Viatamizi vya BBT vya Unenepeshaji Mifugo ni hoi bin taabani. Raisi aliyetoa fedha anafichwa ukweli. Ngombe hawanenepeshwi ni vurugu tupu

Viatamizi vya BBT vya Unenepeshaji Mifugo ni hoi bin taabani. Raisi aliyetoa fedha anafichwa ukweli. Ngombe hawanenepeshwi ni vurugu tupu

Kididimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
4,153
Reaction score
3,800
Mimi binafsi nimetembelea vituo kadhaa vya BBT kwa upande wa Unenepeshaji mifugo kwa lengo la kujifunza. Vikiwemo Kikulula- Karagwe,Mabuki- Mwanza nk. Nimegundua yafuatayo;

1. Vijana wengi waliochaguliwa kushiriki BBT wamekata tamaa . Walichoitiwa sicho walichokikuta. Wameongezewa muda wa kukaa zaidi makambini bila kushirikishwa.

2. Ngombe walitakiwa kunenepeshwa kwa batch 4 kwa mwaka, hadi mwaka unaishilia , hata batch ya kwanza haijamalizika kufika sokoni. Imeonekana ngombe wao hawana sifa za soko, hivyo hakuna mnunuzi wa uhakika.

3. Ngombe walionunuliwa kwa unenepeshaji, hawatunzwi kwa kanuni za ulishaji vyakula vya ziada. Wanachungwa kama wa wanavijiji . Wamekaa karibia mwaka na hawajabadilika uzito.

4. Nilichokigundua ni kama zoezi lilianza bila maandalizi ya kutosha. Nafikiri Kuna watu wanahitajika kuwajibika kwa udanganyifu huo.

5. Inasemekana, hata ile ahadi ya Raisi kumpa kila kijana mtaji wa kununua ngombe 10,anenepeshe kwa mzunguko wa miezi mitatu mitatu,faida iwe yake haipo tena. Hakuna utaratibu wala kumbukumbu za wazi . Vijana wameshaelekezwa wakakope Benki.

Nimeyaeleza haya kwa lengo la kujenga. Vijana hawa ni Taifa la kesho. Tunapowapa ahadi kwa lengo la kuwaandalia ajira ni vyema tutimize yaliyokubaliwa.

Je, Mh. Raisi na Mama yetu, ndivyo hivi alivyotaka? Au kuna watu wanataka kumuangusha au kumchonganisha na vijana wetu?
 
Hakuna kitu serikali ya CCM inaweza hatabkuiba kwenyewe hawajui wanaiba kishamba angalia hata yale mashamba waliosema mambo ya block farming hakuna jipya zaidi bashe anakenua meno hajielewi kabisa yule jamaa na ukimuona alivyosmart unasema hapa tuna waziri kumbe akilini kumejaa maji ya ukoko
 
Subiri wapiga matarumbeta wake wafike
Hakuna kitu serikali ya ccm inaweza hatabkuiba kwenyewe hawajui wanaiba kishamba angalia hata yale mashamba waliosema mambo ya block farming hakuna jipya zaidi bashe anakenua meno hajielewi kabisa yule jamaa na ukimuona alivyosmart unasema hapa tuna waziri kumbe akilini kumejaa maji ya ukoko
 
Miradi mingi ya Serikali huwa inakufa kwa kukosa usimamizi ama wizi.

Angalia BRT magari mengi unakuta yamepaki kwa kukosa spare wakati mwingine ya laki 3

Hii Nchi haitapiga hatua kama tutaendelea kuongozwa na watu hao hao na Vizazi hivyo hivyo kisa Wazee wao walishaingia kwenye System
 
Nadhani Bashe angewapa homework watu wa vituo hivi, moja wapo ni jamii jirani, Mabuki, hapo hapo jirani Kuna wafugaji, lakini vituo hivi ni kama havihusiki nao, walau wachukue wafugaji kadhaa, washirikiane nao kuonyesha ufugaji Bora, wanakijiji watajifunza kwa wenzao.

Kuna kule Maruku, kituo kimezungukwa na wananchi wenye kahawa na migomba iliyokata tamaa, halafu na wananchi wamezungukwa na kikosi Cha wataalamu wa mambo hayohayo.

Kwa nini wasichague wakulima kadhaa, wakawa wa mfano, na wakulima hao wakawa kichocheo kwa wenzao?

Hawa vijana wanaopewa hizo Kambi bado hawajatulia kisaikolojia, wangetafuta wale walioanza kujitafuta, hao wanajihisi bado wako darasani na serikali inawalea, hawana idea ya kilimo biashara
 
Miradi mingi ya Serikali huwa inakufa kwa kukosa usimamizi ama wizi.

Angalia BRT magari mengi unakuta yamepaki kwa kukosa spare wakati mwingine ya laki 3

Hii Nchi haitapiga hatua kama tutaendelea kuongozwa na watu hao hao na Vizazi hivyo hivyo kisa Wazee wao walishaingia kwenye System
Kuna kitu nimekiona maeneo mengi ya kitaaluma. Kuna baadhi ya maeneo yanahitaji msimamizi awe mtaaluma mbobezi wa kitengo hicho. Na hilo halitoshi, pia awe mbunifu na athibitike pasi na shaka. Bila hayo mawili, ufanisi wa hilo eneo lazima uwe mdogo.
 
Vijana wenyewe asaivi tabu tupu. Hata wale maafisa ugani hawakai kwenye kata wanazopangiwa. Wanakaa mijini tu. Unategemea kuna kijana anaeweza kulisha ng'ombe...!!

Kitu cha msingi kwa sasa serkali iboreshe na iwekeze zaidi kwenye nyezo za kilimo. Vifaa vije kwa wingi, vijana na wananchi waelimishwe, ikiwezekena wakopeshwe bila ya riba.

Nyezo za kisasa zinamfanya mkulima avutiwe na kazi ya kilimo. Lakini kwa upuuzi unaoendelea asaivi, hata powerttiler mkulima anauziwa 15milioni.wakati bei ya kiwandani ni milion 6 au 7. serkali ipo tu.
 
Kama
Mimi binafsi nimetembelea vituo kadhaa vya BBT kwa upande wa Unenepeshaji mifugo kwa lengo la kujifunza. Vikiwemo Kikulula- Karagwe,Mabuki- Mwanza nk. Nimegundua yafuatayo;

1. Vijana wengi waliochaguliwa kushiriki BBT wamekata tamaa . Walichoitiwa sicho walichokikuta. Wameongezewa muda wa kukaa zaidi makambini bila kushirikishwa.

2. Ngombe walitakiwa kunenepeshwa kwa batch 4 kwa mwaka, hadi mwaka unaishilia , hata batch ya kwanza haijamalizika kufika sokoni. Imeonekana ngombe wao hawana sifa za soko, hivyo hakuna mnunuzi wa uhakika.

3. Ngombe walionunuliwa kwa unenepeshaji, hawatunzwi kwa kanuni za ulishaji vyakula vya ziada. Wanachungwa kama wa wanavijiji . Wamekaa karibia mwaka na hawajabadilika uzito.

4. Nilichokigundua ni kama zoezi lilianza bila maandalizi ya kutosha. Nafikiri Kuna watu wanahitajika kuwajibika kwa udanganyifu huo.

5. Inasemekana, hata ile ahadi ya Raisi kumpa kila kijana mtaji wa kununua ngombe 10,anenepeshe kwa mzunguko wa miezi mitatu mitatu,faida iwe yake haipo tena. Hakuna utaratibu wala kumbukumbu za wazi . Vijana wameshaelekezwa wakakope Benki.

Nimeyaeleza haya kwa lengo la kujenga. Vijana hawa ni Taifa la kesho. Tunapowapa ahadi kwa lengo la kuwaandalia ajira ni vyema tutimize yaliyokubaliwa.

Je, Mh. Raisi na Mama yetu, ndivyo hivi alivyotaka? Au kuna watu wanataka kumuangusha au kumchonganisha na vijana wetu?
KAma rais ni wa ccm wala usiumize kichwa anajua kila kitu...ccm ni baba la uongo na lisemapo uongo linasema yaliyo yske kwani ccm ni baba wa huo uongo tangu mwanzo
 
Back
Top Bottom