Video na picha: Waafrika weusi tii walioishi India miaka elfu 60

Ndugu zangu waafrika,msijione kuwa nyinyi mmetengwa na mungu la hasha, nyinyi ndio mulioanzisha ustaafrika wote huu,wako watu watajaribu kuwadanganya na kuwavunja mioyo lakini ukishajitambua utawaambia mimi ndo "mwanzilishi".
 
Hawa ndio "moors"walioivamia na kuitawala spain kwa karne nyingi.
 
kaka kama umetokea sehemu za ukanda wa pwani au kanda ya ziwa, wavuvi wengi walikuwa wanasafiria nyota, wanaijua nyota flani ya mashariki watafika sehemu yoyote, na wavuvi ni watu wanaweza kutabiri hali mbaya ya hewa baharini au ziwani kuliko hao watu wa mamlaka ya hali ya hewa, nimekaa na wavuvi unguja na mwanza, nimejifunza hicho kitu, hivyo ni nyota ndio zilikuwa zinawaongoza, kuna zile zinazoitwa kilimia, hizi ndo sana walizokuwa wanatumia
 
Elimu ya kutumia nyota ni sisi waafrika ndio wagunduzi,wayunani waliipeleka mabara mengine..na ushahidi tunao.
 
Elimu ya nyota tuliipeleka misri kabla wayunani kuiiba na kuifanya ya kwao.
 
IMHOTEP akiwa ktk jumba la makumbusho la CAIRO karibu na medani ya TAHRIR.
 
Sanamu za majeshi ya farao zikiwa ktk jumba la makumbusho la cairo. Mashujaa hawa walitawala dunia kwa miaka elfu tano na ushee..pia walikuwa warusha mishale hatari kabisa duniani.
 
Baadhi ya mabaki hayo ya wenzetu wakiangalia kwa hamu kubwa mafanikio ya mababu zetu.
 
Hii mada imenifanya niingie youtube kuchimbua mambo, kuna moja inaitwa "The Real Black History they don't want you to know" aisee
 
Hili sanamu linaonyesha mwafrika akishambuliwa na simba inaaminika ulikuwa ni wakati wa mfalme nimrood limefukuliwa nchini irak.kumbuka nimrood pia alikuwa mtu mweusi.
 

Attachments

  • Nimrud_ivory_lion_eating_a_man.jpg
    123.9 KB · Views: 109
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…