Vibarua kiwanda cha Bakhresa Buguruni


Duh kwel kuna watu wanapitia magum sana
 
Jamaa yangu mmoja aliambiwa atoe 50k apate kazi mpaka leo hajapata ameamua kusamehe. Kuna rushwa sana Keds na ukiritimba wa hali ya juu.
2017 nilihangaika sana kuomba kazi pale lakini wapi mpaka nikakata tamaa!
Poole mkuu.
Mi nilishawahi pata kazi pale na ilikua bahati tu maana nilipewa namba ya hr na watu tulokua tunakaa pale nje kusubiri vibarua nikampigia akanambia tu njoo kesho asubuhi .

Nilienda nikafanya interview pale akacheki vyeti vyangu akanipeleka kwa mchina kule Nako nikaulizwa maswali machache nikajibu then nikapewa form ya hospital nikajaze na niliporudisha form ndo nikaanza kazi.

Sikuwahi kupewa mkataba na nilikua nalipwa kama kibarua tu na kipindi hicho wanalipwa 10000 per day.
 
Siku hizi wamepunguza kiwango cha malipo nadhani ni 7500 au 8000.
Mimi bwana nilipata nafasi ya kuingia hadi kule ndani nikakutanishwa na jamaa mmoja hivi, kanichimba chimba biti pale dogo unaweza kazi nikamjibu naweza njoo uone kazi nikapelekwa kwa washkaji wanachimba mashimo sijui yalikuwa ya choo yale aseee jamaa akaniuliza unaweza kazi nikajitutumua naweza bro, akaniambia basi nipe namba yako na majina yako nitakuita, aah wapi nikajua hapa nishalambwa kichwa!!
 
Pale mkuu wajanja wengi sana unaweza pigwa hela na kazi usipate.
 
Nakumbuka nilishawahi fanya kazi kiwanda cha kusaga chai yaani unaingia asubuhi saa 12 unatoka jioni saa 12 au saa zingine unatoka asubuhi kesho yake kwa ujira wa 2500/day na hakuna overtime.... Maisha ni safari mazee.
 
Wanalipa elfu nne hadi tatu then Kazi ni kubeba viroba vya ngano kilo 50 na 25 Kuanzia asubuhi Hadi jioni na pia night shift hipo it about fucking job huyo Bakhressa Ni mpuuzi mmoja. Including Mo dewij and so called matajiri uchwara
Wao hawana shida, shida ni Serikali ya CCM imewapagia kiwango cha kulipa vibarua, Zanzibar wao vibarua analipwa elf 15 serikali ya Dr Shein ilipaga hivyo, Na uku Serikali ikisema kibarua alipwe elfu 10 wahindi watalipa tu wao wanasema wafata Bei elekezi ya serikali
 
Hapo hata mimi lazima tu nile kona [emoji1732][emoji23]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…