Vibao vya Makazi vingekuwa aina moja nchini, Masasi DC ni aibu nyingine

Vibao vya Makazi vingekuwa aina moja nchini, Masasi DC ni aibu nyingine

astalavista

Senior Member
Joined
Jul 7, 2014
Posts
156
Reaction score
160
IMG_20220606_180358.jpg


Nimeona na baadhi ya maeneo uwekaji wa vibao vya barabara na mitaa namna ambavyo imeacha maswali kwa wananchi, binafsi nimeyakuta haya Masasi hasa vijiji vya Masasi Dc.

Wakati zoezi linaanza nilifikiri pengine utaratibu mpya wa kupata majina na vibao elekezi vya mitaa na barabara lingefanyika kwa weledi na umakini wa hali juu ili kuwa mpango utakaodumu muda mrefu.

Ajabu yapo maeneo vibao vimewekwa kwenye Miembe, Mikorosho, kadhalika yapo maeneo ambayo nguzo zilizobeba vibao ni miti ya mwarobaini na Msonobari, miti ambayo haiwezi kuwa imara kwa muda mrefu.

Rai yangu kwa Mamlaka husika, nikimlenga zaidi waziri mwenye dhamana kaka yangu Nape Nnauye kulitazama hili kwa ukaribu zaidi, jambo ni zuri lakini kinachoendelea sasa kwa watendaji huku chini ni kuichafua dhamira ya serikali.

IMG_20220608_181241.jpg
 
Wangepewa maelekezo nchi nzima maandishi yawe size moja na size ya vibao iwe sawa mbona watendaji wote walisoma vipimo kwenye hesabu shuule za msingi
 

Hili Zoezi Ukweli Vigogo Wanatakiwa Kutupwa Ndani Wamekula Cash,Wengine Wameruka Na Helicopter Lakini Tija Hakuna

Subiri Uje Uone Sensa Ambayo Itakuwa Aibu Zaidi
 
Wangepewa maelekezo nchi nzima maandishi yawe size moja na size ya vibao iwe sawa mbona watendaji wote walisoma vipimo kwenye hesabu shuule za msingi
Sahihi, hivi ndiyo ilipaswa kuwa. Sasa hizo namba walitafutwa wanafunzi wakaandika. Watu hawapo serious kabisa.
 
Watu wameshakula kwa urefu..nasikia kuna maeneo mengine wanalipishwa fedha za vibao.

Sijui kwanini nyumbani kwangu sijawekewa namba ya kudumu.
Wakati wanaweka mark...walichora geti, wakati wa kuweka namba za kudumu walikuta namba za mark zimefifia matokeo yake hawakuchora namba za kudumu na majirani wote wamewekewa.
 
View attachment 2254752

Nimeona na baadhi ya maeneo uwekaji wa vibao vya barabara na mitaa namna ambavyo imeacha maswali kwa wananchi, binafsi nimeyakuta haya Masasi hasa vijiji vya Masasi Dc.

Wakati zoezi linaanza nilifikiri pengine utaratibu mpya wa kupata majina na vibao elekezi vya mitaa na barabara lingefanyika kwa weledi na umakini wa hali juu ili kuwa mpango utakaodumu muda mrefu.

Ajabu yapo maeneo vibao vimewekwa kwenye Miembe, Mikorosho, kadhalika yapo maeneo ambayo nguzo zilizobeba vibao ni miti ya mwarobaini na Msonobari, miti ambayo haiwezi kuwa imara kwa muda mrefu.

Rai yangu kwa Mamlaka husika, nikimlenga zaidi waziri mwenye dhamana kaka yangu Nape Nnauye kulitazama hili kwa ukaribu zaidi, jambo ni zuri lakini kinachoendelea sasa kwa watendaji huku chini ni kuichafua dhamira ya serikali.

View attachment 2254753
Wenzao wanakula wanabakiza za dharura wao wamefakamia zote, uongozi wote wote wa wilaya na madiwani wao wajiuzulu kwa upuuzi huu.
 
Back
Top Bottom