Iconoclastes
JF-Expert Member
- May 26, 2014
- 4,091
- 2,511
Wakenya ndivyo walivyo wabaguzi mno.... Cheki
( octopizzo ) anaimba nonsense lakini wanamkubali na kumbagua kimani....
Hapana, hebu weka kando hayo mambo ya ukabila Kenya for once unapodadavua mambo mengine, hasa kama haya. Haufanyii masuala fulani Kenya haki unapoyatazama kwa minzani hiyo tu.Kiukweli nimeshindwa kuelewa kama ni ukabila au wivu ?? Sema vyote viwili vina changia. Wameshadai ni mnigeria sio mkenya.
Victoria Kimani hajajitangaza ipasavyo kwenye soko la Kenya kimziki. Wakenya wengi hawamjui au hata wakiwa wanamjua, nyimbo zake pengine hawazijui. Ikiwa ameshindwa kuunyaka soko hili kimziki, Kosa sasa hapa si ni lake na mapromoters wake?
Hapo Tanzania pia si kuna wanamziki na waigizaji wazuri tu wanaopitia haya ya Victoria Kimani? Hivi Wema Sepetu ni kipi kilichomsibu?
Wewe unayesema mambo ya ukabila/wivu kwani hawa maartistes wengine wenye kutajika humu kama akina King Kaka, Octopizzo, Nyash, Avril etc mbona wasiadhirike na huo ukabila?
Ukabila upo Kenya, hatukatai, lakini nyinyi watz mnaitilia chumvi mno athari ya ukabila kwenye jamii ya wakenya!