Video: Deontay Wilder Akisema Nilichosema Juu Ya Mike Tyson

Umeanza kusema hautapigana na bingwa mpaka uwe number 1 contender. Nimekupa mifano miwili ya mabingwa waliopigana na boxers ambao hawakua number 1 contender umekana ulichokiongea.

Kugoma kupigana na number 1 contender kunakuvua ubingwa? Yes and no. Haiko hivyo direct kama ulivyoandika. Mfano sasa hivi baada ya Tyson Fury kumpiga Wilder anatakiwa kumface AJ lakini mkataba unasema title shot anagewa Wilder ama la amlipe. Umeelewa sijui hapa?

Hoja zako za namba 1 & 2 nilishakujibu. Mzee mimi ninaijua boxing yaani wewe ruka ruka ila kwa hiyo ishu huna cha kunieleza. Tafuta kipya.

Kwanini unang'ang'ania nikutajie boxer aliyekimbiwa na Tyson wakati nimekutajia kua George Foreman? Kwa hiyo Foreman ni average? Hivi upo serious boss?

Hall of Famer hupigiwa kura. Na hupigiwa na hall of famer wenzake. Umeelewa hapa? HUPIGIWA KURA NA HALL OF FAMER WENZAKE. Sasa kama wewe ni kitumbua HOF wanajua wewe ni kitumbua unadhani utapigiwa kura?

So Wilder yupo sahihi. Na ninarudia tena Tyson alimkimbia Foreman. Tyson ni kunguru. Tyson ni overrated.
 
Ivi jeuri ya kusema Mike Tyson alibebwa unaitoa wapi kaangalie mapambano yake vizur kabla hajaenda jela
 
Tujifunze kuheshim Champions boxing sio rahis hivo huyo Wilder hata mapambano 50 bado hajafika na kakutana na kina nan wakail akikutana na Aj wilder atapigwa tena hana balance za miguu kwa sasa
 
We nae sijui unaongea nini,asipigwe yeye MUNGU? Tafuta zile pambano zote alizo shindwa uone jinsi alivyokua anachapwa kipuuzi,mala nyingi tu amekua akizidiwa na unamuona tu mpaka anadondoshwa chini afu we unasema nini,eti kwa ubora wake hakuna mtu angeweza kumpiga, yeye nani?
 
Kumbe hata boxing hujui..
Unamjua frank Bruno?Kapigwa mara mbili
Unamjua Razor radock?Mara mbili kapigwa
 

1. Nimesema hautapigana (kwa mtu kama Foreman) ambaye by then hakuwa na sifa ya #1 contender then anataka kuaminisha kwamba alikimbiwa, angekimbiwa km anavodai basi tukio hilo lingemvua Tyson ubingwa.

2. Issue ya Wilder na Fury iko tied kwenye match contract yao kuwa kuna clause yenye option ya fight #3 kwa hiyo loser akitrigger ile clause na kui-activate ndani ya muda husika automatically anapata rematch, hapo issue ya A. Joshua iko solved. Lakini nadhan pia Wilder bado ni #1 contender mbele ya Fury pamoja na kupoteza last fight.

3. Kwa hiyo Mkuu unasema Hall of famers hawapigii kura 'kitumbua' ila wamempigia kura Tyson kuwa hall of famer ambaye wewe unasema alikuwa 'over rated'. Sasa kati yako wewe na hao hall of famers waliompigia kura Tyson nani mjuvi zaidi?

4. Kwenye mijadala ya watu waliostaarabika huwa hatutumii maneno kama 'yaani mimi najua huwezi niambia kitu'. Hizo ni kauli za kujihami kwa mtu asiye na hoja zenye mashiko. Ni nani aliyekuthibitisha kuwa kwny boxing wewe ni mjuvi kuliko wote humu?
Learn to raise the strength of your arguments not the volume of your voice.
 
Ivi jeuri ya kusema Mike Tyson alibebwa unaitoa wapi kaangalie mapambano yake vizur kabla hajaenda jela
Mbona wengi mnasingizia jela?

Ali alikwenda jela hakwenda?
 
Huyu jamaa naona yuko so obsessed na Tyson, halafu anajiona 'anajua' kuliko kila mtu na anasema kwenye boxing 'hatuwezi kumueleza kitu humu'
Usinilishe maneno.

Nimesema katika swala la namna contender anapatikana hauna cha kuniambia. Basi sijaongeza zaidi.

Pia siko obssessed na Tyson. Nipo obssessed na boxing.
 
1: Sina cha kuongeza.

2: Mimi ndiye niliyepoint ishu yako siyo direct kama ulivyoandika so unadadavua ambacho nimeshakisema.

3: Hoja katika ishu ya HOF ilikua ni kupinga ulivyosema HOF haina maana.

4: Usinilishe maneno boss. Nilikua clear, nikasema hauna cha kuniambia juu ya contender anavyopatikana.
 
Kumbe hata boxing hujui..
Unamjua frank Bruno?Kapigwa mara mbili
Unamjua Razor radock?Mara mbili kapigwa
Boxing najua ila wewe hukunielewa.

Nilisema.

Boxer ambaye amempiga Tyson, mfano Evander.

Walivyorudiana Tyson alishinda?

Siyo kama hiyo mifano uliyotoa ambao hawakumpiga Tyson tangu fight one.
 
3: Hoja katika ishu ya HOF ilikua ni kupinga ulivyosema HOF haina maana.

Nisome vizuri hakuna sehemu nimesema hall of fame haina maana ila nimesema siyo kigezo pekee cha ubora wa boxer.

Na nikaongezea ili mtu awe hall of famer inabidi awe na long and successful ending career. Hapo nilikuwa najibu swali la Wilder kuwa Tyson aliwapiga bondia ambao hawapo kwenye hall of fame, kuna bondia ambao walidrop baadae na wengine career zao zikaishia njiani hivyo hawakupata sifa za kuwa hall of famers.

Unamfahamu bondia aliyeitwa Edwin Valero? Huyu alitamkwa kuwa one of the best boxers the world has ever witnessed. Hadi anajiua 2010 akiwa jela kwa tuhuma za kumuua mkewe, alikuwa na record ya 27-0 with 100% KO record. Lakini huwezi kumsikia akiingia hall of fame sabab ya namna career yake ilivyoishia,huo ni moja ya mifano ya boxers wakali nje ya hall of fame.
 
Kwanini Buster hakuweweseka?
Mkuu mbona Buster aliweweseka mwishoni mwa round ya nane?
Hukumbuki jinsi Tyson akivyosukuma upper cut ya mkono wa kulia iliyompeleka Buster chini? Ilikuwa bonge la opportunity kwa Tyson maana alikuwa amezidiwa tayari na Buster; sema tu referee alifanya usanii kwenye 'counts' kwa kuzitamka taratibu (long counts) hadi pale kengele ilipogongwa.
 
Sijawahi kumsikia Valero
 
Ni bondia aliyepigana uzito wa kati, alikuwa mvenezuela hatari sana. Wakati anafikisha mapambano 18 yote alikuwa ameshinda kwa Ko katika round ya kwanza,alikuwa na speed,power na passion ya boxing. Ila alikuwa na shida ya discpline sana, alikuwa mkorofi na mtukutu mno. Alimuua mkewe na baadaye kujisalimisha polisi ambapo baadae alijiua pia akiwa gerezani mwaka 2010 huku akiwa na record ya mapambano 27-0 na yote alishinda kwa Ko.
Sijawahi kumsikia Valero
 
Muhammad Alli aliwahi kuhukumiwa kwenda jela miaka 5 baada ya kukataa kushiriki katika vita dhidi ya Us na Vietnam lakini hakutumikia kifungo baada ya uamuzi huo wa mahakama kubatilishwa kutokana makosa yaliyoainishwa kwenye hukumu.

Kama sikosei nadhani moja ya mapungufu ilikuwa Alli aliitwa kwa jina lake la Clay wakati wanatajwa wa kwenda vitani wakati huo jamaa alishabadili dini na hivyo aliuchuna kama si yeye.

Ingawa baadae alipohojiwa alisema wazi kuwa hawezi shiriki kwenye vita ya 'watu weupe' na hata hivyo haoni makosa ya Vietnam dhidi ya Us, hawajamtukania asili yake,hawajambaka mama ake na wala hawajampokonya chochote baba yake.
Bro he did
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…