Video: Jeshi la Maji la Uingereza latumia teknolojia ya mtu kupaa kupambana na uharamia

Video: Jeshi la Maji la Uingereza latumia teknolojia ya mtu kupaa kupambana na uharamia

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Jeshi la Maji la Uingereza limefanya majaribio ya kutumia mavazi maalum yanayomwezesha mtu kupaa kwa lengo la kuboresha operesheni za kuzuia uharamia baharini.

Kampuni ya utafiti wa teknolojia ya anga ya Gravity Industries imechapisha video inayoonesha wanajeshi hao wakifanya mazoezi kwa kutumia teknolojia hiyo mpya katika meli ya kivita ya HMS Tamar ya Uingereza.

Wanajeshi hao walifanya mazoezi ya kupanda meli, kufanya ukaguzi na kumkamata adui (ama VBSS) kutokea kwenye boti ya mwendokasi iliyokuwa ikiifuatilia meli hiyo, ambapo wanajeshi hao walitumia teknolojia ya kupaa kwa kutumia mavazi hayo maalum.



Kampuni hiyo imesema Makomando 42 wa Jeshi la Maji walishiriki katika operesheni hiyo kwa muda wa siku 3, operesheni inayotajwa kuwa ya hatari zaidi kwa Jeshi la Maji.

Hata hivyo, Jeshi halijaeleza ikiwa itanunua teknolojia hiyo. Teknolojia hiyo imewahi kutumiwa na wahudumu wa dharura kuwaokoa watu walio katika mazingira ya hatari, na inatajwa kusaidia kuokoa muda ambao ungetumika kuwafikia kwa miguu au kwa gari.

Teknolojia hiyo bado ipo kwenye hatua ya majaribio, na inatajwa na Kitabu cha Kumbukumbu cha Guiness kuwa ndiyo teknolojia inayoshikilia rekodi ya kuwa na kasi zaidi kwa mavazi maalum yanayovaliwa inayomwezesha mwanadamu kupaa, ikifikia maili 85 kwa saa (kilometa 136.8) katika majaribio mwaka 2019.

Chanzo: Business Insider
 
Hili vazi walilionyesha kama si mwishoni mwa mwaka jana ilikuwa mwanzoni mwa mwaka huu. Wakizungumzia utumiaji wa vazi hilo kwa kwa ajili wahudumu wa afya kuwafikia wagonjwa ama watu walio katika mazingi hatarishi ambayo ni magumu kufikika.

Sent from my cupboard using mug
 
Ni teknolojia nzuri sana ila suala la uwezekano wa kutunguliwa kwa mrukaji/mpaaji na maadui limezingatiwaje ili kuhakikisha usalama wake?
 
iron man kumbe ni kweli
 
Richard Browning is a British inventor of a "jet suit". He is the founder and chief test pilot of Gravity Industries Ltd, a company that designs and builds his invention.
Prior to founding Gravity, Richard was a Royal Marine reservist for six years and an oil trader with BP for 16 years.
Richard received initial investment and launched the company Gravity Industries Ltd in April 2017 together with WIRED magazine and Redbull. Public demonstrations of the invention included over 100 flight events across 33 countries before COVID shut down travel in March 2020. Richard was also dubbed the "real-life Iron Man" by several media outlets.
NB;Africa bado tena sana!

images (5).jpeg


images (4).jpeg


images (3).jpeg


images (2).jpeg


images (1).jpeg


images.jpeg
 
Hilo vazi wangeliacha tu kwa matumizi mengine siyo kupambana na uharamia. Yaani utalipuliwa usipate hata nafasi ya kushangaa.

Sent from my cupboard using mug
 
Back
Top Bottom