Video: Dkt. Bashiru aliletwa CCM na Hayati Magufuli; Asilaumiwe kwa aliyotenda

Video: Dkt. Bashiru aliletwa CCM na Hayati Magufuli; Asilaumiwe kwa aliyotenda

Hata kama alikuwa na nia nzuri basi angefuata mchakato wa chama namna ya kumpokea mwanachama mpya. Ila kumleta mtu ambaye hajui chochote kuhusu chama na kumpa majukumu makubwa vile ilikuwa ni UHAYAWANI
Hivi kwani kuwa mwanachama wa CCM lazima uende shule?!

Hizo ilani zao na taratibu zao nyingine si zipo kwenye vitabu kila siku wanazisoma, kwani hao waliozeekea huko CCM wana kipi cha tofauti kuwashinda waliokuja kama sio ufisadi na kuiba kura tu?

Magufuli achukiwe kwa sababu za msingi, sio hizi za kuokoteza okoteza tu na kumtupia.
 
..Dr.Bashiru kuwa Cuf na kuandikishwa ktk Ccm na Magufuli sio tatizo.

..Tatizo ni mwenendo wa Dr.Bashiru alipokuwa ktk Ccm kama Katibu Mkuu wa chama.

..Ccm iligeuka kuwa genge la majambazi na wapiga propaganda za kumtukuza Magufuli. Na Bashiru ndio alikuwa Mtendaji Mkuu wa chama.
 
Kama ni kutekana kulianzia kwa kina Ulimboka, na kuuana, mwenyekiti wa CDM Usa River Arusha akachinjwa kwa chain saw, hapo kwa Magufuli ulikuwa ni muendelezo tu.

..Magufuli uliupaisha huo ukatili unaouzungumzia.

..Mambo mabaya yalianza kufanywa waziwazi huku wanaCcm wakitamba, kufurahia, na kuwakejeli waliofikwa na majanga.

..Kwa mfano, Katibu Mkuu Kinana na Waziri wa mambo ya ndani hawakuwahi kupanda majukwaani na kuanza kumkejeli Dr.Ulimboka.

..Lakini Dr.Bashiru alisikika akimkejeli Tundu Lissu aliyepigwa risasi. Waziri wa Mambo ya ndani alisikika akitoa kauli za kipotoshaji kuhusu kilichotokea.

..Tofauti ya ukatili wa awamu ya 5 na zilizopita ipo ktk kiburi,uthubutu, na ufahari, uliokuwa ukionyeshwa na Ccm na serikali wakati mambo mabaya yakiwatokea wakosoaji wa serikali.
 
Kama ni kutekana kulianzia kwa kina Ulimboka, na kuuana, mwenyekiti wa CDM Usa River Arusha akachinjwa kwa chain saw, hapo kwa Magufuli ulikuwa ni muendelezo tu.
Mkuu ninachojifunza hapa ni kuwa kuna watu hapa nchini walishazoea wizi, so walipoziba mrija wakaanza kumchukia aliyeziba na ndiyo one of the syndicate ambayo jemedari or jeshi la mtu mmoja alifanya.

Hawa wanamsema jeshi utadhani yaliyotokea kipindi chake hayaja wahi tokea huko nyuma.
 
..Dr.Bashiru kuwa Cuf na kuandikishwa ktk Ccm na Magufuli sio tatizo.

..Tatizo ni mwenendo wa Dr.Bashiru alipokuwa ktk Ccm kama Katibu Mkuu wa chama.

..Ccm iligeuka kuwa genge la majambazi na wapiga propaganda za kumtukuza Magufuli. Na Bashiru ndio alikuwa Mtendaji Mkuu wa chama.
Sahizi ccm sio genge la majambazi? Bado Bashiru yupo?
 
Kama ni kutekana kulianzia kwa kina Ulimboka, na kuuana, mwenyekiti wa CDM Usa River Arusha akachinjwa kwa chain saw, hapo kwa Magufuli ulikuwa ni muendelezo tu.
Kwani nimesema utekaji hakukuwepo kabla ya Magufuli?
 
Ni kweli Bashiru Ally bado mwanachama wa CUF. Kadi yake Namba 01201100 ya aliyokata tarehe 14-03- 2009 hii hapa;
View attachment 2425211

Kama kuna mwenye ya CCM atokeze aiweke hapa
Hii kadi iwe original au fake, haina maana, kwasababu haimuondolei Bashiru haki yake ya kutoa maoni.

Hiyo ni haki ya kila mtanzania, awe mwanachama wa chama cha siasa, au asiwe nacho, acheni kuiga ujinga wa wengine.
 
Mkuu ninachojifunza hapa ni kuwa kuna watu hapa nchini walishazoea wizi, so walipoziba mrija wakaanza kumchukia aliyeziba na ndiyo one of the syndicate ambayo jemedari or jeshi la mtu mmoja alifanya.

Hawa wanamsema jeshi utadhani yaliyotokea kipindi chake hawayaja wahi tokea huko nyuma.

..Na Ssh naye kaziba mirija kwa genge la Jpm na ndio hao wanaomsema vibaya sasa hivi.
 
Sijui kama umeitazama hiyo video na kuielewa vizuri, Magufuli alikuwa very clear kwanini alimpeleka Dr. Bashiru CCM, anasema alimpeleka ili kuondoa uozo wa mazoea alioukuta ndani ya CCM, na akasema anawataka kina Bashiru wengi ndani ya CCM.

Unapolaumu ujio wa Dr. Bashiru ndani ya CCM unaonekana hujui hata sheria za vyama vya siasa, ulitaka CCM wamtenge Dr. Bashiru kwa sababu gani? utambue kila mtanzania anatakiwa kujiunga na chama chochote cha siasa akipendacho, hiyo ni haki ya kila mmoja, usiendekeze siasa za makundi ndizo zinazoitafuna nchi.

Unaigeuza CCM mali ya watu binafsi ndio maana sasa wamejaa viburi, majibu ya dharau, na kuteuana kwa kujuana, kumbe tatizo ni letu wenyewe tunalea huo ujinga bila kujua.
halinaga akili hilo.
 
..Magufuli uliupaisha huo ukatili unaouzungumzia.

..Mambo mabaya yalianza kufanywa waziwazi huku wanaCcm wakitamba, kufurahia, na kuwakejeli waliofikwa na majanga.

..Kwa mfano, Katibu Mkuu Kinana na Waziri wa mambo ya ndani hawakuwahi kupanda majukwaani na kuanza kumkejeli Dr.Ulimboka.

..Lakini Dr.Bashiru alisikika akimkejeli Tundu Lissu aliyepigwa risasi. Waziri wa Mambo ya ndani alisikika akitoa kauli za kipotoshaji kuhusu kilichotokea.

..Tofauti ya ukatili wa awamu ya 5 na zilizopita ipo ktk kiburi,uthubutu, na ufahari, uliokuwa ukionyeshwa na Ccm na serikali wakati mambo mabaya yakiwatokea wakosoaji wa serikali.
Unaposema Magufuli aliupaisha huo ukatili maana yake unakiri ulikuwepo kabla.

Kumbe basi, kosa sio la Magufuli peke yake, hata wapinzani nao wana kosa kwa kushindwa kuulaani huo ukatili ulipotokea mwanzo kwa nguvu ile ile waliyotumia kuulaani wakati wa Magufuli.

Masuala mengine uliyoandika hapo ni tabia binafsi za watu, kwasababu hata kama Ulimboka alitekwa akapigwa, tayari aliumizwa, kutokusemwa vibaya baada ya kupigwa, hakuondoi ukweli kwamba alipigwa na kuumizwa.
 
Hivi kwani kuwa mwanachama wa CCM lazima uende shule?!

Hizo ilani zao na taratibu zao nyingine si zipo kwenye vitabu kila siku wanazisoma, kwani hao waliozeekea huko CCM wana kipi cha tofauti kuwashinda waliokuja kama sio ufisadi na kuiba kura tu?

Magufuli achukiwe kwa sababu za msingi, sio hizi za kuokoteza okoteza tu na kumtupia.
Wewe una mapenzi ya dhati na Mwendazake. Maana unatetea uvunjaji taratibu, endelea na mahaba yako
 
Kumbe hata hujui kutekana kunaangukia kwenye kundi la ubabe, nyie bado wachanga sana, endeleeni kuimba tu mapambio yenu!.
Huelewi hoja, hoja sio kuwa CCM ilikuwa haifanyi ubabe huko nyuma, hoja ni kuwa Magufuli ndio ilikuwa next level
 
Kwenye video Hayati Magufuli anasema alimtoa Bashiru Ally CUF na kumleta CCM, hivyo basi wanaomlaumu Bashiru hawamtendei haki. Yeye siyo mwanachama wao.

View attachment 2425193


Magufuli aliharibu sana misingi ya CCM
Acha upotoshaji wewe. Umewahi kusikia cuf wanasema popote Bashiru Ally alikua mwanachama wao? Niwale wezi wa mali za ccm peke yao ndio walipoona kawapopoa macho kwenye uchunguzi kuhusu mali za chama wakashikwa na kiwewe kuona anakua katibu mkuu wa ccm.
 
Back
Top Bottom