Victor Wanyama Vs Mbwana Samatta

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Sijajua maendeleo ya mchezaji victor wanyama kwa record yake ya upachikaji magoli kwa sasa ipo vipi,lakini wakati kuna taarifa zikidai macho ya ma agent wengi kwa sasa afrika na ulaya yakiwa kwa samatta nini basi tofauti iliopo kati yake na wanyama?kwa kiwango aliokionyesha tutegemee atatuwakilisha katika anga za ulaya?
 
Ni mapema sana kumlinganisha Wanyama na Sammata,Wanyama alishacheza Celtic akachukua ubingwa na akacheza Champions Club dhidi ya timu kama Barcelona,now anacheza Southampton na ni mchezaji muhimu sana kwenye kikosi chao
 
Ok asante tukubali Wanyama yupo juu kwa records hizo
 
..Samatta bado hajatoka nje ya Afrika; Wanyama alishaifunga barcelona kwenye champions league akiwa na celtic, bado safari ipo.
 
Wanyama ni mkenya, Samatta ni Mzalamo wa mwanalumango "aka" wa hapa hapa.
 
Wanyama mbona yuko mbali sana, labda ungemlinganisha Wanyama na Aubemeyang ningekuelewa ingawa wanacheza ligi na nafasi tofauti.
Samatta kwa Afrika kajitahidi, ila kama anataka kwenda ulaya bado ana shughuli pevu.
 
Wanyama mbona yuko mbali sana, labda ungemlinganisha Wanyama na Aubemeyang ningekuelewa ingawa wanacheza ligi na nafasi tofauti.
Samatta kwa Afrika kajitahidi, ila kama anataka kwenda ulaya bado ana shughuli pevu.

Labda mpaka afanyeje africa ndio atapata nafasi ulaya?
 
Ngoja tumuombee samatta aende ulaya tuwalinganishe vizuri ingawa wako nafasi tofauti
 
Mleta mada Wanyama umewahi kumuona hata akicheza?
...Maana umeandika km humfahamu hivi, unasikia sikia tu n Mkenya anacheza EPL...
 
..Samatta bado hajatoka nje ya Afrika; Wanyama alishaifunga barcelona kwenye champions league akiwa na celtic, bado safari ipo.
Umeiona Barcelona tu
 
bado sana kuanza kumlinganisha samatta na mchezaji yoyote wa afrika alioko ulaya,samatta anahitaji kujituma zaidi ili kufikia malengo na sio kuskliza sifa za wabongo mwishowe akapoteza ata nafasi aliokua nayo hivi sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…