Video: Polisi wavunja ofisi ya CHADEMA mkoani Kigoma


Muogope Mungu unaita binadamu wenzako manyani. Wewe ukiitwa hivyo utafurahi. Hata Kama ni siasa tupunguze chuki. Hakuna aijuaye kesho. Anayecheka Leo kesho anaweza kuwa ndio muombolezaji.
 
Yaani nyie genge mmefight sana kurudisha haya mambo ya kishenzi ya bwana wenu ili tu mje mpost utumbo kama huu ulioandika.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mafiningo tuwe wazalendo na wenye hekima. Hii ni chi yetu sote, hatuna nchi nyingine zaidi ya hii Tanganyika/Tanzania. Kama umewahi kuishi nje za nchi utakubaliana na mimi ila kama maisha yako yote yamekuwa bongo unaweza usinielewe. Soma historia ya mataifa yote yaliyoendelea, utagundua wasaliti kama akina Mbowe, Lisu waliuawa kwa kunyongwa. Ila sasa wao baada ya kustaarabika na watu wao kuwa incorruptible sasa wana enjoy uzalendo. Mzungu anaweza kuwa na maslahi binafsi ila linapofika suala la kitaifa usahau kumrubuni. Nchi zetu hizi wanasiasa wanageuza siasa kama uanaharakati. Wakumbuke Dr Slaa alivyojenga chama, alikuwa na hoja, kila apoleta hoja zake zilikuwa na mashiko, pamoja na kuchukiwa na serikali lakini alikuwa na heshima linapofika jambo la kitaifa. Huyu huyu Mbowe na Lisu walivyo wasaliti, sidhani kama ukiwapa nchi wanaweza kuwa wazalendo. Yaani ukitaka kuona huyo malaika mnayemtetea ni kimeo wewe angalia tu katiba ya chama aliigeuza ili atawale milele, sasa je angepewa nchi si ndiyo angebadili katiba ili awe Mfalme?

Kikubwa tuendeshe siasa zenye maslahi mapana ya nchi. Usione tulikuwa kimya, tuliwaacha mteme nyongo zote ili tupate ushahidi wa nani mnafiki, nani si mzalendo then tujuie ni nani anafaa kuwa mtumishi wa watanzania kwa vizazi vijavyo, lakini wengi wenu mmeharibu mafaili yenu, yamechafuka yananuka vibaya mno. Msidhani matusi yenu ya kumtukana Dkt JPM hayajarekodiwa, yapo yoote kabisa, na sasa mtaanza kulipia mmoja baada ya mwingine ili mjue hii ni nchi inaendeshwa kwa misingi ya uzalendo na sheria. Na mkitaka kujua JPM alipendwa subirini 2025 muone legacy yake itakavyotumika kuipa CCM ushindi.
 
Viongozi wao wamehaidiwa ubunge hivyo ni lzm wawashughulikie wapinzani
 
Upinzani haujaanza kuonewa leo, ni kuanzia mfumo wa vyama vingi ulipoanza. Yanayotokea Leo ni marudio. Ninachoshangaa ni kwamba pamoja na mateso yote upinzani Bado upo Tanzania. Wapo waliopigwa risasi, wapo walidhurumiwa , wapo waliopotezwa na pia wapo walioharibiwa maisha. Yote hayo yamefanyika lakini upinzani haujafa mpaka siku asili itakapoingilia Kati na kumaliza uonevu huu, ni lini tusubiri wakati wa Mungu.
 
Yes ni kweli upinzani huwa unapata mateso. Kibaya upande wao wapinzani ni kushindwa kuelewa kuwa wao pia ni sehemu ya Tanzania. Yaani mtu kama lema anatoroka madeni then anasingizia kuwa eti anataka kuuawa wakati anajua kabisa anadaiwa na benki, na hela zingine alichezea forex akapoteza kama mil 600.
 
Hio ni level ya mwisho kabisa ya serikali ya CCM. Yaani bila dola mambo hayaendi kabisa. Ningependa kama wangekuwa wanabishana kwa hoja, na si kwa mabavu
Wabishane kwa hoja wazitoe wapi hizo hoja ?
 
Mimi sipendi kabisa uonevu. Ukimwonea mwenzio huwezi kunipa sababu yoyote nikaiona ina mashiko.
Kama hao unaowasema wana usaliti ungeweka wazi hapo usaliti wao ni upi. Unamnutralize Mbowe kwa kisingizio cha kuhujumu taifa na huku kodi zetu wewe unazifisadi,, ni nani hapo atakuwa adui wa taifa kati yenu wawili?
Kwanini mnawaza kufanya uovu juu ya uovu. Kama haya tunayoandika yanawaingia kwenye ubongo basi acheni uovu wenu.
Kila mtu ana haki ya kuenjoy kwenye nchi yake.

MWOVU HASHINDI.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Haohao mnawadharau wao na chama chao, haohao mnataka wawalinde huku mkiwatukana. Mfyuuuuu!

Mngekuwa na japo shukrani kidogo basi mnapokosoa. Hakuna jema kwao wametenda. Kila kitu wamekosea. Acha wakosee mazima pengine mtatofautisha mliyeshangilia alipokufa na anayeongoza ngome kwa sasa. Msipotofautisha basi mtateseka sana mkiwa Tanzania.
 
Wasifie wanaowaumiza ?! Roho gani umezaliwa nayo ?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…