Vietnam: Mmiliki wa Tovuti ya kusambaza Filamu haramu akamatwa

Vietnam: Mmiliki wa Tovuti ya kusambaza Filamu haramu akamatwa

Kidagaa kimemwozea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
3,680
Reaction score
6,554
Anayedaiwa kumiliki na kuendesha tovuti haramu ya kusambaza filamu maarufu ‘FMovies’ mapema mwezi uliopita alitambulishwa baada ya kukamatwa na Polisi wa Mji wa Hanoi nchini Vietnam kufuatia uchunguzi wa muda mrefu.

Phan Thanh Cong, 34, raia wa Vietnam aliyekamatwa na mshirika wake, Nguyen Tuan Anh, wanasemekana waliendesha tovuti hiyo na kujizolea ‘pesa nyingi’ kutokana na matangazo.

Hii ni kwa mujibu wa Torrentfreak, tovuti inayofuatilia habari za hakimiliki mtandaoni.

Tovuti ya Fmovies iliyofungwa na mamlaka ya Vietnam mwezi Julai 2024, ilihudumu tangu 2016 na inadaiwa kusambaza filamu na vipindi vya televisheni takriban 50,000 bila leseni kutoka kwa watayarishaji na wamiliki halali.

Kulingana na Motion Picture Association (MPA) na Alliance for Creativity and Entertainment (ACE), FMovies na tovuti zingine chini ya mwamvuli wake ndizo zilikuwa vyanzo vikubwa zaidi ulimwenguni vya usambazaji haramu wa filamu, ikivutia zaidi ya watumiaji bilioni 6.7.

Disemba mwaka 2023, Makamu wa Rais Mtendaji Mkuu wa Motion Picture Association (MPA), Karyn Temple, alifika mbele ya kamati ya bunge la Marekani, na kuonesha jinsi tovuti hiyo ilivyokuwa ikifanya kazi, akidai kuwa FMovies ilichangia kusababisha hasara ya dola bilioni 29.2 kwa mwaka katika sekta ya filamu ya Marekani maarufu Hollywood.

ACE na MPA ziliandikia barua Idara ya Polisi ya Hanoi kuwashukuru kwa kumkamata Cong, ambaye anatuhumiwa kwa makosa ya kukiuka hakimiliki.
1735672902581.jpg
 
Wanazingua sana Hawa hadi yule mwana wa pirate bays nae alidakwa hadi yule mdau wa moviemod na medeberiyaa waliwekwa lokapu nahisi ukiwa na vibali hii mishe unapiga kama kawa
Livha ya faida wanazopata hao viwanda vya filamu lakini bado wanafanya ukuda wa kuzuia filam zao zisivuje
 
Livha ya faida wanazopata hao viwanda vya filamu lakini bado wanafanya ukuda wa kuzuia filam zao zisivuje
Ni haramu Sana kaka Hawa jamaa wanafanya kazi ya hatari sana mungu hawabariki sana kazi zao nzito mno mpaka mafile yanatufikia si mchezo ila skuizi ukiwa na kibali ni halali kabisa
 
M
Sites za kudownload free movies ni nyingi sikuhizi hakuna mfano ,kiufupi ni nimekuwa nikitumia hiyo site kwa muda mrefu tu ,ila sibabaiki maana najua kuna sites nyingine Lundo tu zipo on bado na ninazitumia
Kublock hizi sites no kama kuzuia mafuriko kwa mikono
Mtu ana gharamikia wewe unaenda kupost bure upate mpunga wa matangazo
 
Ni haramu Sana kaka Hawa jamaa wanafanya kazi ya hatari sana mungu hawabariki sana kazi zao nzito mno mpaka mafile yanatufikia si mchezo ila skuizi ukiwa na kibali ni halali kabisa
Sasa kibali si kitakutaka ulioie? Na ukishalipia itakubidi uwalipishe wanaofuata huduma kwako ili urudishe gharama?
 
Ni haramu Sana kaka Hawa jamaa wanafanya kazi ya hatari sana mungu hawabariki sana kazi zao nzito mno mpaka mafile yanatufikia si mchezo ila skuizi ukiwa na kibali ni halali kabisa
Sasa kibali si kitakutaka ulioie? Na ukishalipia itakubidi uwalipishe ili kupata faida?
 
Sasa kibali si kitakutaka ulioie? Na ukishalipia itakubidi uwalipishe ili kupata faida?
Faida inakuja pale wadau wanapokuja kubeba mzigo kwenye website yako kibali nafikiri wanatoa wenyewe wanasema hivi
Contact the copyright holder directly, or contact the distributor if the distributor has the authority from the copyright owner to grant licenses .
 
Dah,kumbe ndiyo maana siku hizi inanigomea.

Imeniokoa sana hii,99% ya movie zangu nilizichukua humu na niliifahamu humu humu jamvini,wakuu basi wekeni nyengine za kupakulia movies tuishi nazo.
 
Dah,kumbe ndiyo maana siku hizi inanigomea.

Imeniokoa sana hii,99% ya movie zangu nilizichukua humu na niliifahamu humu humu jamvini,wakuu basi wekeni nyengine za kupakulia movies tuishi nazo.
Hadi Mimi tumia yts na medeberiyaa na moviemod hata moviemod nao walidakwa harakati zao
 
Sites za kudownload free movies ni nyingi sikuhizi hakuna mfano ,kiufupi ni nimekuwa nikitumia hiyo site kwa muda mrefu tu ,ila sibabaiki maana najua kuna sites nyingine Lundo tu zipo on bado na ninazitumia
Kublock hizi sites no kama kuzuia mafuriko kwa mikono
Mkuu kama hutojali share na sisi wengine tuzifahamu
 
Back
Top Bottom