikopo (uamuzi wa kisiasa). Uwepo wa bodi ni swala jingine kabisa linaweza kuangaliwa kwa vigezo tofauti.
Retention fee sioni mantiki yake kama taifa ni wajibu wetu kubeba mzigo huo baadala ya kuwapa vijana mzigo juu ya mzigo.
 
Daaah....yani kuna wengne wapo uku vyuoni wanatafuna hzo pesa yaani hawana habar Kama kuna hyo 6%....wengi tunaifahamu hyo percent once board wakianza kuchukua chao .

Ila zile pesa za mkopo si Kodi zetu zile jaman...kwann wasitupe bure coz mwsho wa sku zinarudi kwao tena kwa mfumo wa Kodi.
 
Wakati nasoma chuo kikuu..kozi yangu ada ilikuwa milioni moja kwa mwaka .. kwa miaka mitatu total fees ilikuwa milioni 3..

Kwa sasa hivi wanaosoma kozi kama yangu chuo nilichosoma mimi wanalipa milioni moja na nusu kwa mwaka, mwanafunzi wa sasa hivi anatumia total fees ya milioni 4 na nusu kwa miaka mitatu.

Nashangaa wanasema pesa imepungua thamani.m na kutubambikia deni la milioni 20

Ilipaswa wanidai hela ambayo inatosha kumsomesha mwanafunzi wa leo .. maana ndio dhumuni la kulipa deni.. sio sahihi kunidai deni kubwa la kulipia ada wanafunzi wa nne wa sasa wakati mimi walinisomesha mmoja tu

Nchi hii sio maskini na mliosomeshwa kwa hela ya serikali sasa hivi mmeshakua matajiri.Lipeni deni

CCM oyeeeeeeee.
 
Tulipieni na sisi ambao tangu 2014 hatujapata kazi tunahangaika mtaani mara ya mwisho 2016 status yangu ilikua unasoma 12 million... Sasa ivi kama 100 sijui
 
Kipindi cha nyuma wizara ilikuwa inatoa fungu kufadhili wanafunzi kwenye vyuo vikuu vya umma pekee, mfano UDSM, SUA, Mzumbe na kulikuwa hakuna ujinga kama huu wa bodi ya mikopo. Baadaye mapiga dili yakaleta sheria ya bodi ya mikopo ambapo ufadhili ukatolewa hadi vyuo binafsi wakaanza kufungua vyuo hadi vichochoroni. Hapa suluhisho ni kufuta hili dude linaitwa loan board na kurudisha ufadhili kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vikuu vya umma pekee...
.
.
.
Acha ubinafsi. Kwa fikra kama hizi ukizeeka utakuwa mchawi. Keki ya taifa ni kubwa acha ubaguzi wewe.
 
Acha nijipange mwanangu asije ingia kwenye mtego wa HSLB!!ni mateso tu!!
Itakuwa vyema dogo asianze maisha na deni. Lkn pia mbali na ubabe wa kidikteta wa Magufuli wa kulazimisha sheria zifanye kazi retrospectively, bado kuna makando kando mengi huko loan board ambayo ukiyazungumzia kwa sasa wataishia kukuita mkosa uzalendo. Mfano, unakuta watu wamesoma chuo kimoja, muda mmoja, course moja, lkn madeni tofauti tena kwa mpishano mkubwa sana!.
 
wadau kwa masikitiko makubwa nasema value retension ya 6% ya kila salio baada ya makato ni shida kubwa sana

kwanza wanufaika walilazimishwa kulipa asilimia kumi na tano wakakubali bado haitoshi wamewekewa 6% kila baada ya mwaka wa fedha kweli haki iko wapi.

watu wa sheria wanajua makubaliano ya mwaka jana wakati sheria haijabalika yatabaki yale yale hayataingiliwa lakini awamu hii wakavunja makubaliano hayo na kulazimisha watu wote walipe fifteen percent.

serikali hii inajinasibu serikali ya wanyonge wanyonge gani inawajali?

je msalaba huu kuwatwisha watoto wa maskini na kuwapaka kwa mgongo wa chupa eti serikali ya wanyonge ni sentensi nzuri kweli?

Ebu tujadiliane haya tunapoelekea serikali ya chama kimoja ccm hapo octoba itatokea nini.
Ideally kama uzalishaji wa ajira kwenye private sector ungekuwa mkubwa, graduates wangekuwa absorbed na mifumo ili walipe deni.

Serikali in most cases ni muajiri wa sekta ya huduma kuliko uzalishaji (production).

Kwa lugha nyingine, ilitakiwa kuwa na "loan board" kwa innovators/inventors ambao kila mwaka wanapata mikopo ya uwekezaji ili in the course of production of consumable products za kahawa, pamba, chai, korosho, katani, nyama, ngozi, samani mwisho wa siku watu waliosoma sales/marketing, accounts, logistics, engineering, legal, et la; wanapata kazi kwenye private and public sector.

Otheriwse kuna penalties zingine nchi hii huwa haziko realistic. Mfano, ukipigwa fine kwa traffic office ambayo ni sh. 30,000 in a week time kama hujalipa, deni likakuwa 37,500. Interest ya 25% in a week time haiko realistic.
Hakuna anaebariki makosa ya barabarani, ila interest ya 25% ndani ya siku 7, sijui walioiweka walikuwa wanafikiria nini. Na ndani ya mwaka kama haijalipwa inajilimbikiza.

Calculations za malipo ya mikopo kwa wale wanaolipa ambao ni wachache kwa kuwa kazi zinazotengenezwa ni chache, iko haja kuwekeza kwenye kutafuta watu wenye DNA ya kubuni uwekezaji wa kuzalisha products zenye uhitaji mkubwa kama uniforms za wanafunzi chekechea mpaka vyuo vya kati; vitambaa, viatu na mikanda ilitakiwa karibu vyote kwenye mnyororo wa thamani vizalishwa locally.

Sasa, ilitakiwa Wizara ya elimu iwe "education content model" toka kwenye mfumo wa elimu ikiwekwa kwenye vitendo iwe na uwezo wa kuatatua mambo haya kwa picha kubwa.

Hata watunga sheria wetu toka vyama karibu vyote pale mjengoni, wengi kwenye hard issues za mambo ya kitaifa kukuza uchumi na kuleta usatawi wa jamii pana, wapo kimyaaa; ila kwenye habari "nyepesi" na kubishabishana kila mmoja anachangamka

Shalom
 
Binafsi huwa najisemea ukute hii wanayoita retention fee iliwekwa makusudi kabisa ili hawa wachache wanaobahatika kupata ajira watumike kulipa na deni la wanaokosa ajira

Kila mwaka kunakuwa na ongezeko la deni, hili deni linaishaje?

Ki ufupi ukipiga mahesabu, riba ya loan board ni kubwa kuliko hata riba za mabenki.

Mbaya zaidi hakuna mwanasiasa wala chama cha wafanyakazi au nani anayelipazia sauti hili matokeo yake wametulia tuliiii wanaendelea kudunisha hali za wafanyakazi

Hii nchi ina mifumo mingi sana ya unyonyaji.

Mkopo umetokana na kodi za wananchi halafu ukichelewesha kulipa kwanza kuna penalty halafu Kuna hii value retention fee. Pamoja na makato yote hayo bado kinachobaki kinakatwa tena kodi (PAYE) bado bank ukienda kuchukua unatakatwa transaction fee, bado ukienda kutumia unakutana na indirect tax

Halafu mwisho wa siku mfanyakazi hathiminiwa, ananyanyaswa na vitu vingi vya kuudhi na mamlaka za mapato hazimjali Kama mlipa kodi mzuri badala yake unakuta certificate za walipakodi bora zimejazana kwa wafanyabiashara na hao ndio wanaosifiwa na serikali
 
Back
Top Bottom