VIDEO: Msanii Roma na wenzake warejea rasmi uraiani. Kufunguka Jumatatu

VIDEO: Msanii Roma na wenzake warejea rasmi uraiani. Kufunguka Jumatatu

..polisi wamewahi kuua raia nchi hii sembuse kuteka? Hukuona kilichomtokea Daudi Mwangosi?
Mzee tunaongelea utekaji. Mauaji hata madereva wa mabasi kila siku wanaua watu barabarani
 
Huku zanzibar kuna mazombi yanajifunika nyuso kushambulia raia,mamlaka za nchi hawawatambui mazombi hayo kwa hiyo si ajabu hata huko kwenu watekaji hawatambuliwi na mamlaka za serekali,kilichobakia kwa raia ni kujihami zidi ya vikundi hivyo la sivyo mtamalizwa watanganyika.
 
Nilishawah kujiuliza hiki kitu kuwa ikitokea hawa watekaji wakizidiwa nguvu/ timing na wakafanywa vibaya ikaja kugundulika n sehemu ya vyombo vya dola, je watakanwa na govt, ama watatetewa na govt!!???
 
Kuna uwezekano watekaji sio part ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama. Which means ni vijana tu makatili wanaotumiwa kwa ujira na kufanya kazi kwa maelekezo ya mabosi wao wanasiasa.
Lakini inawezekana pia ni vijana waliochomolewa kwenye taasisi yetu ile nyet na kufanya kazi nije ya utaratibu wao rasmi. Afadhali kama ni kundi la kwanza maana kwa jinsi walivyo kanwa na mamlaka rasmi kama ni hilo kundi la pili patakua shida.
From now on kosa dogo kwenye timing yao ndugu zao na taifa litapata hasara maana ni vijana wetu. They are working day and night for safety of this nation na sio kulinda interest za mtu mmoja.
Nimewahi kushuhudia askali wa voda fasta akipigwa hadi kuzimia na mob justice pamoja na bastora yake pale Mindu village morogoro. Hao watekaji wamekanwa na mamlaka zinazo tambulika. And they are not that invisible wasijidanganye, i dont want to imagine what will happen to them siku wakistukiwa.

Hivi hakuna namna ingine which is the best way kusolve What ever the misunderstandings tulizo nazo?
Hii komoana, visasi , kutekana itapelekea maafa kwa victims na hata watesaji wenyewe. Narudia tena they are not that invisible na vijana ambao wanatii amri haramu huku

Kama unaelewa nguvu za Serikali. Usingeandika gazeti refu. Na sijaona ukisema kuwa katika mazingira haya ya Watz wengi wa mitandaoni kupenda kutuhumu bila ushahidi ni rahisi mtu wa pembeni ambaye anwajua kondoo zake walivyo kufanya matukio ya ajabu. CIA Wanafanya sana kwenye nchi ambazo wanabania masslahi ya USA. Wtz hatujui tunataka nini. Kwa maana hiyo. Hakuna kiongozi mtakayempenda. Labda muuza Nchi. Ambaye .siasa kwa kiongozi wa juu huwa tunahitaji will power na msimamo ,wtz wanataka mtoa hela. Tukijua kabisa Sisi ni maskini sana. Ila kila siku Mifano USA. Oh Ulaya. Nk.
 
Hivi pale ofisini Ilala watu wanaangalianaje bosi wao anapoingia huku kagubikwa na tuhuma nyingi na chafu namna hii? Mara vyeti, mara kunyang'anya matajiri mali, mara kusingizia uongo watu, mara tena malinda na sasa utekaji watu!
Hivi kweli huyuhuyu aliyekuwa anasema ofisi yake yote wafanyakazi wa kweli hawazidi wanne wengine ni mzigo hata wakiondoshwa anaweza kweli kufanya kazi kwa ufanisi tena?
 
Bongo ina mengi mama ee, kila kukuchapo mambo mapya - King Kikii
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Kama unaelewa nguvu za Serikali. Usingeandika gazeti refu. Na sijaona ukisema kuwa katika mazingira haya ya Watz wengi wa mitandaoni kupenda kutuhumu bila ushahidi ni rahisi mtu wa pembeni ambaye anwajua kondoo zake walivyo kufanya matukio ya ajabu. CIA Wanafanya sana kwenye nchi ambazo wanabania masslahi ya USA. Wtz hatujui tunataka nini. Kwa maana hiyo. Hakuna kiongozi mtakayempenda. Labda muuza Nchi. Ambaye .siasa kwa kiongozi wa juu huwa tunahitaji will power na msimamo ,wtz wanataka mtoa hela. Tukijua kabisa Sisi ni maskini sana. Ila kila siku Mifano USA. Oh Ulaya. Nk.
Sijaelewa ushuzi ulioandika Hata kwa kurudia rudia. Usk mwema
 
Vyombo vya dola vya bongo vinatuchukulia poa sana ndo maana watu wanathubutu kwenda nyumbani kwa mtu na kubeba vifaa na kukamata watu bila hata mjumbe kujulishwa-ambapo hata akijulishwa ni kinyume cha sheria kwenda kwa mtu na kupekua na kubeba vitu usiku bila hata search warrant.

Vyombo vyetu vya dola vinatumia mwanya wa watanzania wengi kutokuwa na silaha. Yes! Ukiwa na silaha yako una haki ya kupiga risasi na kuua mvamizi yoyote anayekuja kwako usiku. FBI learnt the hard way about taking matters into their own hands during what is famously known as the Waco Siege.

Kwa kifupi, familia ya mchunguji flani jamii ya kibwetere alikuwa na ranchi yake ambapo waumini wake walikuwa wameleweshwa imani na walikuwa hawaambiliki. Mchungaji huyo pia alikuwa na duka la kuuza silaha. FBI walikwenda kwake bila search warrant, tena mida ya usiku wakiwa wanamtuhumu kwa makosa ya silaha na madawa ya kulevya. Walipoingia kwenye ranchi hiyo sekeseke walilolipata hawatakuja kulisahau maana liliua watu 82 wakiwemo askari na waumini wa jamaa. Na risasi zilipigwa kwa siku 50! Kosa la FBI lilikuwa kwenda kwa jamaa bila search warrant, kama Roma alivyodakwa bila search warrant wala mwenyekiti wa mtaa kujua, Tena unapobeba mali za mtu nyumbani kwake, kimsingi unampekua. Ndugu zangu, sheria inawalinda siku mkikutana na askari wajinga kama hawa, if you are loaded, take them down.

Kwa mengi zaidi kuhusiana na Waco Siege:Raid, fire and rubble: The Waco siege in pictures 20 years on from the cult massacre

Nakubaliana na uchambuzi wako 1000%.

Wow! Good story, I remember that day very well It was summer of 1996...This saga is also well known as "The Davidians" It happened during Clinton administrations under the order of the Attorney General (AG) the late "Iron lady" Janet Reno.

Kwa kifupi, US government, hata kama iliwashinda waumini wale kimabavu kwa kuwachoma kwa moto wa gesi waumini wale mchana kweupe na huku ikitumia silaha zote nzito za kivita vikiwemo vifaru na magari ya dereya ndani ya himaya (ranch) ya "The Davidians" haitokaa isahau upinzani mzito walioupata kwa wahanga wa kundi/jamii ile lililokuwa linajitambua na kutambua haki zake. Binafsi naweza kusema lilikufa kishujaa.

Serikali ya Tanzania ya sasa inawachukulia WaTanzania for granted...lakini wakae na wajue mbegu ya "radicalism" wanayoipanda kwa dhuluma hizi siku moja itafika mahali watu watasema 'enough is enough" kama "mbwai na iwe mbwai "
 
wenye akili tumeshajua kilichoendelea!!!!! wamefungwa speed gavana kama Dr. olimboka, Serikali hii ya CCM majanga@
 
nimeyaamini maneno yako leo mara baada ya Waziri mwenye Dhamana kujiumauma kujibu maswali ya waandishi
Eti mimi ndiye waziri mwenye dhamana na yoyote anaetaka kumhoji msanii nifahamishwe. Maaana yake ni kuwa serikali haihusiki. Hawa wanatufanya sisi ni watoto wa chekechea ehh.
 
Eti mimi ndiye waziri mwenye dhamana na yoyote anaetaka kumhoji msanii nifahamishwe. Maaana yake ni kuwa serikali haihusiki. Hawa wanatufanya sisi ni watoto wa chekechea ehh.
ngoja tuone mwishowe... Hii nchi ...puuuuuuuuu!!!!!!iiiii
 

..aisee?!

..let me give u hint na haya mambo ya utekaji.

..tafuta habari za kisa cha Matiko Matare aliyekuwa kiongozi wa mgomo wa wanafunzi udsm na Jaji Warioba wakati huo akiwa Waziri Mkuu.
 
Back
Top Bottom