Vanilla; yafika $600 kwa kg 1 ikiyapiku madini ya silver yanayouzwa $550 kwa kilo

Vanilla; yafika $600 kwa kg 1 ikiyapiku madini ya silver yanayouzwa $550 kwa kilo

Mara ya kwanza kusikia hili nilishtuka sana mbona hapa kwetu inauzwa cheap sana lakini vanilla Madagascar imetajirisha wengi sana Na ndio zao lao kuu kule vijana wanamaisha mazuri sana nakumbuka mwaka 2016/2017 ilikuwa kwenye $500

Sent using Jamii Forums mobile app
Hali ya vijana wa Madagascar unaijua ndugu?
 
Kampuni ziko kibao kuna kampuni moja Australia wananunua bila shida kuanzia kilo 50 na kuendelea maana zimekuwa adimu Duniani hivyo demand yake imeraise maradufu.

Sasa hivi muhimu ni kuwa na Vanilla, soko litakufuata ulipo Mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo kampuni zipo bongo au? Pia kuanzia 50kg parefu sana maana kwa Tanzania bado kilimo chetu si cha biashara bali kile cha kilo 2,tatu basi labda kwa wakulima wengi. Bei yke bukoba kweli kwa sasa ipo kwenye laki mbili hadi 3 kwa kilo
 
Kitu Kizuri sema bado maelezo yakutosha atujapata hapa
 
Hali ya vijana wa Madagascar unaijua ndugu?
Nakumbuka miaka ya 92 ndo zao Hilo lililetwa Kagera na kilo moja ilianzia kumi elf, ikapanda hadi 20 elf na sasa ni laki mbili

Watu walilima sana na mwisho wa siku bei ikawa sio rafiki na kukatisha tamaa.

Kilimo chenyewe kilikuwa ni subsistence farming. Kiukweli tatizo kubwa la vanilla linaanzia kwa wanunuzi, kwani wanapunjwa sana, na pia ina grade zake km madini.

Kwenye kilimo ni kweli huchukua miaka 3-5 na ikikomaa basi huwa kama maharage na inatakiwa kukaushwa.

Suala kubwa la kukatisha tamaa ni kuwa endapo kutakuwa na kuku, panyabuku, mvua nyingi sana, dawa na uangalizi mdogo pindi inapoanza kuzaa na hadi kukaribia kukomaa basi Muda wowote mzizi au zao lenyewe huoza Bila kujali stage gani imefika.

Kwa kifupi inahitajika iwapo utajitoa katika zao la vanilla basi ni kama unavyoenda kutafuta madini. Na tatizo ni kutokuwepo kwa wataalam wa zao Hilo na hvyo kupandwa Bila kufuata vigezo na masharti.

Kushuka mara kwa mara kwa soko ndo ilipelekea watu kukata tamaa. Maringo na kutokuwepo kwa bei elekezi napo ni tatizo.

Kwa sasa kutokn na kuongezeka kwa viwanda vingi vinavyohitaji bidhaa hvy na uhaba wa wakulima kulima zao Hilo au kupunguza au demand kuwa kubwa imeipa heshima zao Hilo kipindi ambacho wakulima imewashtua na tatizo si zao la kupanda leo kesho ukavuna.

Kwa wale wanaopenda kwenda kulima zao Hilo, ujitoe muhanga kwani zao Hilo linahitaji hasubuh hadi jioni uwepo shambani, kwani wadudu, au ndege au kushindwa kuprune kwa baadhi ya matawi kwa siku chache tu zao Hilo litakuwa hasara kwao. Hata kwenye mitandao na mengineyo weka pembeni kwa miaka hyo, utafanikiwa
 
Fred1149 nikilima naweza kuuza hapa hapa nchini?
 
linaitaj miaka mingap kukua na mazngra gan linakua vzur...
 
Tulikuwa na matikiti, mayai ya kware, mahindi, sasa vannila......haya ngoja tujionee wajasiriamali wa Tanzania ambao huwa wanakwenda na misimu maana akili zao ni za kuambukizwa.....na si za uhalisia
 
Demand and Supply ..., bei imepanda kutokana na matatizo ya biggest supplier Madagascar, kwahi ukipanda leo usitegemee hio bei three years down the road.., kuwa realistic tatizo wabongo kila kitu kikipanda mwaka huu kila mtu anahamia huko na kuacha mbachao siku ya kuvuna hakuna soko.. alafu wanaacha wanahamia kwingine ukiamua vanilla usiache tafuta masoko na jenga long term relationship na buyers sababu buyers like people who deliver..
 
Back
Top Bottom