Video hii ya Kangi Lugola inatukumbusha kwamba madaraka ni dhamana ya Muda mfupi sana, Napendekeza itumike mashuleni kufundishia

Miezi takriban 18 iliyopita Kangi Lugola alimdhalilisha mkuu wa magereza na team yake mbele ya kamera na waandishi wa habari. Wiki hii Kangi Lugola atakua mgeni wa team ile ile aliyoidhalilisha.
ITAENDELEA......
Omba yasikukute 😂😂🤣🤣🤣
 
Hawa askari magereza baadhi ya watu wanawadharau sana lakini ukiingia kwenye anga zao ihiiiiiiiiiiiiiiii!!
 
Lugola alimdharau CGP sasa anaenda kupangiwa kazi na kiherehere aka msaidizi wa nyapara.
Halafu magereza wanatakiwa wajilishe wenyewe, yule mheshimiwa sijui jembe analiweza?
 
Bado sitaki kuamini kama Mh Kangi aliwahi kuamini kama kuna siku atakuja kuondoka madarakani kwa aibu kiasi hiki .

Nawaomba sana vijana mnaopata madaraka leo mjifunze sana kwenye jambo hili
View attachment 1335233
Hahahaaa maisha yanaenda kwa kasi sana maana alio wasulubu bado wanamadaraka wakati yeye akiwa huko kusiko julikana kwakweli hawa wateuliwa waache sifa za kijinga na uonevu kwa kiburi cha madaraka
 
Heh. This country buana!!!
Lugola amechomoa kirahisi tu.
 
Hili la watendaji wa serikali kulazimishwa kubeba ilani ya CCM, linapaswa kukemewa. Kazi ya kubeba ilani ya Waziri sio IGP
 
Hapa ndio utajua Mungu yupo majigambo majivuno peleka kwa mkeo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…