Viatu na Kivuli cha Magufuli kwa Tanzania ya Samia - Kuna cha Kuhofia?

Viatu na Kivuli cha Magufuli kwa Tanzania ya Samia - Kuna cha Kuhofia?

Rais SSH achokihitaji ni kujenga taasisi imara ya ofisi yake. Asifuate kabisa nyayo za mtangulizi wake za kutokutii kwa makusudi matakwa ya katiba, sheria na kanuni, hasa kwa upande wa matumizi ya fedha za umma na vipaumbele vyake.

Anaweza akachagua kuendelea na ujenzi wa bwawa la umeme, na SGL ikasubiri pengine kwa muda wa mbele zaidi, labda tuseme mpaka ifikapi bajeti ya mwaka 2023, ili mambo mengine muhimu nayo yafanyike kwa wakati. Hawezi kutoa kipaumbele pekee ktk hiyo inayoitwa miradi ya kimkakati iliyoachwa na mtangulizi wake.

Mathalani, hapaswi kuendelea kuwanyima wafanyakazi wa umma stahiki zao za kila mwaka ama kuchelewesha kulipa mafao kwa wastaafu. Maendeleo ya watu na vitu ni lazima viende sambamba.
 
Hakuna cha kuvaliana viatu. Kila mtu atavaa viatu vyake mwenyewe na atakuwa na miondoko yake mwenyewe.

Kuwa rais wa nchi haina maana uwe bora sana kwa kila kitu kuwazidi raia wote.

Rais atakaye fanikiwa zaidi ni yule atakayewatumia vizuri zaidi wasaidizi wake.

Tulie naye anatosha na atatuvusha salama salmini.
 
Kwanamna alivyoanza amefufua matumaini kwenye mioyo ya watu.
Ni vyema avae kiatu kitachomtosha yeye atatembea vizuri
 
Ataheshimiwa Atapongezwa Atahukumiwa kutokana na namna ataliongoza Taifa
Kuondoa makandokando
Kuondoa Ukabila
Kuondoa Udini
Kuondoa Hofu
Haki kwa kila Mtz
Kuupinga Ubadhirifu wa mali za Umma (miradi mikubwa ni moja ya Ubadhirifu period)
Kuruhusu Uhuru wa Vyama vya Siasa, Vyombo vya Habari
Nidhamu makazini( ameagiza wasiinue mabega)
Kuthamini Utu (Mahakama zinahusika hapa)
Uchaguzi Huru na wa Haki
Tume Huru
Katiba mpya (amesema tusubiri kidogo)
Zaidi Kujenga na Kuimarisha Umoja Upendo Aliyotuachia Baba wa Taifa

Si swala la kuvaa au kuvua viatu vya mtu
Rais Mpya ni Mama Samia yeye kama yeye
Yaliyopita si ndwele
Ana mapungufu ni mwanadamu
Akikosea atashauriwa atakosolewa hivyo tu
Umenena vyema sana🙏🙏 Swala hapa sio kuvaa au kuvua viatu vya mtu, au kuwa na image ya mtu mwingine as long as Yule Ni JPM na huyu ni SSH, cha msingi ni uongozi ambao unafata sheria na kanuni zake, utawala wa kijamii unaozingatia haki ya kila mwana jamii, unaotambua wajibu wake, unaotambua tofauti mbali mbali zilizo kwenye jamii na kuweza kuleta pamoja jamii hiyo na kuwa kitu kimoja kama taifa lenye msukumo wa dhati wa kujenga nchi.
Mimi binafsi sioni taswira yoyote kwa Mh. Raisi wa sasa kutoka kwa mtangulizi wake.
 
Ila jamani kuwa kiongozi kazii!!!

Najiuliza huyo m'mama sijui m'bibi kama atakuwa na wasaa wa kupita JF akasoma japo headings tu za post zinazotumwa humu wajumbe wakiwa na matumaini makubwa kwenye uongozi wake hakika kesho hataamka maana ni pressure tupu.

As for me,lolote litakalokuja uwe msoto sawa iwe heri sawa maana wakati wa hayati mpera mpera wake umenifunza kuishi mazingira yote.
 
Rais Mama Samia Suluhu Hassan hapaswi kuvaa viatu au kutembelea kivuli cha Mwendazake Hayati JPM.

Mzee Ruksa hakutembelea kivuli cha Mwl Nyerere,Marehemu Mzee Mkapa hakutembelea kivuli cha Mzee Ruksa vile vile Mzee wa Msoga hakutembelea kivuli cha Mkapa.

Ikiwa wengi hawakutembelea vivuli vya watangulizi wao kwanini Rais Mama Samia atembelee kivuli cha mwendazake.

Rais Mama Samia kumuhimiza au kumtaka kwa namna yoyote atende kama mtangulizi wake kwa maoni yangu mimi ni kumkosea heshima.Yaani mnataka Mama naye aanze kubambika kesi,atudanganye ATCL inatoa gawio kumbe mihasara kibao,au na yeye ajenge Chake Chake International Airport ndio muone kafanana na Magufuli.Enzi za Magufuli zimepita kama ziluvyopita enzi za Mwl Nyerere.Tuondolee uchuro wa Magufuli utawala wake ulimalizika Rais Mama Samia alipakula kiapo.
Yaani hi komenti yako ndio ilifaa kuwa mada yenyewe.
Safi Sana Ngongo.
 
Team JPM mnapush ajenda zenu kwa kisingizio cha viatu vya Magufuli.. no one is going to buy your propaganda Mr.
HE Samia ameanza vizur sana, tumpe nafasi aoneshe uwezo wake
1.Ubabe kwenye kodi
2.Demokrasia
3.Diplomacy
4.Media freedom
5. Kazi zenye Tija
Hiyo miradi "mikakati" ya wiz simshauri hata kidogo
 
Ila jamani kuwa kiongozi kazii!!!

Najiuliza huyo m'mama sijui m'bibi kama atakuwa na wasaa wa kupita JF akasoma japo headings tu za post zinazotumwa humu wajumbe wakiwa na matumaini makubwa kwenye uongozi wake hakika kesho hataamka maana ni pressure tu.
Mkuu sio kazi Sana ,ila mama kazi kutokana na Jiwe kuvuruga misingi ya utawala Bora inabidi mama aanze upya.
Yule jamaa alikua akilala akiamka anakuja na yake,hafuati katiba wa sheria Wala kanuni za uongozi.
Anajifanyia Mambo kivyake.
 
Team JPM mnapush ajenda zenu kwa kisingizio cha viatu vya Magufuli.. no one is going to buy your propaganda Mr.
HE Samia ameanza vizur sana, tumpe nafasi aoneshe uwezo wake
1.Ubabe kwenye kodi
2.Demokrasia
3.Diplomacy
4.Media freedom
5. Kazi zenye Tija
Hiyo miradi "mikakati" ya wiz simshauri hata kidogo
Safi Sana Mkuu wewe pia umeona wanavyohangaika kutaka kumpush mama afate njia ovu.
 
Safi
Akifuata katiba,hakuna kitu kigumu. Hakuna cha kiatu cha magufuli au kivuli cha magufuli. Hapa ni maisha yanaendelea kama kawaida tu. Alikuwa ni wa kawaida kama wanadamu wengine tu. Aliyoyafanya aliyoyafanya kwa sababu ni mwajiriwa kama wengine waliokuwa wakilipwa na fedha za umma. Kwa hiyo,tumwache huyu aliyeingia naye afanye kwa mujibu wa katiba na asijaribu kufanya nje ya maamuzi sahihi kwa mujibu wa katiba na sheria zinazomwongoza.
Maoni Safi Sana haya kuliko hoja za mtoa mada.
Mtoa mada ameanza kuteseka anaona huenda mama akafuta kabisa Jina la Jiwe kwa uovu aliotutendea.
 
..namshauri Raisi Samia Hassan awapangie majukumu tofauti wahusika wa genge la watu WASIOJULIKANA.

..Tanzania bila matusi, ubaguzi, na ukatili, inawezekana.
Majukumu tofauti kwa hao watu ni kama yapi?...taja mfano ikibidi.
 
..hili genge kulishitaki inaweza kuwa ni kazi ngumu.

..kwa hiyo wapangiwe majukumu mengine yatayawapatia kipato halali.
...vipi kuhusu waliohujumiwa na hao jamaa, wao watapataje haki yao?.
 
Kwake Mama Samia tunategemea hii miradi mikubwa iliyoanza haitaishia njiani. Nina imani naye kubwa sana na kusema ukweli yeye kama Rais ana hiari ya kuchukua namna nzuri ya kufanikisha bila kuiga nyayo za mtangulizi wake.
Lakini ili hii miradi iweze kuwa na tija, lazima tuanze kuboresha mahusiano mazuri ya majirani na wadau wengine wa maendeleo. Tufungue milango ya uwekezaji, hasa kwenye natural resources zetu. Itakuwa ngumu sana kukusanya mapato bila kuhakikisha wigo wa kupata hizo kodi unaongezwa.
Kusema kweli sasa ndio wakati wa kukumbatia dhana nzima ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, ili tufikie azma ya kujitegemea
 
Uongozi wa Magufuli ulikuwa wa propaganda na uonevu mkubwa, siyo aina ya utawala wa kuchukulia mfano mwema.

ni disaster haufai!
Ni kweli. Hebu chukua mfano wa rais kujibu maswali ya waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla. Mimi nilishasahau kama rais anatakiwa kuulizwa maswali na kutoa majibu mara kwa mara. Mwendazake alishafanya nchi kama ufalme wake, hakuna kuuliza hakuna kuhoji. Hili rais Samia anatakiwa alifutilie mbali na awe anafanya mikutano na waandishi mara kwa mara kujibu na kufafanua mambo ya kitaifa na kimataifa.
 
Rais Mama Samia Suluhu Hassan hapaswi kuvaa viatu au kutembelea kivuli cha Mwendazake Hayati JPM.

Mzee Ruksa hakutembelea kivuli cha Mwl Nyerere,Marehemu Mzee Mkapa hakutembelea kivuli cha Mzee Ruksa vile vile Mzee wa Msoga hakutembelea kivuli cha Mkapa.

Ikiwa wengi hawakutembelea vivuli vya watangulizi wao kwanini Rais Mama Samia atembelee kivuli cha mwendazake.

Rais Mama Samia kumuhimiza au kumtaka kwa namna yoyote atende kama mtangulizi wake kwa maoni yangu mimi ni kumkosea heshima.Yaani mnataka Mama naye aanze kubambika kesi,atudanganye ATCL inatoa gawio kumbe mihasara kibao,au na yeye ajenge Chake Chake International Airport ndio muone kafanana na Magufuli.Enzi za Magufuli zimepita kama ziluvyopita enzi za Mwl Nyerere.Tuondolee uchuro wa Magufuli utawala wake ulimalizika Rais Mama Samia alipakula kiapo.
Nakubaliana na wewe 100%.
Kila mtu ana namna yake ya uongozi, kufuata legacy ya mtu mwingine ni dhana ambayo naona haina mashiko. Kilicho kikuu ni sheria,kanuni na taratibu ndiyo mambo ya msingi ambayo Mh mama yetu asimamie hapo(kwa lugha rahisi Katiba)
 
Back
Top Bottom